Ilulu
Senior Member
- Mar 22, 2008
- 161
- 31
Hatimaye leo muda si mrefu nikiwa nawasiliana na wakala wa Usafiri wa Ndege, ameniarifu kuwa Kampuni ya Air Zara International imesitisha huduma zake until further notice. Niliulizia usafiri wa Dar-Mwanza-Dar.
Nakumbuka kumekuwa na vitimbi kadha wa kadha Air Zara wamekuwa wakifanyiwa hivi siku za karibuni, na wapo walioandika juu ya hali hiyo hapa jamvini... siikumbuki ile nyuzi (thread).
Matukio kama haya yaliikuta Kampuni ya Community Air na hatimaye kutoweka kabisa katika anga ya Tanzania.
Ninachojiuliza, kwanini makampuni ya bei nafuu katika huduma hasa hii ya usafiri wa anga hupata misukosuko mingi hapa Tanzania?
Bei ya return Ticket ya Air Zara, Dar-Mwanza-Dar ni Tshs 262,000 ambayo ni cheap mara dufu ulikilinganisha na Makapuni mengine.
Wenye taarifa ya kina tafadhali tufahamishane
Nakumbuka kumekuwa na vitimbi kadha wa kadha Air Zara wamekuwa wakifanyiwa hivi siku za karibuni, na wapo walioandika juu ya hali hiyo hapa jamvini... siikumbuki ile nyuzi (thread).
Matukio kama haya yaliikuta Kampuni ya Community Air na hatimaye kutoweka kabisa katika anga ya Tanzania.
Ninachojiuliza, kwanini makampuni ya bei nafuu katika huduma hasa hii ya usafiri wa anga hupata misukosuko mingi hapa Tanzania?
Bei ya return Ticket ya Air Zara, Dar-Mwanza-Dar ni Tshs 262,000 ambayo ni cheap mara dufu ulikilinganisha na Makapuni mengine.
Wenye taarifa ya kina tafadhali tufahamishane