Jabali la Siasa
JF-Expert Member
- Jul 10, 2020
- 2,545
- 2,177
AG Mstaafu Mhe Jaji Warema azungumzia sakata la kumwita RC David Kafulila "tumbili"
Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema amezungumzia sakata la kumuita tumbili aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila.
Jaji Warema amezungumzia sakata hilo wakati wa mahojiano maalumu na waandishi wa Mwananchi huku akibainisha alitumia jina hilo kama msemo wa Kiganda ukimaanisha ukiwa jikoni ndivyo unavyoweza kubaini mambo.
Sakata hilo ambalo lilikuwa gumzo bungeni na kuibua mvutano kati ya Jaji Warema na Kafulila ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu lilitokea Juni mwaka 2014.
Jaji Werema alimwita Kafulila tumbili huku ikiwa ni katika hali ya kujibu mapigigo, Kafulila akamuita mwanasheria huyo mwizi.
Katika mahojiano hayo maalumu na Mwananchi yaliyofanyika hivi karibuni, Jaji Warema amesema “Tumbili haamui mambo ya jikoni, maana yake nilikuwa namaanisha kuwa tumbili haamui mambo ya msituni,
Sasa mnageuza kuwa anamwambia kuwa ni tumbili, maana yake ni kwamba wewe kama hujui mambo ya huko jioni huwezi kujua” amesema Jaji Werema