Afande Sele: CHADEMA Morogoro walitaka Milioni 30 ndio nigombee Ubunge

Magnesium

JF-Expert Member
Nov 9, 2014
317
185
Kupitia kipindi cha XXL cha Clouds Fm msanii na mtia nia wa kugombea ubunge wa Morogogoro kupitia ACT, Suleiman Msindi maarufu kama Afande Sele, amesema kuwa kilichomfanya atoke CHADEMA kutimkia ACT ni kutokuwepo kwa demokrasia katika chama hicho cha 'Zamani' katika kile alichosema ni viongozi kung'ang'ania madaraka.

Ameongeza kuwa ilifika wakati alitakiwa kutoa kiasi cha pesa kipatacho milioni 30 ili kuwashawishi wajumbe kuteuliwa kuwa mgombea ubunge ilhali yeye hayuko tayari. Ameongeza kuwa aliambiwa kama hawezi kufanya hivyo agombee udiwani kwani watia nia wa ubunge ni wengi.

Afande Sele amesema kuwa hawezi kutoa pesa kugombea ubunge wakati wananchi wa Morogogoro ndio wanaomtaka agombee na yeye haendi bungeni kufuata maslahi bali kuwatumikia wananchi ndio maana katimkia ACT.
 
Tutamwaminije hayo aliyoyasema? si alienda kimya kimya ACT? Kwa nini siku ile anahojiwa baada ya kupewa kadi ya ACT hakuyatamka hayo?

Naona kafuata philosophy ya zito ya kusema uongo kila anapoenda....

Kwahiyo unataka kusema mtu akienda ACT kuna kaphilosophy flani lazima ajifunze..
 
Inasaidia nini kutumia propaganda za chuki kwa sababu ya maslahi binafsi ya mtu? Sele ni msanii anaweza kutumia sanaa nyingine kujikwamua badala ya hii ya maji taka!
 
Tulishasema na tutaendelea kusema, CHADEMA ni Saccos na itaendelea kuwa hivyo na wanufaika ni wachache hawazidi sita.
 
Ukistajabu ya musa kwel utaona ya filauni huyo ndo afande a. K. a.............teeeh teeeh ..........na mwaka huu tutaona vimbwenga vingi Sana bt wa Tanzania tunataka mabadiiko sio ngojera
 
kupitia kipindi cha xxl cha clouds fm msanii na mtia nia wa kugombea ubunge wa morogogoro kupitia act, suleiman msindi maarufu kama afande sele, amesema kuwa kilichomfanya atoke chadema kutimkia act ni kutokuwepo kwa demokrasia katika chama hicho cha 'zamani' katika kile alichosema ni viongozi kung'ang'ania madaraka. Ameongeza kuwa ilifika wakati alitakiwa kutoa kiasi cha pesa kipatacho milioni 30 ili kuwashawishi wajumbe kuteuliwa kuwa mgombea ubunge ilhali yeye hayuko tayari. Ameongeza kuwa aliambiwa kama hawezi kufanya hivyo agombee udiwani kwani watia nia wa ubunge ni wengi.

Afande sele amesema kuwa hawezi kutoa pesa kugombea ubunge wakati wananchi wa morogogoro ndio wanaomtaka agombee na yeye haendi bungeni kufuata maslahi bali kuwatumikia wananchi ndio maana katimkia act.

ngojs tuone maajabu....
 
Tutamwaminije hayo aliyoyasema? si alienda kimya kimya ACT? Kwa nini siku ile anahojiwa baada ya kupewa kadi ya ACT hakuyatamka hayo?

Naona kafuata philosophy ya zito ya kusema uongo kila anapoenda....
Sio lazima uamini! Ukweli utabaki ni ukweli hatakama nyoote hamkuamini.
 
Back
Top Bottom