AC Milan 1-0 Chievo...Good & Bad newz for Milan and Becks

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,301
4,681
1) Dikteta wa kiungo anayekipiga ktk klabu yenye mafanikio zaidi duniani yaani AC Milan Clarence Seedorf ameipatia ushindi klabu yake Hiyo kwa kufanikiwa kufunga goli ktk dakika ya 90+1 kufuatia kazi nzuri ya mtakatifu Gaucho na kupelea vijana hawa watoto wa mkuu wa nchi kuwa pointi 1 nyuma ya Inter.

2) ktk mechi hiyo pia wapenzi wa Diavoli tulisimama na kumpongeza kiungo wetu mkabaji kamanda Massimo Ambrosini kwa kutimiza mechi yake ya 400 akiwa ndani ya jezi yenye upako ya AC Milan.
Kwa niaba ya wapenzi wote wa AC Milan hapa Tanzania napenda kuchukua wasaa huu kumpongeza Ambro kwa yoote mema aliyotutendea.
Na kama kuna mapungufu basi tulishamsamehe kwani tunaamini kuwa yalitokana na hali ya ubinaadamu.

3) mbali na furaha ya ushindi, wafurukutwa wa AC Milan tulipatwa na pigo baada ya kiungo mahili David Joseph Robert Beckham kupata ajali ktk mguu wake wa kushoto hivyo kulazika kutoka uwanjani akiwa amebebwa, ajali ambayo kwa taarifa zisizo thibitishwa zimetanabaisha kuwa huenda akaikosa safari ya kushuka bondeni hapo mwezi wa 6.
kwa masikitiko makubwa napenda kuchukua fulsa hii kumtakia kiungo wetu huyu kheri na apone haraka na aje kulisaidia taifa lake ambalo linamuhitaji ktk mashindano yajayo ya kombe la dunia.

Forza Milan
Grazier seedorf...
I've done my Job...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom