JESHI la Polisi mkoani Rukwa linawasaka watu wasiojulikana ambao wanatuhumiwa kumbaka, kumuua kwa kumnyonga Martha Zacharia (40), kisha mwili wake kuutupa pembezoni mwa barabara.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi (ACP) Mayila Mashenene, amesema tukio hilo lilitokea usiku wa Februari 14, mwaka huu, katika Mtaa wa Makutano, Manispaa ya Sumbawanga huku akibainisha kuwa uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.
Amesema Martha alikuwa mwimbaji wa kwaya ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Epiphania, Jimbo la Katoliki Sumbawanga na inadaiwa kuwa kabla ya kuuawa, alitoka kanisani kusali misa ya Jumatano ya Majivu.
Source - Nipashe
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi (ACP) Mayila Mashenene, amesema tukio hilo lilitokea usiku wa Februari 14, mwaka huu, katika Mtaa wa Makutano, Manispaa ya Sumbawanga huku akibainisha kuwa uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.
Amesema Martha alikuwa mwimbaji wa kwaya ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Epiphania, Jimbo la Katoliki Sumbawanga na inadaiwa kuwa kabla ya kuuawa, alitoka kanisani kusali misa ya Jumatano ya Majivu.
Source - Nipashe