Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Kwa kuwa naamini kuwa; Tunaweza kutofautiana katika mitizamo ya kisiasa lakini sote ni sharti tuishi na kutumika kwa ajili ya MAendeleo ya watu na Taifa kwa ujumla.
Na kwa vile Chama chetu cha Mapinduzi kimeonekana kuwa sasa kimepoteza imani toka kwa wananchi wengi (ndani na nje ya CCM) na hatuoni dalili za kujirekebisha.
Na kwa sababu mwakani tuna muda mfupi wa mwaka kabla ya uchaguzi mkuu, basi tunapaswa kupanga sasa mkakati madhubuti usio na unafiki ili kuwapata Viongozi ambao UTII WAO UTAKUWA KWA WANANCHI KWANZA KABLA YA CHAMA WALA URAFIKI.
Sijui ninyi mnafikiria nini, mimi niko njia panda ama:-
1. Tuwashinikize kwa nguvu zote, kila siku, popote, kwa namna yeyote ya amani vyama vyote vya upinzani Tanzania (wavunje vyama vyao) waungane na tupate mgombea na mwenza wake wanaofafa na kukubalika halafu sote tuwapigie kampeni iliyoenda shule kwa ajili ya kupokea ushindi 2010.
au
2. Tunaoona kuwa CCM ya sasa imepoteza mwelekeo lakini bado tuna nafasi kuliko vyama vingine vya sasa vya upinzani, tujimegue kwa kishindo na kuunda chama tukiite mfano :- CCM-Wananchi na tuwateuwe wawili wasio na mawaa na wenye uwezo wa kuongoza tuwapigie kampeni ya kitaalamu kujiandaa kurejesha Tz katika kuelekea ustawi wa Wananchi.
Pengine wengine mna mawazo tofauti yote yanakaribishwa maana nimeona kuwa siwezi kuendelea kuugua moyoni kwa jinsi ninavyokaa kimya tu wakati nakufa na tai-mbano ya CCM shingoni.
Na kwa vile Chama chetu cha Mapinduzi kimeonekana kuwa sasa kimepoteza imani toka kwa wananchi wengi (ndani na nje ya CCM) na hatuoni dalili za kujirekebisha.
Na kwa sababu mwakani tuna muda mfupi wa mwaka kabla ya uchaguzi mkuu, basi tunapaswa kupanga sasa mkakati madhubuti usio na unafiki ili kuwapata Viongozi ambao UTII WAO UTAKUWA KWA WANANCHI KWANZA KABLA YA CHAMA WALA URAFIKI.
Sijui ninyi mnafikiria nini, mimi niko njia panda ama:-
1. Tuwashinikize kwa nguvu zote, kila siku, popote, kwa namna yeyote ya amani vyama vyote vya upinzani Tanzania (wavunje vyama vyao) waungane na tupate mgombea na mwenza wake wanaofafa na kukubalika halafu sote tuwapigie kampeni iliyoenda shule kwa ajili ya kupokea ushindi 2010.
au
2. Tunaoona kuwa CCM ya sasa imepoteza mwelekeo lakini bado tuna nafasi kuliko vyama vingine vya sasa vya upinzani, tujimegue kwa kishindo na kuunda chama tukiite mfano :- CCM-Wananchi na tuwateuwe wawili wasio na mawaa na wenye uwezo wa kuongoza tuwapigie kampeni ya kitaalamu kujiandaa kurejesha Tz katika kuelekea ustawi wa Wananchi.
Pengine wengine mna mawazo tofauti yote yanakaribishwa maana nimeona kuwa siwezi kuendelea kuugua moyoni kwa jinsi ninavyokaa kimya tu wakati nakufa na tai-mbano ya CCM shingoni.