Buswelu
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 1,998
- 352
Inasikitisha sana, inaumiza roho mno!...na polisi wanasema (watu wasio fahamika na wakti huo huo wanasema huenda ikawa mauaji ya kulipiza kisasi, kauli mbili zinazopingana!....
Mara nyingi kwa kuzingatia kuwa Mwalimu alitokea Mkoa huu wa Mara wenye kila aina ya vitendo visivyo vya kibinadamu, napata shaka sana kuamini kama kweli Mwalimu aliongoza hii nchi kwa mfumo uliosawa na alimuia iwe ya amani kwa misingi ya kuondoa kila aina ya vichocheo vya uhasama kama ukabila, udini, rangi, na Itikadi...Kama Mwalimu huyu tunayemuezni kwa kupenda amani aliweza kuwa "depoti" wahujumu uchumi na waliopinga maendeleo na kuleta chuki (makabaila, Makupe, Mabepari, Vingunge na Mabwenyenye), kwa nini hakufanya hivyo kwa kuwasambaza hawa watu wa kwake ili wakajichanganye na makabila mengine wajue ustaarabu wa kiutu?...
Hii amani aliyokuwa anaihubiri Mwalimu kwa mataifa mengine duniani ambayo haionekani katika eneo alilolazwa yeye mwenyewe imezimikia wapi?....Kama alituma majeshi kwenda kulinda amani nchi za wenzetu, kwa nini huko Mara hakukuwekwa kituo maalumu cha Ulinzi wa Amani na Kufundisha Ustaarabu kwa Watu wake ambao chuki na uhasama vipo kwenye damu?...
Na hata hivi sana, baada ya miaka 10 ya kifo cha "Mwenyeheri Julius Kambarage Nyerere," kwa nini wale wanaodai majukwaani "tunamuenzi Mwalimu" na kuanzisha mchakato wa kumtambua kuwa Mtakatifu, wameshindwaje kuwasaidia hawa watu wake wasichinjane kama Sungura juu ya ardhi aliyozikwa Mwalimu?....Hii ni makasudi na aibu kubwa kwa Taifa iwapo Mara ardhi ambayo mwasisi wa taifa hili linaamani mkubwa dunainai na wametoka pia Makamanda wa Jeshi letu la Wanachi la Ulinzi linaloheshimia pia dunian kwa ulinzi wa amani alktkumbe katika mihimili ya milango yao, mapigao yameshindwa kudhibitiwa...
Mungu Ibariki Tanzania, Wabariki Viongozi Wake....
Mshamalizana usiongelee siasa hii ni mambo ya watu binafsi...Kuua koo ingine tena watu wengi mpaka na watoto...huwezi kuandika kwa maneno mekundu humu...kitendo hiki hakikubaliki hata kama kimeshatokea.