Utachaguaje 10 wakati wote 108 wanasifa?? Je yule atakayeachwa, si ndo atajua kua wale 10 wametoa rushwa??? Mie nafikiri hawa jamaa walikuwa sawa kabisa. Jambo kuu hapa ilikuwa wale wasailiwa kujichuja kwa kujua uwezo wake. Yaani angejirank kama ataweza kupambana na wale wenzake 107 waliobaki.
Jamani hawa jamaa wa CUF yaani wamegoma kabisa kumpa kura Marando?? Kweli nimeamini wao nao ni kama Lyatonga Mrema (watoto wa CCM kwa nyumba ndogo). Sasa wale washikaji wetu MAFISADI mambo lainiiii.
Sielewi wale wote wanaojaribu kupoteza ule ukweli wa kwamba kuna element ya ubaguzi wa rangi, hilo sioni kama ni point ya kuwaambia wana Jamii. Mimi ninachoamini ni kwamba kama kuna mtu anaona kuwa hii ni issue ya ubaguzi wa Rangi na si kweli basi na awatetee hao MAFISADI papa. Well, wasemao...
Hii habari inaukweli mwingi sana, kwani hilo la ufisadi kupitia clearing agency lilianza tangia enzi za RUKSA. Sasa huyo mhesimiwa balozi Omar R. Mapuri anajisikia vipi kumlinda FISADI?? Halafu kumbukeni kuwa huyu ndo alikuwa Katibu Mwenezi wa CCM. Inasikitisha!!!
Hivi huyu mbumbumbu anafikiri kuwa ubunge ni GENGE lake binafsi?? Hajui kuwa nayo ni kazi ya serikali?? Tena ni kati ya MIHIMILI ya nchi?? Kazi kweli kweli!!!!
Siasa na uongozi wa chuki hauna nafasi tena. Naamini kabisa Bwana Mwakipesile ni binadamu, hivyo hastahili kuacha watu wafe kwa njaa kwaajili tu ya mahangaiko yake ya kisiasa.
Nimejaribu kufuatilia kwa takribani miaka miwili hivi sijaona JK akitembelea mikoa ya Iringa na Mbeya, je kuna nini?? Au ni coincidence ...?
Pinda asilete usanii wa Makamba: So far ni serikali ya CCM ipo madarakani na hao viongozi wa serikali wanateuliwa na kuripoti kwenye CCM, then CCM ndio ya...
Ni ukweli mtupu ulioundika. Kwasababu hawa jamaa hawatakawia kusema kuwa wanafunzi wameharibu mali zenye thamani ya kiasi fulani, lakini kiasi hicho wala si 0.05% ya visenti au milions za waheshimiwa. Hawa wanafunzi mara moja wamewafikisha mahakamani, je vijisenti vitapelekwa lini mahakamani??
Poleni sana kwa hayo matatizo ya kusingiziwa.
Lakini kwanini mvunje mageti na vioo n.k.??? Huoni na nyie mnakuwa VIJIFISADI vyetu? Je maji yakishatoka kwenye mabweni yenu nani ataweka hivyo VIOO na mageti mliyovunja?? Je nasie wa Kimara tukikosa maji tukavunje jengo IKULU?? Kuandamana ni haki...
Mwiba, unauhakika wa haya uliyoyaandika? Au unataka kutufurahisha na KUTUUDHI?? Au ndo unalengo la kuficha ukweli wa akina AC? Na maanisha hiyo story yako ya Jamal na Nyerere. "Mungu mlaze pema peponi mwl. Nyerere."
Na wala si fisadi bali ni LIJIFISADI la nguvu. Haiwezekani watu wake wakafisadi yeye akatulia.
Ni jambo jema sana kuzipata hizo form na ndo zitakazotupa mwanga wa jinsi gani mgonjwa huyu "TANZANIA" ni mahututi. Hima tuliokoe taifa letu tukufu.
Mara chache sana migomo huleta mafanikio, bali mara nyingi sana migomo huleta mwanga wa kuonyesha mapungufu mengi kwa wanaogomewa. Ushauri binafsi, next time kabla ya kugoma leteni matatizo yenu hapa ili tuwashauri mfanye nini kutatua hayo matatizo.
Kwa kuwa mmeshagoma basi inabidi mshupalie...
Inawezekana kuwa alikuwa FISADI, lakini ikumbukwe kua Kiula yeye naye alishughulikiwa na mkapa. Hivyo anayodai ni haki tupu, yaani nao wenzake wenye VIJISENTI vyetu washughulikiwe, tena haraka sana.
Kujizulu pekee haitoshi, bali sheria ichukue mkondo wake na hivyo VIJISENTI vyetu turudishiwe. Mbona yule aliyekuwa balozi wetu Italy, prof. ..., wamemburuza mahakamani kwa VIJISENTI hivyo???
Bwana Chenge na nduguzo tunataka vijisenti vyetu tukajengee japo zahanati
Hata kama data zisingekuwa zimetolewa na SFO, bado jamaa hana sababu ya kuzidi kututukana na VIJISENTI vyetu. Kama wapo hao wenye MAJISENTI na anawajua basi afanye lile lililojema kwa kuwaweka hadharani, ili ya kwamba tuamini kuwa hivyo vyake ni vijisenti na MAPESA yametulia pembeni.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.