Nilishawahi kuwaambia wana JF kuwa huyu Lusinde ni mwendawazimu, bahati nzuri yeye mwenyewe amewathibitishia. Nafikiri huyu ni mmoja wa wale vijana ambao Wasira alisema wanavuta bangi.
Kwani unafikiri ni vilaza! ni kwamba wanajua kuwa wao ndo wateule hivyo hata wakijibu utumbo kutakuchwa kama kawa! Ila cc wananchi tunaowachagua ndiyo vilaza zaidi.
Unafkiri ni kweli zile posho hazitoshi!!?? Kinachowasumbua ni kwamba wengi wao hawana uhakika wa kurudi tena bungeni hivyo wanataka kuchukua chao mapema. Mtu kama Lusinde unafkiri anaweza tena kurudi bungeni kwa busara zile alizonazo? Labda kama na wapigakura wake nao wana busara kama yeye!!
Makamba alisema JK ni maarufu kuliko CCM hivyo wabunge wa CCM hawawezi kumgomea CCM. Hawawezi kukiangusha chama maana na wao watakuwa wameanguka.Asilimia kubwa wa wabunge CCM hawawezi wakacmama peke yao mambo yakawanyookea!
Ngurumo usihangaike na wasoma udaku hao,hawawezi kukuelewa. Kukosa nafasi kwako hakuwezi kukufanya usiwe na fikra huru sasa. Mbona Anne Kilango alikuwa ni mwana-CCM tena Mbunge wakati anarusha makombora.
Kipindi cha dakika 45 pale ITV ni kama jukwaa la kisiasa la wanasiasa kutangaza sera zao kwa sababu mtangazaji hana uelewa wa maswali anayouliza hivyo kuwaacha jamaa wanajimwaga tu na majibu ya uongo. Mfano wa karibu ni jana ambapo Mh. Kasimu Majaliwa alipokuwa anadanganya kuwa wanasimamia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.