Daah hautakuja kuendesha gari unalolipenda maana mimi nimeendesha Disco 3 mwaka 2012 ilikua ya 2005 mwaka huu 2024 unazungumzia kushauriwa kuhusu Disco wakati zimekuja gari tofauti nyingi tu na wengine wanaenda nazo hizo na hizo ninyi kuja kushauliwa hizi za 2024 ni huko 2040...
Gharama za kuendelea kukarabati huo Uwanja zitafika gharama walizotumia kujenga Mkapa toka nimeanza kusikia ukarabati ukarabati walikua wanaweza kujenge Uwanja sehemu ingine na ukawa wa kisasa vile vile ila nilichogundua huo Uwanja ni sehemu ya kuibia pesa maana ukarabati utaendelea kuwepo hata...
Uliuza kwa sababu ya rate biashara ya Malawi na Tanzania inategemeana na Exchange rate pia kama chenji wenyewe wanavyosema ikiwa sio nzuri huwezi kwenda kuuza biadhaa iwe Malawi au Zambia...sasa hivi hela ya Malawi ipo juu ukipeleka bidhaa kwa chenji iliyopo utapata kitu mwaka juzi iliwahi...
Unachobisha ni nini mazee nenda hapo Isongole uone Truck za Tanzania zikitoa mahindi Malawi pamoja na Karanga mwezi uliopita Malawi wamepiga marufuku uuzaji wa Maharage kuyatoa nje...Kasungu,Malawi pana soko kubwa la Mazao yanayokuja Tanzania sisi wengine tumezurula sana aisee...
Sio lini mahindi mapana yanatoka Zambia na ndio yanauzwa Nairobi mimi kipindi cha Corona nishapakia mahindi ya wafanyabiashara wakitoa Chinsali /Zambia na kupeleka transit Nairobi kwa kupitia mpaka wa Holili..
Ukiishi mipakani utajifunza kitu ipo hivi kama sasa hivi Zambia wana ukame mahindi yatatoka huku kwenda Zambia na kipindi mahindi yakiwa hapa bei kubwa mahindi yatatoka Zambia na kuja kuuzwa kwenye mikoa ya mipakani huu ni mzunguko wa kawaida tu..
Daah unaambiwa peleka Arusha au Nairobi unazungumzia Dodoma hautaki hela wewe au hauna njaa ya hela Mkuu..mwenye njaa ya pesa akiambiwa kazi vifungo vya shati anafungia kwenye Bus vizuri la Mbeya vizuri na ukifanya uje na mrejesho hapa..
Hautasumbuka hapo Uyole, Mbeya wapo pia wasafirishaji wa Fusso ila uweke alama vizuri za mzigo wako na Mafiati hapo unachukua tani moja ambayo ni 1000 Kg kule wanauza kwa debe utapima utajua ununue kiasi gani Karanga Nyekundu kwa kaskazini ni kama madawa yao ya kulevya hata bei tofauti ni kubwa...
Usifanye biashara haramu mpakani TRA wakikukamata utadhani umerogwa kumbe wewe mwenyewe ulikua na tamaa na ulikua hauna code zao ukiwa na hela kidogo lipa vitu vyote vya Serikali hela utapata kidogo kidogo kuliko ukikutana na TRA harafu hela yenyewe ndio hiyo hiyo wahuni wanaichukua...
Jinsi ya kusafirisha Karanga kutoka Mkoa wa Mbeya tumia posta wao tani moja ni Tsh 70,000 mpaka Dodoma kutoka pale kwenda Arusha ni pua na mdomo magari mengi mwanzo ilikua mpaka Arusha ni bei hiyo hiyo ila wamefuta safari ya kupeleka mizigo Mbeya mpaka Arusha...hiyo kazi ukiifanya kwa muda mrefu...
Nenda Isongole ipo ileje pale wanauza mazao mengi kutoka Malawi na hasa mnada wao upo Ijumaa kama ntakua sijasahau unaweza kuchukua Karanga pale na kwenda kuuza mpakani na Kenya wowote watanunua ukiweza unapeleka Nairobi na pia hapo Isongole nyuma kidogo panaitwa Ikumbilo nadhani pana Njia ya...
Shocks za Subaru ya 2012 nilinunua SA za mteja kutoka Subaru mpya ilikua 2.8m za kitanzania zote nne...wakati gari zingine napata Nuggets pale hata kwa Tsh 500,000 zote mpya hizo au Bumper to bumper..baadhi ya Subaru parts zake zipo juu kushinda Mercedes benz si bora nikae kwenye Benz tu..
Wabongo waongo sana mimi nilikua na disco 3 mwaka 2012 ilikua ya 2005 maisha yalienda mpaka niliiuza ukiwasikiliza wabongo hautafanya kitu unakuta mtu kanunua gari imempita umri wa kutengenezwa harafu anataka matatizo ya hiyo gari yawe ya Jumla wakati sio kweli..Disco 4 ina tatizo gani kama...
Hizi LR 110 za toka 1998 mpaka 2002 bado zipo sokoni mnataka kutumia Cat mashine sasa nazo pia hydronic pump ikisumbua ina mtihani kwenye bei kuhusu gari ni kwamba kutokana na kodi kuwa kubwa Watanzania wengi tunanunua gari ishakua chakavu ukiikuta na uchakavu wake kila muda inashinda gereji...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.