Ahaaah nilitaka kufanya QT ili nibadilishe majina, nikarudie kidato cha nne maana hii digri ya physics (bsc in physics) haijaniwezesha kujiunga na kuwa askari JW. Ili badae nisake gamba jipya la kuzaliwa nishushe umri kisawasawa kwa kadri ya hawa wanangu wa "Juliet Whiskey Tango Zulu"...
Morali ipo ya kutosha imejaa mpaka inamwagikia lakini nafasi hupewi anapewa mhuni ambaye yani jeshi siyo hobi yake kiufupi mwana kule anafuata mshahara tuu kwa sababu Inakuwa hana namna nyingine ya kufanya yani ajira imeshindikana kupatikana kitaa ndiyo sasa akipata nafasi kule anaona bora...
Ikitokea naenda tuu, maana hakuna namna. Ili mradi niwe nalinda usiku, kupiga kwata kwa unaa mkubwa, kombati ya jeshi niwe naitupia kwa mwili ile imenyooshwa kwa pasi mpaka nzi anakatika akijichanganya ! Buti inang'ara kama kioo ....kidevu kiwe kipara kichwani kuwe na upara, kila siku mabio...
Nipo Dar kwa sasa NIda ipo mda sana tangu 2017 mkuu, nilitaka kujua kama hawaulizi ķwenye usaili ili nijipige kifua nikajaribu tena bahati JKT. Au kama inawezekana nijisajiri upya nibadilishe mwaka wa kuzaliwa na jina kabisa. Ili wakiihitaji jeshini nisipate taabu maana hii iliyopo umri wake ni...
Sawa. Mwenyezi Mungu ninamuomba sana, sichoki. Japo hajanifungulia baraka nikawa Jeshini. Sema kusali na kutubu dhambi muhimu maana mtu hajui anakufa lini, isije ikawa taabu katika maisha mengine yanayofuatia baada ya hapo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.