Vijana tunaomba umri wa kustaafu uwe miaka 45 hiari na 55 lazima

Kuelekea siku ya wafanyakazi nchini Mei mosi, vijana ambao wanahitimu elimu ya vyuo vikuu tunaomba Serikali yetu chini ya Rais wetu mpendwa Mama Samia na timu yake yote tunamuomba jambo moja nalo ni;

1. Umri wa kustaafu upunguzwe uwe miaka 45 hiari na 55 iwe lazima, badala ilivyo sasa kuwa 50 hiari na 55 hadi 65 lazima.

Suala hili la umri wa kustaafu limekuwa kikwazo kikubwa kwa upatikanaji wa nafasi kwa kundi kubwa la vijana wanao hitimu vyuo vikuu.

Utafiti unaonyesha kwenye idara mbalimbali za serikali kuna wazee wengi ambao tayari wamechoka, hawana tija, hivyo ni vyema umri wa kustaafu ukapunguzwa ili kupisha vijana nao walitumikie taifa lao.

Tunaomba pendwkezo hili lizingatiwe.
Nnakupongeza sana kwa kuwaza Kisomi na kimkakati ,kongole kwako mtoa Mada on top of that naishauri serikali au nnaiomba serikali yangu pendwa mikataba ya serikali isiwe ya kudumu(permanent and pensionable kama ilivyo sasahivi bali iwe yamiaka kumi kumi au mitano mitano,kulingana na mahitaji ya mtumishi maana unakuta mtu katumikia let say miaka kumi na tano ashachoka kuitumikia serikali anataka kutoka ila anaogopa kuacha pension yake hivyo kupelekea kufanya kazi kimazoea ,Niheri kuwe na room ya wafanyakazi ku-exit waonapo kua wamechoka kuitumikia serikali ili kupisha damu mpya zenye uhitaji wa kuchapa kazi kuitumikia serikali yao.iwe kama mpishano tu wengine wanaingia wengine wanatoka hii huenda ikapunguza msongamano wa kundi lisilo na ajira ila pia waliochoka kuitumikia serikali walipwe madai yao kwa mda walipotumia serkali waende kulitumikia taifa kwa namna nyingine,sio kulazimishana hadi tufike miaka 60.
 
Wazeni kujiajiri na sio serikali kuajiri nyie ndiyo muongeze kampuni binafsi mtakazo ajiri kuipunguzia serikali mzigo
 
Nnakupongeza sana kwa kuwaza Kisomi na kimkakati ,kongole kwako mtoa Mada on top of that naishauri serikali au nnaiomba serikali yangu pendwa mikataba ya serikali isiwe ya kudumu(permanent and pensionable kama ilivyo sasahivi bali iwe yamiaka kumi kumi au mitano mitano,kulingana na mahitaji ya mtumishi maana unakuta mtu katumikia let say miaka kumi na tano ashachoka kuitumikia serikali anataka kutoka ila anaogopa kuacha pension yake hivyo kupelekea kufanya kazi kimazoea ,Niheri kuwe na room ya wafanyakazi ku-exit waonapo kua wamechoka kuitumikia serikali ili kupisha damu mpya zenye uhitaji wa kuchapa kazi kuitumikia serikali yao.iwe kama mpishano tu wengine wanaingia wengine wanatoka hii huenda ikapunguza msongamano wa kundi lisilo na ajira ila pia waliochoka kuitumikia serikali walipwe madai yao kwa mda walipotumia serkali waende kulitumikia taifa kwa namna nyingine,sio kulazimishana hadi tufike miaka 60.
Ahsante sana kwa kuongeza nyama.
 
Kwakuwa umeanza mwenyewe kusema kuelekea mei mosi (Siku ya wafanyakazi) unafikiri hao wafanyakazi watakuwa na hoja hiyo?

Kumbuka hao ndio wahusika wakuu wa Siku hiyo na Sio wewe kijana uliopo chuoni

🤣🤣🤣🤣
 
  • Thanks
Reactions: FWC
Wazeni kujiajiri na sio serikali kuajiri nyie ndiyo muongeze kampuni binafsi mtakazo ajiri kuipunguzia serikali mzigo
Sawa, lakini hiyo haimaanishi kuwa serikali haito ajiri la! hivyo tunapaswa tutengeneze mazingira muafaka ya kuajiri nguvu mpya. wapo watakao ajiriwa na wapo watakao jiajiri.
 
Mnataka vijana wenzenu wa miaka 45 wastaafu! Yaani wenzenu walisota mtaani baada ya kuhitimu vyuo wakaja kupata ajira in the late above 30 then warudi mtaani baada ya miaka kumi ? Hicho kikokotoo mnakijua lakini? Hebu acheni wenzenu nao wale keki ya taifa mpaka wafie huko kama hawatafikia umri wa miaka 60 ya kustaafu kwa lazima. Vumilieni mitaani kuna fursa nyingi za kiuchumi huko, sio lazima muajiriwe wote kwa kuwa mmesoma. Wengine mjiajiri wenyewe
 
Mifuko ya pension haina pesa, fatilia ulaya wanataka iwe 70. France maandamano yalikua mengi kupinga 65.

Tatizo ni mifuko ya pension haina hela kulipa ukistaafu mapema.
@jeffvar naomba kuuliza ni kwasababu gani zinapelekea hii mifuko ya hifadhi ya jamii kurun-bankrupt ilihali imekua ikikata pesa zawanachama nakuwatunzia.
 
Kwanza umeshasema siku ya wafanyakazi halafu wewe sio mfanyakazi nani atakupa nafasi ya kutoa hilo wazo lako.

Subiri siku ya Jobless duniani ndio utoe wazo lako huenda likapewa kipaumbele.

Waliopo kazini sidhani kama wanatamani kustaafu iwe kwa hiyari au lazima.
 
Kwanza umeshasema siku ya wafanyakazi halafu wewe sio mfanyakazi nani atakupa nafasi ya kutoa hilo wazo lako.

Subiri siku ya Jobless duniani ndio utoe wazo lako huenda likapewa kipaumbele.

Waliopo kazini sidhani kama wanatamani kustaafu iwe kwa hiyari au lazima.
naamini wapo wafanyakazi wazee watakuwa wamenielewa na watanisaidia kufikosha ujumbe kunako stahili.
 
Sawa, lakini hiyo haimaanishi kuwa serikali haito ajiri la! hivyo tunapaswa tutengeneze mazingira muafaka ya kuajiri nguvu mpya. wapo watakao ajiriwa na wapo watakao jiajiri.

Anza na ujasiriamali hatu kwa hatua na kukuza mtaji najua utaniuliz mtaji nitapata wapi, there is always away. Lakini hilo la Kuishauri serikali kupunguza miaka ya kustaafu ni uongo wazee wanateseka sana baada ya kustaafu kwa umri uliowep kisheria kwa kuwa kikokotoo hakijaaandaliwa kumtunza mzee huyo alielitumikia taifa katika ofsini za serikali na hata binafsi sasa kupunguza umri wa kustaafu kwa kujiangalia vijana tu mnakosea, vijana ni nguvu kazi muwaze nje ya box kuleta msaada katika jamii kutatua kero ya ajira na sio kuililia serikali kwa vitu vilivyondani ya uwezo wenu
 
Back
Top Bottom