Venezuela gets its first shipment of gold bars back from Europe

The treasure safes at BOT were an designed only for $$$$$ , ££££££££ and Tsh . It expensive and risky for Tanzania to have gold reserve ............................ lol .
Usintake nitukane bure mon ami kwa kunikumbusha ujinga wa viongozi wetu na hasa jinsi Faiza Foxy anavyo watetea. Nyerere katika press comference moja wakati anaongelea shinikizo la IMF aliwahi kusema ".. and we have too many stupid leaders... Can't you say no? ".

Yaani kweli hawa wezi wa IMF wanakwambia usitunze dhahabu yako bali uweke makaratasi (fiat money) ambayo thamani yake haina uhalisia (no intrinsic value) halafu unakubali, Khaa! Unajua tulipokuwa watoto tulikuwa tunawacheka wakinachifu Mangungo lakini bado tunao wengi hata sasa, japokuwa wamesoma. Unajua hili neno msomi siku hizi linaanza kunipa shida kidogo...
 

Ndio namimi nashangaa, eti utajiri wa nchi unakuwa defined kwa kuwa na dola nyingi, hizi si ni rahisi sana ku manipulate, teh teh teh. Hivi kwanini serikali isiwafukuze wawekezaji wa madini kwa week moja, hiyo week inatumika kuijaza BOT dhahabu.

Harafu baada ya week moja wanawarudisha, vyombo vya magharibi wakipiga kelele waanaabiwa ilikuwa ni kiusalama maana AL-shabaab na Alqaida walikuwa pale wanaanda mashambulizi. Mnawaonyesha mabomu ya gongo la mboto. Teh teh teh
 

Dr. jakaya anaagiza turudishiwe vyura na mijusi yetu.

black pipo ukiwachunguza ni sawa na kuchunguza kuku.
 
Which risk?
I dont know but tusaidiane kuuwauliza wahusika.......
Kama umesoma vizuri comment zangu za awali nadhani utaelwa nilimanisha nini.
Am sure wasomi wetu na wachumi wetu "waliboboea" waliona kuhifadhi dhahabu ni risk na mpaka leo hata baada matatizo ya uchumi wa dunia bado wanaona ni "risk" kuwa na reserve ya dhahabu ndio maana unaona they don't care. Usishange tukapewa sababu ama anazotoa FF. Wamekariri kuwa kila ushausri wa IMF ni mzuri. na ho magavana wa BOT wengi si wanakuwa wameshafanya kazi huko.........

Hahahah chamoto tukana kimyo moyo lakini ni "dhambi" teh teh teh teh
Best paying public insititution ya tanzani ni BOT . Tunaamini kuna vichwa vya uchumi na mambo ya fedha pale lakini mimi njuliza hivi wanafanya nini? mimi siyo mchumi lakini dah. hata kama yalikuwa makosa basi ilikuwa muda waone ushauri wa iMF ulikuwa mbovu kulingana a current economic situation.
Dr. jakaya anaagiza turudishiwe vyura na mijusi yetu.

black pipo ukiwachunguza ni sawa na kuchunguza kuku.
Wanarudisha vyura huku tunahujumu utalii wenyewe kwa kuuza swala, twiga, simba na wanyama pori wengine . So watalii wanaweza kuona twiga simba hata akienda Qatar. Ulizia mapato ya zoo ya UK iliyojaza wanyama kutoka frica mashariki. mapatao yanazidi income ya serengeti. ingependeza wasomi wetu wakau hawa wayanyam kama kuna ulazima basi tukwakodishe na hakimiliki ibaki kwetu hata kama gharama yake ni $20 kwa siku. Sio kuwauza.
 
Kwani serikali hawawezi kuchimba dhahabu Buzwangi kwa siku 3 na kujaza BOT? ama mnaongelea dhahabu gani? wanachumi tusaidieni.
Labda yawezekana munaongelea dola??

Mkama,

Tatizo sio wao kushindwa kuchimba dhahabu tatizo nilishalieleza mapema: hawa tunawowaita wataalamu wetu wa uchumi ni malimbukeni na watumwa wa Bretton Woods institutions, leo hii uchumi wa nchi unaangamia na hata mtoto wa darasa la tatu atakwambia hivyo lakini wao bado watakwambia kuwa uchumi unakua. Kumbuka kipindi cha Mwalimu tulikuwa na maprofesa wachache sana wa uchumi lakini tulikuwa na hifadhi ya dhahabu na Shilingi na Dola havikuwa vikipishana sana.
 

Nimekuelewa mkuu,
Lakini tatizo letu ni nini hasa, maana mie kwa kweli huwa sielewi . Na hua naenda mbali na kufikiria tatizo sio elimu, nafikiri tatizo liko ndani ya sisi wa afrika kuna kitu kimejificha labda ndani yake.
 
Harafu baada ya week moja wanawarudisha, vyombo vya magharibi wakipiga kelele waanaabiwa ilikuwa ni kiusalama maana AL-shabaab na Alqaida walikuwa pale wanaanda mashambulizi. Mnawaonyesha mabomu ya gongo la mboto. Teh teh teh

Nimeipenda hii lakini inahitaji mtu anaye jiamini kifikra katika kujitegemea.
 
Nimekuelewa mkuu,
Lakini tatizo letu ni nini hasa, maana mie kwa kweli huwa sielewi . Na hua naenda mbali na kufikiria tatizo sio elimu, nafikiri tatizo liko ndani ya sisi wa afrika kuna kitu kimejificha labda ndani yake.

Unajua kivitendo huwezi ku-download 2 TB file kwa kutumia 50 MHz 80486 processor kwenye dial up connection itachukua muda mrefu sana.

Kwahiyo tatizo siyo vifaa vya kiutendaji (elimu) bali uwezo wa kufikiri. Haijalishi umesoma wapi na kwa miaka mingapi kama uwezo wako wa kifikiri kutatua matatizo yako ni mdogo hutaweza kutumia hiyo elimu uliyopata vilivyo.

Neno elimu (education) linatokana na neno la kiyunani 'educo' (to draw out from within) yaani kuchomoa maarifa yaliyo katika ubongo wako. Sasa unapo kwenda shule huwa unaongeza idadi ya vifaa vya kupakuwa kile ambacho teyari kipo ndani ya ubongo wako.

Elimu ya darasani in yakukusaidia kuwezesha kuchomoa marifa mengi ili kutatua matatizo ya maisha ya kila siku. Tatizo ni kwamba tunaangalia idadi ya madarasa kama kigezo cha ufahamu wakati ukweli ni kwamba kama hauna huo ufahamu haijalishi umekariri formula ngapi. Ndiyo maana watu kama nyerere walikuwa wakiongea unasema, "huyu mtu kweli ni kichwa", kwasababu alikuwa na uwezo wa kufikiri kama yeye bila ya kuangalia tools alizonazo (usomi).

Ili kurahishisha ninacho kisema nitakupa mfano wa herufi. Peke yake herufi hazina umuhimu wowote, ni random letters tuu lakini mtu kama Shabaan Robert akizipanga vizuri kutengeneza shairi unasema, "sijui kwanini sikufikiria vile". Lakini herufi hizo hizo zikipangwa na baadhi ya wapiga upupu wa hapa JF unajiuliza hivi kweli huyu anaamini anacho kisema au ni kuudhi watu tuu.

Kuhusu uwezo wetu wa kufikiri kama waafrika, hilo linategeneana na vitu vingi kwasababu maarifa hayatokani na rangi ya mtu. Hata umagharibini kuna vilaza wengi sana ila nafikiri waafrika kwa ujumla tuna tatizo la kujiamini. Na hii inatokania na mfumo uliopo wa "it's alright because it's all white" .

kuanzia mavazi, elimu, vitabu na utamaduni kwa ujumla unaonyesha kuwa utamaduni wa kizungu ni bora. Hivyo wengi tunakuwa tumerogwa na weupe bila kujijua. Ndiyo maana huko nyuma niliwahi kusema inatubidi tuwe na wavumbuzi wetu ili vizazi vijavyo vikisoma, " kanuni hii ya kutendeneza umeme iligunduliwa na MkamaP", anajisemea YES na mimi siku moja nitaweza kufanya hivyo. Lakini kama kila tunachosoma kinatoka kwa wamagharibi basi hii itatufanya kuendelea kuwa daifu kwa miaka mingi ijayo bila kujijua.
 
maamuzi ya kigumu,wazungu kitu gani bwana?
wezi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…