Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Haya ni maoni ya Mhariri wa gazeti la Habari Leo. (msisitizo wa rangi nyeusi wangu na maoni ya kwenye mabano - MM)
Tukarabati haraka miundombinu bila kuogopa gharama
Imeandikwa na Mhariri;
Tarehe: 26th January 2010
UHARIBIFU wa miundombinu uliotokana na mvua kubwa zilizonyesha Tanzania Bara, si siri tena kuwa ni mkubwa na unaohitaji hatua za haraka ili kuirekebisha na shughuli za kawaida zirejee.
Hilo linajidhihirisha hasa kutokana pia na Rais Jakaya Kikwete, kushtuka na kutaka kuchukuliwa kwa hatua za kutengeneza upya miundombinu hiyo, hasa reli na barabara, katika baadhi ya mikoa nchini.
Kama alivyotahadharisha Rais, tukicheza, Watanzania tutashuhudia uchumi wetu ukiishiwa nguvu na kuanza kuhaha tena kutafuta misaada kwa wahisani na wafadhili, ambao wengi wao wamekuwa wakirudi nyuma katika misaada kutokana na sababu zao.
Cha msingi ni kuelewa tu kuwa hatuna mjomba wa kutubebea misalaba yetu na hivyo hatuna budi kujizatiti kwa lengo la kurejesha miundombinu yetu ili kunusuru uchumi huu ambao tayari ulishaguswa na kudorora kwa uchumi wa dunia. (really?)
Wataalamu wanasema uharibifu uliofanyika katika Reli ya Kati na hasa kati ya Stesheni za Gulwe na Kilosa, katika mikoa ya Dodoma na Morogoro, kutokana na mvua zilizonyesha Mpwapwa na Kilosa kati ya Desemba 24 mwaka jana na Januari 10 mwaka huu, ni mkubwa. (kweli walihitajika wataalamu kusema kilicho wazi?)
Walimwambia Rais kuwa katika maeneo ya Kilosa, mvua hizo na mafuriko, yalingoa kabisa sehemu ya Reli ya Kati na kusimamisha huduma za reli hiyo kati ya Dar es Salaam na Dodoma. (hakuna aliyeona?)
Pia madaraja tisa yalisombwa na maji na mengine matatu yako katika hatari ya kusombwa. Ukarabati huo ni kazi kubwa kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo, kwamba unaweza kuchukua hadi miezi mitatu na gharama inakadiriwa kuwa Sh bilioni 13.2 na hasa ikizingatiwa kuwa uharibifu huo umefanyika katika mikoa 18 nchini.
Sisi tunauelewa uzito wa kazi yenyewe, lakini pia umuhimu wa kurejeshwa kwa miundombinu hiyo ambayo ni uti wa mgongo wa maendeleo ya uchumi wa nchi hii masikini ambayo inajikongoja kufikia maendeleo ya kweli.
Huu ni mzigo wa Watanzania wote, hivyo tuitie moyo Serikali iweze kuzipata fedha hizo na kuanza kazi mara moja, ili wakulima waweze kusafirisha mazao yao kwenda sokoni na pia wafuate huduma na bidhaa kutoka wanakozihitaji. (kama ni mzigo wa Watanzania wote kwanini tusiubebe?)
Lakini pia wadau wanapaswa kujitokeza kushirikiana na serikali kwa namna moja au nyingine, kwa hali na mali, katika kurejesha miundombinu hii, tunazungumzia wafanyabiashara wakubwa na kampuni mbalimbali zenye uwezo wa kuchangia. (Habari Leo je?)
Tunaamini kampuni zenye migodi mathalan, ni wasafirishaji wakuu wa zana na mazao yao kupitia barabara na reli, hivyo kuvurugika kwa miundombinu hii ni jambo ambalo linawasibu zaidi na watakuwa na uchungu na watajitolea kwa sababu kutoa si utajiri.
My Take:
Tuna tatizo kubwa kweli katika kutazama mambo. Yaani hawa jamaa kitu ambacho wameona ni kikubwa zaidi kuathirika ni miundo mbinu! Vipi kuhusu "watu"? Yaani kuvurugika kwa miundo mbinu kumewaathiri zaidi makampuni ya migodi kwa vile sasa hawawezi kusafirisha madini?
Kilichoniacha hoi zaidi ambacho ni kufanana kule kule kwa fikra za Guardian na Habari Leo ni hilo la kichwa chao cha habari. Kwa vile ni dharura basi tusijali gharama? kama huu siyo kuitisha mlango wa ufisadi tuiteje. Hivi kuna mtu yeyote anayefikiria suala la kuangalia matumizi ya serikali na kubana matumizi au sasa hivi ndio imekuwa "spend spend spend"..!?
Tukarabati haraka miundombinu bila kuogopa gharama
Imeandikwa na Mhariri;
Tarehe: 26th January 2010
UHARIBIFU wa miundombinu uliotokana na mvua kubwa zilizonyesha Tanzania Bara, si siri tena kuwa ni mkubwa na unaohitaji hatua za haraka ili kuirekebisha na shughuli za kawaida zirejee.
Hilo linajidhihirisha hasa kutokana pia na Rais Jakaya Kikwete, kushtuka na kutaka kuchukuliwa kwa hatua za kutengeneza upya miundombinu hiyo, hasa reli na barabara, katika baadhi ya mikoa nchini.
Kama alivyotahadharisha Rais, tukicheza, Watanzania tutashuhudia uchumi wetu ukiishiwa nguvu na kuanza kuhaha tena kutafuta misaada kwa wahisani na wafadhili, ambao wengi wao wamekuwa wakirudi nyuma katika misaada kutokana na sababu zao.
Cha msingi ni kuelewa tu kuwa hatuna mjomba wa kutubebea misalaba yetu na hivyo hatuna budi kujizatiti kwa lengo la kurejesha miundombinu yetu ili kunusuru uchumi huu ambao tayari ulishaguswa na kudorora kwa uchumi wa dunia. (really?)
Wataalamu wanasema uharibifu uliofanyika katika Reli ya Kati na hasa kati ya Stesheni za Gulwe na Kilosa, katika mikoa ya Dodoma na Morogoro, kutokana na mvua zilizonyesha Mpwapwa na Kilosa kati ya Desemba 24 mwaka jana na Januari 10 mwaka huu, ni mkubwa. (kweli walihitajika wataalamu kusema kilicho wazi?)
Walimwambia Rais kuwa katika maeneo ya Kilosa, mvua hizo na mafuriko, yalingoa kabisa sehemu ya Reli ya Kati na kusimamisha huduma za reli hiyo kati ya Dar es Salaam na Dodoma. (hakuna aliyeona?)
Pia madaraja tisa yalisombwa na maji na mengine matatu yako katika hatari ya kusombwa. Ukarabati huo ni kazi kubwa kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo, kwamba unaweza kuchukua hadi miezi mitatu na gharama inakadiriwa kuwa Sh bilioni 13.2 na hasa ikizingatiwa kuwa uharibifu huo umefanyika katika mikoa 18 nchini.
Sisi tunauelewa uzito wa kazi yenyewe, lakini pia umuhimu wa kurejeshwa kwa miundombinu hiyo ambayo ni uti wa mgongo wa maendeleo ya uchumi wa nchi hii masikini ambayo inajikongoja kufikia maendeleo ya kweli.
Huu ni mzigo wa Watanzania wote, hivyo tuitie moyo Serikali iweze kuzipata fedha hizo na kuanza kazi mara moja, ili wakulima waweze kusafirisha mazao yao kwenda sokoni na pia wafuate huduma na bidhaa kutoka wanakozihitaji. (kama ni mzigo wa Watanzania wote kwanini tusiubebe?)
Lakini pia wadau wanapaswa kujitokeza kushirikiana na serikali kwa namna moja au nyingine, kwa hali na mali, katika kurejesha miundombinu hii, tunazungumzia wafanyabiashara wakubwa na kampuni mbalimbali zenye uwezo wa kuchangia. (Habari Leo je?)
Tunaamini kampuni zenye migodi mathalan, ni wasafirishaji wakuu wa zana na mazao yao kupitia barabara na reli, hivyo kuvurugika kwa miundombinu hii ni jambo ambalo linawasibu zaidi na watakuwa na uchungu na watajitolea kwa sababu kutoa si utajiri.
My Take:
Tuna tatizo kubwa kweli katika kutazama mambo. Yaani hawa jamaa kitu ambacho wameona ni kikubwa zaidi kuathirika ni miundo mbinu! Vipi kuhusu "watu"? Yaani kuvurugika kwa miundo mbinu kumewaathiri zaidi makampuni ya migodi kwa vile sasa hawawezi kusafirisha madini?
Kilichoniacha hoi zaidi ambacho ni kufanana kule kule kwa fikra za Guardian na Habari Leo ni hilo la kichwa chao cha habari. Kwa vile ni dharura basi tusijali gharama? kama huu siyo kuitisha mlango wa ufisadi tuiteje. Hivi kuna mtu yeyote anayefikiria suala la kuangalia matumizi ya serikali na kubana matumizi au sasa hivi ndio imekuwa "spend spend spend"..!?