Elimu ya Kinywa: Usafi wa meno na kinywa kwa ujumla, sababu, kinga na tiba za harufu mbaya

Napiga mswaki mara mbili kwa siku asubuhi na usiku kabla ya kulala, pia baada ya kupiga mswaki huwa nasukutua mdomo kwa kutumia mouth wash ya listerine. Dawa za meno ambazo naona ziko vizuri ni Colgate, sensodine na close up ila ni muhimu kununua original.
Natafuta sana hizo mouth wash, nina mchumba wangu japo hajaniambia ila naona tukiwa tumelala hataki kunigeukia, ananipa mgongo hivyo nahisi labda nina harufu mbaya inayotoka mdomoni na puani.

Japokuwa tukitaka kulala huwa tunapiga mswaki. Nipeni ushauri nifanyeje ili nisimpoteze shemeji yenu.
 
Sijawahi kuona wala kusikia dawa ya kuondoa harufu mbaya ya mdomo.

Ila nijuacho kuna mbinu na bidhaa kadhaa ambazo mtu unaweza kutumia na kupunguza hilo tatizo kwa kiasi kikubwa sana.
Tusaidie basi hizo mbinu za kuondokana na harufu mbaya. Ni tatizo kwangu
 
Nyani Ngabu,
Asante kwa uzi huu, juzi nimeng'oa jino kwa sababu lilikuwa limetoboka na hivyo lilikiwa linaniuma sana.

Nikajiuliza ni mdudu gani huyo anayeweza kutoboa jino gumu kiasi hicho?

Na naweza kumkwepaje asitoboe tena? Maana kama ni mswaaki napiga kila siku tena marambili. Alipata wapi nafasi ya kulitoboa jino langu wqkati nasafisha wakati wote?

Nilimuuliza daktari ni dawa gani ya meno nzuri tanzania akaniambia ni cologate total je ni kweli?

pole kwa maswali mengi
 
Huo muda wa miezi mitatu ni kweli kabisa, pia wataalamu wanadai kwamba kama utaugua magonjwa kama mafua au kukohoa basi utakapopona tu mswaki huo uliokuwa unatumia wakati ukiugua uutupe na kuanza na mpya ili kuepuka bacteria ambao ulikuwa nao wakati unaugua kifua/mafua. Pia wanasema kunywa maji husaidia usafi wa kinywa, kuwa na kinywa ambacho kiko kikavu (dry) huongeza uwezekano wa bactreria kuongezeka kinywani.

Nyani Ngabu,
 
Usafi wa kinywa pia huendana na mishughuliko ya kinywa (activities) mate yana enzyme inayosaidia kusafisha kinywa in between meals. Ukipitisha muda mrefu bila kula ni muhimu kunywa sips ndogo za maji kila mara. Kama umefunga uzalishaji wa mate unapungua hivyo kumbuka kupaka vaseline kwenye lips kuzuia midomo kupasuka.
 
kuna clip niliona YouTube on how to whiten teeth wakaonyesha unaweza Tunis baking powder unachanganya na lemon mpka itengeneze paste then upige kwenye me no ila kwa usiku tu for a week...nisaidienu is this an effective method?
 
kuna clip niliona YouTube on how to whiten teeth wakaonyesha unaweza Tunis baking powder unachanganya na lemon mpka itengeneze paste then upige kwenye me no ila kwa usiku tu for a week...nisaidienu is this an effective method?
To be honest with you, dentist wangu amenishauri niachane hata na hizi whitening toothpaste, zinaharibu meno. Kama nenda kwa dentist wanaprocedure zao zinga gharama kidogo ndizo celebrities wanatumia.
 
Back
Top Bottom