X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Salaam nawatumia, wa bara na visiwani,
Mwenzenu nimeumia, ulimi umenihaini,
Tamko limetimia, kutenda naona soni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Nilisema kwa dhihaka, nakutaka mwafulani,
Naye akaniitika, kasogea barazani,
Neno liliponitoka, hakuwa na ukinzani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Mwili ulinitetema, joto kapanda mwilini,
Natikisika kwa homa, palepale barazani,
Bint akinitazama, huku atweta moyoni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Sikuweza kuthubutu, kumkaribu chumbani,
Akili ikawa butu, kama mfu kuzimuni,
Rijali sikuwa kitu, macho kitazama chini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Binti kazidi sogea, karibu na mlangoni,
Macho akikodolea, wanaopita njiani,
Pale alipokolea, akanisukuma ndani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Nilitamani kulia, ili waje majirani,
Naye akanitishia, nisilie asilani,
Na ndani akaingia, akanivuta chumbani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Nilishikwa na butwaa, hakika sikuamini,
Ilikuwa ni fadhaa, kubwa iso na kifani,
Binti yule akakaa, uchagoni kitandani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Namshukuru Rabbuka, Rabbi aso na kifani,
Binti aloyatamka, ni mambo mema ya dini,
Kaka mimi nakutaka, tuwe sote maishani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Hii kwenu changamoto, naomba yenu maoni,
Nipeni mawazo moto, mwenzenu nifanye nini,
Binti kwa kweli ni moto, tena msomi wa dini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Mwenzenu nimeumia, ulimi umenihaini,
Tamko limetimia, kutenda naona soni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Nilisema kwa dhihaka, nakutaka mwafulani,
Naye akaniitika, kasogea barazani,
Neno liliponitoka, hakuwa na ukinzani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Mwili ulinitetema, joto kapanda mwilini,
Natikisika kwa homa, palepale barazani,
Bint akinitazama, huku atweta moyoni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Sikuweza kuthubutu, kumkaribu chumbani,
Akili ikawa butu, kama mfu kuzimuni,
Rijali sikuwa kitu, macho kitazama chini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Binti kazidi sogea, karibu na mlangoni,
Macho akikodolea, wanaopita njiani,
Pale alipokolea, akanisukuma ndani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Nilitamani kulia, ili waje majirani,
Naye akanitishia, nisilie asilani,
Na ndani akaingia, akanivuta chumbani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Nilishikwa na butwaa, hakika sikuamini,
Ilikuwa ni fadhaa, kubwa iso na kifani,
Binti yule akakaa, uchagoni kitandani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Namshukuru Rabbuka, Rabbi aso na kifani,
Binti aloyatamka, ni mambo mema ya dini,
Kaka mimi nakutaka, tuwe sote maishani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
Hii kwenu changamoto, naomba yenu maoni,
Nipeni mawazo moto, mwenzenu nifanye nini,
Binti kwa kweli ni moto, tena msomi wa dini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?