Shairi: Ulimi Mbona Umenisaliti?

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
Salaam nawatumia, wa bara na visiwani,
Mwenzenu nimeumia, ulimi umenihaini,
Tamko limetimia, kutenda naona soni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Nilisema kwa dhihaka, nakutaka mwafulani,
Naye akaniitika, kasogea barazani,
Neno liliponitoka, hakuwa na ukinzani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Mwili ulinitetema, joto kapanda mwilini,
Natikisika kwa homa, palepale barazani,
Bint akinitazama, huku atweta moyoni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Sikuweza kuthubutu, kumkaribu chumbani,
Akili ikawa butu, kama mfu kuzimuni,
Rijali sikuwa kitu, macho kitazama chini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Binti kazidi sogea, karibu na mlangoni,
Macho akikodolea, wanaopita njiani,
Pale alipokolea, akanisukuma ndani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Nilitamani kulia, ili waje majirani,
Naye akanitishia, nisilie asilani,
Na ndani akaingia, akanivuta chumbani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Nilishikwa na butwaa, hakika sikuamini,
Ilikuwa ni fadhaa, kubwa iso na kifani,
Binti yule akakaa, uchagoni kitandani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Namshukuru Rabbuka, Rabbi aso na kifani,
Binti aloyatamka, ni mambo mema ya dini,
Kaka mimi nakutaka, tuwe sote maishani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Hii kwenu changamoto, naomba yenu maoni,
Nipeni mawazo moto, mwenzenu nifanye nini,
Binti kwa kweli ni moto, tena msomi wa dini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?
 
Kiushairi siwezi kukujibu,
Ila pole kwa ulimi, ulimi unaendelea kutusaliti wote siku kwa siku.
siku hizi na vidole vya kubofya.
 
Salaam nawatumia, wa bara na visiwani,
Mwenzenu nimeumia, ulimi umenihaini,
Tamko limetimia, kutenda naona soni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Nilisema kwa dhihaka, nakutaka mwafulani,
Naye akaniitika, kasogea barazani,
Neno liliponitoka, hakuwa na ukinzani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Mwili ulinitetema, joto kapanda mwilini,
Natikisika kwa homa, palepale barazani,
Bint akinitazama, huku atweta moyoni,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Sikuweza kuthubutu, kumkaribu chumbani,
Akili ikawa butu, kama mfu kuzimuni,
Rijali sikuwa kitu, macho kitazama chini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Binti kazidi sogea, karibu na mlangoni,
Macho akikodolea, wanaopita njiani,
Pale alipokolea, akanisukuma ndani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Nilitamani kulia, ili waje majirani,
Naye akanitishia, nisilie asilani,
Na ndani akaingia, akanivuta chumbani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Nilishikwa na butwaa, hakika sikuamini,
Ilikuwa ni fadhaa, kubwa iso na kifani,
Binti yule akakaa, uchagoni kitandani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Namshukuru Rabbuka, Rabbi aso na kifani,
Binti aloyatamka, ni mambo mema ya dini,
Kaka mimi nakutaka, tuwe sote maishani,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?

Hii kwenu changamoto, naomba yenu maoni,
Nipeni mawazo moto, mwenzenu nifanye nini,
Binti kwa kweli ni moto, tena msomi wa dini,
Ee wangu ulimi, mbona umenisaliti?


Eksipasta tulia jukwaani umefika
kilio kimesikika, wako ulimi ullivyokutenda
Majuto kuendeleza, simanzi kukaribisha
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu

Hisia kuzitoa, hukufanya baya jambo
Binadamu kueleza, moyoni yanayowasibu
Binti kumwona, moyoni uliguswa
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Kosalo ulielewe, dhihaka ulitumia
Japo hisia ulijenga, za kupita kama moshi,
Mzuka ulikupanda, ghafula ukaropoka,
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Ushauri nakupa, binti usimkwaze,
Kwako amefika, hasilani hatanii,
Nafasi anaitaka, upweke kuumaliza
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Kwako kashaingia, hapo amefika,
Mlotenda chumbani, wazi hujayaweka,
siri baki nayo, ila huyo usimmwage,
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Ukweli kuukabili, mkeo umempata,
Ustaarabu kaonesha, mapepe hakutanguliza,
Ukweli kauonesha, kwako katia nanga,
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Angekuwa mapepe, uchagoni asingekaa,
Kanga moja kuja nayo, kitovu kukuonesha,
Kitandani angefika, kihasara angekaa,
Ulimi hadaa, wengi umewangarimu.

Umrio waruhusu, shemeji kutupatia,
Huyo mkubalie, maisha myapange,
Hadaa ya ulimi, igeuke ngekewa,
Huyo kwako amefika, mkeo twamwita.
 
Eksipasta tulia jukwaani umefika
kilio kimesikika, wako ulimi ullivyokutenda
Majuto kuendeleza, simanzi kukaribisha
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu

Hisia kuzitoa, hukufanya baya jambo
Binadamu kueleza, moyoni yanayowasibu
Binti kumwona, moyoni uliguswa
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Kosalo ulielewe, dhihaka ulitumia
Japo hisia ulijenga, za kupita kama moshi,
Mzuka ulikupanda, ghafula ukaropoka,
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Ushauri nakupa, binti usimkwaze,
Kwako amefika, hasilani hatanii,
Nafasi anaitaka, upweke kuumaliza
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Kwako kashaingia, hapo amefika,
Mlotenda chumbani, wazi hujayaweka,
siri baki nayo, ila huyo usimmwage,
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Ukweli kuukabili, mkeo umempata,
Ustaarabu kaonesha, mapepe hakutanguliza,
Ukweli kauonesha, kwako katia nanga,
Ulimi hadaa, wengi umewagharimu.

Angekuwa mapepe, uchagoni asingekaa,
Kanga moja kuja nayo, kitovu kukuonesha,
Kitandani angefika, kihasara angekaa,
Ulimi hadaa, wengi umewangarimu.

Umrio waruhusu, shemeji kutupatia,
Huyo mkubalie, maisha myapange,
Hadaa ya ulimi, igeuke ngekewa,
Huyo kwako amefika, mkeo twamwita.

Nashukuru muungwana, kwa pole kunipatia
Ila mwezenu nanena, kauri ilinipotea
meno yaliumana, ububu ukaniingia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Kila ninapo muona, maungo yananilegea
akinikaribia sana, naishia kumwamkia
maneno nakuwa sina, kauri inanipotea
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Mzee wa Gumzo sikiza, si zihaka kutumia
Binti kimuona kapendeza, hakika ninakwambia
hakuna anaye mbeza, kila mtu amsifia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Mtoto kwa hakika, sifaze nitawambia
hakika kakamilika, Mungu amependelea
Ni zaidi ya malaika, umbo na yake tabia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Kiuangalia mwendo, anapo kukaribia
Kama aso na fundo, Maungo memlegea
pole pole mwendo, kwa pozi atakujia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Ananukia na udi, Kila anapo nipitia
Udi wa mawardi, ndio anao tumia
Nikimpata nitafaidi, Hakika nawambia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Nalipenda umbo lake, kama nyuki na maua
Kamuumba Mola wake, kiwa mgonjwa upoa
Nyororo ngozi yake, nikimpata tatulia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Naomba nimalizie hapa mbele sito endelea
Msije mumzengee, Risasi nitawafyatulia
Wala msimsogelee, onyo nisha waandikia
Mtoto ameumbika, tasema malaika

Ewe kiumbe wa shani, Nalipenda umbo lako
Kila chozi machoni, laandika jina lako
Maua bustanini, yanatoa harufu yako
Naomba sinizaini, niurumie mwenzako

Moyo wangu unadunda, kila uendako
Mwenzio nakupenda, naomba niwe wako
Ona nilivyo konda, kwa fikra zako
Mungu anijaalie, niwe wako peke yako

Kama mapenzi wazimu, mi sitaki nitibiwe
Bora niwe chakalamu, nipige watu mawe
Nipo ndani maamumu, tabibu wangu ni wewe
Nipo naangamia, Kimuona napata kiwewe
 
Back
Top Bottom