Ubabe wa John Magufuli huu

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Jana Rais Jakaya Mrisho Kikwete alifanya 'ziara' katika Wizara ya Ujenzi.Alitumia ziara hiyo 'kumvua nguo' Waziri wa Wizara hiyo John Pombe Magufuli kwa kumuita mbabe na mchonganishi.

Ubabe wa Magufuli ni kusema kuwa hata jengo lolote la CCM lililo eneo la hifadhi za Barabara atalibomoa. Je, wanajamii mnakubaliana na Rais Kiwete, no Kikwete kuwa Magufuli ni mbabe na mchonganishi?
 
Magufuli sijui anasubili nini CCM....binafsi namuona ni mtu anasimamia sheria bila kujari masila ya mafisadi na chama chao
 
Magufuli jiuzulu hao sio wenzio wewe ni mtendaji na wao ni wababaishaji wanaosaka deal hamtaiva pamoja milele...
 
Mkuu umepotea njia huku hatuna siasa.
Mods peleka hii post mahala husika
 
mimi niliipost kwenye jukwaa la Siasa lakini nimeshangaa kuikuta huku.Usumbufu wowote usamehewe
 
CCM ya JK, EL, RA, AC etc watampendaje na kuthamini kazi ya Magufuli? SIkio la kufa haliwezi sikia dawa.......
 
Jana,Rais Jakaya Mrisho Kikwete alifanya 'ziara' katika Wizara ya Ujenzi.Alitumia ziara hiyo 'kumvua nguo' Waziri wa Wizara hiyo John Pombe Magufuli kwa kumuita mbabe na mchonganishi.Ubabe wa Magufuli ni kusema kuwa hata jengo lolote la CCM lililo eneo la hifadhi za Barabara atalibomoa.Je,wanajamii mnakubaliana na Rais Kiwete,no Kikwete kuwa Magufuli ni mbabe na mchonganishi?

mkuu ccm hakuna collective responsibility, good governance etc. kumvua nguo magufuli mbele ya junior officers kama alivyofanya jk ni kutomtendea haki. Hata kama magu alikuwa na kosa alipaswa kumweleza na kumwelekeza wakiwa wawili tu. Mbona yeye jk alikuwa anaelekezwa na Mzee mkapa wakiwa wawili tu.
in ccm there is a lot of insubordination ni bora hata kijiwe cha wavuta bangi.
 
Jana,Rais Jakaya Mrisho Kikwete alifanya 'ziara' katika Wizara ya Ujenzi.Alitumia ziara hiyo 'kumvua nguo' Waziri wa Wizara hiyo John Pombe Magufuli kwa kumuita mbabe na mchonganishi.Ubabe wa Magufuli ni kusema kuwa hata jengo lolote la CCM lililo eneo la hifadhi za Barabara atalibomoa.Je,wanajamii mnakubaliana na Rais Kiwete,no Kikwete kuwa Magufuli ni mbabe na mchonganishi?

magufuli sio mbabe na mchonganishi, tofauti ya mtu wa rushwa (mrushwa) na kufuli ni kubwa. Kufuli linafanya kazi ya kulinda (taaluma) na mrushwa a.k.a mrisho, yeye ni ombaomba (siasa, a.k.a si-hasa) hofu hapa atakosa kuraaaa!!! :)
 
mkuu ccm hakuna collective responsibility, good governance etc. kumvua nguo magufuli mbele ya junior officers kama alivyofanya jk ni kutomtendea haki. Hata kama magu alikuwa na kosa alipaswa kumweleza na kumwelekeza wakiwa wawili tu. Mbona yeye jk alikuwa anaelekezwa na Mzee mkapa wakiwa wawili tu.
in ccm there is a lot of insubordination ni bora hata kijiwe cha wavuta bangi.
Huyo JK ndiye mbabe, tena anavunja ethics za leadership. Huwezi kumuaibisha kiongozi tena waziri wa serikali.
Amefanya hivyo kwenye wizara nyingi tuu bila aibu. Hiyo ni kukosa maadili, upuuzi mtupu!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom