Mauaji ya Profesa Jwani Mwaikusa: Kesi ni geresha tu?

bongisa

Member
Apr 12, 2011
25
14
Jana nilikuwa kunduchi salasala kwenye kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kifo cha profesa Jwani Mwaikusa aliyeuawa kwa kupigwa risasi katika mazingira ya kutatanisha nyumbani kwake kama mnakumbuka wadau.

Katika maongezi ya hapa na pale nikapata kuambiwa kuna watuhumiwa walikamatwa wamewekwa ndani, na kesi inaendelea.

Cha kushangaza tokea wakamatwe na kesi kuanza sasa ni mwaka mmoja, hiyo kesi hata mahakama kuu haijafika, bado ipo Kisutu kwa hivyo inatajwa na kuahirishwa tu hata kusikilizwa bado haijaanza kwani kesi za mauaji husikilizwa mahakama kuu.

Hii ina maana upelelezi bado haujakamilika sijui, hivi katika mazingira haya kuna haki kweli au maigizo?

Na sababu ya mauaji yale mpaka leo ni giza nene kwa mujibu wa wanafamilia.

Wadau hebu tuchangie mawazo kwenye hili.
 
mhh! jamani nchi hii!!!!!!!!!!, kwa kweli inasikitisha sana.
 
Waache hao wauaji waendelee kusota knako mahabusu mpaka wazeeke ndipo kesi ianze kusikilizwa. Huo ndio utawala wa haki na sheria hapa bongoland.
 
Oooo,kweli alifariki last year........nakumbuka mwili wake uliagwa NKRUMAH HALL UDSM,sijui familia yake inajiskiaje??????
 
Mambo mengine ni mazito sana ndugu yangu. Solution ni kuyaacha kama yalivyo na kumshuluru Mungu!
 
Mauaji ya prof. kwa kweli yanasikitisha sana....................................................
....................................................................................................................
........................................................................................................
 
Justice will be served! Hata kama c hapa duniani.. Yaani late prof. was an amazing person kwa tuliofanikiwa kumjua kiasi. May his soul rest in peace.
 
Unajua kilichonisukuma kuandika thredi hii ni baada ya kusoma thread moja kwenye jukwaa hili kuhusu ile kesi ya Babu Sea.

Sina uhakika lakini naona kama kesi yao ilikwenda haraka sana kulinganisha na hii, naomba mdau anayefahamu ile kesi ya wakina babu seya ilitumia muda gani atujuze, au hawa wakubwa wanapanga kulingana na matakwa yao?
 
Ni kweli wakati mwingine ukifuatilia fuatilia haya mambo hasa ya case za mauaji unapoteza muda na pengine hutafanikiwa. Ni vyema wakati mwingine kumwachia mungu pekee ambaye aliona kila kitu na walio muua ni viumbe vyake vile vile. Atahukumu hapa hapa duniani kama tutakuwa hai tutasikia tu......
Poleni sana ndugu wa marehemu profesa
 
Sasa ndugu unataka tuchangie nini?

Wajua kifo hiki kinasikitisha sana, wewe mtu wa karibu wa familia na kama memba wa JF tupe in black and white kile ambacho wanafamilia wanasema juu ya chanzo cha kifo cha prof, hii itasaidia kwa baadhi ya watanzania kuepuka vifo vya aina hii where possible.

Pili tueleze ni kipi hasa kinachoendelea juu ya uendeshaji wa kesi ili members wazoefu watupe uzoefu wao bcos huenda mwenendo wa kesi niwa kawaida.

Na mwisho tetesi za vijiweni zinasema kuwa prof aliponzwa na utashi wake wa kukataa uhuni na ubabaishaji ulioko kwenye uendeshaji wa mahakama ya ICTR hivyo Rais wa Rwanda akaona atakuwa amevuliwa nguo- akaamua kumu.......................

Mwenye ukweki atujuze.
 
Kwakweli mwenyewe ni hivo juzi ndiyo nimesikia kuna watu walishakamatwa na wapo ndani, kesi inaendelea lakini ndio kwa mwendo wa kutajwa tu hivyo.

Kuhusu chanzo cha kifo wanafamilia hawajui pia, sijaweza kufukunyua sana kutokana na mazingira ya tukio lenyewe lakini inaonyesha wazi kutofahamu ukweli wa nini kilichosababisha kwao kinawatatiza sana, na katika mazingira hayo hata kuwahoji inakuwa ngumu.

Ndio maana nilikuwa naulizia mwenendo wa hiyo kesi je ni sawa? Sababu kama kuna watuhumiwa na kama ni wenyewe basi ukweli upo mahakamani sasa kwanini uzidi kuahirishwa kila siku?
 
Huyo Prof si aliuwawa na system chini ya uratibu wa jk..unataka nani amshtaki nani?
Tusihukumu tu jamani, labda kama una lolote la kutwambia, aliuwawa na system kwa uratibu wa jk kwa faida ya nani? Huyo jk ana maadui wangapi na wangapi amewaua kwa kutumia hiyo system? Kumbuka prof mwenyewe alikuwa na msaada mkubwa kwa serikali, je alikosana nini hasa na jk mpaka aamue kumhukumu umauti?
 
Profesa Juani Mwaikusa alikuwa eliminated na nguvu za Paul Kagame ambazo tumeona zikivuka mipaka ya Rwanda na kuwafuata watu huko huko waliko kama akina Generali Kayumba aliye nusurika kufa baada ya kupambana na paid assassins.

Jiulize: Kwanini Profesa mwingine wa USA alivyokataa kuja Kigali kumwakilisha mteja wake kwa kuogopa kupatwa na yaliyompata Profesa Mwaikusa.

Fuata link hii Wakili Peter Erlinder na kifo cha Prof Juani Mwaikusa - JamiiForums
 
Hivi mdau, kuna uwezekano mtu mwenye umuhimu kwa serikali kama alivyokuwa prof mwaikusa akauwawa na serikali ya nchi jirani bila ya serikali yetu kupitia vyombo vyake vya usalama kupata fununu?
 
Back
Top Bottom