Vigogo Wamshutumu Rais kwa Kukosa Kuchukua Hatua Dhidi ya Rushwa, Ubadhirifu na Ufisadi

Madilu, CCM watasema kuwa Butiku analalamikia kunyimwa ulaji, na yeye angekuwa kwenye mkao wa kula sijui kama angepiga kelele hivyo. Kuna baadhi ya watu wanadai kuwa yeye na Mkapa hawakuiva na Mkapa alimwonyesha mlango wa kutokea mapema Zaidi. Nasema CCM watasema hivyo kwa sababu wao huwa hawajibu hoja, wanawashambulia watoa hoja!
Nafikiri kilichomuudhi, Butiku, Mwinyi, Ulimwengu et al. ambao wamesimama upande wa dhati wa kumuenzi Mwl. JKN (RIP). Ni ile hali inayoendelea ya wanaoendesha serikali kama viongozi kuhubiri kumuenzi Mwl. Kinadharia lakini matendo yao yapo mbali sana na Mwl.
 
Ni vita ya Butiku kushindwa kumpitisha Salim pale Chimwaga, wadau wote pale Mlimani waliotia fora kwa hoja zao ni walewale. Sijajua Jenerali alitaka nani awe rais.

Kuvunja baraza la mawaziri na blabla za Mkapa, Butiku anapigana na kivuli chake mwenyewe. Kwa ufupi hana jipya, ila tusubiri akija na lingine, maana hapo MNF hali si njema. Sasa mzee lazima apige kelele na asikike, otherwise hata yeye itabidi abinafsishiwe MNF. Tuwe na subira na watu wa aina ya Butiku na Jenerali, watajipambanua soon.
 
Kubadili mawazo ni kitu cha kawaida na kinaonyesha uelevu. Kama akina jenerali wamefanya ni vizuri. Hata kama Butiku hajabadili mawazo, pia ni muhimu kama kila analosema ni la maana. Sasa yeye kaja na data za historia ameridhisha wale wote waliokuwepo. Sasa wewe ukikaa na kulalamika bila hoja ya msingi au kutuletea data za kutosha, tutampuuzia nani, wewe au Butiku?
 
I feel this Butiku guy!! Kikwete man up!! Shame on your lousy government.... And once again you are out on an overseas adventure!! Sit your ass down and deal with the country's problems!! CCM and the whole government make me sick!!
 
Ni vita ya Butiku kushindwa kumpitisha Salim pale Chimwaga, wadau wote pale Mlimani waliotia fora kwa hoja zao ni walewale. Sijajua Jenerali alitaka nani awe rais.

Kuvunja baraza la mawaziri na blabla za Mkapa, Butiku anapigana na kivuli chake mwenyewe. Kwa ufupi hana jipya, ila tusubiri akija na lingine, maana hapo MNF hali si njema. Sasa mzee lazima apige kelele na asikike, otherwise hata yeye itabidi abinafsishiwe MNF. Tuwe na subira na watu wa aina ya Butiku na Jenerali, watajipambanua soon.

Yote tisa ndugu yangu, mie siangalii Butiku na Jenerali wanamtaka nani awe rais, hiyo sio kazi yetu. Kazi yetu ni kulinda maslahi ya nchi, kupambana na nyang'aus wote. Pigana na ufisadi, pigana na Lowassa, pigana na Kikwete (Rais huyo huyo ndiye waziri wa mambo ya ndani, ziara kibao,ombaomba sugu). Aibu hii ndio tunataka tufute, soma signature yangu hapo chini, ipo simple tu, abiria chunga mzigo wako.
 
Former Nyerere aide blasts Mkapa`s actions

I DARE YOU: Joseph Butiku challenged the ex-president Mkapa to defend himself against mounting allegations of abuse of office, pointing out that the late Father of the Nation was a firm believer in the principle that State House and presidents should always remain ``beyond suspicion`` as far as leadership ethics and integrity were concerned.

-'Mwalimu would have considered it a terrible thing ...he would certainly have disapproved,' Butiku

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

A CLOSE personal aide of the late Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku, has added his voice to a growing public outcry of scathing criticism over former president Benjamin Mkapa's alleged private business activities conducted while at State House.

Speaking during a live call-in local television talk show on Sunday, Butiku - who was Nyerere's personal secretary at Ikulu for more than 20 years and is now executive director of the Mwalimu Nyerere Foundation ? said the late founding president and Father of the Nation was very categorical about not mixing the noble work of the presidency with private business undertakings.

And when asked by one caller what he believed Nyerere would have thought of Mkapa's well-documented actions which appear to have trashed this principle altogether, Butiku replied candidly:

''Mwalimu would have considered it a terrible thing ...he would certainly have disapproved.''

''Mwalimu was very clear and categorical about the importance of (presidents) avoiding the temptation of turning Ikulu into some sort of private shop or business,'' Butiku further elaborated on the Hamza Kassongo Hour talk show broadcast by Channel Ten.

He said the late founder president strongly believed that State House and incumbent presidents should always remain ''beyond suspicion'' as far as leadership ethics and morals were concerned.

''We have become miserable. He (Mwalimu) wouldn't have done it (engaged in business) even after he left Ikulu,'' said Butiku.

THISDAY has already established through a series of exclusive reports that Mkapa, who served as president from 1995 to 2005, started a private company called ANBEM Limited with first lady Mrs Anna Mkapa in 1999, with the official registration documents listing the State House couple as sole directors and describing them as ?entrepreneurs?.

In 2002, while Mkapa was still at State House, ANBEM Limited was granted hefty loans of $500,000 (approx. 620m/-) and 250m/- from the National Bank of Commerce Limited and CRDB Bank respectively. And in 2004, the then president teamed up with senior cabinet minister Daniel Yona to form another private company, TANPOWER Resources, with their close relatives including wives, children and in-laws listed as shareholders.

In mid-2005 ? again with Mkapa still occupying the presidency - TANPOWER Resources bought majority shares in the hitherto state-run Kiwira coal mine, which was then renamed Kiwira Coal and Power Limited and shortly afterwards entered into a huge, $271.8m (approx. 340bn/-) contract with the state-run Tanzania Electric Supply Company Limited (TANESCO) for the supply of 200MW of coal-fired electricity to the national power grid.

Investigations by THISDAY have also established that both Mkapa and Yona, by virtue of their powerful positions in government, were heavily involved in 'fast-tracking' the Kiwira coal mine privatisation process, prior to TANPOWER Resources buying the majority shares.

Speaking on the TV show last Sunday, Butiku described the actions of a former president and cabinet minister to set up a joint private business arrangement, along with their spouses and children, while still occupying public office as clearly being unethical conduct.

Said Butiku: ''When you are a president or minister, who would dare refuse to register your (private) company, or even delay it? It is a very serious issue of conflict of interest.''

He said there was a need for the current government to go back to the drawing board and rewrite the rules of public leadership ethics, noting: ''Many of our (government) ministers today look overly prosperous, owning shares in various high-flying private companies and educating their children abroad.'' he noted.

Earlier on Sunday, when speaking at a public forum at the University of Dar es Salaam to mark the eighth anniversary of Nyerere's death, Butiku threw a challenge to Mkapa to come out and defend himself against the mounting allegations of corruption and abuse of public office he now faces.

Butiku said it was quite baffling to see Mkapa remaining so silent in the face of such serious allegations.
 
kazi kweli kweli........ yawezekana huundio ukawa mwanzo wa mwisho wa mafisadi
 
Butiku ataka mawaziri wajiuzulu

na Irene Mark
Tanzania Daima

MKURUGENZI wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, amewataka viongozi wote wa Serikali ya Awamu ya Nne, ambao wametajwa kwa tuhuma mbalimbali za rushwa, ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma, kujiuzulu.
Butiku, mmoja wa watu waliofanya kazi kwa karibu na Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere tangu mwaka 19965 hadi alipostaafu urais mwaka 1985, alisema viongozi hao watakuwa wakifanya makosa kusubiri hadi rais awawajibishe.

Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana, Butiku ambaye aliendelea kufanya kazi na Mwalimu hadi mauti yalipomfika, alisema kuwa, rais anapaswa kuchukua hatua madhubuti dhidi ya viongozi wanaotuhumiwa kwa mabaya katika serikali yake.

Alisema hatua hizo zinapaswa kuchukuliwa na pande zinazohusika wakati huu kwa sababu maadili ya uongozi yanahusu zaidi imani ambayo wananchi wanakuwa nayo juu ya viongozi wao.

Alisema kuwa iwapo viongozi wanazingatia maadili, tuhuma za ufisadi zilizotolewa hazihitaji kuwa na ushahidi wa mahakamani ili viongozi hao wawajibike.

Katika hatua nyingine, Butiku alisema maadili ya viongozi ni jambo la msingi kufuatiliwa hivi sasa, kuliko wakati mwingine wowote, kutokana na kushamiri kwa vitendo vya rushwa.

Katika hilo, alisema ufisadi ni suala la imani kati ya wananchi na viongozi wao, hivyo kutafuta ushahidi wa mahakamani hakutasaidia.

“Kwa hali ilivyo sasa, maadili mema kwa viongozi, hasa wa ngazi za juu, ni jambo la msingi kuliko wakati mwingine wowote… wala siyo jambo la kutafutia ushahidi mahakamani.

“Hili ni suala la imani kati ya wananchi na viongozi wao, tuzingatie hadithi ya mke wa Ceaser,” alisema akirejea mfano wa mke wa mfalme, ambaye alituhumiwa kwa uzinzi na akaachwa baada ya kuthibitika kuwa hakufanya kosa hilo.

Akihimiza kuhusu hilo kwa mfano huo huo ambao uliwahi kutumiwa na Baba wa Taifa wakati wa mchakato wa kumtafuta mgombea urais wa Tanzania mwaka 1995, Butiku alisema kiongozi yeyote anapaswa kuchukua hatua za kuzuia uwezekano wa imani juu ya kupungua kwa kuhusishwa na rushwa.

“Kiongozi ukipatwa na tuhuma za rushwa, inatosha kujiuzulu, tusisubiri rais atafute ushahidi mahakamani… tukifanya hivyo (kujiuzulu) tutamsaidia rais, lakini tukipuuza haya tutamharibia uongozi wake, tutakuwa wafa maji pamoja naye,” alisisitiza Butiku.

Butiku anatoa kauli hizo nzito siku moja tu baada ya kuzungumza katika mdahalo wa kumbukumbu ya miaka minane ya kifo cha Mwalimu Nyerere ulioandaliwa juzi na Chuo Kikuu cha Dare es Salaam.

Katika mdahalo huo, Butiku alizungumzia kwa kirefu suala la viongozi kujiuzulu kabla ya ‘kumlazimisha’ rais kulivunja baraza lake la mawaziri.

Alitoa mfano wa maamuzi aliyofanya Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, ambaye alilazimika kulivunja Baraza la Mawaziri kutokana na serikali kuandamwa na tuhuma za rushwa, na alipounda jipya alilazimika kuwaacha kando mawaziri saba.

Alisema enzi za uhai wake, Mwalimu Nyerere, alijitahidi kupinga rushwa kwa vitendo, hali ambayo ni tofauti kabisa na sasa ambapo kelele nyingi zinapigwa bila vitendo.

Butiku aliongeza kuwa katika siku za hivi karibuni, rushwa imekuwa ikifanyika bila kificho huku wanaotoa tuhuma hizo za kupokea rushwa wakiachwa bila kuchukuliwa hatua.

“Rushwa ilikuwepo tangu zamani… siku hizi tunapiga tu kelele, Mwalimu alijitahidi sana kupingana na rushwa, ila siku hizi rushwa ipo wazi, na wanaotoa wanajulikana,” alisema.
 
Old is Gold keep it up Butiku ingawa huo ni mfupa kwa viongozi wetu kujiuzulu because wamejawa na ubinafsi.
Mbaya zaidi wanajua mkuu anawaonea haya kisa ni wana mtandao bila kujua kuwa raisi anaweza watema kwa msemo"kikulacho kinguoni mwako"

Mungu umjalie raisi wetu maamuzi sahihi na kulinda maslai ya Taifa letu katika kipindi iki kizito ili aweze rudisha imani ya wananchi kwa viongozi wao.
 
Nasubiri kusikia Salim anaunga mkono mawazo hayo na kama Butiku alizungumza kama Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu.
 
Ndugu yangu Mwanakijiji upo huonekani ndugu yangu, karibu tende na haluwa kule kwetu Zanzibar na hasa pale Mchamba wima
 
CCM imepoteza dira

na Mwandishi Wetu


JOSEPH Butiku, mmoja wa wasaidizi wa karibu wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kwa zaidi ya miaka 20, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepoteza dira.

Butiku ambaye ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Alisema kutokana na kuuona mwelekeo huo wa CCM kupoteza dira, Agosti 10, mwaka 2005 aliandika barua kwenda kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM na Rais wa Tanzania, Benjamin Mkapa kumueleza kuhusu hali hiyo ya kusikitisha.

Kauli hiyo ya Butiku kwa kiwango kikubwa inaweza ikawarejesha Watanzania wengi kuikumbuka kauli kama hiyo iliyotolewa miaka ya mwanzo ya 1990 na aliyepata kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Horace Kolimba, ambaye alisema ‘CCM imepoteza dira.’

Butiku ambaye alisema aliamua kuifanya siri barua yake hadi hivi sasa anapoiweka hadharani, alimtaka Mkapa kuisoma kwa umakini barua yake yote, ili aweze kutambua kile alichokiona kuwa ni mpasuko mkubwa uliokuwa ndani ya chama hicho tawala.

“Nilimwandikia barua aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wakati huo Ndugu Benjamin Mkapa…ndani yake nilimweleza kuhusu ubaguzi, rushwa na maovu ya CCM wakati wa mchakato wa uchaguzi wa mwaka 2005,” alisema Butiku jana.

Baadhi ya mambo aliyomweleza mwenyekiti huyo ni kuporomoka kwa misingi, maadili ya chama na ubaguzi uliojionyesha wazi wakati wa harakati za uchaguzi ulioiweka madarakani Serikali ya Awamu ya Nne.

Katika barua hiyo ya kurasa 14, ambayo Tanzania Daima imeiona, Butiku katika sehemu moja anaandika: “Mimi naamini CCM sasa imeanza safari ya kuelekea kwenye KIFO chake-imekumbatia jambo ovu-rushwa, ambayo imeua viongozi wazuri wengi, vyama vya siasa na serikali makini duniani. CCM imeanza kushindwa kusema na kutetea HAKI na UKWELI; imeanza kuvumilia na kutetea UBAGUZI.”

Mbali ya hilo, Butiku katika barua yake hiyo ambayo jana aliiambia Tanzania Daima, anaamini bado ina maana kubwa leo hii kwani mambo hayajabadilika, alisema CCM ya sasa imeanza kujenga matabaka miongoni mwa viongozi wake hata kuifanya mali ianze kuchukua nafasi ya uzalendo.

Aidha, alisema pia kwamba, hali hiyo imeanza kuchukua sura mbaya zaidi kutokana na viongozi wakuu wa chama hicho wamekuwa kimya wakishindwa kutetea maovu.

Akianzia katika chama, Butiku katika barua yake hiyo ambayo Tanzania Daima inakusudia kuichapa kesho, alivilaumu vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa kwa kile alichokielezea kuwa ni kuvunja miiko na maadili kwa kuruhusu rushwa na ubaguzi kwa kiwango cha kukifanya chama kibinafsishwe na wenye fedha.

Akitoa mfano, Butiku alisema viongozi wakuu wa CCM wamefikia hatua ya kutokutana nje ya vikao na wamekuwa wakikwepana na kusengenyana, hali inayosababisha wakose uongozi wa pamoja wa kushauriana na kuelewana.

Kama hiyo haistoshi, Butiku alilaumu namna Mkapa akiwa Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho alivyomuengua mapema Makamu Mwenyekiti wake, John Malecela, ili asigombee urais, hatua ambayo ameielezea kuwa ilizusha mabishano aliyoyaita ‘aibu’.

Akirejea kuhusu kile kilichotokea wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya CCM ambao Rais Jakaya Kikwete aliibuka mshindi, Butiku alimlaumu Mkapa kwa kubadili kanuni za uchaguzi katikati ya vikao na bila ya ushauri wa kiongozi mwingine yeyote.


Source: Tanzania Daima 16/10/2007
 
Kwa mara nyingine nakupa tano Sam au Mzee FM kwani hii barua uliieleza sana kule kijiweni enzi zile.
 
Butiku umenikuna kichwa,hakuna kufichana bwana,hili taifa si la mtu mmoja wala wana mtandao,tusaidiane,maana wakisema wapinzania,wanaambiwa wana wivu.Salim,Mwandosya tunakutegemeeni,.
 
Butiku tupe mambo,maana tulifikiri ccm yote imeoza baada ya mwl,kumbe bado kuna mashujaa,lete huo moto.
 
..hiyo barua iko wapi?

..huyu naye asije kushambuliwa kama Dr.Slaa.
 
Msimamo wa Butiku unahamasisha hisia kali, Mungu amsaidie aendelee kuhimiza jambo hilo muhimu sana katika taifa letu, kwa kuwa Mtandao wa viongozi una ngome kubwa sana kiasi kwamba inaleta hisia kuwa pengine Rais anaogopa akianza kuwapangua watataja na yeye madili Yake.
 
Kwa kauli kama hivi wanaweza kurudisha heshima ya Mwalimu Nyerere Foundation na wananchi wakaanza kuicnagia tena!
 
Back
Top Bottom