sawa nakubaliana nawe. Lakini tuende hivyo hivyo sasa. Hizo hila zilizofanya Tanganyika kuwepo ndio hizo hizo (Nyerere huyo) zinazoifanya Zanzibar kupumuwa na kutamba hivi sasa. Sawa -Tukipumua kule kwa kutumia misngi hiii hii ya Muungano musilete fujo. Acheni yale mazowea aliyokufundisheni Baba...
Mueleze huyo. Na kwa kweli Kisiwandui ndiyo wanaoamua wakati mwengine hata Rais wa Jamhuri ya Muungano awe nani. Ama kweli Duniani kuna mambo!!!! na Dunia rangi rangile.
Wacheni ushamba huo. Sisi hatubabaiki na vijipesa kama hivyo. Na kwa taarifa yako wajumbe wa Visiwani(sema Zanzibar mara nyengine) are not cheap as you are. Lakini huyo Spika wenu haizungumzii Zanzibar -uzuri- ndiyo anakandiwa hivyo. Tafuta kumbu kumbu kuna wakati fulani Spika aliepita (Msekwa...
Wewe Bwana, anunue tu ziwepo nyingi hizo. Tupo wengi hivi sasa- unafikiri sote tunaweza kujibanza ITV na kwa Tido tu. Wacha wigo upanuke - tunahiataji ajira Bwana.
PM pengine bado anajifikiria kuwa akiwemo Bungeni mle yumo kama wakati ule alivyokuwa TAMISEMI au yumo kama akina Mheshimiwa Seleli. Anasahau kuwa ni Waziri Mkuu tena wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na busara zake zinahitajika sana katika matamshi.
Sawa kwa kumsifia Vuai. lakini mbona hushauri kuwa Pinda naye afuate nyayo za Vuai. Kwa nafasi yake aliyonayo matamshi yake yasiyo na busara (yaliyojaa ubabe) ni karaha -hayo matamshi si awaachie akina Mh. Seleli na wenzake wale wa back-bench.. Pinda mambo yanamzonga Bwana!!!!
Inachukliza zaidi kuona CUF wanataka kuingia madarakani huko Zenj kwa njia za ubabe , za kijahilia, za kiharamia zisizo za kistaarabu na zenye kuhatarisha maisha ya wanajamii.
Sivyo Hivyo ukweli ni kuwa Hapa Zanzibar sewhemu amabayo CUF inaweza kushinda ni Wilaya ya Micheweni, Wilaya ya Wete na Wilaya ya Chake. Wilaya ya Mkoani inagawana majimbo nusu kwa nusu na wapinzani wake. Unguja haiwezi kushinda katika Wilaya yoyote ya huko.
Mawazo yako ni mgando. Unataka referendum leo? Kwa nini hujataka 1970, 1980, 1990, 2000. Usiwazonge kizazi chetu cha hivi sasa na kijacho. Muungano is here to stay. Tumezaliwa katika Muungano na tutabakia katika Muungano. Lete hoja za namna gani ya kuendesha Muungano wetu.
Hili suala ni pana kabisa. SMZ ina jukumu la kuwahudumia Wazanzibari katika mambo yale ya kijamii (elimu, afya, makaazi, kilimo, uvuvi, na kadhalika). Mambo hayo niliyoyaorodhesha hapo wa-Tanzania bara (Wa-tanganyika) wanahudumiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(ambayo ni yetu...
Nyinyi watu mna matatizo kweli! Msiunganishe masuala ya Utamaduni (Mila) na masuala ya dini. Nenda katika dini -inasema mtu avae nguo inayositiri mwili-Jee suruali haisitiri? haijafunika sehemu zinazotakiwa kufunikwa? Sasa ugomvi uko wapi? Hayo ya Sudan ni ya Utamaduni wao. lakini hata US kule...
CUF walianza na gia siyo wakati wa mfumo vyama vingi unaanza. Ukweli ni kwamba wakati huo wa-Zanzibari wengi tu walikuwa wamechoshwa na visa vya CCM na walikuwa tayari kwa Chama mbadala. Lakini kwa bahati mbaya visa vya CUF (na hasa vinara) ndivyo vilivyowafanya Wazanzibari walio wengi -waone...
Bwana Muregezi "U stand to be corrected-kweli". Kila kitu cha Bara kilichukuliwa na kuingizwa katika Muungano -ni kweli hilo. Lakini ni kweli pia kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano inawahudumia Wananchi wa Bara kwa kila kitu. Haifanyi hivyo kwa Wananchi wa Zanzibar. Isipokuwa wananchi wa...
Shauri lenu. OCD wa Wilaya Mjini yupo. Anatosha -ilimradi tu apate mgao kidogo, kati ya wale vijana wa FFU 7,000 ambao Wizara ya mambo ya ndani imeamua kuwaajiri na kuwapa mafunzo kumarisha nguvu ya Jeshi letu la Polisi.
Unayozungumza hasa katika sehemu hii mimi kwa mawazo yangu nafikiri ni sahihi. Na nafikiri umefika wakati Katika Katiba na sheria zetu tukasema bayana kuwa Nchi yetu ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na inabakikia kuwa hivyo daima na milele. sasa hapo hakuna tena nafasi ya kulumbuna kama...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.