Hiyo inadhihirisha maana halisi ya ARI ZAIDI, KASI ZAIDI, NGUVU ZAIDI......
Kibwagizo........... Wizi zaidi, Ufisadi zaidi, Utapeli zaidi, Usanii zaidi...
Maisha bora yatakuwepo kwa wale wenye NACHO ..... yaani matajiri wakubwa wanaokwepa kulipa kodi na wanaifadhili CCM...
Sisi wengine ni maumivu kwenda mbele
Wataweka tu wewe subiri JK azidi kuongeza Wanajeshi wastaafu kwenye Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Makatibu wakuu, Mabalozi nje ya nchi na Makatibu wakuu wa Mawizara....
Tutegemee Cabinet yake watakuwemo Wakuu wa Mikoa na wilaya kujazwa Wanajeshi wastaafu toka JWTZ .... ili wananchi wakileta maandamano na manung'uniko ni kupelekwa jeshini kupata adhabu za kijeshi toka kwa MP (Military Police)....
Vile vile bila kusahau kurudishwa kwenye uongozi mafisadi...
Unamshusha cheo.... Ni Colonel Mstaafu wa JWTZ, sambamba na Mwenyekiti wake wa kampeni za CCM Kitaifa, Raia wa Somalia, Colonel Mstaafu wa JWTZ Abdulrahman Kinana, bila kumsahau Katibu Mkuu mwenye porojo nyingi, Luteni Mstaafu wa JWTZ, Yussuf Rajab Makamba....
Sheikh Yahya alisema uchaguzi hakuna, inawezekana kweli ukarudiwa baada ya wateule kuaga dunia au kupingwa mahakamani. Tusishangae majimbo yote walioshinda CCM, wapinzani wakaenda mahakamani
Jamani na bado Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa anakuja kuwa Waziri Mkuu wenu..... Tutakoma kuringa!
Masha, Batilda, Diodorus Kamala, Phillip Marmo watakuwa wabunge wa kuteuliwa kwenye nafasi 10 za Rais
Na bado kuna majimbo mengine watachukua.... Nkenge, Mpanda Mjini, Mpanda Kati. Achilia mbali yale yatakayotenguliwa na Mahakama kisha uchaguzi mdogo kuitishwa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.