Wakurya wana utaratibu wa kukaa kwa matabaka,wakati wa majadiliano. Wenye mke mmoja hukaa tofauti na wale wenye wake wawili. Wenye wake watatu nao hukaa tofauti na wenye wake wanne nk. Karume kwa hadhi yake ni sawa na mtu mwenye wake wengi. Kwanini akae na watu wasio na hadhi kama yake?
Nadhani tunakuwa wepesi kukimbilia kwenye kulaumu au kunung'unika kabla hatujapata ukweli wa jambo lenyewe. Hapa hatujaambiwa ni kiasi gani kimetumika katika sherehe hizi. Je ni kiasi ambacho JK mwenyewe kama JK hawezi kukimudu! Tupate details kwanza.
Naamini kila mtu ana mwisho wake. Unaweza kuwa mzuri au mbaya. Huu ndiyo mwisho wa Nyaisanga. Kama hakuzichanga karata zake sawa sawa sijuwi ......Labda Tido Mhando amsaidie huko TBC.
Mramba na Yona hivi sasa wanaumia sana wakiona wao wamekwenda Keko na mshirika wao wa karibu Mkapa hawezi kushitakiwa. Wananchi walio wengi wangependa( waulizwe kwa kura ya maoni) kinara wa ufisadi Mkapa anashitakiwa kama walivyoipata wengine.Nadhani ipo haja ya kufanya marekebisho yanayostahili...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.