KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba ameomba kukutana na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad wazungumze kuhusu hatima ya mwafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar.
Habari zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi waandamizi wa makao makuu ya CCM...
WAHISANI wameitaka serikali kuhakikisha inatekeleza mapendekezo ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, iliyoundwa kuchunguza mchakato wa zabuni ya umeme ulioipa ushindi Kampuni ya Richmond ya Marekani, ifikapo Juni, mwaka huu la sivyo hawatachangia bajeti ya 2008/9.
Uamuzi huo wa Wahisani...
*Ni wale wa makosa ya jinai waliompekua Dar
*Asema wana mkono mrefu katika kuchunguza
Na Ramadhan Semtawa
SIKU moja baada ya wakili wake J Lewis Madorsky, kuibuka na kutema cheche, Andrew Chenge amesema makachero wa kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai kutoka Uingereza yaani Serious...
UAMUZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kugoma kusaini makubaliano ya mwafaka wa kisiasa ili iundwe serikali ya mseto visiwani Zanzibar, umeibua mapya, baada ya Chama cha Wananchi (CUF), kuanzisha rasmi kampeni ya kulirudisha suala hilo kwa wananchi ili waamue kuchukua hatua watayakayoiona...
HATMA ya mpasuko wa kisiasa visiwani Zanzibar, kati ya Chama cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM), imezidi kugubikwa na giza, baada ya vyama hivyo, kuanzisha mchezo wa kutegana katika kulipatia ufumbuzi wa kudumu suala hilo.
Mchezo huo, umedhihirika baada ya kila upande kueleza...
MAJINA ya viongozi waandamizi wa serikali ya awamu ya tatu wanaohusishwa na mikataba mibovu, ambayo yameanza kutajwa waziwazi bungeni yameongezeka baada ya jana, aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba, naye kuingizwa katika orodha hiyo.
Mramba alitajwa na Godfrey Zambi (Mbozi...
KITUO cha Seria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufuta kauli yake ya kuwa Serikali inashindwa kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wa ufisadi waliojichotea mabilioni ya shiling katika Ankauti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kutokana na utajiri mkubwa walio...
Waziri Chenge atua Dar,agoma kujiuzulu,asema ni tuhuma za vijisenti
Na Muhibu Said
WAZIRI wa Miundombinu, Andrew Chenge, jana alirejea nchini akitokea China na kukataa kujibu tuhuma za ufisadi wa mabilioni ya shilingi anazodaiwa kuzihifadhi katika akaunti nje ya nchi.
Chenge ambaye...
VITA dhidi ya ufisadi iliyoanza kupamba moto katika miezi ya hivi karibuni sasa inaonekana kubadili mwelekeo na kuanza kuwarudi baadhi ya wanasiasa na wananaharakati waliojitokeza kwa nyakati tofauti kupambana dhidi ya vitendo vya ubadhirifu, wizi na uporaji wa rasilimali za taifa.
Dodoso...
UPELELEZI kuhusu mahali zilipo Sh133 bilioni zilizochotwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) umeibua mambo zaidi mapya yanayokihusisha Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwananchi Jumapili limebaini.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Timu ya Rais inayochunguza...
na Antidius Kalunde (Bukoba) na Salehe Mohamed
JINAMIZI la kashfa ya mkataba tata wa uzalishaji umeme wa Kampuni ya Richmond, bado linaendelea kuwasumbua baadhi ya viongozi, tangu lilipoibuka zaidi ya mwezi mmoja uliopita.
Hali hiyo inajidhihirisha kuwepo kwa tukio la aliyekuwa Waziri...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.