Mwezi August binamu yangu katembea nayo israel na mwenzie kakatwa mguu, mbaya zaidi kila siku lazima nipite hiyo barabara na litukutuku langu kwenda na kurudi kazini...Mola aturehemu.
Zaidi ya mwaka wamepanda nguzo zao hapa mtaani kisha wamekuja na swaga za transformer, wakati mita 200+ kuna wadau wanaingiziwa umeme kwa transformer hiyo hiyo wanayodai haitakidhi hadi kwetu, tumeaachia mradi wao hadi wakipata wazo waje, hawataki waendelee kubaki tu, hakuna wa kutoa hela...
Dah maskini....!! Kuna kunguru hapa alikuwa na kijidonda mguuni kajipendekeza kusimama kwenye nyaya ya umeme, kilichompata kamuacha mwenza wake mpweke, rest in peace kunguru, mwenzio yupo katika majonzi makubwa mnoo, atakukumbuka daima.
Hao wachina unaowasema walipewa eneo wachimbe madini na wakataka wenyeji wahamishwe kibabe, wazee wakakaa kitako, hadi kesho mchina hakuona hayo madini na mitambo ameisusa hana mpango nayo, imebaki historia tu.
Same applied kwangu, aliyeniuzia eneo alitaka nigeuzia kibao, baadae maneno yakatoka kwamba anasema haiwezekani watu wa kuja waje wafanye maendeleo kwenye mji wao, kwangu amelegeza sasa kilio kwa majirani na kila mmoja ananyoosha kidole kwake
Nilivyohamia kwangu kila usiku wadogo ni kuweweseka baadae ikahamia kwangu mandoto ya kula vyakula na "mzigo" na kuendesha gari usiku, asubuhi nakuwa mchovu hatari, nikaona isiwe tabu... Nikafanya mambo, baada ya siku kadha nasikia stori za kiwaki mtaani, nikajua mbaya anajitangaza
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.