Kwa bahati mbaya wengi akiwemo mtoa mada hawajui coconut value chain. Madafu ni biashara ya kimataifa na nchi kama India wanaingiza pesa nyingi za kigeni kwa kuuza madafu na bidhaa nyingine za minazi.
Siyo gubu bali ameongea ukweli. Futari inatakiwa wapewe masikini na mafukara wasio na uwezo. Yaani wapewe wafungaji ambao hawajui watafuturu nini. Sasa ukiandaa futari halafu ukawaita wasiofunga na wanasiasa waje kula hiyo siyo futari bali ni dhihaka kwa dini.
Mkuu ingia youtube tafuta bamboo products utaona faida nyingi sana za mianzi. Kwa ufupi ni dili sana kwa Wachina na watu wa Asia kwa ujumla. Sisi huku tumelala sana na umasikini wetu ni mtaji kwa wanasiasa.
Nakushauri kitu kimoja usile wala kunywa chochote hapo ofisini na ikiwezekana hata unapoishi hao wafanyakazi wenzako wasipajue. Watu wengi wameuawa kwa sumu au njia nyingine kwa misimamo ya kupenda haki kama wewe.
Mabao tunapiga na malezi tunatoa kulingana na hali zetu. Yeye asitushauri kwani kila mtu ana mipango yake. Asichukulie maisha ya familia yake ndio akafanya rejea ya maisha ya kila mtu. Ndoa zote zina changamoto hata hizo za mke mmoja.
Mara ngapi tunashuhudia watu wenye mke mmoja wametelekeza...
Siyo kwa sababu baba yako alikuwa na wake wengi akashindwa kuwalea basi watu wote watashindwa. Usichukue kesi ya nyumbani kwetu ukaifanya ni kesi ya watu wote. Kuoa watu wengi siyo suala la kidini tu hata mila na desturi za makabila yetu zinahimiza mwanaume kuoa wake wengi. Wewe kama hutaki kwa...
Acha kutetea ujinga. Unaruhusu vipi watu watembee na silaha katika nchi iliyostaarabika kama Zanzibar? Visu na marungu vya nini Zanzibar? Kama wanataka kutembea na visu na marungu yao warudi huku Bara ambako wamezoeleka na siyo kwenye nchi za watu.
Nimezaliwa Tabora na kukulia kule. Miaka hiyo kulikuwa na minazi kibao tena yenye kuzaa nazi nyingi. Tabora minazi inakubali ila hakuna wenye mwamko wa kuipanda. Mingi ilipandwa na Waarabu na ilishajifia kama ilivyo kwa miembe.
Mkuu ekari moja miche 100-120 kwa spacing ipi? Kimataifa minazi mirefu ni meta 10 kati ya mche na mche na minazi mifupi ni meta 7 kati ya mche na mche. Kwa wastani ekari moja ni miche 70 hadi 80.
Kuna utajiri mkubwa sana kwenye kilimo cha minazi. Kwanza kama una ardhi gharama za kuanzia siyo kubwa ukilinganisha na mazao mengne. Minazi haihitaji huduma nyingi kama mazao mengine. Mtu mwenye minazi 300 tu kwa mfano inayozaa vizuri ambayo kama kila mnazi utampa nazi 200 tu kwa mwaka na kila...
Kama minazi inahudumiwa vizuri kwa kuwekewa mbolea ya samadi, kuondoa takataka juu ya mnazi na kupaliliwa mnazi mmoja unaweza kukupa nazi 200-300 kwa mwaka.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.