Watakuwa jamaa wa Afrika Magharibi hao ndo wamefanya hako kamchezo. Lakini na wa Tz nao siku hizi wameanza hako kamchezo, hasa hasa kupitia facebook. Wanatumia picha za wasichana warembo ili kumvuta mtu. Ukishaingia kwenye mtego, wanasema wana njaa; uwatumie pesa kwa tigopesa, m-pesa, airtel...
ki ukweli mimi si mkazi wa maeneo ya wabunge uliowataja mimi niko
ubungo, tulimchagua Mnyika tukitegemea mabadiliko ya kweli, lakini anachofanya ni kumtusi Rais bungeni, je sisi tulimtuma hayo? Anafikiri wabunge wengine hawajui kutumia maneno ya kebehi dhidi ya Rais? Anatudhalirisha
Haya sasa Nape, babu ameshatetewa sana; anika mtiririko wa vile amekuwa akilipia uanachama wake CCM. Timiza ahadi; usipofanya hivyo utadharaurika wewe na chama chako.
Yaani wote mnaomshambulia Nape mnasahau kuwa yeye hayo anayoyasema yawe ya kweli au siyo ya kweli ndiyo yanamuweka mjini? Mimi mchumi kazi yakangu ni "ni kudevelop models na kuforecast" ili kufahamu kama mwaka ujao kampuni yetu itatengeneza faida au la; Nape kazi yake ni kupiga propoganda asi...
Kinana ni bingwa wa mikakati ya wizi wa kura au pale ambapo wapinzani wanapokubalika sana karatasi za kupigia kura hazipelekwi. Zikipelekwa na CCM ikashindwa basi anailazimisha tume ya uchaguzi, uchaguzi urudiwe.
Labda hicho ndo kimbumbuga anachokimaanisha Kibanda; maana hajadadavua hoja yake...
Kwani alionekana ana kosa gani? Hayo yote majungu. Bravo madamme Blandina Nyoni; bado tunahitaji mchango wako uliotukuka katika kujenga nchi yetu changa na maskini.
Jitahidi kuongea kiswahili fasaha maana ukiongea american English utakosa kura za Lusinde, Ngonyani, Lameck Airo, nk. Hawa wote elimu zao darasa la saba.
Tell me brother: Hivi EAC ina idadi ya watu wangapi? Na pato lake kwa mwaka ni kiasi gani?
S kwamba Dr. Mwakyusa alimtelekeza Baba wa Taifa kule Butiama tu, bali hata alipoenda naye St. Thomas Hospital aliendelea kumpuuza. Yaani alikuwa amuangalii kwa ukaribu kama daktari wake!
Tunaomba na wale walioko Wizara ya Ardhi na wizara zote alizopita watupe ufisadi wa Katibu Mkuu Patrick Rutabanzibwa; maana naye anajifanya Mungu mtu. Hana tofauti na Blandina, halafu naye ana roho mbaya sana!
Kweli kabisa; madaktari wakiboronga sawa lakini mtu mwingine akiboronga anashikiwa bango mpaka basi!! Kwani lazima wafanyie mazoezi Muhimbili Hospitali tu?
Asilimia mia maana yake nini? Hata nikiongeza bei andazi toka sh50 hadi sh 100 ni asilimia mia moja!!!
Watanzania tufanye kazi kwa bidii; tuache manung'uniko.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.