Uzoefu wa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge hautoshi kumpa sifa ya kuwa waziri mkuu, hata kuwa mwandishi mzuri wa makala ama vitabu vile vile haiwi kigezo cha kigwangala kutosha kuwa waziri mkuu. haya ni majukumu makubwa sana yanayohitaji mtu kuwa na uzoefu wa wizara walau mbili ama tatu hivi...
CV yake iliwahi kuwekwa hapa, Kigwangalla kasoma MBA na amebobea kwenye mambo ya uongozi, hiyo siyo shida kabisa sema kwa uwaziri mkuu hapana ila uwaziri anaweza kufaa wizara yoyote tu kwa uwezo wake wa siasa na uongozi
kwani CCM imeishiwa watu hata kuanza kuwafikiria the likes od Makamba, Kigwangala na Mwigulu kwenye nafasi nyeti kama ya Uwaziri Mkuu kweli? Kwenye Uwaziri wala sina shaka...wanaweza wakapewa, na in fact wapewe tu wataweza, tena wizara kamili, wala siyo unaibu na naamini watafanya kazi kwa kasi...
Hivi CCM huko watu wameisha mpaka watajwe na hawa madogo kwenye uwaziri mkuu kweli? Kigwangala, Mwigulu na Makamba wanafaa kwenye kupewa wizara lakini siyo uwaziri mkuu jamani.
Tangazo: Mkutano na waandishi wa habari, Jumatatu, Juni Mosi, 2015.
Ndugu,
Salaam.
Dkt. Hamisi Kigwangalla (MB) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya TAMISEMI, amepanga siku ya Jumatatu, wiki ijayo, Tarehe 1, Juni, 2015 kuzungumza na wanaCCM na watanzania wote kupitia kwa waandishi wa habari ...
Nimesoma hapa JF, nikaenda na Bidii Forums na Mabadiliko Forums nikakuta kuna mtu mmoja anayejiita mchunguzihuru@gmail.com amesambaza habari kuwa Kigwangalla amenukuu hotuba ya Obama ya DNC 2004. Nikafuatilia hapa ID ni tofauti lakini aliyepost hapa amekuwa akifanya jitihada za kuijaza hii post...
Nadhani kuna watu wanamuogopa mpaka wanaamua kumshambulia kila kona. kwa sababu nimeisoma hotuba yake na ya Obama na kubaini kuwa alichonukuu ni maneno e pluribus unum na hayo hata Obama naye hayakuwa yake, yapo kwenye nembo na mihuri ya serikali ya marekani...maana ningeshangaa sana atumie...
siyo jambo rahisi kuwa Dr...kwa vyovyote vile he has some intelligence sema siasa huwa haina watu wenye akili sana, wakitokea kuwemo basi hawaeleweki! wajinga wajinga ndiyo wanapendwa. kwa moyo wake huu, atafika mbali sana huyu
Una ushahidi gani?
Hivi Rais Kikwete anaandaa watu wangapi? Maana ilisemwa anamuandaa Membe, ikaja kamtuma Wassira, mara hakukutana na Lowassa barabarani? Mara anataka kuwaachia nchi vijana....which is which???
Sidhani kama umefanya utafiti wa kutosha kuhusu huyu Mheshimiwa. Maana elimu na uwezo wake kitaaluma hautiliwi shaka hata kidogo, tumuhukumu kwa mengine, labda kama elimu yake imemsaidiaje yeye mwenyewe kulisaidia Taifa letu, lakini siyo uhalali wa elimu yake ama uwezo wake kitaaluma! Mtu mwenye...
Logo nyingine ni hii hapo juu inapatikana kwenye Ukurasa wa facebook wa hii wanayoita 'movement'.
OMBI KWA MODERATORS: Kwa nini msituletee huyu Mheshimiwa hapa tumuulize maswali kama mna access naye na kama hatokimbia kama mwenzake January Makamba?
My Take: ni vizuri wakajitokeza na hawa...
hii ni logo ya kitu kipya mtaani hapa kinachojulikana kama 'Citizens For Kigwangalla' ambayo ni movement ya wapenzi na mashabiki wa Mbunge wa Nzega na Mwenyekiti wa Kamati ya TAMISEMI , Dr Hamisi Kigwangala. Kwenye twitte kuna handle inayoonekana kama citizensfork ambayo imeandikwa disclaimer...
Kwa hapa tulipo kwenye nafasi ya Urais na viti vingi vya Ubunge, hata CCM wakisimamisha jiwe watashinda bila shaka seuze Kigwangallah! Hivi tusemeni ukweli jamani, kuna mtu anaona kabisa kuna chama cha upinzani kinachoweza kuiangusha CCM leo hii? Hawa wanaogombana kwa sababu ya ruzuku na vyeo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.