Umenena mkuu. Hofu yangu ni tabia za Wabongo, watamwangusha muda si mrefu akiwa anawabembeleza hivi. Hivi kuna mfanyabiashara anapenda kulipa kodi? Bila kutumia nguvu nafikiri anaweza kujikuta hana fedha ya kutosha kuendesha nchi. Muhimu tumuombee mambo yaende vizuri maana yakivurugika tunaumia...
Maneno yako yanauma sana. Dunia inamhukumu Lulu akiwa mtoto mdogo sana, sio haki. Hili tukio lilitokea akiwa mtoto, Mungu amsaidie. Maisha yamembebesha mzigo mzito hadi nafikir akiwaza hata yeye hutamani angekufa tu siku hiyo.
Namba 5 na 7 ni ukweli mtupu. Kumbuka kuna wanawake wana kazi nzuri na mishahara ya maana tu (pesa kwao sio tatizo kivile) lakin hizo 5 na 7 zinawakera hadi wanaamua kutafuta pa kupunguza machungu. Wanaume ishini na wake zenu kwa akili......
Juhudi kubwa inahitajika ktk kuelimisha jamii yetu, kumbe bado kuna wenye mawazo mgando kiasi hiki!!!!
Daaaah nimesikitika aiseeee. Hao wateule wa rais kama akina Bulembo wana sifa zipi kubwa kuwazidi wanawake wote Tz?
Pasco umekosea, muungwana hukiri kosa. Ila kwa vile unajinadi kutoka...
Kama wewe unayeonekana umeenda shule na unaishi mjini lakini bado una mawazo haya!!!!!!Daaaah kazi ipo!Umenifanya nitafakari akili za hao walioko kijijini zikoje.!?? Mila na desturi ni mazoea tu ya kimaisha sio kitu biological, badilikeni muachane na mila za kipumbavu kama hizi. Mijanaume mijitu...
Aiseeee nilifikiri ni mimi tu kumbe ni kweli hawa voda ni wezi.nilijiunga kifurushi cha 1gb lakin kiliisha ndani ya siku mbili, wakati asubuhi mpaka jioni natumia wi fi ya ofisi!!!!!! Natoka ofsin saa moja jioni!! Hawa voda ni wezi wakubwa. Halafu vifurushi vyao bei juu bado hawaridhiki wanaiba...
Pole sana mkuu, nimeumizwa sana na maneno yako. Apumzike kwa amani. Wanaomhukumu Mungu awasamehe. Nina experience na maisha ya ughaibuni, ni magumu sana. Nyumbani wanaona umeukata but wewe ndo unakuwa unajua mateso na upweke unaopambana nao. Mlioko ughaibuni Mungu awalinde hakika. let him rest...
Mleta thread umefanya jambo jema sana kuanzisha huu uzi. Yaani hii bima ni zaidi ya JIPU, labda tuseme ni donda ndugu. Magufuli sikia kilio chetu wafanyakazi. Hawa bima ukianza kazi tu waanza kukata hata kama hujajiunga, lakin cha ajabu hawatoi hizo kadi haraka kama wanavyochukua hela yako...
Ukiona mtu analalamika ujue huyo naye alikuwa jipu. Magufuli ana kazi hii nchi imejaa majipu, hawa nao lilikuwa jipu sugu. Kanyaga twende mr president watanyooka tu
Mkuu hongereni kwa kupata mtoto. Nakubaliana na mkeo, acha kumpa lift mwanamke mwingine tena asubuhi na jioni. Jamani tusiwe vipofu ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya marafiki dizaini hii. Mwanzo anakuwa rafiki mzuri lakin anakuja kugeuka shetani aliyekubuhu. Hivi unaona shida gani kuacha...
Hili ndiyo tatizo ambalo upinzani waliambiwa lakin wakaziba masikio! Kumpokea lowasa lilikuwa kosa kubwa sana tena mbaya zaidi kumpa nafasi ya kugombea urais. Sasa nafikiri mnajionea, mkitaja escrow mnaambiwa na richmond je?!
Njia rahisi zaidi ni kumkamulia maji ya nyanya hata vijiko viwili tu, itamsaidia sana. Nimeitumia hii njia mara nyingi kwa mwanangu na imemsaidia sana. Juisi ya ukwaju pia hata kwa watu wazima inasaidia sana.
Nakubaliana nawe mkuu. Ukienda nje ndo utajua umuhimu wa hizi bomoa bomoa. Wabongo tunaboa sana, kila sehemu hata kama ni barabarani tunageuza sehemu za biashara. Njia za waenda kwa miguu hazionekan maana watu wamefanya parking za bajaji, wanamwaga nyanya barabarani hadi kero. Ukiwagusa kama...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.