Yeah, It all makes sense now. Serikali yake ilijawa na usiri mwingi, na sasa ni mengi tu mengine tutaanza kujasikia. Ingawa hili la maradhi ya moyo pia lilikuwa linasikika kama tetesi tu, na tetesi huwa zinakuaminika kichwa kichwa.
Hiyo itategemea umakamu wa rais ataupata nani. Kwakuwa huku bara idadi ya Waislamu na Wakristo ni nusu kwa nusu, inawezekana kabisa kukawa na shinikizo kwamba makamu wa rais awe Mkristo ili kubalance na rais ajaye ambaye ni "Muislamu."
Tukumbuke kwamba marais watatu waliopita kuanzia Mkapa...
Ingawa katiba haikutaja dini, ila imetaka rais akitoka bara, basi makamu ni visiwani, na kinyume chake ni kweli. Kwa utamaduni wa CCM, hiyo ina maana pia kibarua cha waziri mkuu Majaliwa kimeshaota nyasi, kwakuwa rais atakuwa "mwislamu" basi waziri mkuu atakuwa "mkristo."
roselina john,
roselina john , nimekuwa natafuta kamusi nzuri ya Kiswahili - Kingereza na kinyume chake. Kama hiyo hapo juu inaonekana ni nzuri, je una dondoo zozote namna ya kuipata?
Labda niongeze ufafanuzi kidogo ndugu yangu, hawa wanaodai mtu anatakuwa "hatari kwa usalama wa Tanzania" kwa kujua kwamba mtu akipata uraia na haki zake (kwa kawaida) zina ongezeka ndani ya Tanzania. Kwa mfano, haki ya kuchagua na kuchaguliwa, na ile ya kuteua na kuteuliwa pia. Hivyo basi...
Tatizo la CCM kwenye hii issue ya uraia pacha ni kuogopa tu ushindani utakaoletwa na Watanzania wa diaspora, ambao wengi wameelimika au kutokana na kuishi kwao kwenye nchi za kigeni zilizoendelea, wamekuwa na uelewa wa mambo ambao utaleta shida kwa viongozi wa CCM waliozoea kuabudiwa na wajinga...
Asante kwa kujitahidi kufafanua hili suala kwa ndugu zetu, ambao wengi bado hawaelewi au wengine wanapotosha kwa makusudi. Binafsi, napingana na hii dhana ya kusema kwamba mtu "ameukana uraia wa Tanzania", kitu ambacho si kweli. Watanzania wengi niwajuao mimi, nikiwemo na mimi mwenyewe...
Asante Mh. kwa majibu yako, ila hizo sifa zinazofanya mtu asiwe muoga kwenye siasa bado hazijanishawishi. Labda nikupe tafsiri yangu ya "mwanasiasa muoga" ndio labda tutaelewana vizuri. Mwanasiasa muoga ni yule anayekaa kimnya dhidi ya maovu ya kisiasa, kiuchumi, au kijamii kwenye nchi yake kwa...
Huyu mtu ni muoga sanaa, na amezoea vya bure na vya kutafuniwa. Hivyo basi, mikiki mikiki ya upinzani hawezi kabisa, na akienda upinzani basi atarudi chama dola kabla hata uchaguzi wenyewe wa 2020 kwisha, maana haitokuwa uchaguzi, bali ni ujambazi.
Ni bora audhurie na kuondoka tu kwenda Namibia. Akipewa nafasi ya kuongea basi jiandaeni kabisa kisaikolojia. Huko Namibia pia aandaliwe speech maalum (kwa Kiswahili na mkalimani au Kingereza), na kusisitizwa sana kuisoma, vinginevyo akileta ule utaratibu wake wa kuseleleka "free style" pia...
KUHUSU DHIHAKA ZINAZOENDELEA BAADA YA JENEZA LA MENGI KUWASILI
Hiyo ni njia ambayo tutapitia wote, endapo tutafia nje ya nchi, na kua na ulazima wa kuzikwa nyumbani Tanzania. Kitu ambacho naona ni cha ajabu kidogo katika suala hili ni kumtumia marehem mzee wetu Mengi kama mfano dhidi ya wale...
Tunao ushahidi wa kimazingira kama yalivyo matukio mengine ya kutekana na kupigana risasi. Kama unasubiri "uhakika" basi utasubiri sana, kwasababu matukio kama haya huwa polisi hawatoi ushirikiano wowote kwani wanajua kinachoendelea na "mchunguzi, hajichunguzi."
Kweli lugha mbaya, lakini sheria za kudhibiti mambo haya (i.e., sheria ya makosa ya mtandao) si ipo? Sasa maguvu mpaka kutekana na uuana ya nini? Napinga lugha chafu, lakini napinga zaidi vitendo vya utekaji na mauaji!
Ni kweli, tulio makini tunajua kwamba Ndugai na wenzie ni wacheza ngoma tu, ila mpigaji ngoma mwenyewe yupo Magogoni. Ila mpigaji ngoma huyu anayo sifa ya kuanzisha/ kusimamia matukio na baadae kujatatua ili kujizolea sifa za kisiasa, mfano ni kikokotoo. Sasa tunamtaka aache mara moja hizi hila...
Kumbe wewe ulimsikia vizuri kama nilivyomsikia mimi. Alisema "Watanzania sio wajinga sana," na sio kama watu wengi wanavyosema humu JF kwa kuliondoa hilo neno "sana" ambala linapotosha maana nzima ya ujumbe wa mkuu. Ni hivi...mkuu ana amini kwamba Watanzania ni wajinga, ila sio sana. Yaani...
Jibu la hoja yako na mshangao wako ni rahisi sana. Ni hiviii...waliopo CCM na wenye akili wanajua kwamba kitendo alichofanyiwa Lissu si sahihi na cha kinyama, na sasa amesalimika kutoka kwenye njama hiyo ovu, hoja zake ni nzito mno. Hoja za Lissu ni nzito na zimejaa ukweli kiasi kwamba kama una...
Hii ni miongoni mwa michango inayonisikitisha kutoka kwa Ndg. Paskali. Ila kwakuwana naheshimu uhuru wa maoni, nitakwenda kwenye mada. Lissu amekabiliana vizuri sana na maswali ya Mr. Sukur, ambaye Kama kawaida yake huwa na maswali magumu yanayoakisi jina la kipindi chake cha "Hardtalk." Tukija...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.