Timu ya Wanasheria ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo LEAT imetoa tamko la kulaani kwa nguvu zote wale waliomshambulia kwa risasi mfanyakazi mwenzetu wa zamani Ndugu Tundu Antiphas Mughwai Lissu huko Dodoma. LEAT inataka kusakwa na kushitakiwa wote waliohusika na jinai hii ya kiovu...
Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) imetoa tamko juu ya Ripoti ya Kamati Maalumu ya Raisi Juu ya Mchanganyiko wa Madini (Makinikia) katika Makontena yaliyozuiliwa bandarini. Tamko hilo limeambatanishwa hapa.
Kwa ufupi LEAT haishangazwi na kile kilichobainika kwani ni...
Re-calculation ipi wakati mtu alitakiwa alipwe pesa zake. PAP alitakiwa kumlipa VIP pesa zake suala la "re-calculation" haliwahusu VIP usichanganye mambo hapa.
Kosa ni la kiuandishi na haliondoi ukweli kuwa muhuri na saini ya Jaji. Kosa hili linasahishika kwa mujibu wa kifungu cha 96 cha Kanuni za Mwenendo wa Kesi za Madai Sura ya 33 ya Sheria za Tanzania kama zilivyorejewa mwaka 2002.
Nadhani ungepitia kwa makini hiyo Amri ya Mahakama ungeelewa kile nilichokisema tokea nilipoiweka hapo juu shida ni kuwa wenye nia ovu (Cabal) wamefanikiwa kuwafanya watu wote waliopokea fedha kutoka VIP kuwa ndio mafisadi wakati wakijua Mahakama ilitoa amri ya VIP kulipwa fedha zake za mauzo ya...
Ujasiri wangu ni kukuleta Amri hiyo ya Mahakama kama unafahamu sheria utaelewa nguvu ya amri hiyo. Unaweza kusema nimechanganya kuiita hukumu au uamuzi suala ni kuwa hata uwe na uamuzi au hukumu havitekelezeki mpaka uwe na Amri na ndiyo hiyo hapo chini. Mahakama ndiyo ilikuwa msuluhishaji na...
Mtu asiyependa ukweli hawezi kuelewa ukweli. Yeye atapenda kuwahukumu watu wasio na hatia na kuwaita wezi huku hana hata chembe ya ujasiri kuwakamata wezi wenyewe. Yeye ni yule apendaye kuchangia kupiga watu mawe bila hata kujua kosa lao. Kama ungesikiliza maelezo ya Prof. Tibaijuka mchango...
Hiyo ndiyo hukumu ya mahakama sasa kama wewe una mtindo wako wa kuandika tarehe kauanzishe katika mahakama yako na si ya Tanzania tuliyo nayo sasa. Shida ni kukataa kusikia ukweli ili kutekeleza nia ovu ya kuhukumu watu bila kuwasikiliza.
Walilipa $7.5milioni na wakataka kutokomea na Rugemalira akawafungulia kesi ya kudai kutekelezwa kwa mkataba mnamo tarehe 8 Januari 2014 ambayo ndiyo ilisababisha Amri hii ya maridhiano. Rugemalira alikataa kutapeliwa na akapigania haki zake leo hii anaitwa kila aina ya tusi kana kwamba mtu...
Inabidi urudi darasani kusoma sheria na kuelewa maana na nguvu ya Consent Settlement Order. Kwa faida yako hiyo ni amri iliyotokana na usuluhishi wa mahakama. Isome vizuri Amri hiyo na ujue maana yake!
Mahakama iliamuru VIP alipwe pesa zake zilikotoka si suala la VIP kwani yenyewe ilitakiwa ilipwe pesa zake kwa mujibu wa mkataba na hata muda wa malipo na kodi vyote vimetajwa katika Amri hiyo. Na hiyo ndiyo amri ya Mahakama na siku zote hakuna anayeizungumzia Amri hii na watu wanaaminishwa kuwa...
Hiyo ni hoja ambayo Kamati ya Zito na Bunge hawakutaka hata kuizungumzia na kuaminisha umma kuwa ilikuwepo kesi ya IPTL na TANESCO huko ICSID ambayo eti iliamuriwa februari mwaka huu wakati kesi iliyokuwepo ilikuwa kati ya SBC v. TANESCO. Haki ikipotea uongo, dhuluma na ukuwadi utamalaki!
Uharamu wake ni upi wakati mahakama imeamua alipwe fedha zake na PAP na ndivyo ilivyofanywa? Je ndugu yangu umesoma Amri ya Mahakama Kuu na kuielewa au unaamua kuwa mbishi kama mshipa?
Mimi nimeleta ushahidi wa amri ya mahakama kuu juu ya wao kulipwa fedha? Wewe leta ushahidi unaopinga au kukanusha hilo na si kuanza kuzungumza kwa hisia na kudhania. Mtu mweledi atasimamia ukweli unaoendana na ushahidi. Yes I know Tanzanians are smarter but I don't want them to be duped through...
Kimbunga cha mabadiliko kinapita nchini Tanzania. Wananchi wa Tanzania wamefahamu wazi kuwa hivi sasa nchi yetu inahitaji mabadiliko. Hitaji hilo limejionyesha katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Licha ya CCM kuwa ndiye mshindi wa jumla lakini kupoteza kwake kwa mitaa, vitongoji na vijiji...
Umesema vema iweje mtu asiyehusika na wizara yenye dhamana na uchotwaji wa fedha hizi awajibishwe wakati wale waliotoa amri ya kutolewa fedha wakiachwa na huku wakipangwa kupongezwa kuwa ni watendaji kazi wazuri ambao ni lazima wabaki katika serikali. Suala ni kuwa VIP ililipwa fedha zake halali...
Mbayuwayu ni yule asiyependa kusikia upande wa pili na kung'ang'ania hukumu iliyotolewa bila mtu kumsikiliza na kutaka mtu awajibike kwa makosa yaliyotendwa na wizara asiyo na dhamana nayo. Je nchi ya Tanzania inakataza mtu kupokea mchango? Nasema haipo ila mbayuwayu kama wewe ndiye unayetaka...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.