Nipo Dar maeneo ya Mbezi, nimelima nyanya aina ya Money Maker kama nusu heka huku. Ninamwagilia kwa maji ya kisima nilichochimba. Tatizo nilipatalo ni kupukutika kwa maua kila zinavyoanza kutoa maua. Nimejaribu kupanda aina ya Roma nazo ni hivyo hivyo, naombeni kujua nitumie dawa gani.
Ndugu zangu natafuta mtaalamu ambaye atanishauri kuhusu banda, vifaranga, madawa na ufugaji mzima wa kuku wa kienyeji na wa kisasa. Pliz inbox kama upo maeneo ya jirani. Naishi Masaki DSM.
Mimi sijaona hiyo mikataba ndiyo maana nachelea kusema kilichomo ndani. Huenda hizo nyumba 5000 zimo humo maana siamini kama mikataba hiyo yote ni ujenzi wa msikiti
Hakuna watu wanaonichefua kama ambao kila siku wanataka kujilinganisha na Rwanda. Ni nchi mbili zenye historia tofauti, vipaumbele tofauti na ukubwa tofauti. Sasa ulitaka na sisi tuombe nyumba 5000. ungekuwa wa maana kama ungesema umeiona mikataba haina lolote, hapo ningekuelewa.
Nina eneo kama hekali 5 huko Mbondole hapa DSM. Nataka kulitumia eneo hilo kwa ajili ya ufugaji pamoja na kilimo cha mboga mboga. Natafuta mtu/Kampuni ambayo itanifanyia tathmini ya matumizi ya eneo hilo ikiwa ni pamoja na design ya majengo kutokana na kusudio langu.
Hivi unajua pamoja na kubana matumizi lazima masuala mengine yaende kama kawaida. Kwa hiyo mazoezi ya ndege vita yasiwepo ili ziharibike zife kesho tuwe hatuna ndege. Think big kaka. Jiongeze kidogoooo siasa zisikupeke huko. Najua una akili lakini sa iasa zinakutesa.
Katika Video hii Rais Uhuru anasema Tanzania, Uganda na nchi nyingine katika ukanda huu zinapata zaidi ya 40% ya recurring budget kutoka kwa wazungu. Hivi ni kweli?? Tunategemea mzungu kulipa mshahara? Anajua recurring budget ninini kweli.... Ni nawazo tu
Ukweli sijaona point ya maana ambayo inaweza kuitwa ya Kaibu Mkuu wa Chama tena CHADEMA zaidi ya kupayuka. Unadhani Dr Slaa angeweza kutoa tamko hili? Mtaisoma namba..yeye huyooooooo
Yaani hakuna habari positive ya nchi hii ambayo itaandikwa ukurasa wa mbele na kuipa uzito unaostahili kwenye Gazeti la Mwananchi.
Nimefuatilia kwa muda mrefu sana na ukweli nimeanza kuamini yaliyosemwa huko nyumaaa kuwa Gazeti hili lina ajenda ya kuona nchi yetu inaingia kwenye mgogoro na...
Kama hujui jambo afadhali ukae kimya. CSR ni moja kati ya mambo yaliyopo katika mikataba ya uanzishaji wa Migodi. Ni lazima na siyo kujiamlia. Kutokujua sheria kwako ndo kumekuwa kunatuumiza kila siku.
Kuna kodi za aina mbili, Cooperate Social Responsibility (CSR) na Service Levy. Sasa hiyo CSR ilikuwa inapangwa na Mgodi badala ya wananchi. Wao wana shida ya barabara, mgodi unawapa msaada wa maji...utofauti huu wa perceptions na priorities umekuja kumalizwa na RC huyu. Anastahili pongezi kwakweli.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.