Akili za mtukufu hizi, kuona wenye nazo wanapata shida. Hakuna nchi duniani inaendelea bila middle class (kwa lugha za mtaani matajiri). Unafarijika kwa vyuma kukaza kwa mtu baki, akili hizi unazipata chattle tu
Hauitaji sababu zaidi ya kuwa na dhumuni la kwenda nje, shida hamsomi sheria, tunatumia ubabe zaidi, nimekuwekea jinsi ya kupata passport kisheria na hakuna takwa linalotaka uwe na sababu zaidi ya kuwa na nia ya kwenda nje ya nchi.
Nimekuwa nafuatilia passport tangu mwezi wa saba mwaka huu, kila siku napigwa kalenda. Passport ilitakiwa kuchukuliwa mwezi wa nane lakini mpaka leo bado.
Ukifuatilia unaambiwa nenda makao makuu, kule napo wana majibu ya rejareja kweli, unaambiwa passport yako bado, bila kuambiwa iko hatua gani...
Magufuli inabidi asikilize ushauri wa watu na aache mambo ya you can’t question rais. Wengi kwenye mioyo tunasononeka na yeye, tunamuachia mungu tu, na mimi sio mpiga dili kama ambavyo yeye anapenda ku ‘generalize’
Yaani kila siku zinavyozidi kwenda kwenye awamu hii, sielewi focus ni nini. Viwanda? Kushika madini? Kufunga watu bila makosa? Kukamata wapinzani? Kuboresha maisha? Sielewi yaani...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.