Duh tumeisha sahau mara hii tenaa!!!!!!! Ila si vibaya tukakumbushana mwaka 2005 moja kati ya sifa ya mkuu wa kaya wakati wa harakati zileee tuliambiwa kuwa ni mtu wa watu na anahudhuria misiba hata ya watu wa kawaida sasa mambo yamegeuka tunaambiwa ni umaarufu. Ingependeza kama waanzilishi...
Kwa hili naomba nitofautiane kidogo na ndugu Mbatia. Msiba wa mufti shinyanga kama ulipata kuhudhuria japo hayakuzungumzwa sana uwepo/ ujio wa ndugu Lowasa pale msibani haukuleta tafsiri nzuri ya msiba kwani uligeuka kuwa ni sehemu ya siasa. Busara iliwaongoza wakazuia watu kulisukuma gari lake...
Usipumbazwe na uwingi wa watu kutoka eneo moja kwenda kujiandikisha sehemu nyingine. Tatizo ni upungufu wa mashine za BVR ukilinganisha na idadi ya watu kwenye baadhi ya maeneo, maeneo waliyotoka watu wanakesha kusubiri kuandikishwa na wengine wanafanya biashara kati ya shilingi 5000 mpaka 20000...
Napenda majibu yako ila hayana tofauti na mkubwa sana na msomi kushinda wote kuhusiana na mambo haya uliyo yaleta hapa anaitwa profesa Sospeter Muhongo. Chige unaweza kuwa unajua A mwenzio akajua B na vitu hivi ni lazima viwe mstari mmoja. Na usijipe haki ya kujua kwako mambo A ukaona kuwa wanao...
Chige
Sio kwamba wadanganyika ni wajinga kiasi hicho ila tambua kwamba kuna baadhi ya mambo hayako sawa kwenye sekta hiyo. Hakuna kitu kibaya kama kuwaaminisha wadanganyika kuwa huwezi kuwa na maendeleo bila wawekezaji, ni ujuha uliopitiliza na dharau kwa binadamu aliye huru kifikra. Maendeleo...
Suala la midahalo ni muhimu katika kuwatambua wale wote wanaotarajia kugombea nafasi muhimu kabisa katika ngazi za maamuzi kitaifa. Itatupa fursa za kuweza kuwatambua umahiri wao katika kunadi sera zao. Suala hili lingependeza zaidi kama lingewekwa kwenye katiba yetu na si suala la hiari ya...
Huwezi tetea muungano kwa makongamano nje ya nchi, kero za muungano zinafahamika na watu wamejaribu kuainisha suluhisho zake kwenye rasimu ya katiba mpya. Ifike mahali wadanganyika tutambue thamani ya kodi zetu na tusiruhusu hawa wahuni wa kisiasa kutumia kodi zetu kwa makongamano au ziara nje...
Tunarudia tena makosa yaleyale kama ya kipindi kile cha kampuni ya RITES. Tulisema sana kuhusu uzembe ule wa kwenye reli lakini tuliendelea kupuuzwa kama kawaida ya wadanganyika na leo tena tunaletewa ngonjela zilezile na wataalumu wetu wazalendo saaana. Kwanini lakini tunakuwa wazembe wa...
Emanuel Buhohele amejitahidi kuongoza kipindi kulinganisha na jamaa wa kwanza kwani alikuwa ameisha badili nia na madhumuni ya kipindi na kukigeuza kuwa kipindi cha kujengana kisiasa. Unapopata nafasi ya kufanya mahojiano na mtu kama Jaji Warioba unapaswa kufanya utafiti wa kina kuhusu mtu huyo...
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi tafiti zinaonyesha kuwa baada ya miaka hamsini ijayo visiwa vya Pemba na Unguja vitakuwa vimemezwa na bahari. Hii pia haihitaji wageni wa nje waje wawaonyeshe bali ni nyie kufanya juhudi kidogo tu kuwauliza wazee wenu wa miaka ile na kuangalia kingo za bahari...
Mkuu inapendeza pale tunapofuatilia masuala ya kisiasa nchini mwetu hasa kama wewe ni muumini wa mafungamano ya siasa na maisha. Katika makala zako zote za ushauri juu ya kadhia hii ya Zitto vs Chadema inapendeza zaidi kama ni mwandishi, mchambuzi au mfuatiliaji wa masuala ya kisiasa kuwa...
Najisikia fahari kuwa mwanafunzi wa Dkt. Charles Kitima na mafundisho yake aliyonipa mwaka wa tatu yalikuwa yameejaa weredi wa kujitambua na kuwa open minded kwenye masuala yanayo gusa jamii. Mzee Farjalah with due respect plz personal attacks kwa Dkt kuhusu yeye kuikosoa serikali kwa mambo ya...
Guys ni kweli maneno matamu ndo yamejaa ndani ya mambo ya Gesi na viongozi wetu ni malenga wazuri wa kuhubiri lakini naomba tutambue kitu kimoja nacho ni kuwa kuna watu wamebahatisha kufanya shughuli kwenye hivi vitalu na kushuhudia madudu yaliyoko. Sehemu kubwa ya watu hawa (wawekezaji) ni...
Hizo ndo dharau za kiafrika anaamini kuwa anajua kila kitu kwenye suala la gesi lakini kila akienda kwenye hivyo vitalu wanaishia kukaa maofisini na hao wadau wenye fedha na kupuuza kuongea na wazawa ili wawape madhaifu na dhuluma wanazo zipata.Inshaalah mungu akijalia document zikikamilika uozo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.