Dkt. Gwajima D
JF-Expert Member
- Nov 28, 2015
- 602
- 3,973
Wasaalam.
Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.
Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.
Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).
Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.
Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.
Asubuhi njema🙏🏽
Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25
Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.
Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.
Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).
Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.
Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.
Asubuhi njema🙏🏽
Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25