Ahsante kufuatilia Bajeti ya Wizara ya Jamii 2024/24

Dkt. Gwajima D

JF-Expert Member
Nov 28, 2015
602
3,973
Wasaalam.

Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.

Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.

Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).

Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.

Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.

Asubuhi njema🙏🏽

IMG-20240517-WA0222.jpg


Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25
 
Hongera Mh Waziri. Kazi yako ni nzuri inaonekana.

Nguvu zaidi iongezwe katika kudhibiti vitendo vya unyanysaji wa kijinsia Pamoja na Ukatili. Ikiwezekana adhabu Kali ziongezwe kukomesha
Ahsante Sana kwa maoni, tunaomba ushirikiano, tunaanza kwa upya kabisa mapambano kama timu moja ya taifa ngazi zote, huku maoni yenu yakiwa chachu kwenye safari ya utekelezaji. 🙏🏽
 
Hongera Ila nimeona wabunge wengi hawana uelewa kuhusu wizara yako.

Msikariri USHOGA tu wala msikariri ukatili wa kijinsia wanafanyiwa waototo na wanawake tu.

Kuna kitu kinabidi kifanyie ikiwemo kuwa na mentorship program za Ku-raise awarsness kwa WATU ili waielewe hii sector yako vzr hasa wabunge naona they know nothing kuhusu wizara yako.
 
Kwanza hongera sana, hata kwa kujitahid kwenda na wakati na kuwa humu. Naamin umejua hili n moja ya majukwaa machache yenye kuweza kuchangia vema mjadala na bajeti yako 👏 👏.

Maoni yangu n machache tu katika upambanaj wa ukatili wa kijinsia msitazame tu kaya masikin na kaya za vijijin. Maana huko mjini na haomnazozan wanauwezo na wasomi wanaongoxa kwa ukatili, madada wa kazi za nyumbn wanateswa sana, wafanyakaz wa kwenye ma bar na masekta kama madin ni unyana wanafanyiwa.

La mwisho kwangu ni yale mambo ya USHOGa nazan ni vema serikari ikawa wazi na kuonesha mlengwa wake, mtu asie na maadili anaefanya kwa kuiga au kushinikizwa ni ngumu kuepuka ukatili wa jinsia. Kama taifa tunataman kuona tunajua ni namna gan tunapamban na hata mambo ya magharibi ........ ahsante
 
Kwanza hongera sana, hata kwa kujitahid kwenda na wakati na kuwa humu. Naamin umejua hili n moja ya majukwaa machache yenye kuweza kuchangia vema mjadala na bajeti yako 👏 👏.

Maoni yangu n machache tu katika upambanaj wa ukatili wa kijinsia msitazame tu kaya masikin na kaya za vijijin. Maana huko mjini na haomnazozan wanauwezo na wasomi wanaongoxa kwa ukatili, madada wa kazi za nyumbn wanateswa sana, wafanyakaz wa kwenye ma bar na masekta kama madin ni unyana wanafanyiwa.

La mwisho kwangu ni yale mambo ya USHOGa nazan ni vema serikari ikawa wazi na kuonesha mlengwa wake, mtu asie na maadili anaefanya kwa kuiga au kushinikizwa ni ngumu kuepuka ukatili wa jinsia. Kama taifa tunataman kuona tunajua ni namna gan tunapamban na hata mambo ya magharibi ........ ahsante
Habari za asubuhi. Ahsante kwa mchango wako. Shukrani
 
Wasaalam.

Nawashukuru watanzania wote kwa ufuatiliaji wa wasilisho la bajeti ya wizara ya jamii 2024/25.

Namshukuru Mungu kwamba, mjadala mkubwa wakati wa uwasilishaji, ni ishara ya elimu kuifikia jamii kwa kina kuhusu kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia na kudhibiti mmomonyoko wa maadili unaosababisha vitendo mbalimbali viovu.

Kuzinduliwa kwa mpango wa pili wa kutokomeza ukatili huu na mmomonyoko wa maadili kwa ujumla, utaipeleka ajenda hii hadi ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri, vikao vya mabaraza ya madiwani, baraza la madiwani, baraza la maendeleo la wilaya na mkoa kwa kina zaidi. Na hapo ndiyo tutakuwa tumeungana wote kama taifa kwenye vita hivi kupitia ugatuaji madaraka na kuyasogeza karibu na jamii (DxD).

Tuendelee kushirikiana kwa upya kabisa, inawezekana kutunza maadili.

Elimu zaidi kuhusu bajeti yetu, Sera mpya ya jinsia na maendeleo ya wanawake na mpango mkakati wa pili wa MTAKUWWA tuliozindua 15 Mei, 2024: tukutane wiki ijayo Jamii Forums online na Twitter space pia na space zingine. Ratiba inakuja. Kisha kutoka online kwenda halmashauri kwa halmashauri.

Asubuhi njema

View attachment 2992948

Unaweza kuisoma yote hapa: Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa mwaka 2024/25
Sawa Mh.Hongera lakini na wanaume wanakula vitasa majumbani kutoka kwa wake zao muwatetee nao jamani wanaume wawe wanasikilizwa nao.
 
Hongera kwa uwasilishaji wa bajeti ya wizara yako.
Kuna mdau hapo juu amezungumzia suala la wanaume kupigwa na wake zao, hili jambo lipo na linakua kwa kasi kubwa sana.
Inaelekea wanaume wanakosa ujasiri wa kujitokeza na kuweka bayana madhila wanayopitia kutokana na kaulimbiu iliyowekwa na serikali ya kumtetea MWANAMKE. Hebu hili mliangalie upya.

Jambo lingine(nje ya mada)....Mahudhurio ya wabunge yanatia aibu. Ina maana hiyo hali haimkeri kiongozi wa bunge!!?
 
Wizara ikasimu madaraka yake katika ngazi ya mtaa na kata na vitongoji na vijiji, huko ndiko wanaishi wanajamii, iwekwe namna ya maafisa wa nfazi hizo watatakiwa kutoa taarifa ya matatizo au mafanikio katika ngazi zao, taarifa ikitolewa uweze kuiona moja kwa moja, na pia ngazi ya juu ikishughulikia, uone moja kwa moja, kuwe na mfumo wa tehama.

Pia ku-audit utendaji kazi wa mifumo ya serikali, wananchi wawe na platform ya kuripoti mambo hayo katika ngazi zao, na uongozi wa wizara uone, na uongozi mikoani uone, na pia kuwe na time frame ya kuchukua hatua.

Wizara isimamie uanzishwaji wa vikundi vya kijamii ngazi ya mtaa au kata au kijiji, ambavyo vitakuwa vinafuatilia kama kuna jambo la kijamii linahitaji hatua za haraka, inaweza kuwa pilot project kwa maeneo korofi ambayo yanaonekana haki jamii inakiukwa mara kwa mara. Hao watafanya vommunity policing/auditing, na watembelewe na maafisa ustawi wa jamii mara kwa mara, hii itakuwa preventive measure. Kama mtoto anateswa, au mwanamke, au mwanaume, au mlemavu, hawa kwa kuwa wanaishi humo, watatoa utambuzi wa haraka, na ikibidi kumuita muhusika.

Wale wanaopokea mikopo ya akina mama na vijana, wanaweza kuongezewa component hii, na waitolee taarifa
 
Sawa Mh.Hongera lakini na wanaume wanakula vitasa majumbani kutoka kwa wake zao muwatetee nao jamani wanaume wawe wanasikilizwa nao.
Kweli, nami nimeendelea kupokea sms nyingi za wanaume na kuwapa huduma kupitia Dawati la jinsia. Changamoto kubwa ninayoona ni kuwa, mindset ya wanaume wengi hawajakubali kuwa, kama binadamu, hata wao kuna wakati wanahitaji hizi huduma, wanaona kama vile wao siyo watu wa kukutwa na msongo wa mawazo kwa kuwa hiyo ni dalili ya udhaifu na udhaifu ni ishara ya wanawake. SAIKOLOJIA. Hii ndiyo shida.....
 
Hongera kwa uwasilishaji wa bajeti ya wizara yako.
Kuna mdau hapo juu amezungumzia suala la wanaume kupigwa na wake zao, hili jambo lipo na linakua kwa kasi kubwa sana.
Inaelekea wanaume wanakosa ujasiri wa kujitokeza na kuweka bayana madhila wanayopitia kutokana na kaulimbiu iliyowekwa na serikaliya kumtetea MWANAMKE. Hebu hili mliangalie upya.

jambo lingine(nje ya mada)....Mahudhurio ya wabunge yanatia aibu. Ina maana hiyo hali haimkeri kiongozi wa bunge!!?
Ahsante Sana kwa maoni. Wanaume wengi hawajakubali kuwa, binadamu wote Wana udhaifu wakati fulani fulani na udhaifu siyo ulemavu bali inaweza kuwa ni kiwango cha hekima fulani katika kuepusha madhara. Sasa tuna mikakati ya kuelimisha jamii ya wanaume tangu wadogo, vijana na hata watu wazima. Tunashirikiana na vyama vya wanaume pia. Mwaka huu wengi wataijua zaidi hii wizara na tutaenda pamoja.

Hata hivyo, mimi binafsi nimepokea na kuwaunganisha na mifumo ya Dawati la jinsia wanaume wengi tu. Nimeshauri Hadi kuundwa kwa vyama vya wanaume, na Sasa tunavyo. Tunaelekea sasa kwenye Kampeni kubwa ya "male champion, he for she".

Mambo yaja ndugu zangu, wizara ina miaka 2 tu na hata nusu bado.
 
Back
Top Bottom