JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,247
- 5,731
Wadau wa JamiiForums,
Benki ya dunia kwa mara nyingine imetoa ripoti ya 'Tanzania Economic Update' ikilenga utalii kwa namna ipi inaweza kuleta mafanikio kwa Tanzania na Watanzania. Ripoti hiyo imeanisha mengi kuhusiana na Sekta ya Utalii. Baadhi machache ni;
Ujumbe Muhimu toka kwenye ripoti "Unloacking the Potential of the Tourism Industry for Tanzanians"
Kwa wapenzi wengi wa Ligi ya Mpira wa Miguu ya Uingereza, vivutio vya kitalii vya Tanzania vyenye hadhi ya kimataifa vinafahamika vyema. Mlima Kilimanjaro, nyumbu wanaohama kwa makundi kutoka Serengeti kwenda Masai Mara na kurudi, fukwe mwanana za Zanzibar, vyote hivi vimetangazwa wakati wa michezo zaidi ya 100 kwenye viwanja mbalimbali vya Uingereza.
Tanzania ilivutia zaidi ya watalii milioni moja mwaka 2013. Aina ya watalii wenye uwezo wa kifedha ambao sasa hivi Tanzania huwavutia wako tayari kulipa kiasi kikubwa cha fedha ili kutembelea vivutio vyake vya kipekee, hivyo kulipa fedha za kigeni katika nchi ambayo takribani theluthi moja ya watu wake bado wanaishi chini ya mstari wa taifa wa umasikini. Ijapokuwa sekta ya utalii nchini Tanzania imekua kwa haraka katika muongo mmoja uliopita, ingeweza kutumika kuleta manufaa makubwa zaidi kwa idadi kubwa ya Watanzania.
Kama ilivyo kwa matoleo yaliyopita, toleo hili la sita la hali ya uchumi lina sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inatoa tathmini ya hali ya sasa ya uchumi wa Tanzania pamoja na matarajio yake ya muda mfupi na wa kati, wakati sehemu ya pili inajikita katika jinsi watunga sera wanavyoweza kupata manufaa makubwa zaidi kutokana na utalii.
Hali ya Uchumi wa Tanzania
Mtazamo wa kawaida wa uchumi wa Tanzania umekosolewa baada ya kufanyika kwa tathmini mpya hivi karibuni ya mahesabu ya taifa na matokeo ya utafiti wa bajeti ya kaya kwa mwaka 2012. Kwa misingi ya tathmini mpya, Tanzania inaonekana kukaribia kufikia hadhi ya nchi ya kipato cha kati, ambapo wastani wa kipato cha mtu ni takribani Dola za Marekani 1000. Pia inaonyesha wazi kwamba ukuaji wa uchumi umewafika hadi kwa watu masikini, wakiwemo walio masikini sana. Hii ni habari njema kwa uchumi wa Tanzania na matarajio yake kwa ukuaji unaozingatia usawa.
Hata hivyo, maendeleo haya yanahitaji maelezo ya ziada. Takribani asilimia 40 ya Watanzania watu wazima wana kipato cha chini ya Dola za Marekani 1.25 kwa siku, wakati Watanzania 9 kati ya 10 wana kipato cha chini ya Dola za Marekani 3 kwa siku.
Uchambuzi wa hivi karibuni wa ukuaji uchumi wa Tanzania haujaathirika kwa kiwango kikubwa na takwimu hizi mpya zilizoboreshwa. Kiwango cha ukuaji uchumi kimekuwa hakiendi mbali na asilimia saba, ijapokuwa kasi ya ukuaji imekuwa ikibadilika mara kwa mara kuliko ilivyokokotolewa hapo mwanzoni. Kiwango cha mfumuko wa bei kwa mwaka uko kati ya asilimia 5 na 6, wakati urari wa malipo kwa ujumla haujabadilika.
Udhaifu wa usimamizi wa uchumi mkuu wa Tanzania unabaki kuwa sera yake ya fedha. Wakati nakisi ya fedha kwa ujumla imepungua kwa kiasi kikubwa katika mwaka 2013/14, kutoka asilimia 5 (kwa tathmini mpya) ya Pato Ghafi la Taifa (GDP) hadi asilimia 3.4, kupungua huko kulifikiwa kwa gharama kubwa. Hii iliwezekana tu kupitia malimbikizo makubwa ya madeni ya makandarasi na mifuko ya pensheni.
Thamani ya madeni haya kwa sasa yamefikia viwango vya kutisha. Kupungua huko pia kulipatikana kwa kupunguza matumizi ya umma katika sekta za kipaumbele, matokeo yake ni kwamba ile programu iliyotangazwa sana ya ‘Matokeo Makubwa Sasa" ilipata rasilimali chache kuliko ilivyokuwa mwaka 2012/13. Vivyo hivyo, matumizi ya maendeleo yalipungua kwa asilimia 1.2 ya GDP. Thamani ya jumla ya fedha iliyotumwa kwa serikali za mitaa pia ilipungua, na kuhatarisha utoaji wa huduma za elimu na afya. Mwenendo huu hasi katika bajeti unadhoofisha mipango mikubwa ya Serikali ya kutoa huduma nzuri za miundombinu na za kijamii kwa idadi ya watu inayokua kwa kasi.
Marekebisho makubwa katika viwango na maudhui ya matumizi katika kipindi cha mwaka 2013/14 kwa sehemu kubwa yalitokana na kiwango cha chini cha makusanyo ya ndani. Sio tu kwamba malengo ya mapato hayakufikiwa kwa kiwango kikubwa, lakini pia utendaji, kwa maana ya ukusanyaji wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) umekuwa mbaya sana, mapato hayo yakilingana na thamani ya asilimia 3 tu ya Pato Ghafi la Taifa (GDP) katika mwaka 2013/14. Uwiano huu ni moja ya viwango vya chini zaidi duniani, mbaya kuliko Madagascar na mbaya zaidi ya kiwango kilichofikiwa na Burkina Faso na Msumbiji, nchi ambazo pia ni masikini na zenye chumi zinazotegemea zaidi kilimo.
Shinikizo la fedha limeendelea kuongezeka kuanzia mwanzoni mwa mwaka wa fedha 2014/15. Mwaka huu tena malengo ya mapato hayakufikiwa, kwa asilimia 10 katika robo ya kwanza, wakati thamani ya madeni kwenye mifuko ya pensheni imeendelea kuongezeka, na kusababisha mmoja kati mifuko mikubwa kukaribia kufilisika. Aidha, Wadau wengi wa Maendeleo wamechelewesha kutoa fedha kwa ajili ya kusaidia bajeti kwa sababu wanasubiri ufafanuzi kuhusu kadhia yenye utata ya IPTL, ambayo inaweza kuwahusisha baadhi ya viongozi wa juu wa serikali kufanya makosa.
Mwitikio wa Serikali kwa matukio haya hasi ni kwa kudhibiti baadhi ya matumizi yake na kuongeza kiwango cha kukopa kutoka soko la ndani. Serikali pia imeanza kupanga mipango ya kulipa madeni yake kwa mifuko ya pensheni na makandarasi wakati matokeo ya uchunguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali katika sakata la IPTL na mapendekezo ya Bunge pia yanafanyiwa kazi. Serikali pia itoe kipaumbele kwa utekelezaji wa haraka wa Sheria mpya ya VAT. Kwa kifupi, inaonekana mamlaka imetambua haja ya kudhibiti hali ya kifedha wakati gurudumu la kisiasa linaongeza kasi. Kura ya maoni imepangwa kufanyika Aprili mwaka huu, wakati uchaguzi mkuu utafanyika mwezi Oktoba.
Matarajio ya muda mfupi na wa kati yanabakia chanya kwa uchumi wa Tanzania. Ukuaji wa Pato Ghafi la Taifa (GDP) unatabiriwa kubakia asilimia saba, wakati kiwango cha mfumuko wa bei na urari wa malipo utabakia katika viwango vyake vya sasa. Hata hivyo, mfumuko wa bei na akaunti za nje huathirika kwa urahisi na kuyumba kwa bei za bidhaa za kimataifa, hususani bei za chakula, dhahabu na nishati.
Utabiri huu chanya unachukulia kwamba hali ya kifedha itabaki ikiwa imedhibitiwa, nakisi ya fedha ya jumla ikiendelea kuwa sawa na takribani asilimia tatu ya GDP katika miaka michache ijayo. Hii itahitaji juhudi kubwa ili kuboresha makusanyo ya mapato, hususani iwapo mamlaka zitataka kutekeleza programu zao za uwekezaji wa umma, ambalo ni jambo linalofanyika kwa nia ya kuleta maendeleo na ni muhimu. Mamlaka pia zitahitaji kupanua wigo wa fedha wa kutosha ili kulipa na kuzuia madeni mapya, na kuzuia kujikopesha katika masoko ya ndani na ya kimataifa.
Kuna uwezekano wa faida kwa utabiri huu kwa maana kwamba nchi inaweza kutumia kwa kiwango cha juu fursa ilizo nazo. Tanzania imejaaliwa kuwa na maliasili za kila aina, rasilimali hizo zinajumuisha gesi asilia, madini, udongo wenye rutuba na wanyama pori wengi. Kwa kutumia rasilimali hizi, Tanzania iko katika nafasi nzuri ya kuweza kupenya katika masoko ya kanda na kimataifa.
Aidha, Tanzania ina fursa nzuri katika utalii, ambao unaweza kutumika kuongeza nguvu ili kuharakisha ukuaji uchumi, kuongeza mapato ya fedha na mapato ya ziada ya fedha za kigeni. Hii ni sekta ambayo sio tu inakua kwa haraka duniani, lakini pia inahitaji nguvu kazi nyingi hivyo kuwa na uwezo wa kutengeneza idadi kubwa ya ajira. Matokeo yake ni kwamba maendeleo ya sekta ya utalii yako juu katika ajenda ya Rais pia na Baraza la Taifa la Biashara.
Kutumia utalii ili kuleta manufaa makubwa zaidi
Utalii tayari huleta manufaa makubwa kwa uchumi wa Tanzania na ungeweza kuleta manufaa makubwa zaidi katika siku zijazo iwapo utasimamiwa ipasavyo. Sekta hii imepanuka kwa haraka katika miaka ya hivi karibuni, ikivutia idadi inayoongezeka ya wageni kila mwaka. Kwa sasa inaajiri takribani watu nusu milioni na ni chanzo muhimu sana cha fedha za kigeni.
Licha ya faida ambazo tayari zinatokana na sekta hii, Watanzania walio wengi bado hawajafaidika kadri iwezekanavyo. Kwanza, wakati watalii wengi wako tayari kutumia kiasi kikubwa cha fedha kutembelea Tanzania, sehemu ya matumizi haya yanabakia huko huko ng'ambo. Hili ni jambo la kutarajiwa, na Tanzania haina tofauti na nchi nyingine, kwani watalii wengi ni watu wa mataifa ya nje na huandaa safari zao kupitia taratibu zilizotayarishwa kabla.
Pili, karibu shughuli zote za kitalii zimejikita katika maeneo mawili - kanda ya kaskazini kuzunguka Arusha na kisiwa cha Zanzibar – ambayo inaelezea kwa nini sehemu nyingine za nchi hazijaunganishwa.
Tatu, hata katika maeneo ambayo yanatembelewa sana, umasikini umekithiri, hususani karibu ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ikiashiria kwamba bado mahusiano na wana jamii wa maeneo hayo hayajanzishwa.
Nne, wakati sekta ya utalii ikipanuka kwa kasi, bado haijatengeneza kazi zenye tija za kutosha kwa wananchi katika miaka ya karibuni, iwe ni za moja kwa moja au kupitia njia nyingine. Mwisho, mfumo wa kodi usiotabirika na usioeleweka umekatisha tamaa wawekezaji, wakati taratibu zisizo wazi za mgawo wa mapato umefanya kuwa vigumu kufuatilia matumizi ya mapato yanayokusanywa kutoka kwenye sekta ya utalii.
Masuala yote haya yanaelezea kwa nini kutayarisha mkakati mpya wa utalii kwa Tanzania ili kuleta manufaa makubwa zaidi katika sekta ambayo tayari ina mchango mkubwa katika uchumi ni muhimu. Hili ni jambo ambalo kwa sehemu kubwa limekubalika, na majadiliano ya kina baina ya wadau tayari yanafanyika. Wadau wanaonekana kukubaliana kwamba ni muhimu kufanikisha malengo makuu mawili: (i) ongezeko la idadi ya watalii wanaotembelea nchi; na (ii) juhudi za makusudi kuelekeza shughuli za utalii kusini mwa nchi. Ijapokuwa malengo haya kimsingi ni mazuri, mafanikio yake yanahitaji kusimamiwa kwa uangalifu iwapo yatatakiwa kuleta matokeo chanya badala ya hasi.
Sekta ya utalii inalenga kuzidisha mara nane mapato yake ifikapo mwaka 2025. Lengo hili lina maana kwamba Tanzania itapokea idadi sawa ya watalii ambao sasa hivi Moroko na Afrika Kusini wanapokea. Ili kufanikisha lengo hili, itakuwa ni lazima kufikia kiwango cha ongezeko la takribani asilimia 20 kila mwaka, karibu mara mbili ya kiwango cha sasa cha kukua. Ijapokuwa kinafikika, kufanikisha lengo hili kunahitaji uwekezaji wa kutosha katika miundombinu, kutolewa kwa msaada kwa sekta binafsi, na kuendeleza rasilimali watu katika maeneo mbalimbali ya kijiografia.
Kwa sababu rasilimali za umma ni finyu na zitaendelea kuwa hivyo, Serikali lazima ifikirie njia bora zaidi ya kuvutia uwekezaji binafsi na kuchukua hatua za kutengeneza mazingira yanayofaa zaidi ya kufanya biashara. Njia bora zaidi ya kufikia hapa ni kwa kuanzisha ubia wa kimkakati na kupitia kuanzishwa kwa miradi inayojitegemea yenyewe, kama nchi nyingine zilivyofanya.
Iwapo litafanikiwa, lengo la kuvutia idadi kubwa zaidi ya watalii kuja Tanzania, ijapokuwa ni jambo jema lakini hii itasababisha kuwepo kwa athari ambazo lazima tukubaliane nazo na itatulazimu kuzisimamia vyema. Ongezeko kubwa la wageni litasababisha onegezeko la shinikizo katika maliasili zetu ambazo ndizo zinazobeba utalii wa nchi. Tayari, ujangili usiodhibitiwa umesababisha kupungua kwa idadi ya tembo na faru katika maeneo mengi. Kama asemavyo mfanya biashara mmoja wa utalii, kwa kifupi na kwa masikitiko: "Hakuna tembo, hakuna utalii." Pia kutakuwa na ushindani mkubwa kwa rasilimali maji, na uwezekano wa kutokea migogoro ya maslahi baina ya wakulima, shughuli za kuzalisha umeme na mifumo ya ekolojia asilia.
Kupanua kanda za utalii kuelekea Kusini kutahusisha kuendeleza bidhaa mpya za utalii katika maeneo kama vile Pori Tengefu la Selous, Hifadhi ya Taifa ya Ruaha au fukwe katika pwani ya kusini. Hata hivyo, wakati haja ya kupanuka kuelekea maeneo mengine imetambuliwa na kujadiliwa kwa muda mrefu, ni kama hakuna kitu kilichonyika. Bado kuna wageni takribani 20,000 kwa mwaka wanaoenda Ruaha, asilimia kumi tu ya idadi ya wanaotembelea Hifadhi ya Serengeti. Sababu za kutokuwepo maendeleo ni pamoja na kukosekana kwa miundombinu, vikwazo vikubwa kwa uwekezaji binafsi, uhaba wa rasilimali watu inayohitajika, na kukosekana kwa mkakati wa kutangaza vivutio vya utalii zaidi ya kupanda Mlima Kilimanjarpo, kuangalia nyumbu wanaohama na kurudi katika Serengeti, au kufurahia fukwe za Zanzibar.
Wakati kuongeza mapato yatokanayo na utalii na kupanua wigo wa vivutio vinavyotolewa kwa watalii ni kiini cha mkakati wowote wa kuendeleza utalii nchini Tanzania, kuna haja ya watunga sera na watendaji wa sekta kufikiria nje ya mfumo tuliouzoea na kufanya mambo kwa ubunifu. Hii itahitaji watunga sera kuridhia hatua chini ya nguzo tatu tofauti.
Nguzo ya kwanza inahusu upanuzi kuingia maeneo mapya. Hata hivyo, upanuzi huu usiwe wa upande mmoja. Lazima ihusishe sio tu upanuzi kwa misingi ya kijiografia; pia itahusisha kukidhi mahitaji ya sehemu tofauti za soko la utalii kwa kuanzisha shughuli mpya ambazo zinakidhi mahitaji ya wigo mpana wa watalii. Hadi sasa, msisitizo umekuwa katika kukidhi mahitaji ya watalii wenye uwezo wa kifedhai ambao wanaweza kulipa Dola za Marekani elfu kadhaa kwa ajili ya kuona wanyama wakati wanakaa katika hoteli za kifahari. Aina nyingine za utalii ziendelezwe, ikijumuisha shughuli za ufukweni ili kukidhi mahitaji ya watalii wenye bajeti za chini na kati. Miundo ya aina hizi za utalii ambayo inakidhi masoko haya tayari imeanza kuibuka kisiwani Zanzibar, ambayo hutoa malazi rahisi na ndege za kukodi, hivyo kufanya maeneo ya vivutio kufikika kwa urahisi kwa wigo mpana wa watalii, ikijumuisha wageni kutoka ndani ya nchi na katika kanda, na kukuza mahusiano na biashara za wenyeji na wafanyakazi.
Aina nyingine za utalii ambazo zinaweza kupanuliwa ni pamoja na utalii wa kibiashara katiika majiji ya Dar es Salaam na Arusha, utalii wa kitamaduni katika maeneo kama vile magofu ya Kilwa, na kutembea katika milima ya Usambara na Udzungwa. Mchanganyiko wa aina zote hizi za utalii pia unawezekana kupitia taratibu maalum ambazo zinawawezesha watalii kukaa kwa muda mrefu zaidi na kutawanya faida za kiuchumi.
Nguzo ya pili inahusu muunganisho wa shughuli za utalii katika maeneo yaliyopo. Ni jambo lililo wazi kwamba sekta ya utalii hadi sasa haijaweza kutengeneza ajira za kutosha za thamani kubwa na zenye tija kwa wananchi, pia haijawezesha maendeleo ya mahusiano ya pande zote na wadau wa nchini kwa kadri inavyowezekana. Kwa mfano, mfanyakazi wa kawaida mwenyeji wa Tanzania kwa wastani anaingiza kipato ambacho ni theluthi moja ya mwenzake nchini Kenya. Hoteli nyingi zinategemea vifaa, zana na chakula vinavyoagizwa kutoka nje.
Hivyo sera shirikishi zinahitajika ili kushughulikia maeneo haya mawili. Misaada mingine ya ziada inahitajika kwa jamii za wenyeji kwa kuwahusisha wananchi wa jamii hizi katika usimamizi wa hifadhi, na kwa kutumia mapato yanayotokana na shughuli za utalii kujenga miundombinu ya eneo husika; kwa kusaidia miradi ya biashara ya wenyeji na kwa kutoa fedha moja kwa moja kwenye uhawilishaji wa fedha.
Nguzo ya tatu inahusu hatua za kuboresha utawala bora. Hususani hii itahusisha utekelezaji wa mfumo unaotoa haki kwa wote na ulio rafiki kibiashara, na utayarishaji wa taratibu za wazi za kugawana mapato. Juhudi zinahitajika sana kutayarisha vipengele hivi vya mfumo wa utawala kwani sekta ya utalii kwa sasa inakwazwa na utozaji wa kodi na ada nyingi ambazo hukatisha tamaa wawekezaji, hasa wawekezaji wadogo, na kuongeza fursa kwa kampuni zinazonyonya nchi bila ya kunufaisha jamii pamoja na rushwa. Ushuru mwingi ambao hauna tija unaweza kuondolewa au kurasimishwa na hivyo kuongeza ushindani wa sekta.
Ni vigumu kuamini, kwamba licha ya kodi zote hizo, kiwango cha ukwepaji kodi kinaonekana ni kikubwa katika mchango wa jumla wa sekta ya utalii kwa mapato ya ndani, ukiwa ni theluthi ya ule wa sekta ya madini, licha ya kwamba utalii huchangia sehemu kubwa zaidi ya Pato Ghafi la Taifa (GDP). Ili iweze kuinua viwango vyake vya ukusanyaji wa mapato, Serikali inapaswa kuweka mkazo katika kuboresha viwango vya makusanyo katika sekta hii, kuweka vikwazo dhidi ya wakwepa kodi pale ambapo ni lazima. Motisha za kodi zenye nafuu kwa wawekezaji pia zipunguzwe, ukichukulia kwamba matokeo yake ni ya kutia shaka sana. Serikali iandae mkakati utakaolenga katika kurahisisha mfumo uliopo, kwani ni utata wa mfumo uliopo ndio lalamiko kuu la waendesha biashara ya utalii na vyama vyao. Aidha, Serikali ichukue hatua ya kupanua wigo wa kodi. Serikali ilenge kufanya haya kupitia ushirikiano kuliko mapambano na sekta binafsi.
Ili kuhakikisha utawala bora, ni muhimu kuhakikisha kwamba sekta ya utalii inatumika katika njia yenye ufanisi na uwazi. Kwa mazingira ya sasa, kufuatilia mgawo wa mapato haya ni kama haiwezekani kwa sababu ya sheria ngumu zinazotumika kutofautisha mapato haya. Kwa mfano, mapato kutoka kwenye uwindaji kinadharia hutumwa Hazina, Wizara ya Maliasili na Utalii, na serikali za mitaa, ripoti ya hivi karibuni ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali haikuweza kuhakiki iwapo fedha hizo zilipelekwa kwa taasisi lengwa. Huu si mkasa wa kipekee, wakati masuala yanayofanana mara kwa mara hutokea sehemu nyingine kutokana na idadi kubwa ya mawakala wanaojihusisha na ukusanyaji wa kodi na ada.
Nadharia ya uchumi inapendekeza uwezekano wa njia mbili zinazoshamirishana: (i) inaweza kuwa na taratibu ya sehemu moja kuu ya kufanya makusanyo na kutumia vigezo vya wazi vya mgawo kupitia taratibu za bajeti pale ambapo walengwa ni wengi na anuwai; na/au (ii) inaweza kugatua taratibu za makusanyo kwa serikali za mitaa pale ambapo walengwa wanatoka eneo hilo (kanuni ya kisaidizi).
Kuzingatia kanuni tatu za upanuzi katika maeneo anuwai, muunganisho na utawala bora kutawezesha Tanzania kupata manufaa mengi zaidi kutoka kwenye rasilimali na vivutio vyake vya utalii. Iwapo Tanzania inataka kupata manufaa makubwa kutokana na sekta hii, lazima iweke msisitizo sio tu katika hatua za kuongeza idadi ya watalii, lakini pia katika kuhakikisha kwamba sekta inaleta manufaa kwa sehemu kubwa ya wananchi na kwamba wanyamapori, utamaduni na maliasili vinalindwa ili faida hizi ziwe endelevu.
Benki ya dunia kwa mara nyingine imetoa ripoti ya 'Tanzania Economic Update' ikilenga utalii kwa namna ipi inaweza kuleta mafanikio kwa Tanzania na Watanzania. Ripoti hiyo imeanisha mengi kuhusiana na Sekta ya Utalii. Baadhi machache ni;
- Tanzania imeajiri karibu watu laki tano katika sekta ya utalii
- Watanzania karibu millioni mbili maisha yao yanategemea sekta ya Utalii
- Ripoti inaibua swali endapo kuna uhusiano kati ya ukuaji wa Uchumi katika kuongeza kazi kwa vijana
- Wananchi wana matumaini (as per conducted survey) kuwa itafika wakati Uchumi wa Tanzania utaimarika Tanzania
- Sekta ya utalii inalenga kuzidisha mara nane mapato yake ifikapo mwaka 2025
- Utalii tayari huleta manufaa makubwa kwa uchumi wa Tanzania na ungeweza kuleta manufaa makubwa zaidi katika siku zijazo iwapo utasimamiwa ipasavyo.
- Wadau wengi wa Maendeleo wamechelewesha kutoa fedha kwa ajili ya kusaidia bajeti kwa sababu wanasubiri ufafanuzi kuhusu kadhia yenye utata ya IPTL
Ujumbe Muhimu toka kwenye ripoti "Unloacking the Potential of the Tourism Industry for Tanzanians"
Kwa wapenzi wengi wa Ligi ya Mpira wa Miguu ya Uingereza, vivutio vya kitalii vya Tanzania vyenye hadhi ya kimataifa vinafahamika vyema. Mlima Kilimanjaro, nyumbu wanaohama kwa makundi kutoka Serengeti kwenda Masai Mara na kurudi, fukwe mwanana za Zanzibar, vyote hivi vimetangazwa wakati wa michezo zaidi ya 100 kwenye viwanja mbalimbali vya Uingereza.
Tanzania ilivutia zaidi ya watalii milioni moja mwaka 2013. Aina ya watalii wenye uwezo wa kifedha ambao sasa hivi Tanzania huwavutia wako tayari kulipa kiasi kikubwa cha fedha ili kutembelea vivutio vyake vya kipekee, hivyo kulipa fedha za kigeni katika nchi ambayo takribani theluthi moja ya watu wake bado wanaishi chini ya mstari wa taifa wa umasikini. Ijapokuwa sekta ya utalii nchini Tanzania imekua kwa haraka katika muongo mmoja uliopita, ingeweza kutumika kuleta manufaa makubwa zaidi kwa idadi kubwa ya Watanzania.
Kama ilivyo kwa matoleo yaliyopita, toleo hili la sita la hali ya uchumi lina sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inatoa tathmini ya hali ya sasa ya uchumi wa Tanzania pamoja na matarajio yake ya muda mfupi na wa kati, wakati sehemu ya pili inajikita katika jinsi watunga sera wanavyoweza kupata manufaa makubwa zaidi kutokana na utalii.
Hali ya Uchumi wa Tanzania
Mtazamo wa kawaida wa uchumi wa Tanzania umekosolewa baada ya kufanyika kwa tathmini mpya hivi karibuni ya mahesabu ya taifa na matokeo ya utafiti wa bajeti ya kaya kwa mwaka 2012. Kwa misingi ya tathmini mpya, Tanzania inaonekana kukaribia kufikia hadhi ya nchi ya kipato cha kati, ambapo wastani wa kipato cha mtu ni takribani Dola za Marekani 1000. Pia inaonyesha wazi kwamba ukuaji wa uchumi umewafika hadi kwa watu masikini, wakiwemo walio masikini sana. Hii ni habari njema kwa uchumi wa Tanzania na matarajio yake kwa ukuaji unaozingatia usawa.
Hata hivyo, maendeleo haya yanahitaji maelezo ya ziada. Takribani asilimia 40 ya Watanzania watu wazima wana kipato cha chini ya Dola za Marekani 1.25 kwa siku, wakati Watanzania 9 kati ya 10 wana kipato cha chini ya Dola za Marekani 3 kwa siku.
Uchambuzi wa hivi karibuni wa ukuaji uchumi wa Tanzania haujaathirika kwa kiwango kikubwa na takwimu hizi mpya zilizoboreshwa. Kiwango cha ukuaji uchumi kimekuwa hakiendi mbali na asilimia saba, ijapokuwa kasi ya ukuaji imekuwa ikibadilika mara kwa mara kuliko ilivyokokotolewa hapo mwanzoni. Kiwango cha mfumuko wa bei kwa mwaka uko kati ya asilimia 5 na 6, wakati urari wa malipo kwa ujumla haujabadilika.
Udhaifu wa usimamizi wa uchumi mkuu wa Tanzania unabaki kuwa sera yake ya fedha. Wakati nakisi ya fedha kwa ujumla imepungua kwa kiasi kikubwa katika mwaka 2013/14, kutoka asilimia 5 (kwa tathmini mpya) ya Pato Ghafi la Taifa (GDP) hadi asilimia 3.4, kupungua huko kulifikiwa kwa gharama kubwa. Hii iliwezekana tu kupitia malimbikizo makubwa ya madeni ya makandarasi na mifuko ya pensheni.
Thamani ya madeni haya kwa sasa yamefikia viwango vya kutisha. Kupungua huko pia kulipatikana kwa kupunguza matumizi ya umma katika sekta za kipaumbele, matokeo yake ni kwamba ile programu iliyotangazwa sana ya ‘Matokeo Makubwa Sasa" ilipata rasilimali chache kuliko ilivyokuwa mwaka 2012/13. Vivyo hivyo, matumizi ya maendeleo yalipungua kwa asilimia 1.2 ya GDP. Thamani ya jumla ya fedha iliyotumwa kwa serikali za mitaa pia ilipungua, na kuhatarisha utoaji wa huduma za elimu na afya. Mwenendo huu hasi katika bajeti unadhoofisha mipango mikubwa ya Serikali ya kutoa huduma nzuri za miundombinu na za kijamii kwa idadi ya watu inayokua kwa kasi.
Marekebisho makubwa katika viwango na maudhui ya matumizi katika kipindi cha mwaka 2013/14 kwa sehemu kubwa yalitokana na kiwango cha chini cha makusanyo ya ndani. Sio tu kwamba malengo ya mapato hayakufikiwa kwa kiwango kikubwa, lakini pia utendaji, kwa maana ya ukusanyaji wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) umekuwa mbaya sana, mapato hayo yakilingana na thamani ya asilimia 3 tu ya Pato Ghafi la Taifa (GDP) katika mwaka 2013/14. Uwiano huu ni moja ya viwango vya chini zaidi duniani, mbaya kuliko Madagascar na mbaya zaidi ya kiwango kilichofikiwa na Burkina Faso na Msumbiji, nchi ambazo pia ni masikini na zenye chumi zinazotegemea zaidi kilimo.
Shinikizo la fedha limeendelea kuongezeka kuanzia mwanzoni mwa mwaka wa fedha 2014/15. Mwaka huu tena malengo ya mapato hayakufikiwa, kwa asilimia 10 katika robo ya kwanza, wakati thamani ya madeni kwenye mifuko ya pensheni imeendelea kuongezeka, na kusababisha mmoja kati mifuko mikubwa kukaribia kufilisika. Aidha, Wadau wengi wa Maendeleo wamechelewesha kutoa fedha kwa ajili ya kusaidia bajeti kwa sababu wanasubiri ufafanuzi kuhusu kadhia yenye utata ya IPTL, ambayo inaweza kuwahusisha baadhi ya viongozi wa juu wa serikali kufanya makosa.
Mwitikio wa Serikali kwa matukio haya hasi ni kwa kudhibiti baadhi ya matumizi yake na kuongeza kiwango cha kukopa kutoka soko la ndani. Serikali pia imeanza kupanga mipango ya kulipa madeni yake kwa mifuko ya pensheni na makandarasi wakati matokeo ya uchunguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali katika sakata la IPTL na mapendekezo ya Bunge pia yanafanyiwa kazi. Serikali pia itoe kipaumbele kwa utekelezaji wa haraka wa Sheria mpya ya VAT. Kwa kifupi, inaonekana mamlaka imetambua haja ya kudhibiti hali ya kifedha wakati gurudumu la kisiasa linaongeza kasi. Kura ya maoni imepangwa kufanyika Aprili mwaka huu, wakati uchaguzi mkuu utafanyika mwezi Oktoba.
Matarajio ya muda mfupi na wa kati yanabakia chanya kwa uchumi wa Tanzania. Ukuaji wa Pato Ghafi la Taifa (GDP) unatabiriwa kubakia asilimia saba, wakati kiwango cha mfumuko wa bei na urari wa malipo utabakia katika viwango vyake vya sasa. Hata hivyo, mfumuko wa bei na akaunti za nje huathirika kwa urahisi na kuyumba kwa bei za bidhaa za kimataifa, hususani bei za chakula, dhahabu na nishati.
Utabiri huu chanya unachukulia kwamba hali ya kifedha itabaki ikiwa imedhibitiwa, nakisi ya fedha ya jumla ikiendelea kuwa sawa na takribani asilimia tatu ya GDP katika miaka michache ijayo. Hii itahitaji juhudi kubwa ili kuboresha makusanyo ya mapato, hususani iwapo mamlaka zitataka kutekeleza programu zao za uwekezaji wa umma, ambalo ni jambo linalofanyika kwa nia ya kuleta maendeleo na ni muhimu. Mamlaka pia zitahitaji kupanua wigo wa fedha wa kutosha ili kulipa na kuzuia madeni mapya, na kuzuia kujikopesha katika masoko ya ndani na ya kimataifa.
Kuna uwezekano wa faida kwa utabiri huu kwa maana kwamba nchi inaweza kutumia kwa kiwango cha juu fursa ilizo nazo. Tanzania imejaaliwa kuwa na maliasili za kila aina, rasilimali hizo zinajumuisha gesi asilia, madini, udongo wenye rutuba na wanyama pori wengi. Kwa kutumia rasilimali hizi, Tanzania iko katika nafasi nzuri ya kuweza kupenya katika masoko ya kanda na kimataifa.
Aidha, Tanzania ina fursa nzuri katika utalii, ambao unaweza kutumika kuongeza nguvu ili kuharakisha ukuaji uchumi, kuongeza mapato ya fedha na mapato ya ziada ya fedha za kigeni. Hii ni sekta ambayo sio tu inakua kwa haraka duniani, lakini pia inahitaji nguvu kazi nyingi hivyo kuwa na uwezo wa kutengeneza idadi kubwa ya ajira. Matokeo yake ni kwamba maendeleo ya sekta ya utalii yako juu katika ajenda ya Rais pia na Baraza la Taifa la Biashara.
Kutumia utalii ili kuleta manufaa makubwa zaidi
Utalii tayari huleta manufaa makubwa kwa uchumi wa Tanzania na ungeweza kuleta manufaa makubwa zaidi katika siku zijazo iwapo utasimamiwa ipasavyo. Sekta hii imepanuka kwa haraka katika miaka ya hivi karibuni, ikivutia idadi inayoongezeka ya wageni kila mwaka. Kwa sasa inaajiri takribani watu nusu milioni na ni chanzo muhimu sana cha fedha za kigeni.
Licha ya faida ambazo tayari zinatokana na sekta hii, Watanzania walio wengi bado hawajafaidika kadri iwezekanavyo. Kwanza, wakati watalii wengi wako tayari kutumia kiasi kikubwa cha fedha kutembelea Tanzania, sehemu ya matumizi haya yanabakia huko huko ng'ambo. Hili ni jambo la kutarajiwa, na Tanzania haina tofauti na nchi nyingine, kwani watalii wengi ni watu wa mataifa ya nje na huandaa safari zao kupitia taratibu zilizotayarishwa kabla.
Pili, karibu shughuli zote za kitalii zimejikita katika maeneo mawili - kanda ya kaskazini kuzunguka Arusha na kisiwa cha Zanzibar – ambayo inaelezea kwa nini sehemu nyingine za nchi hazijaunganishwa.
Tatu, hata katika maeneo ambayo yanatembelewa sana, umasikini umekithiri, hususani karibu ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ikiashiria kwamba bado mahusiano na wana jamii wa maeneo hayo hayajanzishwa.
Nne, wakati sekta ya utalii ikipanuka kwa kasi, bado haijatengeneza kazi zenye tija za kutosha kwa wananchi katika miaka ya karibuni, iwe ni za moja kwa moja au kupitia njia nyingine. Mwisho, mfumo wa kodi usiotabirika na usioeleweka umekatisha tamaa wawekezaji, wakati taratibu zisizo wazi za mgawo wa mapato umefanya kuwa vigumu kufuatilia matumizi ya mapato yanayokusanywa kutoka kwenye sekta ya utalii.
Masuala yote haya yanaelezea kwa nini kutayarisha mkakati mpya wa utalii kwa Tanzania ili kuleta manufaa makubwa zaidi katika sekta ambayo tayari ina mchango mkubwa katika uchumi ni muhimu. Hili ni jambo ambalo kwa sehemu kubwa limekubalika, na majadiliano ya kina baina ya wadau tayari yanafanyika. Wadau wanaonekana kukubaliana kwamba ni muhimu kufanikisha malengo makuu mawili: (i) ongezeko la idadi ya watalii wanaotembelea nchi; na (ii) juhudi za makusudi kuelekeza shughuli za utalii kusini mwa nchi. Ijapokuwa malengo haya kimsingi ni mazuri, mafanikio yake yanahitaji kusimamiwa kwa uangalifu iwapo yatatakiwa kuleta matokeo chanya badala ya hasi.
Sekta ya utalii inalenga kuzidisha mara nane mapato yake ifikapo mwaka 2025. Lengo hili lina maana kwamba Tanzania itapokea idadi sawa ya watalii ambao sasa hivi Moroko na Afrika Kusini wanapokea. Ili kufanikisha lengo hili, itakuwa ni lazima kufikia kiwango cha ongezeko la takribani asilimia 20 kila mwaka, karibu mara mbili ya kiwango cha sasa cha kukua. Ijapokuwa kinafikika, kufanikisha lengo hili kunahitaji uwekezaji wa kutosha katika miundombinu, kutolewa kwa msaada kwa sekta binafsi, na kuendeleza rasilimali watu katika maeneo mbalimbali ya kijiografia.
Kwa sababu rasilimali za umma ni finyu na zitaendelea kuwa hivyo, Serikali lazima ifikirie njia bora zaidi ya kuvutia uwekezaji binafsi na kuchukua hatua za kutengeneza mazingira yanayofaa zaidi ya kufanya biashara. Njia bora zaidi ya kufikia hapa ni kwa kuanzisha ubia wa kimkakati na kupitia kuanzishwa kwa miradi inayojitegemea yenyewe, kama nchi nyingine zilivyofanya.
Iwapo litafanikiwa, lengo la kuvutia idadi kubwa zaidi ya watalii kuja Tanzania, ijapokuwa ni jambo jema lakini hii itasababisha kuwepo kwa athari ambazo lazima tukubaliane nazo na itatulazimu kuzisimamia vyema. Ongezeko kubwa la wageni litasababisha onegezeko la shinikizo katika maliasili zetu ambazo ndizo zinazobeba utalii wa nchi. Tayari, ujangili usiodhibitiwa umesababisha kupungua kwa idadi ya tembo na faru katika maeneo mengi. Kama asemavyo mfanya biashara mmoja wa utalii, kwa kifupi na kwa masikitiko: "Hakuna tembo, hakuna utalii." Pia kutakuwa na ushindani mkubwa kwa rasilimali maji, na uwezekano wa kutokea migogoro ya maslahi baina ya wakulima, shughuli za kuzalisha umeme na mifumo ya ekolojia asilia.
Kupanua kanda za utalii kuelekea Kusini kutahusisha kuendeleza bidhaa mpya za utalii katika maeneo kama vile Pori Tengefu la Selous, Hifadhi ya Taifa ya Ruaha au fukwe katika pwani ya kusini. Hata hivyo, wakati haja ya kupanuka kuelekea maeneo mengine imetambuliwa na kujadiliwa kwa muda mrefu, ni kama hakuna kitu kilichonyika. Bado kuna wageni takribani 20,000 kwa mwaka wanaoenda Ruaha, asilimia kumi tu ya idadi ya wanaotembelea Hifadhi ya Serengeti. Sababu za kutokuwepo maendeleo ni pamoja na kukosekana kwa miundombinu, vikwazo vikubwa kwa uwekezaji binafsi, uhaba wa rasilimali watu inayohitajika, na kukosekana kwa mkakati wa kutangaza vivutio vya utalii zaidi ya kupanda Mlima Kilimanjarpo, kuangalia nyumbu wanaohama na kurudi katika Serengeti, au kufurahia fukwe za Zanzibar.
Wakati kuongeza mapato yatokanayo na utalii na kupanua wigo wa vivutio vinavyotolewa kwa watalii ni kiini cha mkakati wowote wa kuendeleza utalii nchini Tanzania, kuna haja ya watunga sera na watendaji wa sekta kufikiria nje ya mfumo tuliouzoea na kufanya mambo kwa ubunifu. Hii itahitaji watunga sera kuridhia hatua chini ya nguzo tatu tofauti.
Nguzo ya kwanza inahusu upanuzi kuingia maeneo mapya. Hata hivyo, upanuzi huu usiwe wa upande mmoja. Lazima ihusishe sio tu upanuzi kwa misingi ya kijiografia; pia itahusisha kukidhi mahitaji ya sehemu tofauti za soko la utalii kwa kuanzisha shughuli mpya ambazo zinakidhi mahitaji ya wigo mpana wa watalii. Hadi sasa, msisitizo umekuwa katika kukidhi mahitaji ya watalii wenye uwezo wa kifedhai ambao wanaweza kulipa Dola za Marekani elfu kadhaa kwa ajili ya kuona wanyama wakati wanakaa katika hoteli za kifahari. Aina nyingine za utalii ziendelezwe, ikijumuisha shughuli za ufukweni ili kukidhi mahitaji ya watalii wenye bajeti za chini na kati. Miundo ya aina hizi za utalii ambayo inakidhi masoko haya tayari imeanza kuibuka kisiwani Zanzibar, ambayo hutoa malazi rahisi na ndege za kukodi, hivyo kufanya maeneo ya vivutio kufikika kwa urahisi kwa wigo mpana wa watalii, ikijumuisha wageni kutoka ndani ya nchi na katika kanda, na kukuza mahusiano na biashara za wenyeji na wafanyakazi.
Aina nyingine za utalii ambazo zinaweza kupanuliwa ni pamoja na utalii wa kibiashara katiika majiji ya Dar es Salaam na Arusha, utalii wa kitamaduni katika maeneo kama vile magofu ya Kilwa, na kutembea katika milima ya Usambara na Udzungwa. Mchanganyiko wa aina zote hizi za utalii pia unawezekana kupitia taratibu maalum ambazo zinawawezesha watalii kukaa kwa muda mrefu zaidi na kutawanya faida za kiuchumi.
Nguzo ya pili inahusu muunganisho wa shughuli za utalii katika maeneo yaliyopo. Ni jambo lililo wazi kwamba sekta ya utalii hadi sasa haijaweza kutengeneza ajira za kutosha za thamani kubwa na zenye tija kwa wananchi, pia haijawezesha maendeleo ya mahusiano ya pande zote na wadau wa nchini kwa kadri inavyowezekana. Kwa mfano, mfanyakazi wa kawaida mwenyeji wa Tanzania kwa wastani anaingiza kipato ambacho ni theluthi moja ya mwenzake nchini Kenya. Hoteli nyingi zinategemea vifaa, zana na chakula vinavyoagizwa kutoka nje.
Hivyo sera shirikishi zinahitajika ili kushughulikia maeneo haya mawili. Misaada mingine ya ziada inahitajika kwa jamii za wenyeji kwa kuwahusisha wananchi wa jamii hizi katika usimamizi wa hifadhi, na kwa kutumia mapato yanayotokana na shughuli za utalii kujenga miundombinu ya eneo husika; kwa kusaidia miradi ya biashara ya wenyeji na kwa kutoa fedha moja kwa moja kwenye uhawilishaji wa fedha.
Nguzo ya tatu inahusu hatua za kuboresha utawala bora. Hususani hii itahusisha utekelezaji wa mfumo unaotoa haki kwa wote na ulio rafiki kibiashara, na utayarishaji wa taratibu za wazi za kugawana mapato. Juhudi zinahitajika sana kutayarisha vipengele hivi vya mfumo wa utawala kwani sekta ya utalii kwa sasa inakwazwa na utozaji wa kodi na ada nyingi ambazo hukatisha tamaa wawekezaji, hasa wawekezaji wadogo, na kuongeza fursa kwa kampuni zinazonyonya nchi bila ya kunufaisha jamii pamoja na rushwa. Ushuru mwingi ambao hauna tija unaweza kuondolewa au kurasimishwa na hivyo kuongeza ushindani wa sekta.
Ni vigumu kuamini, kwamba licha ya kodi zote hizo, kiwango cha ukwepaji kodi kinaonekana ni kikubwa katika mchango wa jumla wa sekta ya utalii kwa mapato ya ndani, ukiwa ni theluthi ya ule wa sekta ya madini, licha ya kwamba utalii huchangia sehemu kubwa zaidi ya Pato Ghafi la Taifa (GDP). Ili iweze kuinua viwango vyake vya ukusanyaji wa mapato, Serikali inapaswa kuweka mkazo katika kuboresha viwango vya makusanyo katika sekta hii, kuweka vikwazo dhidi ya wakwepa kodi pale ambapo ni lazima. Motisha za kodi zenye nafuu kwa wawekezaji pia zipunguzwe, ukichukulia kwamba matokeo yake ni ya kutia shaka sana. Serikali iandae mkakati utakaolenga katika kurahisisha mfumo uliopo, kwani ni utata wa mfumo uliopo ndio lalamiko kuu la waendesha biashara ya utalii na vyama vyao. Aidha, Serikali ichukue hatua ya kupanua wigo wa kodi. Serikali ilenge kufanya haya kupitia ushirikiano kuliko mapambano na sekta binafsi.
Ili kuhakikisha utawala bora, ni muhimu kuhakikisha kwamba sekta ya utalii inatumika katika njia yenye ufanisi na uwazi. Kwa mazingira ya sasa, kufuatilia mgawo wa mapato haya ni kama haiwezekani kwa sababu ya sheria ngumu zinazotumika kutofautisha mapato haya. Kwa mfano, mapato kutoka kwenye uwindaji kinadharia hutumwa Hazina, Wizara ya Maliasili na Utalii, na serikali za mitaa, ripoti ya hivi karibuni ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali haikuweza kuhakiki iwapo fedha hizo zilipelekwa kwa taasisi lengwa. Huu si mkasa wa kipekee, wakati masuala yanayofanana mara kwa mara hutokea sehemu nyingine kutokana na idadi kubwa ya mawakala wanaojihusisha na ukusanyaji wa kodi na ada.
Nadharia ya uchumi inapendekeza uwezekano wa njia mbili zinazoshamirishana: (i) inaweza kuwa na taratibu ya sehemu moja kuu ya kufanya makusanyo na kutumia vigezo vya wazi vya mgawo kupitia taratibu za bajeti pale ambapo walengwa ni wengi na anuwai; na/au (ii) inaweza kugatua taratibu za makusanyo kwa serikali za mitaa pale ambapo walengwa wanatoka eneo hilo (kanuni ya kisaidizi).
Kuzingatia kanuni tatu za upanuzi katika maeneo anuwai, muunganisho na utawala bora kutawezesha Tanzania kupata manufaa mengi zaidi kutoka kwenye rasilimali na vivutio vyake vya utalii. Iwapo Tanzania inataka kupata manufaa makubwa kutokana na sekta hii, lazima iweke msisitizo sio tu katika hatua za kuongeza idadi ya watalii, lakini pia katika kuhakikisha kwamba sekta inaleta manufaa kwa sehemu kubwa ya wananchi na kwamba wanyamapori, utamaduni na maliasili vinalindwa ili faida hizi ziwe endelevu.