Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Je Watanzania watakufa kwa kutoenda Marekani?Hatua hiyo inakuja saa chache baada ya serikali ya Trump kumpiga marufuku mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuingia nchini humo.
Bahati nasibu hiyo hutoa viza kwa watu takribani 50,000 kutoka nchi zenye kasi ndogo ya maendeleo kila mwaka kuingia na kufanya kazi Marekani.
Nchi ya Sudani pia raia wake wamepigwa marufuku kuingia katika bahati nasibu hiyo.
Wakati huo huo raia wa nchi nne ikiwemo mbili za Afrika Nigeria na Eritrea wamepigwa marufuku kabisa kuomba viza za kuhamia Marekani.
Marufuku hiyo pia itazihusisha nchi za Myanmar na Kyryzstan.
Hata hivyo raia wa nchi hizo ambao watataka kuingia Marekani kwa kutalii ama biashara wataruhusiwa.
Sent using Jamii Forums mobile app