Zuieni Ballal Kuchomwa Moto

Kubwajinga

JF-Expert Member
Jan 23, 2008
2,194
297
Nimesoma tetesi kuwa Marehemu Ballal atachomwa moto na sio kuwa atazikwa. Kwa nini watanzania walioko US wasiwasiliane na mwanasheria mkuu au kuomba mahakama izuie kuchomwa kwa Ballal mpaka mwili wake ufanyiwe uchunguzi kuhakikisha au kukanusha kuwa alipewa sumu? Kama aliuawa basi uchunguzi uweze kufanyika. Je kuna wakereketwa wenye ubavu wa kulisimamia hili??


Prof Baregu ataka Interpol wachunguze kifo cha Ballali

Na Jackson Odoyo

SIKU moja baada ya serikali kusema kuwa hakuna sababu ya kuchunguza kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu nchini (BoT), Daudi Ballali, Mhadhiri Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwasiga Baregu amesema kuna haja ya tukio hilo kuchunguzwa.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili jana, Profesa Baregu alisema serikali inatakiwa ku kubali kufanya uchunguzi juu ya suala hilo na kama wao hawawezi watumie wataalamu wa Polisi wa Polisi wa Kimataifa (Iterpol).

Alisema suala la uchunguzi wa kifo cha Ballali bado lina umuhimu kwasababu yawezekana serikali haikuhusika, lakini watuhumiwa wengine katika suala lake wakahusika ili kupoteza ushahidi, kwa sababu walifahamu kuwa Balali alikuwa shahidi muhimu katika suala la Akaunti ya ya Madeni ya Nje (EPA).

Alisema suala hilo likipuuziwa litasababisha watuhumiwa hao wazidi kujificha kwani baadhi ya wananchi wanaamini kuwa Balali hakuchuwa fedha peke yake katika sakata hilo na amekufa kabla hajajibu tuhuma zilizo kuwa zikimkabili.

"Serikali haiko makini katika suala hili, kwa sababu kama kweli wanadai kuwa hawakuhusika, kwanini wasitoe hata historia ya ugonjwa kuanzia alipokuwa BoT hadi alipoondoka kwenda kutibiwa," alisema Profesa Baregu

Alisema kitendo cha serikali kuendelea kuzuia uchunguzi wa kifo chake, inazidi kupoteza ushahidi juu ya suala la EPA na kwamba ikiendelea na ukimya huo itadhahirisha kuwa wanaohusika katika sakata hilo wataendelea kuneemeka na fedha hizo na hazitapatikana na kabisa .

Profesa alisema kutokana na uzito na unyeti wa suala hilo wananchi hawataacha kuhoji na kuendelea kupoteza imani na serikali yao, jambo ambalo ni hatari kwa mfumo wa utawala.

Juzi serikali kupitia kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilitoa kauli zilizozidisha utata juu ya suala la kifo cha Balali kwamba, haina sababu ya kufanyia uchunguzi wa kifo cahe kwa kuwa alikuwa mgonjwa siku nyingi.
 
how about you? siyo lazima uwe US ili uweze kuweka hilo pingamizi. and for what reason? unajuaje kama mwili wa marehemu haukufanyiwa autopsy? for your info balali has been sick kwa muda mrefu sasa and his death did not come unexpected!

get off balali's back. the guy is dead. taarifa zote za mafisadi wa EPA ziko mikononi mwa serikali ya tanzania. iwakamate hao wanorudisha pesa (if at all that is true) na iwawajibishe. this is the real issue. focusing on balali and what killed him blah blah is a waste of energy!
 
how about you? siyo lazima uwe US ili uweze kuweka hilo pingamizi. and for what reason? unajuaje kama mwili wa marehemu haukufanyiwa autopsy? for your info balali has been sick kwa muda mrefu sasa and his death did not come unexpected!

get off balali's back. the guy is dead. taarifa zote za mafisadi wa EPA ziko mikononi mwa serikali ya tanzania. iwakamate hao wanorudisha pesa (if at all that is true) na iwawajibishe. this is the real issue. focusing on balali and what killed him blah blah is a waste of energy!


Sidhani kama kuhakiki kifo cha Ballal ni jambo baya, hasa kama hilo halijafanyika. Mengi yameandikwa kuhusiana na ugonjwa wake na kifo chake ambayo yanahitaji maelezo yaliyokamilika. Ingekuwa jambo la busara, sio tu kwa serikali ya Tanzania, bali hata kwa wale wote wanaotaka ukweli wa yaliyotokea BOT, kuondolewa kiwingu cha matukio yote kwa kuufanyia uchunguzi mwili wa Ballal kabla ya kuuchoma, kwani kama atachomwa moto, ushahidi wowote ambao ungewezapatikana kwa autopsy, utakuwa umepotea.
 
how about you? siyo lazima uwe US ili uweze kuweka hilo pingamizi. and for what reason? unajuaje kama mwili wa marehemu haukufanyiwa autopsy? for your info balali has been sick kwa muda mrefu sasa and his death did not come unexpected!

get off balali's back. the guy is dead. taarifa zote za mafisadi wa EPA ziko mikononi mwa serikali ya tanzania. iwakamate hao wanorudisha pesa (if at all that is true) na iwawajibishe. this is the real issue. focusing on balali and what killed him blah blah is a waste of energy!

Conspiracy ya EPA ilimu-involve Balali pamoja na wengine, lakini naona tunaelekea kusahau hilo. Mgonja yuko hai... Why makombora yasielekezwe kwake? This is the right time to do that!!!!
 
Nimesoma tetesi kuwa Marehemu Ballal atachomwa moto na sio kuwa atazikwa. Kwa nini watanzania walioko US wasiwasiliane na mwanasheria mkuu au kuomba mahakama izuie kuchomwa kwa Ballal mpaka mwili wake ufanyiwe uchunguzi kuhakikisha au kukanusha kuwa alipewa sumu? Kama aliuawa basi uchunguzi uweze kufanyika. Je kuna wakereketwa wenye ubavu wa kulisimamia hili??

Ndugu yangu,

hivi kuna mtu anayeweza kuamua mazishi ya yeyote?
 
Conspiracy ya EPA ilimu-involve Balali pamoja na wengine, lakini naona tunaelekea kusahau hilo. Mgonja yuko hai... Why makombora yasielekezwe kwake? This is the right time to do that!!!!

It is good not to leave any stone unturned. Mgonja, conspirancy ya kifo cha Ballal n.k., yote haya yanafaa yakawekwa kwenye rekodi ili hapo baadaye yatakapohitajika yatumike kushughulikia watuhumiwa. Autopsy ya Ballal ni muhimu ikafanyika.
 
It is good not to leave any stone unturned. Mgonja, conspirancy ya kifo cha Ballal n.k., yote haya yanafaa yakawekwa kwenye rekodi ili hapo baadaye yatakapohitajika yatumike kushughulikia watuhumiwa. Autopsy ya Ballal ni muhimu ikafanyika.

Nani atadai hiyo autopsy kufanyika?
 
Nimesoma tetesi kuwa Marehemu Ballal atachomwa moto na sio kuwa atazikwa. Kwa nini watanzania walioko US wasiwasiliane na mwanasheria mkuu au kuomba mahakama izuie kuchomwa kwa Ballal mpaka mwili wake ufanyiwe uchunguzi kuhakikisha au kukanusha kuwa alipewa sumu? Kama aliuawa basi uchunguzi uweze kufanyika. Je kuna wakereketwa wenye ubavu wa kulisimamia hili??

aahh ! kumbe ballali amekufa ! na sio kwamba amefake kifo ! ok !
 
Ndugu yangu,

hivi kuna mtu anayeweza kuamua mazishi ya yeyote?

Kuamua hapana, lakini kutafiti chanzo cha kifo inawezekana kwenye nchi kama US. Attoney General anahitajika tu kupatiwa malalamiko yenye uhakika.
 
Kuamua hapana, lakini kutafiti chanzo cha kifo inawezekana kwenye nchi kama US. Attoney General anahitajika tu kupatiwa malalamiko yenye uhakika.

lazima kwanza kuwe na evidence of foul play ili huyo AG kuamua autopsy ifanyike ! lakini kama ni maneno tu kama haya yanayotolewa hapa yasiyo na kichwa wala miguu kila mtu anasema lake, whoever that AG wont buy anything for sh*t !
 
lazima kwanza kuwe na evidence of foul play ili huyo AG kuamua autopsy ifanyike ! lakini kama ni maneno tu kama haya yanayotolewa hapa yasiyo na kichwa wala miguu kila mtu anasema lake, whoever that AG wont buy anything for sh*t !

Nakubaliana na wewe kabisa, ushahidi ni lazima uwepo. Hapa wanaweza kutumia matukio ya EPA, itinerary za Ballal n.k. yanaweza kuwa ushahidi tosha wa kuombea uchunguzi.
 
Nakubaliana na wewe kabisa, ushahidi ni lazima uwepo. Hapa wanaweza kutumia matukio ya EPA, itinerary za Ballal n.k. yanaweza kuwa ushahidi tosha wa kuombea uchunguzi.

well was he the only one to testify against EPA ?? no, je na hao wengine ambao wangeweza kutestify wameuwawa pia ? NO, wapo hai !

maana hii ishu sio kusema kwamba ballali ndio aliwasha mshumaa, no ni watu wengine kabisa tena wanapeta sasa hivi ! huoni inashangaza sana hao watu kuwa alive na ballali kufa ?
 
Naona Prof. Baregu anakubaliana na mawazo yangu ya kutafiti kifo cha Ballali.




Prof Baregu ataka Interpol wachunguze kifo cha Ballali

Na Jackson Odoyo

SIKU moja baada ya serikali kusema kuwa hakuna sababu ya kuchunguza kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu nchini (BoT), Daudi Ballali, Mhadhiri Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwasiga Baregu amesema kuna haja ya tukio hilo kuchunguzwa.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili jana, Profesa Baregu alisema serikali inatakiwa ku kubali kufanya uchunguzi juu ya suala hilo na kama wao hawawezi watumie wataalamu wa Polisi wa Polisi wa Kimataifa (Iterpol).

Alisema suala la uchunguzi wa kifo cha Ballali bado lina umuhimu kwasababu yawezekana serikali haikuhusika, lakini watuhumiwa wengine katika suala lake wakahusika ili kupoteza ushahidi, kwa sababu walifahamu kuwa Balali alikuwa shahidi muhimu katika suala la Akaunti ya ya Madeni ya Nje (EPA).

Alisema suala hilo likipuuziwa litasababisha watuhumiwa hao wazidi kujificha kwani baadhi ya wananchi wanaamini kuwa Balali hakuchuwa fedha peke yake katika sakata hilo na amekufa kabla hajajibu tuhuma zilizo kuwa zikimkabili.

"Serikali haiko makini katika suala hili, kwa sababu kama kweli wanadai kuwa hawakuhusika, kwanini wasitoe hata historia ya ugonjwa kuanzia alipokuwa BoT hadi alipoondoka kwenda kutibiwa," alisema Profesa Baregu

Alisema kitendo cha serikali kuendelea kuzuia uchunguzi wa kifo chake, inazidi kupoteza ushahidi juu ya suala la EPA na kwamba ikiendelea na ukimya huo itadhahirisha kuwa wanaohusika katika sakata hilo wataendelea kuneemeka na fedha hizo na hazitapatikana na kabisa .

Profesa alisema kutokana na uzito na unyeti wa suala hilo wananchi hawataacha kuhoji na kuendelea kupoteza imani na serikali yao, jambo ambalo ni hatari kwa mfumo wa utawala.

Juzi serikali kupitia kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilitoa kauli zilizozidisha utata juu ya suala la kifo cha Balali kwamba, haina sababu ya kufanyia uchunguzi wa kifo cahe kwa kuwa alikuwa mgonjwa siku nyingi.
 
Back
Top Bottom