Jicho la Tai
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 1,449
- 574
Nimekuwa mara kadhaa nikifutilia ukurasa wa Matangazo ya live (Youtube) ya Ikulu Mawasiliano. Tangu kipindi cha Msigwa na hata sasa kipindi cha Zuhura Yunus.
Leo nimeona tatizo linaendelea sasa naomba nikiri wazi kuna mambo yanakwenda ovyo sana kwenye urushaji wa matangazo Youtube live kipindi hiki cha Zuhura Yunus kuliko alivyokuwepo Msigwa.
Matangazo yamekuwa yakikatakata sana na kuscratch kupita kiasi na wakati mwingine sauti hakuna au inakuwa sauti yenye kelele kupita kiasi.
Kuna muda matangazo yanaka kama vile wameishiwa vifurushi.
Hata sasa uliangalia kwenye Channel ya ikulu mawasiliano utakutana na vitu vilivyokosewa kurusha lakini vipo. (Natumaini vitatolewa baada ya post yangu hii)
Rejea hapa kwenye channeli ya Ikulu Tanzania utaona baadhi ya clip nimewekea X ambazo hazikustahili kuwepo ama zina changamoto ya muonekano zinapoanza. Kuna ambazo matangazo yalikwama kutokana na mtandao yakaishia chini ya dk 1, hayana maana na ulazima wa kuendelea kuwepo. Hata zile ambazo hazina alama ya X ikiwemo inayoruka sasa hivi live ina tatizo la sauti
Ushauri:
Tafuta timu nzuri ya kufanya nayo kazi, ikibidi uuuwe na wataalamu ambao ni technical zaidi ili kutoiaibisha hii channel ya ikulu.
Naamini Serikali ina resources za kutosha na kuna baadhi ya taasisi na wizara zinafanya vizuri sana kwenye matangazo ya live na mitandao ya kijamii pia.
Peleka timu yako ikajifunze ama tafuta watu hukohuko wakusaidie.
Pia muulize msigwa yeye aliwezaje kurusha matangazo vizuri?
Mwisho kabisa, fuatilia kujua nini kinasababisha, yamkini unahujumiwa.
Leo nimeona tatizo linaendelea sasa naomba nikiri wazi kuna mambo yanakwenda ovyo sana kwenye urushaji wa matangazo Youtube live kipindi hiki cha Zuhura Yunus kuliko alivyokuwepo Msigwa.
Matangazo yamekuwa yakikatakata sana na kuscratch kupita kiasi na wakati mwingine sauti hakuna au inakuwa sauti yenye kelele kupita kiasi.
Kuna muda matangazo yanaka kama vile wameishiwa vifurushi.
Hata sasa uliangalia kwenye Channel ya ikulu mawasiliano utakutana na vitu vilivyokosewa kurusha lakini vipo. (Natumaini vitatolewa baada ya post yangu hii)
Rejea hapa kwenye channeli ya Ikulu Tanzania utaona baadhi ya clip nimewekea X ambazo hazikustahili kuwepo ama zina changamoto ya muonekano zinapoanza. Kuna ambazo matangazo yalikwama kutokana na mtandao yakaishia chini ya dk 1, hayana maana na ulazima wa kuendelea kuwepo. Hata zile ambazo hazina alama ya X ikiwemo inayoruka sasa hivi live ina tatizo la sauti
Ushauri:
Tafuta timu nzuri ya kufanya nayo kazi, ikibidi uuuwe na wataalamu ambao ni technical zaidi ili kutoiaibisha hii channel ya ikulu.
Naamini Serikali ina resources za kutosha na kuna baadhi ya taasisi na wizara zinafanya vizuri sana kwenye matangazo ya live na mitandao ya kijamii pia.
Peleka timu yako ikajifunze ama tafuta watu hukohuko wakusaidie.
Pia muulize msigwa yeye aliwezaje kurusha matangazo vizuri?
Mwisho kabisa, fuatilia kujua nini kinasababisha, yamkini unahujumiwa.