Kamanda
Senior Member
- Dec 5, 2007
- 150
- 176
Mchezo wa siasa waanza.
Baada ya Zombe kutamba jana nyumbani kwake kuwa serikali itapoteza muda na fedha kwa kumkatia rufaa, kwani atashinda, leo serikali imeibuka na kukata rufaa.
Leo jioni, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) imewasilisha makabrasha kupinga hukumu hiyo katika Mahakama ya Rufani, Dar es Salaam.
Zombe na maofisa wenzake wanane wa Jeshi la Polisi walikabiliwa na kesi ya kuua wafanyabiashara watatu wa madini wa Mahenge, Moro na dereva taksi mmoja wa Dar.
Rufaa hiyo ambayo iliwasilishwa ilielezea sababu za Serikali kukata rufani hiyo dhidi ya maofisa hao wa zamani ambao ni Zombe, Christopher Bageni, Ahamed Makelle, Rajabu Bakari, Philipo Wabisabi, Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shonza na Abeneth Saro.
Serikali imepinga uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kupitia Jaji wa Mahakama ya Rufani, Salum Massati baada ya kumwona aliyekuwa mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Zombe kuwa hana hatia pamoja na kuwa ushahidi wa kimazingira uliotolewa mahakamani hapo ulikuwa ukimgusa moja kwa moja.
Baada ya Zombe kutamba jana nyumbani kwake kuwa serikali itapoteza muda na fedha kwa kumkatia rufaa, kwani atashinda, leo serikali imeibuka na kukata rufaa.
Leo jioni, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) imewasilisha makabrasha kupinga hukumu hiyo katika Mahakama ya Rufani, Dar es Salaam.
Zombe na maofisa wenzake wanane wa Jeshi la Polisi walikabiliwa na kesi ya kuua wafanyabiashara watatu wa madini wa Mahenge, Moro na dereva taksi mmoja wa Dar.
Rufaa hiyo ambayo iliwasilishwa ilielezea sababu za Serikali kukata rufani hiyo dhidi ya maofisa hao wa zamani ambao ni Zombe, Christopher Bageni, Ahamed Makelle, Rajabu Bakari, Philipo Wabisabi, Jane Andrew, Emmanuel Mabula, Michael Shonza na Abeneth Saro.
Serikali imepinga uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kupitia Jaji wa Mahakama ya Rufani, Salum Massati baada ya kumwona aliyekuwa mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Zombe kuwa hana hatia pamoja na kuwa ushahidi wa kimazingira uliotolewa mahakamani hapo ulikuwa ukimgusa moja kwa moja.