Na Laila Abdulla,
Katika kipindi hiki cha mpito kuelekea katiba mpya,wazanzibari wanajikuta katika JAHAZI ya safari ya mwisho kutoka Dar-es-salaam kurudi Unguj.Wakiikosa safari hii, basi ,wataula na chua kwa uvivu wa kuchagua.Tanzania-bara au Tanganyika, katika kipindi hiki cha mpito hadi sherehe za miaka 50 za Muungano mwaka 2014 ,wanajiandaa kukamilisha ajenda yao ya mwisho -ajenda ya 5 itakayo kamilisha KUIMEZA ZANZIBAR na kuifanya MKOA WA PWANI wa Tanzania. Mkakati huu ulitungwa lini na ipi ilikua ajenda ya kwanza ?
AJENDA I:
Ni pale Mwalimu Julius Nyerere ,kama Mwenyekiti wa TANU kati ya miaka ya 1956-7,alipofunga safari hadi Zanzibar akibeba ujumbe wa kuunganisha iliokua African Association (Jumuiya ya Waafrika) na Shirazi Association (Jumuiya ya Washirazi) .
Mwalimu na chama chake cha TANU, walitambua kwamba ,kwa idadi ndogo ya Wazanzibara wakati ule kule Zanzibar ,kamwe wasigeweza kushika mpini na kuongoza Zanzibar ili kutimiza ajenda iliopangwa. Mwalimu anasemekana aliziambia Jumuiya hizo mbili kama hamtaungana,Waarabu watatawala hapa daima..Kwa njia hii,Mwalimu alisimamia kuundwa kwa chama cha AFRO-SHIRAZI PARTY. Sheikh Karume akiwa Rais na Sheikh Thabit Kombo katibu wake.
AJENDA 2:
Kwa kuunda Ushirikiano kati ya TANU na Afro-Shirazi Party,AJENDA ya pili , ni Kuunda MUNGANO wa Tanganyika na Zanzibar baada ya Uhuru ambao Tanganyika ikitumai, ungeangukia mikononi mwa Afro-Shirazi Party.
Mambo yalipokwenda kombo na uhuru Desemba 10,1963, ulipoingia mikononi mwa wapinzani wao ZNP/ZPPP, shabaha hii ilibidi ifikiwe kupitia MAPINDUZI ya Januari 12, 1964.Historia ya mapinduzi na wapi yalipikwa na nani walishiriki, imeandikwa kwa mapana na marefu na Dr.Harith Ghasani katika kitabu chake KWAHERI UKOLONI,KWAHERI UHURU.
Mara tu baada ya mapinduzi yalioungoa utawala wa Sultani, Mwalimu alianza kupiga hodi mlangoni mwa Sheikh Karume kuulizia juu ya Muungano ? Sheikh Karume alibisha kwanza kuitikia hodi na akisema Sisi ndio kwanza tumekuwa Jamhuri changa baada ya kujikomboa. Ni mapema kuzungumzia Muungano.
April, 1964 shinikizo la Mwalimu lilizidi ; na akiungwamkono na dola kuu za Magharibi zilizoiona Zanzibar ni kitisho (Communist Menance) Afrika Mashariki na ( Mecca ya kiislamu ) , Mwalimu alitimiza Ajenda ya pili.
Ushawishi wa kikoministi Mwalimu aliudhibiti kwa kuwadhibiti wanamapinduzi wa Zanzibar aliowaleta Tanzania-Bara : Abdulrahman Babu aliekua waziri wa nje na biashara alimfanya tu waziri wa mipango ya uchumi chini yake . Katibu wake wa Umma party au (Chicom ) neno waliotumia Marekani kuwaita wafuasi wa Umma party-yaani Chinese communists-Dr.Salim ,akapelekwa nje Balozi na baadae Umoja wa Mataifa. Col.Ali Mahfoudh,alihamihiwa bara baadae Msumbiji.
Kuiua Zanzibar kama Mecca ya Uislamu, Mwalimu alitumia kawa la KUONDOSHA UWARABU NA USULTANI. Kwani, angelitumia KUUPIGA VITA UISLAMU, washirika wake Afro-Shirazi wangengamua. Vedeo za Ustaadh Illunga za hivi karibuni zinafunua kawa.
AJENDA 3:
KUIDHOFISHA ZANZIBAR KIELIMU NA KIUCHUMI NA KUMUACHIA MZEE KARUME WAKWEZI NA WAKULIMA TU: Aliwachukua wasomi wengi wa Zanzibar na kuwafungulia mlango Tanzania-bara.Wizara zisizokuwa za muungano kama Habari na Utalii wakapewa Wazanzibari na wakazipokea bila kutanabahi mtego waliowekewa.Sheikh Idris Abdul-wakil akawa waziri wa habari .Sheikh Hasnu Makame, waziri wa Utlii.
Zote hizo mbili si wizara za Muungano. Wazanzibari wengine waliokimbia utawala wa vitisho vya kimapinduzi,walipokewa kwa raha mustarehe Dar-es-salaam.Wapemba wakajitanua kibiashara na kuisahau Pemba. Kila mzanzibari aliambiwa Tanzania-bara ni njema ,atakae aje.
Muda haukupita,Mwalimu akadai Nipe-ni kupe.Watanganyika nao wafunguliwe mlango kuingia Zanzibar bila vizuwizi na Zanzibar, mwishoe , ikaitikiabila ya kutanabahi kwamba, ule ulikua mtego wa Mwalimu. Kwani, Wazanzibari milioni 1.2 wanaweza wote leo kuhamia Bara bila kuathiri mila,utamaduni au uchumi wake. Lakini, wakiingia Wamasai 100.000 tu Zanzibar na Pemba, baada ya mwongo 1 tu,mila na utamduni na hata dini itaathirika.
Hali ya Uchumi wa Zanzibar na Maendeleo yake kwa jumla, ni mbaya.Zanzibar imerudi nyuma miaka 47. Nchi ya kwanza iliokuwa na umeme Afrika Mashariki, leo kiza kimetanda. Hadi miezi 3 ilikosa umeme mwaka jana.Maji yamekuwa haba. Ule mkakati : Ili kuwa na Tanzania imara, lazima uwe na Zanzibar dhaifu,ungali unfanya kazi. Ni hapa ndipo kipo kielezo :KWANINI ZANZIBAR HAIWACHWI KUNEEMEKA NA MAFUTA AU NA GESI YAKE.Kwani ,kuiachia, kutachafua Ajenda ya 3 ya kuiua kiuchumi na kitaalamu ilioanzia kunyakuliwa akiba yake ya 11% ya mtaji wake kutoka bodi ya sarafu ya iliokua Afrika Mashariki na kutiwa BOT.
AJENDA 4:
Wakati kisiwa kilichokua safu ya mbele kielimu na shina la dini ya kiislamu kusini mwa Afrika -Jangwa la sahara,leo kimerudi nyuma,chini ya Ajenda ya 4: Watoto wa Wazanzi-bara wamepelekwa bara na kwengineko kusoma katika vyuo vikuu na vyenginevyo na wanarudi sasa kushika hatamu za uongozi visiwani. Angalia mwenyewe sekta zote- serikalini, Jeshini,Radio na TV ,bandarini nikitaja sekta chache tu. Ni Wazanzibara hawa ndio mwishoe ,wakamilishe AJENDA ya 5:
AJENDA 5:
KUIMEZA KABISA ZANZIBAR:MFUMO NI SERA YA CCM:KUTOKA SERIKALI 2 KWENDA 1:
Mwishoe,Zanzibar itaangukia kuwa MKOA WA PWANI pamoja na Tanga na Dar-es-salaam chini ya mfumo wa Shirikisho.
Fununu ziliwahi kuchomoza kuhusu kitabu cha aliekuwa waziri-mkuu chini ya Mwalimu:Jaji Warioba kupendekeza mfumo huo.
Fununu zinadai hizo ndizo AJENDA 5 wenzetu wameziandaa kutumaliza. Lakini kuna ule usemi It takes two to tango.Mpira sasa uko katika lango la viongozi wetu na hasa watoto wa Afro-Shirazi Party kuliokoa jahazi lisizame au kuliachia lizame kabisa.Kipindi hiki cha mpito hadi katiba mpya imtungwa na kupitishwa,ni kipindi cha kuamua HATIMA ya Zanzibar na utaifa wake.
Ikiwa wazanzibari sasa hawakuamka ,hawataamka tena,kwan, kishada kitakua kimeshaenda ARIJOJO 2014 tutakapokuwa na katiba mpya tukiadhimisha miaka 50 ya Muungano au ya kumezwa. Wasia wangu leo ni huu: Hakuna tena Uafro-shirazi wala uHizbu.Hakuna U-ccm wala U-Cuf. Zanzibar ikitoweka; na tumeshaambiwa tangu na Waziri-mkuu Pinda na majuzi hata na FIFA kuwa si nchi ,historia ya miaka 2000 ya dola la ZENJ itakuja kutuhukumu . CCM-ZANZIBAR lakini, itabeba jukumu zaidi kwani, ndio ilioshika mpini tanmgu 1964.
Katika kipindi hiki cha mpito kuelekea katiba mpya,wazanzibari wanajikuta katika JAHAZI ya safari ya mwisho kutoka Dar-es-salaam kurudi Unguj.Wakiikosa safari hii, basi ,wataula na chua kwa uvivu wa kuchagua.Tanzania-bara au Tanganyika, katika kipindi hiki cha mpito hadi sherehe za miaka 50 za Muungano mwaka 2014 ,wanajiandaa kukamilisha ajenda yao ya mwisho -ajenda ya 5 itakayo kamilisha KUIMEZA ZANZIBAR na kuifanya MKOA WA PWANI wa Tanzania. Mkakati huu ulitungwa lini na ipi ilikua ajenda ya kwanza ?
AJENDA I:
Ni pale Mwalimu Julius Nyerere ,kama Mwenyekiti wa TANU kati ya miaka ya 1956-7,alipofunga safari hadi Zanzibar akibeba ujumbe wa kuunganisha iliokua African Association (Jumuiya ya Waafrika) na Shirazi Association (Jumuiya ya Washirazi) .
Mwalimu na chama chake cha TANU, walitambua kwamba ,kwa idadi ndogo ya Wazanzibara wakati ule kule Zanzibar ,kamwe wasigeweza kushika mpini na kuongoza Zanzibar ili kutimiza ajenda iliopangwa. Mwalimu anasemekana aliziambia Jumuiya hizo mbili kama hamtaungana,Waarabu watatawala hapa daima..Kwa njia hii,Mwalimu alisimamia kuundwa kwa chama cha AFRO-SHIRAZI PARTY. Sheikh Karume akiwa Rais na Sheikh Thabit Kombo katibu wake.
AJENDA 2:
Kwa kuunda Ushirikiano kati ya TANU na Afro-Shirazi Party,AJENDA ya pili , ni Kuunda MUNGANO wa Tanganyika na Zanzibar baada ya Uhuru ambao Tanganyika ikitumai, ungeangukia mikononi mwa Afro-Shirazi Party.
Mambo yalipokwenda kombo na uhuru Desemba 10,1963, ulipoingia mikononi mwa wapinzani wao ZNP/ZPPP, shabaha hii ilibidi ifikiwe kupitia MAPINDUZI ya Januari 12, 1964.Historia ya mapinduzi na wapi yalipikwa na nani walishiriki, imeandikwa kwa mapana na marefu na Dr.Harith Ghasani katika kitabu chake KWAHERI UKOLONI,KWAHERI UHURU.
Mara tu baada ya mapinduzi yalioungoa utawala wa Sultani, Mwalimu alianza kupiga hodi mlangoni mwa Sheikh Karume kuulizia juu ya Muungano ? Sheikh Karume alibisha kwanza kuitikia hodi na akisema Sisi ndio kwanza tumekuwa Jamhuri changa baada ya kujikomboa. Ni mapema kuzungumzia Muungano.
April, 1964 shinikizo la Mwalimu lilizidi ; na akiungwamkono na dola kuu za Magharibi zilizoiona Zanzibar ni kitisho (Communist Menance) Afrika Mashariki na ( Mecca ya kiislamu ) , Mwalimu alitimiza Ajenda ya pili.
Ushawishi wa kikoministi Mwalimu aliudhibiti kwa kuwadhibiti wanamapinduzi wa Zanzibar aliowaleta Tanzania-Bara : Abdulrahman Babu aliekua waziri wa nje na biashara alimfanya tu waziri wa mipango ya uchumi chini yake . Katibu wake wa Umma party au (Chicom ) neno waliotumia Marekani kuwaita wafuasi wa Umma party-yaani Chinese communists-Dr.Salim ,akapelekwa nje Balozi na baadae Umoja wa Mataifa. Col.Ali Mahfoudh,alihamihiwa bara baadae Msumbiji.
Kuiua Zanzibar kama Mecca ya Uislamu, Mwalimu alitumia kawa la KUONDOSHA UWARABU NA USULTANI. Kwani, angelitumia KUUPIGA VITA UISLAMU, washirika wake Afro-Shirazi wangengamua. Vedeo za Ustaadh Illunga za hivi karibuni zinafunua kawa.
AJENDA 3:
KUIDHOFISHA ZANZIBAR KIELIMU NA KIUCHUMI NA KUMUACHIA MZEE KARUME WAKWEZI NA WAKULIMA TU: Aliwachukua wasomi wengi wa Zanzibar na kuwafungulia mlango Tanzania-bara.Wizara zisizokuwa za muungano kama Habari na Utalii wakapewa Wazanzibari na wakazipokea bila kutanabahi mtego waliowekewa.Sheikh Idris Abdul-wakil akawa waziri wa habari .Sheikh Hasnu Makame, waziri wa Utlii.
Zote hizo mbili si wizara za Muungano. Wazanzibari wengine waliokimbia utawala wa vitisho vya kimapinduzi,walipokewa kwa raha mustarehe Dar-es-salaam.Wapemba wakajitanua kibiashara na kuisahau Pemba. Kila mzanzibari aliambiwa Tanzania-bara ni njema ,atakae aje.
Muda haukupita,Mwalimu akadai Nipe-ni kupe.Watanganyika nao wafunguliwe mlango kuingia Zanzibar bila vizuwizi na Zanzibar, mwishoe , ikaitikiabila ya kutanabahi kwamba, ule ulikua mtego wa Mwalimu. Kwani, Wazanzibari milioni 1.2 wanaweza wote leo kuhamia Bara bila kuathiri mila,utamaduni au uchumi wake. Lakini, wakiingia Wamasai 100.000 tu Zanzibar na Pemba, baada ya mwongo 1 tu,mila na utamduni na hata dini itaathirika.
Hali ya Uchumi wa Zanzibar na Maendeleo yake kwa jumla, ni mbaya.Zanzibar imerudi nyuma miaka 47. Nchi ya kwanza iliokuwa na umeme Afrika Mashariki, leo kiza kimetanda. Hadi miezi 3 ilikosa umeme mwaka jana.Maji yamekuwa haba. Ule mkakati : Ili kuwa na Tanzania imara, lazima uwe na Zanzibar dhaifu,ungali unfanya kazi. Ni hapa ndipo kipo kielezo :KWANINI ZANZIBAR HAIWACHWI KUNEEMEKA NA MAFUTA AU NA GESI YAKE.Kwani ,kuiachia, kutachafua Ajenda ya 3 ya kuiua kiuchumi na kitaalamu ilioanzia kunyakuliwa akiba yake ya 11% ya mtaji wake kutoka bodi ya sarafu ya iliokua Afrika Mashariki na kutiwa BOT.
AJENDA 4:
Wakati kisiwa kilichokua safu ya mbele kielimu na shina la dini ya kiislamu kusini mwa Afrika -Jangwa la sahara,leo kimerudi nyuma,chini ya Ajenda ya 4: Watoto wa Wazanzi-bara wamepelekwa bara na kwengineko kusoma katika vyuo vikuu na vyenginevyo na wanarudi sasa kushika hatamu za uongozi visiwani. Angalia mwenyewe sekta zote- serikalini, Jeshini,Radio na TV ,bandarini nikitaja sekta chache tu. Ni Wazanzibara hawa ndio mwishoe ,wakamilishe AJENDA ya 5:
AJENDA 5:
KUIMEZA KABISA ZANZIBAR:MFUMO NI SERA YA CCM:KUTOKA SERIKALI 2 KWENDA 1:
Mwishoe,Zanzibar itaangukia kuwa MKOA WA PWANI pamoja na Tanga na Dar-es-salaam chini ya mfumo wa Shirikisho.
Fununu ziliwahi kuchomoza kuhusu kitabu cha aliekuwa waziri-mkuu chini ya Mwalimu:Jaji Warioba kupendekeza mfumo huo.
Fununu zinadai hizo ndizo AJENDA 5 wenzetu wameziandaa kutumaliza. Lakini kuna ule usemi It takes two to tango.Mpira sasa uko katika lango la viongozi wetu na hasa watoto wa Afro-Shirazi Party kuliokoa jahazi lisizame au kuliachia lizame kabisa.Kipindi hiki cha mpito hadi katiba mpya imtungwa na kupitishwa,ni kipindi cha kuamua HATIMA ya Zanzibar na utaifa wake.
Ikiwa wazanzibari sasa hawakuamka ,hawataamka tena,kwan, kishada kitakua kimeshaenda ARIJOJO 2014 tutakapokuwa na katiba mpya tukiadhimisha miaka 50 ya Muungano au ya kumezwa. Wasia wangu leo ni huu: Hakuna tena Uafro-shirazi wala uHizbu.Hakuna U-ccm wala U-Cuf. Zanzibar ikitoweka; na tumeshaambiwa tangu na Waziri-mkuu Pinda na majuzi hata na FIFA kuwa si nchi ,historia ya miaka 2000 ya dola la ZENJ itakuja kutuhukumu . CCM-ZANZIBAR lakini, itabeba jukumu zaidi kwani, ndio ilioshika mpini tanmgu 1964.