ziwa nyasa wote upo Malawi

lukme

Senior Member
Apr 18, 2012
191
24
habari kutoka vyombo mbalimbali za kitaifa na kimataifa ikiwapo CNN wamedaiwa kutumia repoti zao kuonyesha kuwa ziwa lote la Nyasa lipo Malawi.
my take. Hawa wasituzingue tuwe tayari kulinda mpaka wetu
 
habari kutoka vyombo mbalimbali za kitaifa na kimataifa ikiwapo CNN wamedaiwa kutumia repoti zao kuonyesha kuwa ziwa lote la Nyasa lipo Malawi.
my take. Hawa wasituzingue tuwe tayari kulinda mpaka wetu

CNN ni chombo cha kichochezi ulimwenguni akiwa na wenzake wanne nyuma yake, kwa hiyo jhawanishangazi kwa maneno yao maana nsiyo kazi waliyonayo katika dunia. Kugombanisha majirani kwao siyo tatizo maana wanaambiwa nini waseme na nini wasiseme
 
Kwani tamko la Amiri Jeshi mkuu LOWASSA la kuivaa Malawi limeishia wapi tena?
 
Mngurumo aliotoa Lowassa ndio uliohitajika sana kwa mazingira haya ndio, kauli ya amiri jeshi mkuu wa ukweli: yale ndio maneno angetamka Nyerere. Mtu kudai sehemu ya ardhi yako sio jambo la mchezo na hakuna chombo chochote cha kimataifa kinachokingia kifua mtu yoyote anayetaka kumega ardhi ya mwingine. Hilo ni la kwetu kulisemea kwa ukali wote na hata tukiingia vitani hakuna wa kutuuliza. Alichosema EL ndicho cha kueleweka kwa wananchi, kwa huyo anayechokoza na kwa mataifa mengine pia. EL alitoa kauli ile kwa kuwa alijua hakuna mwenye ujasiri wa kuito msimuone hana akili yule ni kamanda. Mtu na haki zako utaanzaje kujipatanishapatanisha mwenzio kachukua msimo na wewe toa mimacho chukua msimamo. Walioko pembeni wakiona joto limeenda juu sana watakuja na agenda za upatanishi lakini sio kuanza na kujipatanisha wewe mwenyewe. Hata Malawi wanajua hatuko serious ndio mana wanakomalia hoja. Wao wanadai sisi tunawataka radhi wapunguze munkar mambo gani hayo ya kihuni kabisa.
 
Hawa wanataka tupigane wapate mahali pa kuuzia silaha zao zilizowadodea

Nyinyi c mmekataa kuwatambua na kuwapa haki zao mashoga, mwenzenu Joyce kakubali sa' kwanini vyombo habar vya magharib visimsapoti?
 
cnn.tbc.bbc.skynews. wanatofautiana nini?
Tofauti ipo sana

*CNN ni taasisi binafsi na inawatumikia zaidi wamerekani.

*BBC ni taasisi ya umma Uingereza na iko kwa maslahi ya waingereza.

*SKY ni taasisi binafsi ya uingereza na inatetea zaidi uingereza.

*TBC ni kipeperushi cha magamba, inayomwaga Propaganda za CCM usiku na mchana tena za kichochezi na inachukiwa na watu wengi nchini Tanzania.
 
nahc wewe ni mamluk. au wewe ni msupport ushoga

yeah you are right. africa ilikuwa moja. walioigawa huko Berlin wamegawa ziwa nyasa lote ni la nyasa land ambayo ndio malawi ya sasa. sheria ya kuwa iwapo nchi mbili zinatenganishwa na mpaka wa maji basi kila nchi ichukue nusu hapa hai apply. kwani original yake ndio hivyo. na tunalijua hilo lakini tunataka kuleta ubabe tu.
lake nyasa yote ni ya wamalawi. hata ukiukana ukweli kiasi gani ukweli utabakia pale pale.
Mungu ibariki Tanzania
 
Tofauti ipo sana

*CNN ni taasisi binafsi na inawatumikia zaidi wamerekani.

*BBC ni taasisi ya umma Uingereza na iko kwa maslahi ya waingereza.

*SKY ni taasisi binafsi ya uingereza na inatetea zaidi uingereza.

*TBC ni kipeperushi cha magamba, inayomwaga Propaganda za CCM usiku na mchana tena za kichochezi na inachukiwa na watu wengi nchini Tanzania.
Zote ni sawa kwa mtizamo kuwa vyombo vyoote hivyo vinaeneza propaganda za FREEmasons au illumanati
 
Jamani minahisi kama ile sigara ya amani ina karibia kuzikaaaa au wana jamvi nyi mna onaje?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom