Well Said Zitto. Hapa nakubaliana na ww kwa kiasi kikubwa kwenye ishu ya mikataba. Mambo mengine "No Comment"
Sasa unaposema unakubaliana na Zitto kuhusu mikataba unakubaliana nae nini? Zitto katika jibu lake kwa hoja ya Mbwambo kuhusu DHIHAKA yake anasema yeye anataka kuwa mikataba iwe wazi [ transparent] lakini mkumbuke kuwa ni Zitto huyu huyo aliyesema hatua ya Porf. Muhongo kutaka kuipitia mikataba ya gesi ingewakatisha tamaa na kuwatisha wawekezaji!! Sasa tujiulize je kuipitia hii mikataba sio kuiweka wazi kwa wananchi?
Tukumbuke kuwa kuipitia hii mikataba kwa bodi kama alivyoagiza waziri kunafaida ya kutuwezesha kujua wapi tulipotoka kwenye mikata iliyopita ili tusirudie makosa hayo kwenye mikataba ijayo!! Sio lazima kuwa unapoipitia upya mikataba na ukagundua mapungufu [ mapungufu ya makusudi ya mafisadi ili watu wapate 10% wanazoficha USWISI] hayo mapungufu yatarekebishwa kama tulivyojifunza kwenye mikataba ya madini kuwa ukisha ingia mikataba hii ni lazima uheshimu sheria za kimataifa!! Tanapozungumzia dhana ya kuwa wazi kwa mikataba sio maana yake kila mmoja wetu atapata nafasi ya kuisoma bali wale wawakilishi wetu wakiwa ni wajumbe wa bodi husika au kamati za bunge zenye wajumbe wazalendo na wenye weledi wao wanaweza kuwakilisha jamii katika kukagua na kuona kama mikataba inakidhi matakwa ya jamii yetu.
Hivyo basi kitendo cha Muhongo kuwapa wajumbe wa bodi adidu za rejea za kuipitia ile mikataba ya gesi haitawakatisha tamaa wawekezaji kwa sisi kunufaika nayo kwani wao wanazihiitaji maliasili zetu kwa manufaa yao kama sisi tunavyowahitaji wao ,hivyo ni lazima tunegotiate nao from a strong position badala ya kuwa wanyonge!!