Zitto: Unawezaje kuwa na mabombadia, maSRG, madremliner unashindwa kuwa na vifaa vya kuokoa wanyonge?

Nimekuambia ili mpinzani upate nafasi ya kuonyesha uwezo wako ni lazima ujinyenyekeze na sio kila mtu anaweza hilo. Huyo Kitila Mkumbo anafahamika kwa tabia ni mtu wa kunyenyekea ili apate maisha. Halafu substance inapimwa na mamlaka hizi zilizojaa utashi wa kisiasa? Hivi Phillipo unadhani haya yanayofanyika hapa nchini huwa sisi ni vipofu na wala hatuoni utashi wa maamuzi ukoje? Kama kweli huyo Kitila alikuwa anaamini kwenye upinzani bali uwezo wake ndio ulivutia mamlaka, alikuwa na ulazima gani wa kuhamia ccm kama hakuwa pandikizi tu?
Kama una uwezo kichwani halafu kiburi kimekujaa maana yake huwa uwezo wako ni bora ukabaki nao.

Kama una uwezo kichwani halafu unatawaliwa na chuki au jeuri ya kufa na tai shingoni, basi tambua kuwa wanaosomeshwa kwa sasa kati yao wanaweza kuwa na akili kuliko wewe, hivyo ni bora ufe tu na elimu yako.
 
CCM mganga mliyempa msimuache.
Leo inaonekana viongozi wa upinzani wanatafuta kiki kupitia huu msiba.
KWELI UCHAWI UPO.
 
Bukillo mi napendaga mtu ambae akija na hoja aje na data sio mtu anaekurupuka kwa jazba au mihemko au mahaba.umeisikiliza speech yake akiongea leo au jana trh 21? Google isikilize youtube ndipo ujue Elimu yake ya majanga anaitumia kulisaidia Taifa au lah.
Ni muendelezo wa siasa zile zile. Alishawahi kukaa na wataalam wa sekta na akawapatia hiyo elimu yake aliyonayo?.

Alishaomba nafasi ya kutoa ushauri na akanyimwa?. Ni kazi nyepesi sana kuita waandishi wa habari wakiwa na kamera zao halafu saa mbili usiku mtu akaonekana akiongelea jambo fulani.
 
Mkiambiwaga kabla ya majanga wajinga mnaziba masikio au hukusikia yule mBunge wa Ukerewe
alivyokuwa analalamikia Meli mbovu kuna kipi mlifanya mmesubiri mpaka watu wafe...na hata Taa mmeshindwa kuwanazo jinga nyie
Mkuu hivi karibuni umezinduliwa mradi wa ujenzi wa meli pale ziwa victoria. Tatizo letu mnafikiria kuwa serikali ni kila kitu.

Mnasahau kuwa nchi hii ina mikoa mingi tu yenye changamoto nyingi tu zenye kuhitaji fedha nyingi tu. Umakini ukiwekwa kwenye meli za ziwa victoria, basi hamkawii kusema awamu hii inapendelea eneo fulani. Umakini ukihamishiwa sehemu nyingine hamkawii kusema serikali imeisahau kanda fulani,

Ukubwa ni jalala, kila mtu huja na kutupa takataka zake.
 
Wee jamaa inaonekana una kitambi kilichojaa kinyesi kingi maana umehara sana hapa illa hamna point uliyoongea. Coment ndefu ila point sifuri.

Asante sana

Hata hivyo, ingependeza kwako wewe kwa kidogo ulicho - chana uoneshe hoja (point) yako.

Lakini bahati mbaya sana kwako, umeishia kuandika kwa kutumia lugha ya vijiwe vya wavuta unga na sigara kubwa kuonesha kuwa you belong there, na unahitaji msaada wa ushauri nasaha kuijua lugha ya majadiliano!!

Pole sana
 
Hapa mkuu mnamuonea bure,ilibidi aanzie mahali,
Unanunua ndege,mapesa yakiwa mengi,ndio unanunua vifaa bora vya kuokolea,mkitaka anunue kila kitu tunachokiitaji,hatutaweza,uwezo mdogo,hata hawa wapinzani wanajua,
Mbona wao wanalipwa mamilioni ya pesa baada ya miaka mitano bungeni,kuliko mtumishi aliyefanya kazi kwa miaka 30,hapa Zito hatasema.
Mbunge analipwa 200milioni,wakati mwalimu mashahara wake wa mwezi,ni posho ya Mbunge ya siku moja,mbona hili Zito hulisemi?huyu dogo nae ni mnafiki tu,wakati mwingine.
Hebu hatuambie kuna tija gani kuwa na wabunge 365,kwa nchi kama TZ,kwanini tusiwe na wabunge 50 tu,hapa hawa wanasiasa hutawasikia wakisema,kwa sababu ni maslahi yao.
Hapo ndio huwa na muelewa Mkuu Maghu,anapowatumia Wasiojurikana wawashughurike wanaolopoka lopoka.
 
Mkuu hivi karibuni umezinduliwa mradi wa ujenzi wa meli pale ziwa victoria. Tatizo letu mnafikiria kuwa serikali ni kila kitu.

Mnasahau kuwa nchi hii ina mikoa mingi tu yenye changamoto nyingi tu zenye kuhitaji fedha nyingi tu. Umakini ukiwekwa kwenye meli za ziwa victoria, basi hamkawii kusema awamu hii inapendelea eneo fulani. Umakini ukihamishiwa sehemu nyingine hamkawii kusema serikali imeisahau kanda fulani,

Ukubwa ni jalala, kila mtu huja na kutupa takataka zake.

Bukililo

Ofkoz, serikali si kila kitu. Hilo linaeleweka vyema na ndiyo maana kuna PPP..

Je, kwa kutambua kuwa yenyewe (serikali) siyo kila kitu na kuna maeneo mengi yanayohitaji kuhudumiwa, ni kwa nini tusitumie PPP kuruhusu watu binafsi wa invest ktk eneo hili pia?

Mimi nadhani ipo shida kwenye SERA na MIPANGO yetu na madhara yake ni haya!

Na kwa upande wa serikali yenyewe ktk yale inayoweza kuyafanya kwa wakati uliopo na kwa kutumia raslimali fedha kidogo ilizonazo, ina tatizo la kupanga na kuchagua cha kufanya (yaani priorities)

Wakati huo huo bado mambo mengi yanafanyika kwa misingi ya "upofu" wa manufaa ya kisiasa za sasa na wakati ujao. Whether tunapenda kuambiwa haya ama hatupendi, huu ndiyo ukweli wenyewe!
 
Kama unafikiri Tanzania ilipigana vita 35 yrs ago basi kuna walakini na uraia wako, ningekushauri uanze na JKT kwanza kuielwa hii nchi. Kuzaliwa pekee sio shinikizo la kuwa raia mwenye kuijuwa nchi yake.

Narudia tena, vita pekee tulivyopigana vya kulinda mipaka yetu ni vya Iddi Amini wa Uganda kuanzia 1979-1981 kwa kumbukumbu zangu. Toka hapo hakujawahi kutokea vita vingine vya kulinda mipaka yetu. Piga mahesabu uone ni miaka mingapi halafu pata picha mwanajeshi aliyejiunga 1983 kama amewahi pigana vita zaidi ya mazoezi magumu ya kijeshi. Kama vipo vuta zaidi ya hivyo vitaje na tulipigana na nani na ni mwaka gani. Hivyo vingine ni operations mbalimbali kama mchango wetu kwa UN au AU, na hapa huenda wanajeshi wachache sana.
 
Kama una uwezo kichwani halafu kiburi kimekujaa maana yake huwa uwezo wako ni bora ukabaki nao.

Kama una uwezo kichwani halafu unatawaliwa na chuki au jeuri ya kufa na tai shingoni, basi tambua kuwa wanaosomeshwa kwa sasa kati yao wanaweza kuwa na akili kuliko wewe, hivyo ni bora ufe tu na elimu yako.

Hicho kiburi unadhani ni cha upande mmoja? Kiburi ni cha pande zote.
 
Narudia tena, vita pekee tulivyopigana vya kulinda mipaka yetu ni vya Iddi Amini wa Uganda kuanzia 1979-1981 kwa kumbukumbu zangu. Toka hapo hakujawahi kutokea vita vingine vya kulinda mipaka yetu. Piga mahesabu uone ni miaka mingapi halafu pata picha mwanajeshi aliyejiunga 1983 kama amewahi pigana vita zaidi ya mazoezi magumu ya kijeshi. Kama vipo vuta zaidi ya hivyo vitaje na tulipigana na nani na ni mwaka gani. Hivyo vingine ni operations mbalimbali kama mchango wetu kwa UN au AU, na hapa huenda wanajeshi wachache sana.

Na Mimi nakwambia huijuwi Tanzania, nenda jeshini ukajifunze medali walizo nazo wabajeshi wa Tanzania ni wamezipata kwenye vita zipi. Mimi siko hapa kutoa siri za nchi hii eti kwasababu kuna kijaba fulani ambaye hataki kulipigania hili taifa afaidije. kama ni mtanzania na unauchungu na hii nchi basi tafuta hizo taarifa. Nimekushauri anza na JKT.
 
Nchi zenye akili huwa na viongozi wenye akili na mipango ya akili.
FB_IMG_1537607346707.jpeg
 
Na Mimi nakwambia huijuwi Tanzania, nenda jeshini ukajifunze medali walizo nazo wabajeshi wa Tanzania ni wamezipata kwenye vita zipi. Mimi siko hapa kutoa siri za nchi hii eti kwasababu kuna kijaba fulani ambaye hataki kulipigania hili taifa afaidije. kama ni mtanzania na unauchungu na hii nchi basi tafuta hizo taarifa. Nimekushauri anza na JKT.

Mkuu kwani walioona vita vya Uganda walienda JKT kwanza ndio wakajua vilikuwepo? Kama kuna vita vya siri wanajeshi wetu wamepigana hilo sipingi maana nimekuambia vita vingine ni operations mbalimbali. Lakini sio vita vya kulinda nchi na mipaka yetu. Sihitaji utoe hizo siri za nchi maana sio vyema kwa usalama wetu, lakini haipunguzi ukweli hivyo vita walivyopigana ukiachia vya Uganda havikuwa na hatari ya moja kwa moja ndani ya mipaka yetu. Sasa we kaa hapa ukilazimisha vita vya sirini wakati mimi nakutajia vita vilivyotuhusu moja kwa moja bila usiri usiri usiotugusa wananchi moja kwa moja.
 
Kupanga ni kuchagua, tumechagua Ndege na SGR na sio vifaa vya uokoaji, kwa sababu sisi ni positive thinkers, tunawaza mema tuu na maendeleo na sio mabaya na majanga!. Ajali ni bahati mbaya tuu!.
Kuzaliwa na na kufa ni mipango ya Mungu.
Wote waliokufa ilikuwa ndio siku yao na vifo hivyo ndivyo walivyoandikiwa na Mungu tangu siku wanazaliwa.
Poleni sana.
P
Kwa nini basi tunatenga bajeti ya madawa na vifaa tiba?
Kwa nini tunanunua magari ya zimamoto nasi ni "positive thinkers" tusio wazia wala kutegemea mabaya?
 
Back
Top Bottom