Zitto ulitumia nguvu kubwa kwenye kupinga juhudi za Serikali kwenye mapambano dhidi ya Corona. Sasa iambie dunia kuwa Tanzania sasa ni salama

Mati Mkenda

Senior Member
Mar 4, 2018
171
211
Kati ya watu wachache waliotumia nguvu kubwa sana kuzibeza juhudi zilizochukuliwa na serikali ya awamu ya tano, pamoja na wataalam wetu wa ndani katika kupambana na Ugonjwa wa Corona (COVID-19), ni ndugu yetu Zitto Kabwe. Huyu bwana kwake hakukuwa na jema lolote lililofanywa na serikali, kwani kila kilichofanywa alikibeza.

Na mara nyingi alitumia akaunti yake ya Twitter kuandika ujumbe wa kubeza ambao alikuwa akiwa-tag raia wa Mataifa mengine, na taasisi nyingine za kimataifa ambao yeye aliona kwamba wanatakiwa kujua kile alichokuwa akikisema, au wenyewe kwa nyakati tofauti waliibeza serikali yetu, hao tunaweza kuwaita ni “Accomplices” wake kwenye harakati zake hizo

Zitto alianzisha kampeni yake aliyoiita “M3 Campaign” akisema kuwa “M” hizo zinawakilisha Miguu, Mikono, na Mdomo. Kampeni yake hiyo mbali na kuwa na components za yale yaliyokuwa yanasisitizwa na serikali, lakini ilifunikwa na Mwavuli wa kupinga sehemu kubwa za yale ambayo serikali ilikuwa ikiyafanya. Ilijikita sana kuikosoa serikali hasa pale ilipofanya tathmini na kuona kuwa kwa mazingira ya nchi yetu isingekuwa vema ku-impose “LOCKDOWN” kwa wananchi wake

Zitto kila siku alisisitiza kuwa hali ni mbaya sana hapa nchini, na kuwa nchi ingeingia katika hali mbaya zaidi ikiwa ni pamoja na kutengwa na jumuiya za kimataifa

Kinachonishangaza ni kuwa baada ya Rais kutangaza kuwa sasa tunarudi kwenye mfumo mpya wa maisha, Zitto naye kimya kimya amerudi kwenye utaratibu huo. Na mbaya zaidi yale aliyokuwa akiyasisitiza kwenye kampeni yake ya M3 hakuna analolifuata hata moja kwa sasa. Yeye ndiye amekuwa mzungukaji sana, anawakusanya watu kila siku kwa makundi, anashikana nao mikono, havai barakoa n.k

Kwa nafasi yake nilitarajia ndo awe wa kwanza kuitekeleza kampeni yake, na si kuanzisha kampeni ambayo yeye mwenyewe hawezi kuiishi. Nimuombe tu ndugu yangu Zitto Kabwe awe muungwana; atumie nafasi yake hiyo tena, kuiambia dunia kuwa sasa Tanzania ni salama kwa COVID-19, na kisha awa-tag ndugu zake wale wale aliowatag upotoshaji wa awali. Tanzania ni nchi yetu sote
 
Kwani nani alipima watu Tanzania na kuthibitisha kua hakuna Corona?
 
Mara nyingine nawaza kama watu kweli wanachokiongea ndio fikra zao au basi tu wanajitoa ufahamu....

Hivi unajua kutokana na kwamba Corona inavyosambaa kwa akili yako Tanzania hakuna Corona ?

Ukweli ni kwamba Corona is not deadly... Corona haihui sana ila inaambukiza sana..., mtu mmoja unaweza kuusambaza mji mzima..., sasa kwa akili yako utakuwa haupo ?

Percent kubwa wanaopata wanaweza wasijue kama walipata mpaka wanapopona, na kama kinga zako zipo vizuri basi obviously hauta-pata shida..., kwahio kama afya yako ina gogoro usishangae wewe ukawa katika ile percent moja itakayoambiwa RIP
 
Kati ya watu wachache waliotumia nguvu kubwa sana kuzibeza juhudi zilizochukuliwa na serikali ya awamu ya tano, pamoja na wataalam wetu wa ndani katika kupambana na Ugonjwa wa Corona (COVID-19), ni ndugu yetu Zitto Kabwe. Huyu bwana kwake hakukuwa na jema lolote lililofanywa na serikali, kwani kila kilichofanywa alikibeza.

Na mara nyingi alitumia akaunti yake ya Twitter kuandika ujumbe wa kubeza ambao alikuwa akiwa-tag raia wa Mataifa mengine, na taasisi nyingine za kimataifa ambao yeye aliona kwamba wanatakiwa kujua kile alichokuwa akikisema, au wenyewe kwa nyakati tofauti waliibeza serikali yetu, hao tunaweza kuwaita ni “Accomplices” wake kwenye harakati zake hizo

Zitto alianzisha kampeni yake aliyoiita “M3 Campaign” akisema kuwa “M” hizo zinawakilisha Miguu, Mikono, na Mdomo. Kampeni yake hiyo mbali na kuwa na components za yale yaliyokuwa yanasisitizwa na serikali, lakini ilifunikwa na Mwavuli wa kupinga sehemu kubwa za yale ambayo serikali ilikuwa ikiyafanya. Ilijikita sana kuikosoa serikali hasa pale ilipofanya tathmini na kuona kuwa kwa mazingira ya nchi yetu isingekuwa vema ku-impose “LOCKDOWN” kwa wananchi wake

Zitto kila siku alisisitiza kuwa hali ni mbaya sana hapa nchini, na kuwa nchi ingeingia katika hali mbaya zaidi ikiwa ni pamoja na kutengwa na jumuiya za kimataifa

Kinachonishangaza ni kuwa baada ya Rais kutangaza kuwa sasa tunarudi kwenye mfumo mpya wa maisha, Zitto naye kimya kimya amerudi kwenye utaratibu huo. Na mbaya zaidi yale aliyokuwa akiyasisitiza kwenye kampeni yake ya M3 hakuna analolifuata hata moja kwa sasa. Yeye ndiye amekuwa mzungukaji sana, anawakusanya watu kila siku kwa makundi, anashikana nao mikono, havai barakoa n.k

Kwa nafasi yake nilitarajia ndo awe wa kwanza kuitekeleza kampeni yake, na si kuanzisha kampeni ambayo yeye mwenyewe hawezi kuiishi. Nimuombe tu ndugu yangu Zitto Kabwe awe muungwana; atumie nafasi yake hiyo tena, kuiambia dunia kuwa sasa Tanzania ni salama kwa COVID-19, na kisha awa-tag ndugu zake wale wale aliowatag upotoshaji wa awali. Tanzania ni nchi yetu sote
Serikali yako imepima watu wangapi kuanzia mwezi wa tano hadi sasa ?
 
Kati ya watu wachache waliotumia nguvu kubwa sana kuzibeza juhudi zilizochukuliwa na serikali ya awamu ya tano, pamoja na wataalam wetu wa ndani katika kupambana na Ugonjwa wa Corona (COVID-19), ni ndugu yetu Zitto Kabwe. Huyu bwana kwake hakukuwa na jema lolote lililofanywa na serikali, kwani kila kilichofanywa alikibeza.

Na mara nyingi alitumia akaunti yake ya Twitter kuandika ujumbe wa kubeza ambao alikuwa akiwa-tag raia wa Mataifa mengine, na taasisi nyingine za kimataifa ambao yeye aliona kwamba wanatakiwa kujua kile alichokuwa akikisema, au wenyewe kwa nyakati tofauti waliibeza serikali yetu, hao tunaweza kuwaita ni “Accomplices” wake kwenye harakati zake hizo

Zitto alianzisha kampeni yake aliyoiita “M3 Campaign” akisema kuwa “M” hizo zinawakilisha Miguu, Mikono, na Mdomo. Kampeni yake hiyo mbali na kuwa na components za yale yaliyokuwa yanasisitizwa na serikali, lakini ilifunikwa na Mwavuli wa kupinga sehemu kubwa za yale ambayo serikali ilikuwa ikiyafanya. Ilijikita sana kuikosoa serikali hasa pale ilipofanya tathmini na kuona kuwa kwa mazingira ya nchi yetu isingekuwa vema ku-impose “LOCKDOWN” kwa wananchi wake

Zitto kila siku alisisitiza kuwa hali ni mbaya sana hapa nchini, na kuwa nchi ingeingia katika hali mbaya zaidi ikiwa ni pamoja na kutengwa na jumuiya za kimataifa

Kinachonishangaza ni kuwa baada ya Rais kutangaza kuwa sasa tunarudi kwenye mfumo mpya wa maisha, Zitto naye kimya kimya amerudi kwenye utaratibu huo. Na mbaya zaidi yale aliyokuwa akiyasisitiza kwenye kampeni yake ya M3 hakuna analolifuata hata moja kwa sasa. Yeye ndiye amekuwa mzungukaji sana, anawakusanya watu kila siku kwa makundi, anashikana nao mikono, havai barakoa n.k

Kwa nafasi yake nilitarajia ndo awe wa kwanza kuitekeleza kampeni yake, na si kuanzisha kampeni ambayo yeye mwenyewe hawezi kuiishi. Nimuombe tu ndugu yangu Zitto Kabwe awe muungwana; atumie nafasi yake hiyo tena, kuiambia dunia kuwa sasa Tanzania ni salama kwa COVID-19, na kisha awa-tag ndugu zake wale wale aliowatag upotoshaji wa awali. Tanzania ni nchi yetu sote
Ongelea suaala la ccm wasiibe kura, polisi wasiwe upande mmoja wa siasa
Kila jambo lina muda wa kulijadiri
Hilo la Zitto lilishapita usiturudidhe nyuma
 
Ongelea suaala la ccm wasiibe kura, polisi wasiwe upande mmoja wa siasa
Kila jambo lina muda wa kulijadiri
Hilo la Zitto lilishapita usiturudidhe nyuma

Kwani umeona nimeongelea Uchaguzi hapa? Kinachoongelewa hapa ni kuwa aeleze kwa sasa hali ikoje, siyo kutukusanya tu wakati ameshatutisha.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom