Zitto: Ukweli ndege zinazonunuliwa ni mitumba wanafanya marekebisho na kuuziwa kwa bei ya mpya

Zitto mwenyewe yuko wapi? Ni mwanachama hapa JF. Tunamuomba aje hapa tujadili badala yenu watumwaji.

Kuna mambo yanaleta utoto JF. Au, Zito mwenyewe ignorance iko juu. Taarifa hii yaweza kuwa ni kweli lakini siyo kwa ushahidi huo anaouonyesha Zitto. Boeing siyo duka la mtaa wa Kongo, kariakoo. wanalinda heshima kwa nguvu zote. Sema kwamba serikali imenunua ndege zilizotumika na kudanganya ni mpya, lakini Boeing watatoa wapi ndege zilizotumika? Boeing haina shirika la usafiri! Suala la kusoma ser. # ya kioo cha ndege ni upuuzi mwingine uliozidi. Ndege au hata magari hayatengenezwi kama fanicha za Keko.

Parts za ndege na magari huundwa na makampuni mbali mbali duniani. Ukiangalia gari lako unaweza ukakuta ignition switch imetengenezwa Germany wakati gari limetoka Japan. Au hapo hapo Japan, kuna parts zinatengenezwa na makampuni maalumu nje ya kiwanda cha magari. Ser. # na tarehe inayoandikwa ni ya huko part ilikotengenezwa. Anzeni kuelewa kwamba kutegemea bunge kama kigezo cha ufahamu ni hatari.

Zitto lete ushahidi mwingine na siyo namba za kwenye vioo. That is nonsense!
So long as deals kama hizi za ununuzi wa ndege zitabaki mambo ya kufanywa na mtu na mpwa wake bila kufuata taratibu za kisheria za manunuzi, tutarajie tu taarifa kama hizi nyingi tu huko tuendako.

Mtu hawezi tu kukurupuka kununua ndege utafikiri ananunua kwa fedha zake bila kuhusisha bunge ili yapatikane mawazo ya wawakilishi wa wananchi, hii ni kinyume cha sheria..!!

Kwa mambo kama haya, ni sharti hawa wahusika waelewe kuwa huko mbele lazima watakuja waeleze siku moja wapi walipopata mamlaka ya kufanya hayo waliyofanya.
 
Mtu anaaminiwa kutokana na matendo yake. Matendo ya Magufuli toka akiwa waziri, hayamweki mahala pa yeye kuaminika hata kidogo.

Achoke kushambuliwa? Si yeye kutwa nzima anasema kelele za chura hazimzui tembo kunywa maji? Acheni excuses, kushindwa kwake na CCM kwa ujumla siyo sababu ya kushambuliwa. Kwanza, natamani mashambulizi yaongezeke; angalau iwe 30% ya watanzania. Kwenye nchi ambayo basic services ni kaput, kushambuliwa kwa kiongozi anayetumia nusu trilioni kununua ndege hakuepukiki.



Oh! Kwa hiyo Magufuli na Dotto ndiyo serikali siku hizo, siyo?



Nimekutajia sheria, ni kazi yako kuisoma na kuona shetia inasemaje.



Ukiondoa suala la sheria ya manunuzi ya umma. Pia pesa hizo hazikuidhinishwa na Bunge. Sawa na zile za ujenzi wa Chato airport. Magfuli na mpwa wake Dotto James ndiyo walioamua na kujichotea mapesa Hazina. Huku fedha zilizotengwa (na Bunge) kwa ajili ya sekta zinazomgusa mwananchi moja kwa moja zikipelekwa chini ya 30% ya kilichotengwa.

Hivyo, Bunge lilipaswa kujua na kuidhinisha. Kwani lenyewe ndilo linatuwakilisha sisi walipa kodi. Ili tuone kama wabunge wa CCM wanaweza kukubali kutenga karibu TZS 0.5T kununua ndege, huku sekta za maji, afya, kilimo na elimu zikikosa fedha za kutosha.

Vilevile kwani hujui serikali hii imejitoa kwenye OGP? Kama ana nia njema na taifa hili, kwanini anataka kufanya mambo gizani?



Hivi hiyo awamu ya nne, Magufuli hakuwa kiongozi mwandamizi, tena mjumbe wa Cabinet? Na ni chama kipi kilichokuwa kinatawala? Na hao wapigaji wamechukuliwa hatua zipi?

Hivi umesahau kuwa juzi juzi tu TZS 1.5T zimekosekana na hazijulikana zilipo na zilivyotumika? 1.5 trilioni za kitanzania! Halafu, unataka Magufuli aaminiwe kuwa ana nia njema na taifa hili.

Kumuamini Magufuli ni aidha wewe ni mjinga wa kutupwa, au unafaidika na uwepo wake.
Wastage of precious time! Unarudia hayo hayo tunayoyasikia kwa akina Zitto huko Bungeni.
 
Wastage of precious time! Unarudia hayo hayo tunayoyasikia kwa akina Zitto huko Bungeni.
Kwani ni uongo Magufuli ni fisadi na mwizi? Ripoti za CAG toka akiwa waziri zinaonyesha Magufuli ni mpigaji tu.

Andelea ku-dig na ku-ride on Magufuli. That's what opportunists like you roll.
 
Kwani ni uongo Magufuli ni fisadi na mwizi? Ripoti za CAG toka akiwa waziri zinaonyesha Magufuli ni mpigaji tu.

Andelea ku-dig na ku-ride on Magufuli. That's what opportunists like you roll.
Kwenye miradi ya Ujenzi kuna nafas nzuri ya KUPIGA
 
Kwa hiyo wewe huoni kama kutumia pesa nje ya utaratibu wa Bunge na wa sheria ya manunuzi ya umma, ni ishara ya ufisadi hapo? Tutajuaje kama pesa hazijaliwa iwapo maamuzi ya manunuzi yalifanywa na Magufuli na mpwa wake?

Serikali inawajibika kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia ruzuku, pembejeo na huduma ya ugani. Haya ni majukumu ya msingi ya serikali.

Oh! Unaweza kuweka kifungu cha Katiba kinachoonyesha badiliko hili? Kwa kuwa ninavyojua Katiba ya JMT bado imesema kuwa Tanzania inafuata siasa za ujamaa na kujitegemea.

Hamna cha bure? Mbona Magufuli anajitapa kutoa elimu bure?

Halafu pengine una uelewa mdogo juu ya mifumo ya kiuchumi na itikadi za kisiasa. Hakuna nchi ambayo inafuata ubepari au uliberali kwa asilimia 100, haswa kwenye sekta muhimu za huduma za kijamii. Nchi tunazoziita za kibepari zenyewe, hazifanyi hivyo. Ndiyo maana hadi kesho Marekani inatoa food stumps kwa watu wasio na uwezo. Inatoa ruzuku kwenye public transportation na kilimo. Nchi nyingi za Ulaya, zinatoa elimu bure hadi chuo kikuu, ruzuku kwa wakulima na usafirishaji wa umma, zinasambaza magazeti kadhaa bure ili watu wake wapate habari n.k.

Sasa, nchi ambayo bado 70% ni peasants, halafu watu kama wewe unatetea matumizi ya karibu nusu trilioni kwenye kununua ndege ambazo faida zake mpaka mzifafanue kwa kukaza shingo!! Ati kisa, Tanzania siyo nchi ya kijamaa tena.

Halafu unaji-contradict tu. Sasa kama Tanzania siyo nchi ya kijamaa tena, kwanini Magufuli anataka serikali imiliki biashara ya usafiri wa ndege?

Kujenga miundombinu ya msingi ya kusaidia watu wengi. Lakini hilo halifanyiki sasa. Budget disbursements kwenye sekta za msingi kama elimu, afya, kilimo n.k., hazikufika hata 50%, lakini kwenye kununua ndege, disbursement zilipita hata allocated budget!

Ruzuku, pembejeo na huduma za ugani pia ni miundombinu ya msingi. Lakini ndiyo hivyo tena, ndege ndiyo alama ya nchi. Tunang'ang'a kuwa na national carrier, wakati walioendelea wameshaachana na upuuzi huu.
Nzi, unayejadiliana naye ndio wale wale, unapoteza muda wako bure. Wakati wa Mkapa walimtetea kwa nguvu zao zote, akaja Kikwete wakamtetea kwa nguvu zao zote na sasa wanamtetea Magufuli kwa nguvu zao zote. Nchi ya India juzi imeachana na biashara ya ndege kwa sababu ya hasara, sisi nchi masikini wa kutupwa tunaingia kichwa kichwa! Hatujiulizi ni watu gani watakaopanda hizi ndege zetu waache za mashirika yaliyojijenga kwa miaka inayozidi hata umri wa Tanzania huru.


Twitter



Dr. Vincent Mashinji @Vicent_mashinji

Hawa wanachota maji kwa ajili ya mahitaji ya familia yao. Wakishaoga maji haya watapanda ndege ya ATCL
5:25 AM - May 26, 2018
 
Kwani ni uongo Magufuli ni fisadi na mwizi? Ripoti za CAG toka akiwa waziri zinaonyesha Magufuli ni mpigaji tu.

Andelea ku-dig na ku-ride on Magufuli. That's what opportunists like you roll.
Hao akina Zitto umejiuliza wanalipwa milioni ngapi huko Bungeni? Is it worth paying these useless noise makers? Wanakuingiza kwenye mijadala badala ya kulima nyanya ujiongezee kipato, we unalalamika kama wao wakati wanapiga 11 million! kila mwezi.

Huyo Zitto alipokuwa anazipiga za NSSF ulimsikia akimsema Kikwete?
 
Nzi, unayejadiliana naye ndio wale wale, unapoteza muda wako bure. Wakati wa Mkapa walimtetea kwa nguvu zao zote, akaja Kikwete wakamtetea kwa nguvu zao zote na sasa wanamtetea Magufuli kwa nguvu zao zote. Nchi ya India juzi imeachana na biashara ya ndege kwa sababu ya hasara, sisi nchi masikini wa kutupwa tunaingia kichwa kichwa! Hatujiulizi ni watu gani watakaopanda hizi ndege zetu waache za mashirika yaliyojijenga kwa miaka inayozidi hata umri wa Tanzania huru.


Twitter



Dr. Vincent Mashinji @Vicent_mashinji

Hawa wanachota maji kwa ajili ya mahitaji ya familia yao. Wakishaoga maji haya watapanda ndege ya ATCL
5:25 AM - May 26, 2018
US poor.jpg
 
Kwa hiyo wewe huoni kama kutumia pesa nje ya utaratibu wa Bunge na wa sheria ya manunuzi ya umma, ni ishara ya ufisadi hapo? Tutajuaje kama pesa hazijaliwa iwapo maamuzi ya manunuzi yalifanywa na Magufuli na mpwa wake?



Serikali inawajibika kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia ruzuku, pembejeo na huduma ya ugani. Haya ni majukumu ya msingi ya serikali.



Oh! Unaweza kuweka kifungu cha Katiba kinachoonyesha badiliko hili? Kwa kuwa ninavyojua Katiba ya JMT bado imesema kuwa Tanzania inafuata siasa za ujamaa na kujitegemea.

Hamna cha bure? Mbona Magufuli anajitapa kutoa elimu bure?

Halafu pengine una uelewa mdogo juu ya mifumo ya kiuchumi na itikadi za kisiasa. Hakuna nchi ambayo inafuata ubepari au uliberali kwa asilimia 100, haswa kwenye sekta muhimu za huduma za kijamii. Nchi tunazoziita za kibepari zenyewe, hazifanyi hivyo. Ndiyo maana hadi kesho Marekani inatoa food stumps kwa watu wasio na uwezo. Inatoa ruzuku kwenye public transportation na kilimo. Nchi nyingi za Ulaya, zinatoa elimu bure hadi chuo kikuu, ruzuku kwa wakulima na usafirishaji wa umma, zinasambaza magazeti kadhaa bure ili watu wake wapate habari n.k.

Sasa, nchi ambayo bado 70% ni peasants, halafu watu kama wewe unatetea matumizi ya karibu nusu trilioni kwenye kununua ndege ambazo faida zake mpaka mzifafanue kwa kukaza shingo!! Ati kisa, Tanzania siyo nchi ya kijamaa tena.

Halafu unaji-contradict tu. Sasa kama Tanzania siyo nchi ya kijamaa tena, kwanini Magufuli anataka serikali imiliki biashara ya usafiri wa ndege?



Kujenga miundombinu ya msingi ya kusaidia watu wengi. Lakini hilo halifanyiki sasa. Budget disbursements kwenye sekta za msingi kama elimu, afya, kilimo n.k., hazikufika hata 50%, lakini kwenye kununua ndege, disbursement zilipita hata allocated budget!

Ruzuku, pembejeo na huduma za ugani pia ni miundombinu ya msingi. Lakini ndiyo hivyo tena, ndege ndiyo alama ya nchi. Tunang'ang'a kuwa na national carrier, wakati walioendelea wameshaachana na upuuzi huu.
Kulikuwa na hadithi ya mbwa mwitu aliyekuwa anakunywa maji mtoni akamwona mwana kondoo naye anakunywa maji akatamani kumla. Basi akamwendea mwana kondoo yule na kumwuliza kwa nini unanichafulia maji. Mwana kondoo akajibu akisema kuwa maji ninayokunywa yanakwenda bondeni na wakati wewe uko kilimani; kwa ahiyo sikuchafulii. Mbwa mwitu kwa kuona ameshindwa akabadili swali akamwuliza kwa nini mwaka jana ulinitukana; yule mwanakondoo akamjibu kuwa mwaka jana mimi nilikuwa sijazaliwa, kwa hiyo singeweza kukutakana. Mbwamwitu akaona ameshindwa tena akabadilisha swali akasema kuwa kama wewe hukunitukana basi atakuwa ni shangazi yako hivyo ni lazima nikule wewe.

Naona sasa tunaanza kwenda nje ya mada kutafuta sababu moja moja hadi tufikie sababu ya "atakuwa ni shangazi yako." Mimi nimejibu mada iliyoletwa kuwa dreamliner hiyo ni mtumba; ndipo nikasema siyo kweli na nikafafafanu kwa kina kwa nini siyo terrible teen. Inaelekea kuwa swala la mtumba linashindikana kwa hiyo inakuja sababu nyingine ya kipaumbelea, na manunuzi ya serikali. Hayo ya kipaumbele na manunuzi ya serikali hayamo katika mada, hebu angalia tena. Order ya kunua Dreamliner iliwekwa December mwaka 2016, na ilitangazwa hadharani na kusainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Mwaka jana 2017 Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ilipitishwa na bunge. Leo hii picha za ndege hiyo zimeanza kuonekana kwenye mitandao ikiwa katika hatua za mwisho kuwa delivered ndipo lawama zinaanza; hapo ndipo sikubalini na wakosoaji wote pamoja na sababu za mbwa mwitu kuwa "kama siyo wewe basi ni shangazi yako".

Kumbuka mada yenywe ni hii

Anatujulisha Zitto Kabwe

Serikali inaficha jambo kuhusu Dreamliner 787-8, Tunaambiwa kwamba Ndege tunayonunua Boeing 787-8 Dreamliner Ndio kwanza inaundwa. Sio Kweli. Ndege hiyo iliundwa mwaka 2009 na kinachofanyika Sasa ni kubadilisha Injini yake Kwa sababu Injini za ndege hizo zilikuwa na matatizo ya kuwaka moto ( imetokea Kwa Ethiopian na Nippon Air ya Japan ). Ndege iliyoundwa mwaka 2009 leo inafanyiwa marekebisho kidogo tunauziwa bei ya ndege mpya.!!

Hata hizi Bombardier tulizonunua hazikuundwa baada ya sisi kuweka order. Ndege hizi ziliundwa mwaka 2014 na zilikuwa tayari zimenunuliwa na Kampuni ya ndege ya Kazakhstan kabla ya baadaye kuuziwa sisi. Ushahidi wa hili ni rahisi Sana, ukipanda ATCL Bombardier tafadhali soma maandishi madogo dirishani utaona S/N 0001519017-040 DATE 10/2014. Hiyo 10/2014 ni Oktoba, 2014.

Serikali inaficha jambo katika suala la ununuzi wa Ndege hii ya Dreamliner. Serikali inajua kuwa imenunua Terrible Teen Kwa bei kubwa kuliko ilivyostahili. Shirika la ndege la Boeing linajua kuwa wametupiga bei ya kuruka na kutudanganyia Kwa kubadili injini. Serikali inajua kuwa haikusimamia maslahi ya Taifa katika mazungumzo kuhusu bei.

Hapakuwa na Government Negotiation Team Kama ilivyo kawaida ya manunuzi makubwa ya namna haya. (Bunge halikuhusishwa, baraza la mawaziri halikuhusishwa, wadau wa maendeleo hawakuhusishwa). Bahati mbaya sana mazungumzo ya ununuzi wa ndege yalimhusisha Rais Magufuli na Katibu Mkuu Fedha James Doto peke yao (ambaye Lissu aliwahi kusema ni mtoto wa dada yake. Yani mtu na mjomba wake walijadiliana wakanunua ndege).

Shirika la Boeing wametumia uzoefu wetu mdogo kutupiga na Ni wajibu wa Watanzania wote Kwa kutumia mahusiano yetu yote duniani kuwataka Boeing wawajibike kwa udanganyifu wao kwetu. Boeing wanapaswa kurudisha sehemu ya Fedha yetu. Ni aibu Kwa Kampuni kubwa Kama Boeing kuiibia Nchi masikini Kama Tanzania. Watanzania mnakumbuka sakata la Radar? Hii ni kurushwa zaidi ya radar. Hela zetu zirudi tujenge Reli au kuongeza Ndege.

My uchunguzi:

Tukiangalia mashirika makubwa ya ndege yameweka order tangu 2011 inakuwaje sie tupate faster faster???

In September 2011, the 787 was first officially delivered to launch customer All Nippon Airways.[313] As of September 2017, the top three identified customers for the 787 are: All Nippon Airways with 83 orders (36 -8s, 44 -9s and three -10s), ILFC (an aircraft leasing company), with orders totaling 74 Boeing 787s (24 -8s and 50 -9s), and Etihad Airways with 71 orders (41 -9s and 30 -10s).[1]

Boeing 787 orders and deliveries by type
 
Sio kama hawajui , wanajua lakini ndege zimeuzwa jumba kuu.....wanajua kila kitu ila tumepigwa na ccm wanajua bei ndogo wamekuala hela
Nani atauliza ?
 
Hao akina Zitto umejiuliza wanalipwa milioni ngapi huko Bungeni? Is it worth paying these useless noise makers? Wanakuingiza kwenye mijadala badala ya kulima nyanya ujiongezee kipato, we unalalamika kama wao wakati wanapiga 11 million! kila mwezi.

Huyo Zitto alipokuwa anazipiga za NSSF ulimsikia akimsema Kikwete?
Same applies to Magufuli and his gang. Mfumo wa CCM ndiyo unazalisha hilo ulilolisema.
Nimeridhika na umaskini wangu. Sina haja ya kujiongezea kipato. Ninachofanya sasa ni kuonyesha kwamba hakuna namna Tanzania itaendelea kama hawa viwavi wa CCM wataendelea kutawala.
 
Hakuna ndege inayoundwa mwaka mmoja au miwili.
Kwanza wale Boeing wanatujua vizuri waTz ndio maana wameamua kuitengenezea nje kabisa ili tuanze show off ya mapicha picha. Jiulize huko ndani wameichomoa wapi.

Halafu kwa Boeing current version ni 787-10,

Sasa lazima hii ya kwetu 787-8 ni hizo ambazo hazikuwa na wateja..

Acha watubadilishie injini then watukabidhi.

Unaambiwa kuna kampuni zaidi ya 100 zipo kwenye foleni ya order za ndege Boeing na inachukua miaka 4+ kuundwa.. Tz isingepata ndege mpya saivi.

Nguo mitumba. Viatu mtumba. Hata ndege......malizia..
Viongozi kama ........
 
Kwanini manunuzi ya ndege hayajaanzia bungeni,kama ilivyo ada iwe biashara ya mtu na mjoba?
 
Kwani ni uongo Magufuli ni fisadi na mwizi? Ripoti za CAG toka akiwa waziri zinaonyesha Magufuli ni mpigaji tu.

Andelea ku-dig na ku-ride on Magufuli. That's what opportunists like you roll.

Kwani ni uongo Magufuli ni fisadi na mwizi? Ripoti za CAG toka akiwa waziri zinaonyesha Magufuli ni mpigaji tu.

Andelea ku-dig na ku-ride on Magufuli. That's what opportunists like you roll.
Mzalendo,mtetezi wa wanyonge, msemakweli...my foot. Sijui kwanini watanzania tunakubali huu ujinga.
 
View attachment 786026 Anatujulisha Zitto Kabwe

Serikali inaficha jambo kuhusu Dreamliner 787-8, Tunaambiwa kwamba Ndege tunayonunua Boeing 787-8 Dreamliner Ndio kwanza inaundwa. Sio Kweli. Ndege hiyo iliundwa mwaka 2009 na kinachofanyika Sasa ni kubadilisha Injini yake Kwa sababu Injini za ndege hizo zilikuwa na matatizo ya kuwaka moto ( imetokea Kwa Ethiopian na Nippon Air ya Japan ). Ndege iliyoundwa mwaka 2009 leo inafanyiwa marekebisho kidogo tunauziwa bei ya ndege mpya.!!

Hata hizi Bombardier tulizonunua hazikuundwa baada ya sisi kuweka order. Ndege hizi ziliundwa mwaka 2014 na zilikuwa tayari zimenunuliwa na Kampuni ya ndege ya Kazakhstan kabla ya baadaye kuuziwa sisi. Ushahidi wa hili ni rahisi Sana, ukipanda ATCL Bombardier tafadhali soma maandishi madogo dirishani utaona S/N 0001519017-040 DATE 10/2014. Hiyo 10/2014 ni Oktoba, 2014.

Serikali inaficha jambo katika suala la ununuzi wa Ndege hii ya Dreamliner. Serikali inajua kuwa imenunua Terrible Teen Kwa bei kubwa kuliko ilivyostahili. Shirika la ndege la Boeing linajua kuwa wametupiga bei ya kuruka na kutudanganyia Kwa kubadili injini. Serikali inajua kuwa haikusimamia maslahi ya Taifa katika mazungumzo kuhusu bei.

Hapakuwa na Government Negotiation Team Kama ilivyo kawaida ya manunuzi makubwa ya namna haya. (Bunge halikuhusishwa, baraza la mawaziri halikuhusishwa, wadau wa maendeleo hawakuhusishwa). Bahati mbaya sana mazungumzo ya ununuzi wa ndege yalimhusisha Rais Magufuli na Katibu Mkuu Fedha James Doto peke yao (ambaye Lissu aliwahi kusema ni mtoto wa dada yake. Yani mtu na mjomba wake walijadiliana wakanunua ndege).

Shirika la Boeing wametumia uzoefu wetu mdogo kutupiga na Ni wajibu wa Watanzania wote Kwa kutumia mahusiano yetu yote duniani kuwataka Boeing wawajibike kwa udanganyifu wao kwetu. Boeing wanapaswa kurudisha sehemu ya Fedha yetu. Ni aibu Kwa Kampuni kubwa Kama Boeing kuiibia Nchi masikini Kama Tanzania. Watanzania mnakumbuka sakata la Radar? Hii ni kurushwa zaidi ya radar. Hela zetu zirudi tujenge Reli au kuongeza Ndege.

My uchunguzi:

Tukiangalia mashirika makubwa ya ndege yameweka order tangu 2011 inakuwaje sie tupate faster faster???

In September 2011, the 787 was first officially delivered to launch customer All Nippon Airways.[313] As of September 2017, the top three identified customers for the 787 are: All Nippon Airways with 83 orders (36 -8s, 44 -9s and three -10s), ILFC (an aircraft leasing company), with orders totaling 74 Boeing 787s (24 -8s and 50 -9s), and Etihad Airways with 71 orders (41 -9s and 30 -10s).[1]

Boeing 787 orders and deliveries by type
  • b0092fe38c71e761b2180758030e866a.png
 Orders


 Deliveries


Orders and deliveries through April 2018[1][314]

Habari zaidi, soma=>Diallo amjibu Zitto kuhusu ndege mtumba Dreamliner 787-8


Sometimes ni bora kunyamaza .kwa wanaojua tunakuona mpumbavu....ni vema kupata taarifa kamili.
 
Same applies to Magufuli and his gang. Mfumo wa CCM ndiyo unazalisha hilo ulilolisema.
Nimeridhika na umaskini wangu. Sina haja ya kujiongezea kipato. Ninachofanya sasa ni kuonyesha kwamba hakuna namna Tanzania itaendelea kama hawa viwavi wa CCM wataendelea kutawala.
Pole!
 
You can say this again
Interchanged words. In english an adverb is before the verb. Alternatively, make careful use of the right punctuation mark.
So, say: You can again say this.
 
Sawa tumesikia, lkn 2020 haurudi Bungeni hata kwa mbinde, mimi nimesema, na H.Polepole pia amesema, hivyo tafuta kiki za mwisho mwisho labda utapata kazi Kikwete's foundation, au Wasafi kwa Mondi, who knows?!
Mkuu nitarudi, lakini naona kama una kaupungufu kidogo kwako...Ishu sio ZZK kuna ukweli au la ndio ulitakiwa kulizungumza...
 
Back
Top Bottom