Zitto: Ukweli ndege zinazonunuliwa ni mitumba wanafanya marekebisho na kuuziwa kwa bei ya mpya

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Screenshot_2018-05-25-16-48-54.png
Anatujulisha Zitto Kabwe

Serikali inaficha jambo kuhusu Dreamliner 787-8, Tunaambiwa kwamba Ndege tunayonunua Boeing 787-8 Dreamliner Ndio kwanza inaundwa. Sio Kweli. Ndege hiyo iliundwa mwaka 2009 na kinachofanyika Sasa ni kubadilisha Injini yake Kwa sababu Injini za ndege hizo zilikuwa na matatizo ya kuwaka moto ( imetokea Kwa Ethiopian na Nippon Air ya Japan ). Ndege iliyoundwa mwaka 2009 leo inafanyiwa marekebisho kidogo tunauziwa bei ya ndege mpya.!!

Hata hizi Bombardier tulizonunua hazikuundwa baada ya sisi kuweka order. Ndege hizi ziliundwa mwaka 2014 na zilikuwa tayari zimenunuliwa na Kampuni ya ndege ya Kazakhstan kabla ya baadaye kuuziwa sisi. Ushahidi wa hili ni rahisi Sana, ukipanda ATCL Bombardier tafadhali soma maandishi madogo dirishani utaona S/N 0001519017-040 DATE 10/2014. Hiyo 10/2014 ni Oktoba, 2014.

Serikali inaficha jambo katika suala la ununuzi wa Ndege hii ya Dreamliner. Serikali inajua kuwa imenunua Terrible Teen Kwa bei kubwa kuliko ilivyostahili. Shirika la ndege la Boeing linajua kuwa wametupiga bei ya kuruka na kutudanganyia Kwa kubadili injini. Serikali inajua kuwa haikusimamia maslahi ya Taifa katika mazungumzo kuhusu bei.

Hapakuwa na Government Negotiation Team Kama ilivyo kawaida ya manunuzi makubwa ya namna haya. (Bunge halikuhusishwa, baraza la mawaziri halikuhusishwa, wadau wa maendeleo hawakuhusishwa). Bahati mbaya sana mazungumzo ya ununuzi wa ndege yalimhusisha Rais Magufuli na Katibu Mkuu Fedha James Doto peke yao (ambaye Lissu aliwahi kusema ni mtoto wa dada yake. Yani mtu na mjomba wake walijadiliana wakanunua ndege).

Shirika la Boeing wametumia uzoefu wetu mdogo kutupiga na Ni wajibu wa Watanzania wote Kwa kutumia mahusiano yetu yote duniani kuwataka Boeing wawajibike kwa udanganyifu wao kwetu. Boeing wanapaswa kurudisha sehemu ya Fedha yetu. Ni aibu Kwa Kampuni kubwa Kama Boeing kuiibia Nchi masikini Kama Tanzania. Watanzania mnakumbuka sakata la Radar? Hii ni kurushwa zaidi ya radar. Hela zetu zirudi tujenge Reli au kuongeza Ndege.

My uchunguzi:

Tukiangalia mashirika makubwa ya ndege yameweka order tangu 2011 inakuwaje sie tupate faster faster???

In September 2011, the 787 was first officially delivered to launch customer All Nippon Airways.[313] As of September 2017, the top three identified customers for the 787 are: All Nippon Airways with 83 orders (36 -8s, 44 -9s and three -10s), ILFC (an aircraft leasing company), with orders totaling 74 Boeing 787s (24 -8s and 50 -9s), and Etihad Airways with 71 orders (41 -9s and 30 -10s).[1]

Boeing 787 orders and deliveries by type
  • b0092fe38c71e761b2180758030e866a.png
 Orders


 Deliveries


Orders and deliveries through April 2018[1][314]

Habari zaidi, soma=>Diallo amjibu Zitto kuhusu ndege mtumba Dreamliner 787-8
 

Attachments

  • upload_2018-5-25_10-31-46.png
    2.7 KB · Views: 162
Zitto mwenyewe yuko wapi? Ni mwanachama hapa JF. Tunamuomba aje hapa tujadili badala yenu watumwaji.

Kuna mambo yanaleta utoto JF. Au, Zito mwenyewe ignorance iko juu. Taarifa hii haiwezi kuwa sahihi kwa ushahidi huo anaouonyesha Zitto. Boeing siyo duka la mtaa wa Kongo, kariakoo. Wanalinda heshima kwa nguvu zote. Sema kwamba serikali imenunua ndege zilizotumika na kudanganya ni mpya, lakini Boeing watatoa wapi ndege zilizotumika? Boeing haina shirika la usafiri! Suala la kusoma ser. # ya kioo cha ndege ni upuuzi mwingine uliozidi. Ndege au hata magari hayatengenezwi kama fanicha za Keko.

Parts za ndege na magari huundwa na makampuni mbali mbali duniani. Ukiangalia gari lako unaweza ukakuta ignition switch imetengenezwa Germany wakati gari limetoka Japan. Au hapo hapo Japan, kuna parts zinatengenezwa na makampuni maalumu nje ya kiwanda cha magari. Ser. # na tarehe inayoandikwa ni ya huko part ilikotengenezwa. Anzeni kuelewa kwamba kutegemea bunge kama kigezo cha ufahamu ni hatari.

Zitto lete ushahidi mwingine na siyo namba za kwenye vioo. That is nonsense!
 
Terrible teen .........mzigo mpya ulioko sokoni kwa sasa ni 787-10 nashangaa Tanzania inaenda kununua 787-8 kama sio mtumba ni nini ? bora hata ingekuwa 787-9 maana ni za juzi juzi hii ni used imefanyiwa refurbishment tumepigwa.
 
Anatujulisha Zitto Kabwe

Serikali inaficha jambo kuhusu Dreamliner 787-8, Tunaambiwa kwamba Ndege tunayonunua Boeing 787-8 Dreamliner Ndio kwanza inaundwa. Sio Kweli. Ndege hiyo iliundwa mwaka 2009 na kinachofanyika Sasa ni kubadilisha Injini yake Kwa sababu Injini za ndege hizo zilikuwa na matatizo ya kuwaka moto ( imetokea Kwa Ethiopian na Nippon Air ya Japan ). Ndege iliyoundwa mwaka 2009 leo inafanyiwa marekebisho kidogo tunauziwa bei ya ndege mpya.!!

Hata hizi Bombardier tulizonunua hazikuundwa baada ya sisi kuweka order. Ndege hizi ziliundwa mwaka 2014 na zilikuwa tayari zimenunuliwa na Kampuni ya ndege ya Kazakhstan kabla ya baadaye kuuziwa sisi. Ushahidi wa hili ni rahisi Sana, ukipanda ATCL Bombardier tafadhali soma maandishi madogo dirishani utaona S/N 0001519017-040 DATE 10/2014. Hiyo 10/2014 ni Oktoba, 2014.

Serikali inaficha jambo katika suala la ununuzi wa Ndege hii ya Dreamliner. Serikali inajua kuwa imenunua Terrible Teen Kwa bei kubwa kuliko ilivyostahili. Shirika la ndege la Boeing linajua kuwa wametupiga bei ya kuruka na kutudanganyia Kwa kubadili injini. Serikali inajua kuwa haikusimamia maslahi ya Taifa katika mazungumzo kuhusu bei.

Hapakuwa na Government Negotiation Team Kama ilivyo kawaida ya manunuzi makubwa ya namna haya. (Bunge halikuhusishwa, baraza la mawaziri halikuhusishwa, wadau wa maendeleo hawakuhusishwa). Bahati mbaya sana mazungumzo ya ununuzi wa ndege yalimhusisha Rais Magufuli na Katibu Mkuu Fedha James Doto peke yao (ambaye Lissu aliwahi kusema ni mtoto wa dada yake. Yani mtu na mjomba wake walijadiliana wakanunua ndege).

Shirika la Boeing wametumia uzoefu wetu mdogo kutupiga na Ni wajibu wa Watanzania wote Kwa kutumia mahusiano yetu yote duniani kuwataka Boeing wawajibike kwa udanganyifu wao kwetu. Boeing wanapaswa kurudisha sehemu ya Fedha yetu. Ni aibu Kwa Kampuni kubwa Kama Boeing kuiibia Nchi masikini Kama Tanzania. Watanzania mnakumbuka sakata la Radar? Hii ni kurushwa zaidi ya radar. Hela zetu zirudi tujenge Reli au kuongeza Ndege.


Sawa tumesikia, lkn 2020 haurudi Bungeni hata kwa mbinde, mimi nimesema, na H.Polepole pia amesema, hivyo tafuta kiki za mwisho mwisho labda utapata kazi Kikwete's foundation, au Wasafi kwa Mondi, who knows?!
 
Terrible teen .........mzigo mpya ulioko sokoni kwa sasa ni 787-10 nashangaa Tanzania inaenda kununua 787-8 kama sio mtumba ni nini ? bora hata ingekuwa 787-9 maana ni za juzi juzi hii ni used imefanyiwa refurbishment tumepigwa.
Jamani jamani jamani. Kwa heshima ya jamvi kama huna utaalam na kitu usiingie kwenye mjadala. Tunaonekana kama sisi ni wapumbavu na hata hoja za maana serikali itaona kama ni walewale. Hizo boeing 787-8, 787-9 na 787-10 hazimaanishi kuna muundo wa zamani na mpya. Hizi ni model tofauti za ndege na zote bado zinatengenezwa. Japo ilianza kutengezwa 787-8, lakini hata sasa bado zinatengenzwa, hivyo huwezi kusema ndege kama ni mpya au ya mwaka huu au 2010 kwa kuangalia tu hiyo 787-8
 
Back
Top Bottom