Zitto: Tunafanya makosa kutumia fedha za ndani kujenga reli, ilitakiwa tuwekeze kwenye kilimo

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
“ Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati. Hata hivyo, Serikali ni lazima ifungue masikio kusikiliza maoni mbadala katika utekelaji wa miradi mikubwa kama hii ambayo inatumia fedha nyingi, na tumeamua kutumia fedha za ndani.

Uamuzi wa kutumia fedha za ndani ni uamuzi mchungu kwani maana yake badala ya kuwekeza kwenye miradi ya Kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na bidhaa za kuuza nje, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuongeza vyuo vikuu na vyuo vya ufundi ili kuongeza maarifa na wataalamu katika nchi yetu, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuwekeza kwenye kumaliza kabisa tatizo la mtindio wa ubongo (stuntedness) ambalo ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa kwani Watanzania 34 katika 100 wametindiwa ubongo, tumeamua kujenga reli.

Kupanga ni kuchagua. (Serikali) mmeamua kwa niaba yetu kutumia rasilimali fedha zetu kidogo kujenga Reli (na kununua ndege) na haya mengine yasubiri kwanza. Uongozi ni uamuzi. Mmeamua, hatuna namna. Lakini tusikilizeni sisi wawakilishi wa wananchi, mawazo yetu ni kusaidia kupunguza maumivu ya maamuzi yenu bila kuathiri utekelezaji wa miradi husika. Mimi binafsi ninaunga mkono uwekezaji kwenye Reli, lakini siungi mkono namna uwekezaji huu unafanywa.”

Sehemu ya Hotuba yangu Bungeni April, 2017
 
Leo tuna athari yake gunia la mahndi alfu kumi nane na mahndi enyewe hakuna
 
Hawa watu wamemnukuu alichokisema Zitto kuhusu ujenzi wa SGR mwaka 2017 kwa ku-tweet sehemu ya maneno ya Zitto ambapo alipongeza kwa kusema hilo ni jambo jema lakini akaonyesha kutounga mkono namna mradi huo unavyotekelezwa.

Ziko tweet nne za jinsi Zitto alivyoponda huu mradi kwa kuufanya ndio kipaumbele kuliko kilimo,matatizo ya watoto kudumaa,n.k.


Isingekuwa maswala ya hotliking hapa JF yanayotu-limit ku-share habari, ningeweka tweet zote nne za jinsi Zitto alivyowajibu Jamvi la Habari katika tweet yao.
 
Hawa watu wamechukua tweet moja tu ya alichokisema Zitto kuhusu ujenzi wa SGR ambapo alipongeza kwa kusema hilo ni jambo jema lakini akasema haungi mkono namna mradi huo unavyotekelezwa.

Ziko tweet nne za jinsi Zitto alivyoponda namna mradi huo unavyotekelezwa.

Isingekuwa maswala ya hotliking hapa JF yanayotu-limit ku-share habari, ningeweka tweet zote nne za jinsi Zitto alivyowajibu Jamvi la Habari katika tweet yao.
Mnafik ww

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa watu wamechukua tweet moja tu ya alichokisema Zitto kuhusu ujenzi wa SGR ambapo alipongeza kwa kusema hilo ni jambo jema lakini akasema haungi mkono namna mradi huo unavyotekelezwa.

Ziko tweet nne za jinsi Zitto alivyoponda namna mradi huo unavyotekelezwa.

Isingekuwa maswala ya hotliking hapa JF yanayotu-limit ku-share habari, ningeweka tweet zote nne za jinsi Zitto alivyowajibu Jamvi la Habari katika tweet yao.
sisi wasomi tumekuelewa mkuu .
 
Tunatakiwa tuwekeze sana kwenye kilimo ili Tanzania tufikie uchumi wa kati 2025. Hata Maprofessa nguli akina Samwel Wangwe kwenye toleo la kitabu chao cha juzi walisisitiza sana tujielekeze kwenye kilimo kama kipaumbele cha kutufikisha kwenye uchumi wa kati 2025.
 
Tunatakiwa tuwekeze sana kwenye kilimo ili Tanzania tufikie uchumi wa kati 2025. Hata Maprofessa nguli akina Samwel Wangwe kwenye toleo la kitabu chao cha juzi walisisitiza sana tujielekeze kwenye kilimo kama kipaumbele cha kutufikisha kwenye uchumi wa kati 2025.
Tatizo watanzania kila awamu mnakaririshwa vitu na wanasiasa,wawekeze nini na vipi kwenye kilimo?,ni % ngapi ya vijana na wewe ukiwemo wapo tayari kulima?,tuwe wakweli.. Kipindi cha JK ilianzishwa kitu kinaitwa KILIMO KWANZA, serikali ilikua inakopesha mpaka trekta kwa gharama nafuu sana, wangapi walienda?,leo hii unajua kuna benki ya wakulima inakopesha mpaka milioni hamsini?,tatizo hamuwajui watanzania vizuri na wanasiasa, pesa za SGR zingepelekwa kwenye kilimo hao hao kina Zitto wangelalama mazao yatapelekwaje sokoni bila usafiri wa uhakika hususani Reli.Kwanza ambaye mpaka sasa anaamini Zitto Kabwe anapigania maslahi ya mwananchi wa hali ya chini akapimwe AKILI haraka. Na huu uCCM na uCDM unawafanya vijana wengi hasa humu JF wanakuwa WAPUMBAVU na MALOFA.
 
“ Juhudi za ujenzi wa Reli ya Kati ni juhudi za kimaendeleo na hazina budi kupongezwa na kila mpenda maendeleo. Reli ina faida kubwa kwa nchi na Kiongozi yeyote anayefanya maamuzi muhimu kama haya hana budi kupongezwa kwa dhati. Hata hivyo, Serikali ni lazima ifungue masikio kusikiliza maoni mbadala katika utekelaji wa miradi mikubwa kama hii ambayo inatumia fedha nyingi, na tumeamua kutumia fedha za ndani.

Uamuzi wa kutumia fedha za ndani ni uamuzi mchungu kwani maana yake badala ya kuwekeza kwenye miradi ya Kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na bidhaa za kuuza nje, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuongeza vyuo vikuu na vyuo vya ufundi ili kuongeza maarifa na wataalamu katika nchi yetu, tumeamua kujenga reli. Badala ya kuwekeza kwenye kumaliza kabisa tatizo la mtindio wa ubongo (stuntedness) ambalo ni tatizo kubwa sana kwa nchi yetu kwa sasa kwani Watanzania 34 katika 100 wametindiwa ubongo, tumeamua kujenga reli.

Kupanga ni kuchagua. (Serikali) mmeamua kwa niaba yetu kutumia rasilimali fedha zetu kidogo kujenga Reli (na kununua ndege) na haya mengine yasubiri kwanza. Uongozi ni uamuzi. Mmeamua, hatuna namna. Lakini tusikilizeni sisi wawakilishi wa wananchi, mawazo yetu ni kusaidia kupunguza maumivu ya maamuzi yenu bila kuathiri utekelezaji wa miradi husika. Mimi binafsi ninaunga mkono uwekezaji kwenye Reli, lakini siungi mkono namna uwekezaji huu unafanywa.”

Sehemu ya Hotuba yangu Bungeni April, 2017

cc: Jingalao
 
Back
Top Bottom