Zitto: Tumemtoa Mghwira ili kuondoa dhana kwamba ACT ni "CCM B", asema utaratibu ufatwe kwenye teuzi

Evans-Arsenal

JF-Expert Member
Jan 10, 2016
868
1,385


Mbunge wa Kigoma Mh Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa ACT wazalendo amesema kwamba wameamua kumuweka pembeni mwenyekiti wao wa zamani Mama Anna Mghirwa ili kutoa dhana kwamba ACT ni CCM B.

"Sasa tunaweka kanuni ambazo mtu akichaguliwa na uongozi wa juu unaoongozwa na Chama kingine tofauti na ACT basi tufanye kwanza mazungumzo kabla ya mtu kukubali tu bila kutoa taarifa" alisema Mh Zitto Kabwe.

Pia akaongeza kwa kusema kwamba kwa sasa wameshachagua kaimu mwenyekiti wao wa Chama na anaendelea na majukumu kama kawaida.
 
Mbunge wa kigoma Mh zitto zuberi kabwe ambaye pia ni kiongozi wa ACT wazalendo amesema kwamba wameamua kumuweka mwenyekiti wao wa zamani Mama Anna Mgirwa ili kutoa dhana kwamba ACT ni CCM B Akihojiwa na mwandishi wa habari amesema hayo

Sasa tunaweka kanuni ambazo mtu akichaguliwa na uongozi wa juu unaoongozwa na Chama kingine tofauti na ACT basi tufanye kwanza mazungumzo kabla ya mtu kukubali tu bila kutoa taarifa alisema Mh Zitto Kabwe.

Pia akaongeza kwa kusema kwamba Kwa sasa wameshachagua kaimu mwenyekiti wao wa Chama na anaendelea na majukumu kama kawaida.

ndio maana me na chadema yangu tu.maana kipindi zito anaenguliwa M4C. watu walimlaumu mbowe kumbe zito ccm b.leo imeonekana na ninavyojua ubunge atakosa safari hii
 
ndio maana me na chadema yangu tu.maana kipindi zito anaenguliwa M4C. watu walimlaumu mbowe kumbe zito ccm b.leo imeonekana na ninavyojua ubunge atakosa safari hii
Na yeye amepinga kwamba wao ni ccmB
 
Kwa hiyo mama Anna alipopata taarifa za uteuzi, fasta akakubali bila kumtaarifu "mkuu wa chama". Imagine huyu alikuwa mwenyekiti wa Taifa. Sijui hali itakuwaje siku hao juniors wengi wakipewa shavu.

Zitto anajidanganya tu. Hata waweke kanuni za namna gani, hawa wapinzani njaa wakipewa deal. suala la " kushauriana" na uongozi litakuja baadae baada kwanza ya kukubali teuzi
 
Kwa hiyo mama Anna alipopata taarifa za uteuzi, fasta akakubali bila kumtaarifu "mkuu wa chama". Imagine huyu alikuwa mwenyekiti wa Taifa. Sijui hali itakuwaje siku hao juniors wengi wakipewa shavu.

Zitto anajidanganya tu. Hata waweke kanuni za namna gani, hawa wapinzani njaa wakipewa deal. suala la " kushauriana" na uongozi litakuja baadae baada kwanza ya kukubali teuzi
Vp na lissu akipewa una maana hatokataa!!!
 
Yawezekana kuteuliwa kwake isiwe hoja. Hoja ninayoiona hapo ni yeye kukubali uteuzi haraka haraka bila kuwajulisha wenzake mpaka wanapata habari kupitia magazeti/mitandao. Hivi wewe mama ukitumbuliwa utakuwa mgeni wa nani huko ACT
Mkuu hiyo ni Siasa. Haiwezekani yule Mama akubali uteuzi bila kumwarifu Zitto. Hiyo ni cover up ya ACT na hasa Kiongozi wake Mhe Zitto. Hii taarifa aliyoitoa sasa imeharibu kuliko maelezo yote yaliyotangulia na inatoa twashira zaidi kwamba lile jina walikopewa la CCM B linaweza likawa linaukweli zaidi.
Kwanini Zitto anajaribu kujikosha wakati alishajisifia kuwa ACT ni Chama cha watu Makini na Rais asisite kwenda kivuna tena ? Nashangaa Zitto kujifanya hakujia?! Ukweli ni kuwa wanasiasa wengi wako kwa maslahi binafsi kwa hiyo fursa ikijitokeza hawatiacha. Mama Mghwira asisakamwe bure!
 
Zitto naye anapapatua kisiasa., nakumbuka hiki chama kilipoanzishwa usajili wake ulifanyika haraka sana kwa Msajili hakukua na kusubirisubiri walipewa usajili faster ambapo jambo hili ukilinganisha na yanayotokea ni coincidence.

Lakini jengine Zitto alipofukuzwa chadema kule Mahakamani upande wa jamuhuri ulifanya kila liwezekanalo Zitto ashinde kesi. Hiki chama sioni tofauti sana na ADC kule Zanzibar chama cha HR.
 
bora katiba ibadirishwe viwepo vyama viwili tu kama marekani kama tukienderea kuwa hivi tuta subiri sana na ccm kuondoka madarakani itabaki stori tu vikiwepo vyama viwili maendereo yatakuja haraka
 
Kabwe bwana, angeteuliwa yeye angeyasema haya? Sasa alitaka mama huyo hafanye nini kwani Rais anapo appoint mtu anashauriana naye kama anakubali au la? Nawambieni huyo mama angefanya makosa ya kuongea na Kabwe kwanza hasingemuruhusu sana sana Kabwe angehitisha vyombo vya habari na kuanza kukandia Chama tawala, I salute a lady 4 taking a bold step.
 
Mbunge wa kigoma Mh zitto zuberi kabwe ambaye pia ni kiongozi wa ACT wazalendo amesema kwamba wameamua kumuweka pembeni mwenyekiti wao wa zamani Mama Anna Mgirwa ili kutoa dhana kwamba ACT ni CCM B Akihojiwa na mwandishi wa habari amesema hayo

"Sasa tunaweka kanuni ambazo mtu akichaguliwa na uongozi wa juu unaoongozwa na Chama kingine tofauti na ACT basi tufanye kwanza mazungumzo kabla ya mtu kukubali tu bila kutoa taarifa" alisema Mh Zitto Kabwe.

Pia akaongeza kwa kusema kwamba Kwa sasa wameshachagua kaimu mwenyekiti wao wa Chama na anaendelea na majukumu kama kawaida.


ZZK saa yoyote atateuliwa kwenye nafasi za uongozi! Mzee anaendelea kummulika kama alivyowamulika Kitila na Anna Mgwira!! ACT itabaki inaning'inia kama tambara, na wanachama wake sio wataenda wapi maana watabaki wakiwa kwa sababu familia haina baba wala mama! Too sad..... Chezea kila kitu lakini sio "pesa" aisee. Hata mimi kwa hali ya sasa, nikiitwa napokea cheo na unafiki wangu, maana hakuna namna tena!!
 
Mbunge wa kigoma Mh zitto zuberi kabwe ambaye pia ni kiongozi wa ACT wazalendo amesema kwamba wameamua kumuweka pembeni mwenyekiti wao wa zamani Mama Anna Mgirwa ili kutoa dhana kwamba ACT ni CCM B Akihojiwa na mwandishi wa habari amesema hayo

"Sasa tunaweka kanuni ambazo mtu akichaguliwa na uongozi wa juu unaoongozwa na Chama kingine tofauti na ACT basi tufanye kwanza mazungumzo kabla ya mtu kukubali tu bila kutoa taarifa" alisema Mh Zitto Kabwe.

Pia akaongeza kwa kusema kwamba Kwa sasa wameshachagua kaimu mwenyekiti wao wa Chama na anaendelea na majukumu kama kawaida.

Hicho anachosema hakisaidii, swali ni kuwa Tanzania kuna vyama vingi vya upinzani kwa nini Magufuli arudi mara mbili kuchukua wateule wake kwenye chama kimoja tu cha upinzani?Kwa hiyo hilo ni tawi la CCM.
 
Back
Top Bottom