Zitto: Suala la Palestine, Sahara Magharibi na kusimamia wanyonge ni Msingi muhimu kulindwa

Zitto

Former MP Kigoma Urban
Mar 2, 2007
1,562
10,880
Mchango wa Maandishi wa ndg. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mb kwenye makadirio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


  1. Sisi si Tanzania ya Nyerere, Ni Tanzania Mpya, Tanzania Mbaya - Inayokalia Kimya Mauaji ya Kinyama ya Wapalestina, na Kusapoti Waonevu

[Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika,


Msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa Israel na Palestine unaelezwa vizuri sana na nukuu hii ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa Mwaka 1967 na ndio umekuwa Msingi wa Sera yetu ya Mambo ya Nje kwa miaka mingi kabla ya utawala wa sasa wa CCM mpya.


“[......] Tanzania’s position. We recognize Israel and wish to be friendly with her as well as with the Arab nations. But we cannot condone aggression on any pretext, nor accept victory in war as a justification for the exploitation of other lands, or government over other peoples.”


Kwamba Tanzania inaitambua Israel na inapenda kuwa na urafiki nayo pamoja na urafiki na mataifa mengine ya kiarabu. Lakini hatuwezi kukalia kimya uvamizi kwa namna yeyote ile. Pia ushindi vitani hauhalalishi unyonyaji dhidi ya ardhi ya wengine au dhidi ya Serikali za watu wengine. Msingi huu unaendana kabisa na dhamira ya sasa ya Sera ya Mambo nje. Hata hivyo hali ni tofauti kabisa. Mambo tunayoyafanya kwenye sera yetu ya Mambo ya Nje yanamfanya Mwalimu Nyerere ageuke huko kaburini kwake. Nitaeleza kwa mifano.


Mheshimiwa Spika,


Oktoba 26, 2016 kulikuwa na kikao cha wajumbe wa Nchi 21 zinazounda ‘Kamati ya Urithi wa Dunia’ ya UNESCO - Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, kupiga kura ya kupitisha makubaliano ya kuridhia kuupa hadhi ya Urithi wa Dunia Mji wa Jerusalem pamoja na moja ya majengo ya mji huo (Temple Mount), na kufungamanishwa na uasili wake na si hali ya sasa inayotokana na uvamizi wa Israel juu ya eneo hilo la lililoko Jerusalem Mashariki (lililovamiwa mwaka 1967 na mpaka leo kutambuliwa na UN kama eneo la Palestina, ambao wanauona ndio Mji Mkuu wa nchi ya Palestina iwapo makubaliano ya ’Two States Solution’ yatafikiwa).


Tanzania ilikuwa ni mjumbe wa Kamati hiyo ya nchi 21, na kwa mshangao wa wengi duniani, ilipiga kura kuzuia Azimio hilo, na kutaka azimio ‘Laini’ zaidi kwa Israel. Nchi marafiki zetu wa asili kule Umoja wa Mataifa (UN) ambazo nazo ni wajumbe wa kamati ile, kama Cuba, Vietnam na Angola zilipiga kura kuunga mkono azimio hilo, zikitushangaa mno kwa utetezi wetu kwa Israel ambao haukutarajiwa, hasa ikiwa msimamo wetu kama nchi siku zote umekuwa ni kutambua Jerusalem Mashariki kama eneo la Wapalestina ili kupata muafaka wa nchi mbili.


Sisi ACT Wazalendo tulihoji juu ya jambo hili linalokwenda kinyume na Sera ya Nje ya Nchi yetu. Msimamo wa Tanzania ni kukubaliana na UN kupinga uvamizi wa eneo hilo uliofanywa na Israel. Serikali ilitoa majibu mepesi tu, tena pembeni, kuwa upigaji kura ule haukuwa msimamo rasmi wa nchi yetu, ni ukiukwaji wa sera yetu ya mambo ya nje, na kuwa ni jambo ambalo Afisa wetu kwenye mkutano ule wa UNESCO alilifanya kwa makosa, na hivyo hatua zingechukuliwa dhidi yake.


Ni dhahiri majibu hayo yalikuwa ni ghiliba tu, matukio ya karibuni yameonyesha kwa uwazi sura mpya ya Taifa letu, pamoja na msimamo mpya wa Sera yetu ya mambo ya nje. Kwenye Diplomasia matendo ya nchi huwa na maana zaidi kuliko maneno ya wanadiplomasia wake. Matendo yetu yafuatayo ya karibuni yameonyesha kuwa Tanzania hatuisapoti tena Palestina:


1. Baada ya kuwaangusha Wapalestina kule Paris kwenye Mkutano wa UNESCO, Serikali iliahidi kuwa ingemchukulia hatua Afisa yule wa Wizara ya Mambo ya Nje aliyekwenda kinyume na Sera yetu ya Mambo ya Nje, hatujafanya hilo, zaidi tumempandisha cheo na kumteua kuwa Balozi wetu wa Ankara, Uturuki. Jambo hilo linaonyesha kuwa tulimtuma Balozi Elizabeth Kiondo apige kura namna ile kule UNESCO, na sasa tumempa cheo zaidi kwa kazi njema aliyoifanya. Jambo hili linaonyesha kuwa kwa sasa tunawaunga mkono Waisrael, na hatuko tena na Wapalestina.


2. Kwa sasa tumeamua kufungua ubalozi wetu Israel, Tel Aviv, kuongeza uchungu kwenye Kidonda, tukachagua wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel katika ardhi ya Taifa la Palestina kuzindua ubalozi wetu huo. Jambo hili linafanyika kukiwa na tuhuma kuwa hata huo Ubalozi unagharamiwa na Israel yenyewe, ndio maana tumepangiwa hata kipindi cha kuufungua. Kidiplomasia kuufungua ubalozi wetu katika wakati huu ni kuazimisha uvamizi wa Israel katika ardhi ya Palestina. Maana tulikuwa na uwezo wa kuchagua wakati mwengine wowote kufanya uzinduzi wa ubalozi wetu, lakini kwa kuwa aliyegharamia uwepo wa ubalozi huo (Israel) alitaka tuufungue wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel kwa Palestina, ilitubidi tufanye hivyo. Jambo hilo limeonyesha kuwa kwa sasa hatuungi mkono tena utu (Palestina) bali tunamtumikia Kila mwenye kitu (Israel).


3. Wakati akiwa ziarani Israel, Balozi Mahiga alifika sehemu ya miji inayokaliwa kimabavu na Israel ambayo inapakana na Ukanda wa Gaza. Na baadaye alihojiwa na Televisheni ya Taifa ya Israel, ambako alionyesha tu masikitiko yake kwa Waisrael wanaokaa maeneo hayo kwa kusumbuliwa na mashambulizi ya Hamas. Lakini hakulaani kabisa uendelezaji wa Israel kujenga makazi kwenye maeneo hayo ya uvamizi kama Wanadiplomasia wengine wa nchi zenye msimamo wa ‘Two States Solution’ kama sisi wanavyofanya. Balozi Mahiga mwanadiplomasia mzoefu na mbobezi, Kutokulaani kwake makazi yale haramu ni jambo la makusudi kabisa, si bahati mbaya. Ni kitendo cha kutuma salamu kwa Wapalestina kuwa tunaunga mkono uendelezaji makazi wa Israel katika maeneo hayo iliyoyavamia.


4. Tanzania imetajwa na vituo mbalimbali vya habari vya Kimataifa kuwa ni katika nchi 33 ambazo zilihudhuria ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, Mei 14, kilele cha maazimisho ya miaka 70 tangu uvamizi wa Israel katika maeneo ya Wapalestina. Chanzo cha taarifa ya Tanzania kuhudhuria ni Serikali ya Israel, ikitaja nchi ilizozialika na zilizohudhuria. Serikali yetu inasema inapinga uwepo wa Ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, lakini hapo hapo inatajwa kuhudhuria uzinduzi huo. Picha tunayoitoa hapa kwa Wapalestina ni kuwa tunaunga mkono jambo hili la ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem.


5. Siku ya uzinduzi huo wa ubalozi wa nchi ya Marekani mjini Jerusalem, Jeshi la Israel liliwaua kwa risasi zaidi ya watu 54 wa Palestina, wakiwemo wanawake, watoto, walemavu na hata wanahabari. Nchi mbalimbali duniani zimelaani mauaji hayo. Nchi ya Afrika ya Kusini imekwenda mbali zaidi kwa kumrudisha nyumbani Balozi wake aliyeko Israel. Sisi Tanzania tulioikomboa Afrika Kusini tumekaa kimya, tumeshindwa hata kutoa kauli ya kulaani mauaji hayo. Kuhudhuria kwetu ufunguzi wa ubalozi na kukaa kimya juu ya mauaji hayo kunaonyesha tumewaacha rasmi Wapalestina.


Mambo hayo matano yanaonyesha kuwa sisi si tena ile Tanzania ya Mwalimu Julius Nyerere, sisi kwa sasa ni Tanzania Mpya (kama yasemavyo matangazo ya Ikulu yetu) - Tanzania mpya inayosimama na Waonevu wa dunia, Wauaji na Wavunja haki za wanyonge. Sisi si tena Tanzania ya kusimama na wanyonge, bali ni Tanzania ya kusimama na Wanyongaji kwa sababu ya maslahi ya kiuchumi.


Si ile Tanzania iliyoongoza Ukombozi wa Bara la Afrika kutoka kwenye makucha ya Ukoloni, bali ni Tanzania Mpya inayounga mkono na kushabikia ukoloni na Uvamizi. Sisi si ile Tanzania yenye msimamo mkali tuliyolipinga Taifa kubwa la Marekani dhidi ya Uvamizi wake kwa wanyonge wa taifa la Vietnam, bali sasa ni Tanzania mpya ya kuunga mkono Uvamizi wa Taifa onevu la Israel kule Palestina. Sisi si Tanzania ile iliyoitetea China ipate nafasi na kiti chake stahili kule UNO, bali sasa sisi ni Tanzania mpya inayowaacha watu wa Palestina bila utetezi wa hadhi, kiti na nafasi yake stahili kule UNESCO.


Sisi si ile Tanzania huru tena ya Mwalimu Nyerere, iliyowaheshimu watu na mataifa kwa sababu ya Utu wao na kuamini kwamba binaadam wote ni sawa. Sasa sisi ni Tanzania mpya, inayowapa heshima watu kwa sababu ya kitu inachotuhonga, tukiuza usuli wa Utaifa wetu kwa maslahi machache ya kifedha au kiuchumi.


Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau. Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.


  1. Kujengewa Uwanja wa Mpira na Msikiti Visiifanye Tanzania Iikumbatie Morocco na Kuacha Kuiunga Mkono Sahara Magharibi

[Sehemu ya Pili ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Bado niko kwenye Sera ya mambo ya nje ya nchi yetu, si hii ya Tanzania mpya, bali ile Tanzania ya tangu wakati wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ya kusimama na wanyonge. Wakati tulipoamua kufuata ‘Diplomasia ya Uchumi’ bado msingi wetu huu wa kusimama na wanyonge ulibaki pale pale. Ndio maana wakati wa Rais Ben Mkapa na Jakaya Kikwete bado tulibaki kuwa ni sauti ya mataifa yanayoonewa kama Cuba (tukipinga vikwazo vya Marekani dhidi yao), Palestina na Sahara Magharibi.


Msingi huo wa kusimama na wanyonge ni muhimu zaidi kwa chama chetu cha ACT Wazalendo, ndio maana tulipinga ujio wa Mfalme wa Morocco hapa nchini Oktoba 23 - 25, 2016. Kwa kuwa Taifa hilo bado linaikalia kimabavu ardhi ya wanyonge wa Sahara Magharibi. Ndio msingi pia wa kutangaza wazi mahusiano yetu rasmi na Chama cha cha siasa na ukombozi wa Taifa hilo cha Polisario kinachopigania Uhuru wa nchi ya Sahara Magharibi.


Umoja wa Afrika (AU) uliamua kukubali ombi la Morocco kurudi bila masharti kwenye jumuiya hiyo. Ikimbukwe kuwa kwa zaidi ya miaka 33 Morocco haikuwa na mahusiano na jumuiya hiyo (tangu OAU mpaka sasa AU) baada ya kujitoa kwa kupinga OAU kuitambua Sahara Magharibi kama Taifa huru na kupewa kiti rasmi ndani ya OAU mwaka 1984.


Uamuzi wa OAU wa kuiruhusu Sahara Magharibi Kuwa mwanachama wa Umoja huo ulitokana na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice - ICJ) ya mwaka 1975 iliyopinga madai ya Morocco kuwa ina mahusiano ya kihistoria na kisheria na Sahara Magharibi (na hivyo kuitawala kinguvu) na kutoa haki ya kujitawala kwa Taifa hilo.


Tunaheshimu maamuzi yale mkutano wa AU wa Januari 2017, ulioirudisha Morocco kwenye AU. Lakini tabia za Taifa hilo onevu bado hazijabadilika, ni muhimu tulieleze bunge masuala yafuatayo ili liweke msimamo wake kwa Serikali juu ya kuminywa kwa watu wa Sahara Magharibi:


1. Kikao cha AU cha Januari 28 - 29, 2018 kiliazimia kuwa Morocco iruhusu Kamati Maalum ya Uangalizi ya AU iende kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo inayakalia kimabavu ili kuja kuijulisha AU hali ya mambo ilivyo.


2. Machi 29, 2018 Morocco iliwajulisha UN juu ya kutoruhusu waangalizi wowote wa AU kwenda kwenye maeneo yote ya Sahara Magharibi inayoyakalia.


3. Tangu mwaka 1991 Morocco imetumia mbinu, hila, na uzandiki ili kuzuia Tume ya Umoja wa Mataifa kwaajili ya Kura ya Maoni ya Uhuru wa Sahara Magharibi (MINURSO) kufanya kazi yake kwenye maeneo inayoyakalia kimabavu ya Sahara Magharibi. Siku za karibuni, Umoja wa Mataifa, UN ulipitisha azimio namba 2414 (2018) la kuongeza muda wa mamlaka, uahai na madaraka ya (MINURSO) kwa miezi sita. Morocco imepinga jambo hilo na kutishia kufanya mashambulizi ya kijeshi kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo yameshakombolewa (Liberated Zones).


4. Bado Morocco inaendeleza uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam kwa watu wote wa Sahara Magharibi wanaodai Uhuru wao.


5. Kurudishwa kwa Morocco kwenye AU kulienda pamoja na Taifa hilo kuridhia ‘AU Constitutive Act’ inayoyataka mataifa ya Afrika kuheshimu maazimio ya AU na hata yale ya UN yanatolewa kwa ushirikiano na AU. Lakini kwa matendo yake tuliyoyaainisha hapo juu ni dhahiri kuwa Morocco haitaki usuluhishi na Sahara Magharibi, bado inataka kuitawala na kuikalia kimabavu, bado Morocco inataka kuendelea kuwa mkoloni. Ndio maana imekataa hata kumpa ushirikiano msuluhishi wa mgogoro huu, ndugu Horst Köhler, Rais wa zamani wa Ujerumani


6. Matendo ya Serikali yetu kwa sasa yanaonyesha hatuna msimamo kwenye mambo ya msingi ya kidiplomasia, namna tulivyoenenda kwenye mahusiano yetu na wanyonge wa Palestina ni mfano hai, sasa tukijali vitu kuliko utu kama ilivyo zamani.


Hivyo basi, nataka kulishawishi Bunge lako litoe muongozo kwa Serikali juu ya kuenenda kwenye hili jambo la Morocco na Sahara Magharibi, ili kuzuia ahadi ya kujengewa Uwanja na Msikiti na Serikali ya Morocco (Vitu) isitufanye tu waache ndugu zetu Wanyonge wa Sahara Magharibi.


Nchi yetu ni kimbilio la Nchi ya Sahara, Serikali yetu chini ya Mwalimu Nyerere ililitambua Taifa la Sahara Magharibi tangu siku za mwanzo kabisa za harakati zao, ndio maana wanao Ubalozi hapa nchini. Kumuenzi baba wa Taifa na kulinda misingi ya Taifa letu ni lazima tusimame na watu wa Sahara Magharibi, na tusiwatupe kama tulivyofanya kwa watu wa Palestina.


Naliomba Bunge liibane Serikali ili itoe ahadi hiyo hapa Bungeni, pamoja na kuitaka Serikali kutumia ushawishi wake kule AU na UN kuibana Morocco iruhusu kura ya maoni ya kuamua mustakabali wa watu wa Sahara Magharibi kama ilivyoridhiwa kwenye Azimio la UN.


Viva Sahara Magharibi

Viva Polisario

Mungu Ibariki Afrika


  1. Hakuna Diplomasia Bila Wanadiplomasia: Tuna Uhaba Mkubwa wa Watumishi Kwenye Balozi Zetu

[Sehemu ya Tatu ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Msingi wa tano wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania unatutaka tushirikiane kikamilifu na Nchi, Mashirika pamoja na Taasisi mbalimbali katika nyanja za Diplomasia, Siasa, Uchumi, Utaalam na Teknolojia. Wizara hii ina jukumu la kubuni na kusimami utekelezaji wa misingi yote ya Sera yetu ya Mambo ya Nje.


Pia Wizara hii pia ina jukumu la kusimamia na kuratibu mahusiano kati ya Tanzania na nchi pamoja na mashirika mbalimbali. Utimizaji wa jambo hilo unafanyika kupitia balozi zetu zilizotapakaa kwenye nchi mbalimbali ulimwenguni. Kwa sasa ufanisi wetu ni mkubwa kwa sababu ya uhaba wa watumishi kwenye balozi zetu mbalimbali duniani.


Kwa wastani ukimuondoa Balozi, kila kituo cha Ubalozi wetu nje ya nchi kinapaswa kuwa na Mhasibu, mtu wa TISS na pamoja na Mwanadiplomasia (FSO). Vituo vingi vya balozi zetu havina kabisa Maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Wale wachache waliokuwepo awali walirudishwa nchini kwa sababu mbalimbali (ikiwemo kumaliza muda wao wa utumishi Nje ya Nchi). Tumerudisha watu bila kupeleka mbadala wao.


Kwenye balozi zetu mbalimbali watendaji hasa wa kazi za Kibalozi na kidiplomasia ni hawa maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Sasa kwa uhaba huu tunawezaje kufanya Diplomasia ya nchi yetu? Hiyo Diplomasia ya Uchumi tunafanyaje bila kuwa na hao Wanadiplomasia?


Nitatoa tu mfano wa balozi zetu chache ulimwenguni. China, nchi ambayo ni mshirika wetu mkubwa kidiplomasia na kiuchumi, hatuna kabisa FSO huko, labda ndio sababu mauzo yetu kwenda China yameshuka mno, maana biashara ya nje ni Diplomasia, sasa wakati Spika unamtaka ndugu yangu Mwijage asafiri, ni nani atakayemuandalia hiyo mikutano ya kupata wawekezaji huko China kama hatuna FSO hata mmoja? Wenzetu Uganda wana FSO’s 8 huko China, Kenya na Sudan wao wanao 9 Kila mmoja.


Nchi nyengine ambayo hatuna kabisa FSO ni Ethiopia - Makao Makuu ya AU, utaona tunavyodharau nafasi yetu katika Afrika. Pia hatuna FSO Afrika Kusini, nchi rafiki na moja ya zenye uchumi mkubwa Afrika, hatuna kabisa FSO Ujerumani - Nchi kubwa zaidi kiuchumi katika Umoja wa Ulaya (EU). Hata India ambako tangu Bunge lianze wabunge tunalalamikia kukosa soko la mbaazi kutoka huko nako hatuna FSO hata mmoja. Tumeufanya kuwa ubalozi wa kupokea wagonjwa tu.


Nchi za Brics (ukiondoa China, India na Afrika Kusini ambazo hatuna kabisa FSO’s) zilizobaki, Brazil na Urusi tuna FSO mmoja mmoja tu. Hata DRC Congo - Nchi ambayo zaidi ya theluthi moja ya mizigo ya Transit inayopita kwenye bandari ya Dar inatoka, nayo tuna FSO mmoja tu tofauti na watatu ilivyozoeleka. Kenya - Nchi ya Afrika Mashariki tunayofanya nayo biashara zaidi nayo ina FSO mmoja tu.


Hali iko hivyo karibu katika balozi zetu nyingi ulimwenguni. FSO’s ndio maafisa hasa waliofundwa na kupikwa kutekeleza Sera yetu ya mambo ya Nje. Foreign Service Officers (FSO’s) ndio diplomats (wanadiplomasia wetu). Kama hawapo vituoni, na hatuwatumii maana yake hatufanyi diplomasia, na kwa kuangalia mbali tunaua diplomasia yetu.


Mimi sitapitisha bajeti hii mpaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itakaponihakikishia kuwa itapeleka Maafisa wa Diplomasia (FSO’s) katika vituo ambavyo hatuna kabisa na pia kuwaongeza katika vile vituo ambavyo wako wachache.


Tunasimama na Iran na Qatar, Uonevu Dhidi Yao Si Sawa - Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


Tunasimama na Iran na Qatar - Uonevu Dhidi Yao Si Sawa. Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


[Sehemu ya Nne na ya Mwisho ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Jambo la mwisho kwenye mchango wangu ni juu ya hali ya ulinzi na usalama duniani. Usiku wa kuamkia Disemba 9, 2017, tulipoteza askari wetu 14 na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa huko DRC Congo, wakiwa kwenye Jeshi la kulinda Amani la Umoja wa Mataifa. Nachukua nafasi hii kuwaombea kwa Mola awalaze pema, pamoja na kutoa pole kwa familia zao na kwa Jeshi zima la JWTZ.


Taifa letu linachangia pakubwa katika kulinda amani ya ulimwengu, wanajeshi wetu wakaiwa karibu katika nchi nane duniani. Naamini tunao wajibu kama Taifa kusaidia uwepo wa amani Ulimwenguni ili kuzuia nchi zilizo kwenye machafuko kama DRC Congo kuongezeka na askari wetu wa kulinda amani kupotea.


Tayari, katika siku za karibuni, dunia imeshughudia maafa makubwa ya vita nchini Libya (ambako Rais Kikwete ni msuluhishi), Iraq, Afghanistan, Somalia, Syria, Sudan Kusini na Yemen. Mwenendo wa migogoro na uonevu unofanyika Qatar na unaotaka kufanyika Iran unapaswa kukemewa mapema ili kuchochea amani ulimwenguni, hasa eneo la mashariki ya kati ambalo tayari limeharibiwa na vita.


Hotuba ya Waziri ya Bajeti ya Wizara hii kwa mwaka 2016/17 ilibeba pongezi kwa nchi za Iran, Marekani, China, Urusi, UN na Umoja wa Ulaya (hasa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani) kwa makubaliano ya Nyuklia ya yaliyoiondolea vikwazo Iran kwa masharti ya kutoendeleza urutubishaji wa nyuklia. Makubaliano yale ni muhimu kwa kuwa iliondoa hali ya mashaka iliyokuwa imetanda duniani.


Tumeona Marekani imejitoa kwenye makubaliano hayo, na kutishia kuweka vikwazo vipya kwa Iran. Huku wajumbe wengine wa wakiendelea kubaki kwa kuwa bado Iran imeendelea kutekeleza makubaliano husika, na kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki, IAEA ni kuwa bado Iran inafuata masharti ya makubaliano husika.


Uamuzi huu wa Marekani si mzuri, unarudisha hali ya mashaka kwenye eneo la mashariki ya kati, ni uonevu dhidi ya Iran, hasa kwa kuwa IAEA imethibitisha kuwa Iran haina makosa. Ni maamuzi ya uonevu tu na usiochochea amani, ni uamuzi unaopaswa kupingwa. Serikali yetu iitumie nafasi yake kule UN kupinga uamuzi huu, na kuitaka Marekani kurudi kwenye makubaliano haya ili kudumisha amani.


Pia Julai 26, 2017 Wizara hii ilitoa taarifa yake juu ya mgogoro wa nchi za Ghuba (GCC), baada ya hatua ya nchi nne za Saudi Arabia, UAE, Bahrain na Misri kuiwekea vikwazo vya anga, bahari na ardhini nchi ya Qatar. Msimamo wa Serikali ni kuunga mkono upatanishi unaongozwa na Amir wa Kuwait, Sheikh Sabah Al-Jaber, tunaunga mkono msimamo huo.


Lakini bado pia sisi ACT Wazalendo tunasimamia tamko letu la kupinga uonevu dhidi ya Qatar tulilolitoa July 24, 2017. Kwa karibu miezi 10 sasa watu wa Qatar wamewekewa vikwazo vya kiuchumi na kiusafiri, kwenye anga, ardhi na bahari na nchi hizo nne jirani, jambo hilo si sawa, hasa kwa kuwa masharti yaliyotolewa ili kuondoa vikwazo hivyo yanaingilia uhuru wa nchi hiyo.


Tunaitaka Serikali yetu, pamoja na kusapoti usuluhishi huu wa Kuwait, itumie nafasi yake pia kule UN kuhakikisha inachangia usuluhishi wa jambo hili ili mashaka yaliyoko na vikwazo kwa Qatar viondoshwe.


Ahsanteni kwa Kunisikiliza. Naomba Kuwasilisha


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018
 
Mchango wa Maandishi wa ndg. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mb kwenye makadirio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


  1. Sisi si Tanzania ya Nyerere, Ni Tanzania Mpya, Tanzania Mbaya - Inayokalia Kimya Mauaji ya Kinyama ya Wapalestina, na Kusapoti Waonevu

[Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika,


Msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa Israel na Palestine unaelezwa vizuri sana na nukuu hii ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa Mwaka 1967 na ndio umekuwa Msingi wa Sera yetu ya Mambo ya Nje kwa miaka mingi kabla ya utawala wa sasa wa CCM mpya.


“[......] Tanzania’s position. We recognize Israel and wish to be friendly with her as well as with the Arab nations. But we cannot condone aggression on any pretext, nor accept victory in war as a justification for the exploitation of other lands, or government over other peoples.”


Kwamba Tanzania inaitambua Israel na inapenda kuwa na urafiki nayo pamoja na urafiki na mataifa mengine ya kiarabu. Lakini hatuwezi kukalia kimya uvamizi kwa namna yeyote ile. Pia ushindi vitani hauhalalishi unyonyaji dhidi ya ardhi ya wengine au dhidi ya Serikali za watu wengine. Msingi huu unaendana kabisa na dhamira ya sasa ya Sera ya Mambo nje. Hata hivyo hali ni tofauti kabisa. Mambo tunayoyafanya kwenye sera yetu ya Mambo ya Nje yanamfanya Mwalimu Nyerere ageuke huko kaburini kwake. Nitaeleza kwa mifano.


Mheshimiwa Spika,


Oktoba 26, 2016 kulikuwa na kikao cha wajumbe wa Nchi 21 zinazounda ‘Kamati ya Urithi wa Dunia’ ya UNESCO - Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, kupiga kura ya kupitisha makubaliano ya kuridhia kuupa hadhi ya Urithi wa Dunia Mji wa Jerusalem pamoja na moja ya majengo ya mji huo (Temple Mount), na kufungamanishwa na uasili wake na si hali ya sasa inayotokana na uvamizi wa Israel juu ya eneo hilo la lililoko Jerusalem Mashariki (lililovamiwa mwaka 1967 na mpaka leo kutambuliwa na UN kama eneo la Palestina, ambao wanauona ndio Mji Mkuu wa nchi ya Palestina iwapo makubaliano ya ’Two States Solution’ yatafikiwa).


Tanzania ilikuwa ni mjumbe wa Kamati hiyo ya nchi 21, na kwa mshangao wa wengi duniani, ilipiga kura kuzuia Azimio hilo, na kutaka azimio ‘Laini’ zaidi kwa Israel. Nchi marafiki zetu wa asili kule Umoja wa Mataifa (UN) ambazo nazo ni wajumbe wa kamati ile, kama Cuba, Vietnam na Angola zilipiga kura kuunga mkono azimio hilo, zikitushangaa mno kwa utetezi wetu kwa Israel ambao haukutarajiwa, hasa ikiwa msimamo wetu kama nchi siku zote umekuwa ni kutambua Jerusalem Mashariki kama eneo la Wapalestina ili kupata muafaka wa nchi mbili.


Sisi ACT Wazalendo tulihoji juu ya jambo hili linalokwenda kinyume na Sera ya Nje ya Nchi yetu. Msimamo wa Tanzania ni kukubaliana na UN kupinga uvamizi wa eneo hilo uliofanywa na Israel. Serikali ilitoa majibu mepesi tu, tena pembeni, kuwa upigaji kura ule haukuwa msimamo rasmi wa nchi yetu, ni ukiukwaji wa sera yetu ya mambo ya nje, na kuwa ni jambo ambalo Afisa wetu kwenye mkutano ule wa UNESCO alilifanya kwa makosa, na hivyo hatua zingechukuliwa dhidi yake.


Ni dhahiri majibu hayo yalikuwa ni ghiliba tu, matukio ya karibuni yameonyesha kwa uwazi sura mpya ya Taifa letu, pamoja na msimamo mpya wa Sera yetu ya mambo ya nje. Kwenye Diplomasia matendo ya nchi huwa na maana zaidi kuliko maneno ya wanadiplomasia wake. Matendo yetu yafuatayo ya karibuni yameonyesha kuwa Tanzania hatuisapoti tena Palestina:


1. Baada ya kuwaangusha Wapalestina kule Paris kwenye Mkutano wa UNESCO, Serikali iliahidi kuwa ingemchukulia hatua Afisa yule wa Wizara ya Mambo ya Nje aliyekwenda kinyume na Sera yetu ya Mambo ya Nje, hatujafanya hilo, zaidi tumempandisha cheo na kumteua kuwa Balozi wetu wa Ankara, Uturuki. Jambo hilo linaonyesha kuwa tulimtuma Balozi Elizabeth Kiondo apige kura namna ile kule UNESCO, na sasa tumempa cheo zaidi kwa kazi njema aliyoifanya. Jambo hili linaonyesha kuwa kwa sasa tunawaunga mkono Waisrael, na hatuko tena na Wapalestina.


2. Kwa sasa tumeamua kufungua ubalozi wetu Israel, Tel Aviv, kuongeza uchungu kwenye Kidonda, tukachagua wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel katika ardhi ya Taifa la Palestina kuzindua ubalozi wetu huo. Jambo hili linafanyika kukiwa na tuhuma kuwa hata huo Ubalozi unagharamiwa na Israel yenyewe, ndio maana tumepangiwa hata kipindi cha kuufungua. Kidiplomasia kuufungua ubalozi wetu katika wakati huu ni kuazimisha uvamizi wa Israel katika ardhi ya Palestina. Maana tulikuwa na uwezo wa kuchagua wakati mwengine wowote kufanya uzinduzi wa ubalozi wetu, lakini kwa kuwa aliyegharamia uwepo wa ubalozi huo (Israel) alitaka tuufungue wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel kwa Palestina, ilitubidi tufanye hivyo. Jambo hilo limeonyesha kuwa kwa sasa hatuungi mkono tena utu (Palestina) bali tunamtumikia Kila mwenye kitu (Israel).


3. Wakati akiwa ziarani Israel, Balozi Mahiga alifika sehemu ya miji inayokaliwa kimabavu na Israel ambayo inapakana na Ukanda wa Gaza. Na baadaye alihojiwa na Televisheni ya Taifa ya Israel, ambako alionyesha tu masikitiko yake kwa Waisrael wanaokaa maeneo hayo kwa kusumbuliwa na mashambulizi ya Hamas. Lakini hakulaani kabisa uendelezaji wa Israel kujenga makazi kwenye maeneo hayo ya uvamizi kama Wanadiplomasia wengine wa nchi zenye msimamo wa ‘Two States Solution’ kama sisi wanavyofanya. Balozi Mahiga mwanadiplomasia mzoefu na mbobezi, Kutokulaani kwake makazi yale haramu ni jambo la makusudi kabisa, si bahati mbaya. Ni kitendo cha kutuma salamu kwa Wapalestina kuwa tunaunga mkono uendelezaji makazi wa Israel katika maeneo hayo iliyoyavamia.


4. Tanzania imetajwa na vituo mbalimbali vya habari vya Kimataifa kuwa ni katika nchi 33 ambazo zilihudhuria ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, Mei 14, kilele cha maazimisho ya miaka 70 tangu uvamizi wa Israel katika maeneo ya Wapalestina. Chanzo cha taarifa ya Tanzania kuhudhuria ni Serikali ya Israel, ikitaja nchi ilizozialika na zilizohudhuria. Serikali yetu inasema inapinga uwepo wa Ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, lakini hapo hapo inatajwa kuhudhuria uzinduzi huo. Picha tunayoitoa hapa kwa Wapalestina ni kuwa tunaunga mkono jambo hili la ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem.


5. Siku ya uzinduzi huo wa ubalozi wa nchi ya Marekani mjini Jerusalem, Jeshi la Israel liliwaua kwa risasi zaidi ya watu 54 wa Palestina, wakiwemo wanawake, watoto, walemavu na hata wanahabari. Nchi mbalimbali duniani zimelaani mauaji hayo. Nchi ya Afrika ya Kusini imekwenda mbali zaidi kwa kumrudisha nyumbani Balozi wake aliyeko Israel. Sisi Tanzania tulioikomboa Afrika Kusini tumekaa kimya, tumeshindwa hata kutoa kauli ya kulaani mauaji hayo. Kuhudhuria kwetu ufunguzi wa ubalozi na kukaa kimya juu ya mauaji hayo kunaonyesha tumewaacha rasmi Wapalestina.


Mambo hayo matano yanaonyesha kuwa sisi si tena ile Tanzania ya Mwalimu Julius Nyerere, sisi kwa sasa ni Tanzania Mpya (kama yasemavyo matangazo ya Ikulu yetu) - Tanzania mpya inayosimama na Waonevu wa dunia, Wauaji na Wavunja haki za wanyonge. Sisi si tena Tanzania ya kusimama na wanyonge, bali ni Tanzania ya kusimama na Wanyongaji kwa sababu ya maslahi ya kiuchumi.


Si ile Tanzania iliyoongoza Ukombozi wa Bara la Afrika kutoka kwenye makucha ya Ukoloni, bali ni Tanzania Mpya inayounga mkono na kushabikia ukoloni na Uvamizi. Sisi si ile Tanzania yenye msimamo mkali tuliyolipinga Taifa kubwa la Marekani dhidi ya Uvamizi wake kwa wanyonge wa taifa la Vietnam, bali sasa ni Tanzania mpya ya kuunga mkono Uvamizi wa Taifa onevu la Israel kule Palestina. Sisi si Tanzania ile iliyoitetea China ipate nafasi na kiti chake stahili kule UNO, bali sasa sisi ni Tanzania mpya inayowaacha watu wa Palestina bila utetezi wa hadhi, kiti na nafasi yake stahili kule UNESCO.


Sisi si ile Tanzania huru tena ya Mwalimu Nyerere, iliyowaheshimu watu na mataifa kwa sababu ya Utu wao na kuamini kwamba binaadam wote ni sawa. Sasa sisi ni Tanzania mpya, inayowapa heshima watu kwa sababu ya kitu inachotuhonga, tukiuza usuli wa Utaifa wetu kwa maslahi machache ya kifedha au kiuchumi.


Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau. Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.


  1. Kujengewa Uwanja wa Mpira na Msikiti Visiifanye Tanzania Iikumbatie Morocco na Kuacha Kuiunga Mkono Sahara Magharibi

[Sehemu ya Pili ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Bado niko kwenye Sera ya mambo ya nje ya nchi yetu, si hii ya Tanzania mpya, bali ile Tanzania ya tangu wakati wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ya kusimama na wanyonge. Wakati tulipoamua kufuata ‘Diplomasia ya Uchumi’ bado msingi wetu huu wa kusimama na wanyonge ulibaki pale pale. Ndio maana wakati wa Rais Ben Mkapa na Jakaya Kikwete bado tulibaki kuwa ni sauti ya mataifa yanayoonewa kama Cuba (tukipinga vikwazo vya Marekani dhidi yao), Palestina na Sahara Magharibi.


Msingi huo wa kusimama na wanyonge ni muhimu zaidi kwa chama chetu cha ACT Wazalendo, ndio maana tulipinga ujio wa Mfalme wa Morocco hapa nchini Oktoba 23 - 25, 2016. Kwa kuwa Taifa hilo bado linaikalia kimabavu ardhi ya wanyonge wa Sahara Magharibi. Ndio msingi pia wa kutangaza wazi mahusiano yetu rasmi na Chama cha cha siasa na ukombozi wa Taifa hilo cha Polisario kinachopigania Uhuru wa nchi ya Sahara Magharibi.


Umoja wa Afrika (AU) uliamua kukubali ombi la Morocco kurudi bila masharti kwenye jumuiya hiyo. Ikimbukwe kuwa kwa zaidi ya miaka 33 Morocco haikuwa na mahusiano na jumuiya hiyo (tangu OAU mpaka sasa AU) baada ya kujitoa kwa kupinga OAU kuitambua Sahara Magharibi kama Taifa huru na kupewa kiti rasmi ndani ya OAU mwaka 1984.


Uamuzi wa OAU wa kuiruhusu Sahara Magharibi Kuwa mwanachama wa Umoja huo ulitokana na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice - ICJ) ya mwaka 1975 iliyopinga madai ya Morocco kuwa ina mahusiano ya kihistoria na kisheria na Sahara Magharibi (na hivyo kuitawala kinguvu) na kutoa haki ya kujitawala kwa Taifa hilo.


Tunaheshimu maamuzi yale mkutano wa AU wa Januari 2017, ulioirudisha Morocco kwenye AU. Lakini tabia za Taifa hilo onevu bado hazijabadilika, ni muhimu tulieleze bunge masuala yafuatayo ili liweke msimamo wake kwa Serikali juu ya kuminywa kwa watu wa Sahara Magharibi:


1. Kikao cha AU cha Januari 28 - 29, 2018 kiliazimia kuwa Morocco iruhusu Kamati Maalum ya Uangalizi ya AU iende kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo inayakalia kimabavu ili kuja kuijulisha AU hali ya mambo ilivyo.


2. Machi 29, 2018 Morocco iliwajulisha UN juu ya kutoruhusu waangalizi wowote wa AU kwenda kwenye maeneo yote ya Sahara Magharibi inayoyakalia.


3. Tangu mwaka 1991 Morocco imetumia mbinu, hila, na uzandiki ili kuzuia Tume ya Umoja wa Mataifa kwaajili ya Kura ya Maoni ya Uhuru wa Sahara Magharibi (MINURSO) kufanya kazi yake kwenye maeneo inayoyakalia kimabavu ya Sahara Magharibi. Siku za karibuni, Umoja wa Mataifa, UN ulipitisha azimio namba 2414 (2018) la kuongeza muda wa mamlaka, uahai na madaraka ya (MINURSO) kwa miezi sita. Morocco imepinga jambo hilo na kutishia kufanya mashambulizi ya kijeshi kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo yameshakombolewa (Liberated Zones).


4. Bado Morocco inaendeleza uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam kwa watu wote wa Sahara Magharibi wanaodai Uhuru wao.


5. Kurudishwa kwa Morocco kwenye AU kulienda pamoja na Taifa hilo kuridhia ‘AU Constitutive Act’ inayoyataka mataifa ya Afrika kuheshimu maazimio ya AU na hata yale ya UN yanatolewa kwa ushirikiano na AU. Lakini kwa matendo yake tuliyoyaainisha hapo juu ni dhahiri kuwa Morocco haitaki usuluhishi na Sahara Magharibi, bado inataka kuitawala na kuikalia kimabavu, bado Morocco inataka kuendelea kuwa mkoloni. Ndio maana imekataa hata kumpa ushirikiano msuluhishi wa mgogoro huu, ndugu Horst Köhler, Rais wa zamani wa Ujerumani


6. Matendo ya Serikali yetu kwa sasa yanaonyesha hatuna msimamo kwenye mambo ya msingi ya kidiplomasia, namna tulivyoenenda kwenye mahusiano yetu na wanyonge wa Palestina ni mfano hai, sasa tukijali vitu kuliko utu kama ilivyo zamani.


Hivyo basi, nataka kulishawishi Bunge lako litoe muongozo kwa Serikali juu ya kuenenda kwenye hili jambo la Morocco na Sahara Magharibi, ili kuzuia ahadi ya kujengewa Uwanja na Msikiti na Serikali ya Morocco (Vitu) isitufanye tu waache ndugu zetu Wanyonge wa Sahara Magharibi.


Nchi yetu ni kimbilio la Nchi ya Sahara, Serikali yetu chini ya Mwalimu Nyerere ililitambua Taifa la Sahara Magharibi tangu siku za mwanzo kabisa za harakati zao, ndio maana wanao Ubalozi hapa nchini. Kumuenzi baba wa Taifa na kulinda misingi ya Taifa letu ni lazima tusimame na watu wa Sahara Magharibi, na tusiwatupe kama tulivyofanya kwa watu wa Palestina.


Naliomba Bunge liibane Serikali ili itoe ahadi hiyo hapa Bungeni, pamoja na kuitaka Serikali kutumia ushawishi wake kule AU na UN kuibana Morocco iruhusu kura ya maoni ya kuamua mustakabali wa watu wa Sahara Magharibi kama ilivyoridhiwa kwenye Azimio la UN.


Viva Sahara Magharibi

Viva Polisario

Mungu Ibariki Afrika


  1. Hakuna Diplomasia Bila Wanadiplomasia: Tuna Uhaba Mkubwa wa Watumishi Kwenye Balozi Zetu

[Sehemu ya Tatu ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Msingi wa tano wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania unatutaka tushirikiane kikamilifu na Nchi, Mashirika pamoja na Taasisi mbalimbali katika nyanja za Diplomasia, Siasa, Uchumi, Utaalam na Teknolojia. Wizara hii ina jukumu la kubuni na kusimami utekelezaji wa misingi yote ya Sera yetu ya Mambo ya Nje.


Pia Wizara hii pia ina jukumu la kusimamia na kuratibu mahusiano kati ya Tanzania na nchi pamoja na mashirika mbalimbali. Utimizaji wa jambo hilo unafanyika kupitia balozi zetu zilizotapakaa kwenye nchi mbalimbali ulimwenguni. Kwa sasa ufanisi wetu ni mkubwa kwa sababu ya uhaba wa watumishi kwenye balozi zetu mbalimbali duniani.


Kwa wastani ukimuondoa Balozi, kila kituo cha Ubalozi wetu nje ya nchi kinapaswa kuwa na Mhasibu, mtu wa TISS na pamoja na Mwanadiplomasia (FSO). Vituo vingi vya balozi zetu havina kabisa Maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Wale wachache waliokuwepo awali walirudishwa nchini kwa sababu mbalimbali (ikiwemo kumaliza muda wao wa utumishi Nje ya Nchi). Tumerudisha watu bila kupeleka mbadala wao.


Kwenye balozi zetu mbalimbali watendaji hasa wa kazi za Kibalozi na kidiplomasia ni hawa maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Sasa kwa uhaba huu tunawezaje kufanya Diplomasia ya nchi yetu? Hiyo Diplomasia ya Uchumi tunafanyaje bila kuwa na hao Wanadiplomasia?


Nitatoa tu mfano wa balozi zetu chache ulimwenguni. China, nchi ambayo ni mshirika wetu mkubwa kidiplomasia na kiuchumi, hatuna kabisa FSO huko, labda ndio sababu mauzo yetu kwenda China yameshuka mno, maana biashara ya nje ni Diplomasia, sasa wakati Spika unamtaka ndugu yangu Mwijage asafiri, ni nani atakayemuandalia hiyo mikutano ya kupata wawekezaji huko China kama hatuna FSO hata mmoja? Wenzetu Uganda wana FSO’s 8 huko China, Kenya na Sudan wao wanao 9 Kila mmoja.


Nchi nyengine ambayo hatuna kabisa FSO ni Ethiopia - Makao Makuu ya AU, utaona tunavyodharau nafasi yetu katika Afrika. Pia hatuna FSO Afrika Kusini, nchi rafiki na moja ya zenye uchumi mkubwa Afrika, hatuna kabisa FSO Ujerumani - Nchi kubwa zaidi kiuchumi katika Umoja wa Ulaya (EU). Hata India ambako tangu Bunge lianze wabunge tunalalamikia kukosa soko la mbaazi kutoka huko nako hatuna FSO hata mmoja. Tumeufanya kuwa ubalozi wa kupokea wagonjwa tu.


Nchi za Brics (ukiondoa China, India na Afrika Kusini ambazo hatuna kabisa FSO’s) zilizobaki, Brazil na Urusi tuna FSO mmoja mmoja tu. Hata DRC Congo - Nchi ambayo zaidi ya theluthi moja ya mizigo ya Transit inayopita kwenye bandari ya Dar inatoka, nayo tuna FSO mmoja tu tofauti na watatu ilivyozoeleka. Kenya - Nchi ya Afrika Mashariki tunayofanya nayo biashara zaidi nayo ina FSO mmoja tu.


Hali iko hivyo karibu katika balozi zetu nyingi ulimwenguni. FSO’s ndio maafisa hasa waliofundwa na kupikwa kutekeleza Sera yetu ya mambo ya Nje. Foreign Service Officers (FSO’s) ndio diplomats (wanadiplomasia wetu). Kama hawapo vituoni, na hatuwatumii maana yake hatufanyi diplomasia, na kwa kuangalia mbali tunaua diplomasia yetu.


Mimi sitapitisha bajeti hii mpaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itakaponihakikishia kuwa itapeleka Maafisa wa Diplomasia (FSO’s) katika vituo ambavyo hatuna kabisa na pia kuwaongeza katika vile vituo ambavyo wako wachache.


Tunasimama na Iran na Qatar, Uonevu Dhidi Yao Si Sawa - Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


Tunasimama na Iran na Qatar - Uonevu Dhidi Yao Si Sawa. Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


[Sehemu ya Nne na ya Mwisho ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Jambo la mwisho kwenye mchango wangu ni juu ya hali ya ulinzi na usalama duniani. Usiku wa kuamkia Disemba 9, 2017, tulipoteza askari wetu 14 na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa huko DRC Congo, wakiwa kwenye Jeshi la kulinda Amani la Umoja wa Mataifa. Nachukua nafasi hii kuwaombea kwa Mola awalaze pema, pamoja na kutoa pole kwa familia zao na kwa Jeshi zima la JWTZ.


Taifa letu linachangia pakubwa katika kulinda amani ya ulimwengu, wanajeshi wetu wakaiwa karibu katika nchi nane duniani. Naamini tunao wajibu kama Taifa kusaidia uwepo wa amani Ulimwenguni ili kuzuia nchi zilizo kwenye machafuko kama DRC Congo kuongezeka na askari wetu wa kulinda amani kupotea.


Tayari, katika siku za karibuni, dunia imeshughudia maafa makubwa ya vita nchini Libya (ambako Rais Kikwete ni msuluhishi), Iraq, Afghanistan, Somalia, Syria, Sudan Kusini na Yemen. Mwenendo wa migogoro na uonevu unofanyika Qatar na unaotaka kufanyika Iran unapaswa kukemewa mapema ili kuchochea amani ulimwenguni, hasa eneo la mashariki ya kati ambalo tayari limeharibiwa na vita.


Hotuba ya Waziri ya Bajeti ya Wizara hii kwa mwaka 2016/17 ilibeba pongezi kwa nchi za Iran, Marekani, China, Urusi, UN na Umoja wa Ulaya (hasa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani) kwa makubaliano ya Nyuklia ya yaliyoiondolea vikwazo Iran kwa masharti ya kutoendeleza urutubishaji wa nyuklia. Makubaliano yale ni muhimu kwa kuwa iliondoa hali ya mashaka iliyokuwa imetanda duniani.


Tumeona Marekani imejitoa kwenye makubaliano hayo, na kutishia kuweka vikwazo vipya kwa Iran. Huku wajumbe wengine wa wakiendelea kubaki kwa kuwa bado Iran imeendelea kutekeleza makubaliano husika, na kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki, IAEA ni kuwa bado Iran inafuata masharti ya makubaliano husika.


Uamuzi huu wa Marekani si mzuri, unarudisha hali ya mashaka kwenye eneo la mashariki ya kati, ni uonevu dhidi ya Iran, hasa kwa kuwa IAEA imethibitisha kuwa Iran haina makosa. Ni maamuzi ya uonevu tu na usiochochea amani, ni uamuzi unaopaswa kupingwa. Serikali yetu iitumie nafasi yake kule UN kupinga uamuzi huu, na kuitaka Marekani kurudi kwenye makubaliano haya ili kudumisha amani.


Pia Julai 26, 2017 Wizara hii ilitoa taarifa yake juu ya mgogoro wa nchi za Ghuba (GCC), baada ya hatua ya nchi nne za Saudi Arabia, UAE, Bahrain na Misri kuiwekea vikwazo vya anga, bahari na ardhini nchi ya Qatar. Msimamo wa Serikali ni kuunga mkono upatanishi unaongozwa na Amir wa Kuwait, Sheikh Sabah Al-Jaber, tunaunga mkono msimamo huo.


Lakini bado pia sisi ACT Wazalendo tunasimamia tamko letu la kupinga uonevu dhidi ya Qatar tulilolitoa July 24, 2017. Kwa karibu miezi 10 sasa watu wa Qatar wamewekewa vikwazo vya kiuchumi na kiusafiri, kwenye anga, ardhi na bahari na nchi hizo nne jirani, jambo hilo si sawa, hasa kwa kuwa masharti yaliyotolewa ili kuondoa vikwazo hivyo yanaingilia uhuru wa nchi hiyo.


Tunaitaka Serikali yetu, pamoja na kusapoti usuluhishi huu wa Kuwait, itumie nafasi yake pia kule UN kuhakikisha inachangia usuluhishi wa jambo hili ili mashaka yaliyoko na vikwazo kwa Qatar viondoshwe.


Ahsanteni kwa Kunisikiliza. Naomba Kuwasilisha


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018
Zitto teuzi za nafasi mbali mbali zinaonyesha jinsi gani huyu bwana alivyo na chuki na waislam usiumize kichwa muda wake utaisha ataondoka
 
Mchango wa Maandishi wa ndg. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mb kwenye makadirio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


  1. Sisi si Tanzania ya Nyerere, Ni Tanzania Mpya, Tanzania Mbaya - Inayokalia Kimya Mauaji ya Kinyama ya Wapalestina, na Kusapoti Waonevu

[Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika,


Msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa Israel na Palestine unaelezwa vizuri sana na nukuu hii ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa Mwaka 1967 na ndio umekuwa Msingi wa Sera yetu ya Mambo ya Nje kwa miaka mingi kabla ya utawala wa sasa wa CCM mpya.


“[......] Tanzania’s position. We recognize Israel and wish to be friendly with her as well as with the Arab nations. But we cannot condone aggression on any pretext, nor accept victory in war as a justification for the exploitation of other lands, or government over other peoples.”


Kwamba Tanzania inaitambua Israel na inapenda kuwa na urafiki nayo pamoja na urafiki na mataifa mengine ya kiarabu. Lakini hatuwezi kukalia kimya uvamizi kwa namna yeyote ile. Pia ushindi vitani hauhalalishi unyonyaji dhidi ya ardhi ya wengine au dhidi ya Serikali za watu wengine. Msingi huu unaendana kabisa na dhamira ya sasa ya Sera ya Mambo nje. Hata hivyo hali ni tofauti kabisa. Mambo tunayoyafanya kwenye sera yetu ya Mambo ya Nje yanamfanya Mwalimu Nyerere ageuke huko kaburini kwake. Nitaeleza kwa mifano.


Mheshimiwa Spika,


Oktoba 26, 2016 kulikuwa na kikao cha wajumbe wa Nchi 21 zinazounda ‘Kamati ya Urithi wa Dunia’ ya UNESCO - Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, kupiga kura ya kupitisha makubaliano ya kuridhia kuupa hadhi ya Urithi wa Dunia Mji wa Jerusalem pamoja na moja ya majengo ya mji huo (Temple Mount), na kufungamanishwa na uasili wake na si hali ya sasa inayotokana na uvamizi wa Israel juu ya eneo hilo la lililoko Jerusalem Mashariki (lililovamiwa mwaka 1967 na mpaka leo kutambuliwa na UN kama eneo la Palestina, ambao wanauona ndio Mji Mkuu wa nchi ya Palestina iwapo makubaliano ya ’Two States Solution’ yatafikiwa).


Tanzania ilikuwa ni mjumbe wa Kamati hiyo ya nchi 21, na kwa mshangao wa wengi duniani, ilipiga kura kuzuia Azimio hilo, na kutaka azimio ‘Laini’ zaidi kwa Israel. Nchi marafiki zetu wa asili kule Umoja wa Mataifa (UN) ambazo nazo ni wajumbe wa kamati ile, kama Cuba, Vietnam na Angola zilipiga kura kuunga mkono azimio hilo, zikitushangaa mno kwa utetezi wetu kwa Israel ambao haukutarajiwa, hasa ikiwa msimamo wetu kama nchi siku zote umekuwa ni kutambua Jerusalem Mashariki kama eneo la Wapalestina ili kupata muafaka wa nchi mbili.


Sisi ACT Wazalendo tulihoji juu ya jambo hili linalokwenda kinyume na Sera ya Nje ya Nchi yetu. Msimamo wa Tanzania ni kukubaliana na UN kupinga uvamizi wa eneo hilo uliofanywa na Israel. Serikali ilitoa majibu mepesi tu, tena pembeni, kuwa upigaji kura ule haukuwa msimamo rasmi wa nchi yetu, ni ukiukwaji wa sera yetu ya mambo ya nje, na kuwa ni jambo ambalo Afisa wetu kwenye mkutano ule wa UNESCO alilifanya kwa makosa, na hivyo hatua zingechukuliwa dhidi yake.


Ni dhahiri majibu hayo yalikuwa ni ghiliba tu, matukio ya karibuni yameonyesha kwa uwazi sura mpya ya Taifa letu, pamoja na msimamo mpya wa Sera yetu ya mambo ya nje. Kwenye Diplomasia matendo ya nchi huwa na maana zaidi kuliko maneno ya wanadiplomasia wake. Matendo yetu yafuatayo ya karibuni yameonyesha kuwa Tanzania hatuisapoti tena Palestina:


1. Baada ya kuwaangusha Wapalestina kule Paris kwenye Mkutano wa UNESCO, Serikali iliahidi kuwa ingemchukulia hatua Afisa yule wa Wizara ya Mambo ya Nje aliyekwenda kinyume na Sera yetu ya Mambo ya Nje, hatujafanya hilo, zaidi tumempandisha cheo na kumteua kuwa Balozi wetu wa Ankara, Uturuki. Jambo hilo linaonyesha kuwa tulimtuma Balozi Elizabeth Kiondo apige kura namna ile kule UNESCO, na sasa tumempa cheo zaidi kwa kazi njema aliyoifanya. Jambo hili linaonyesha kuwa kwa sasa tunawaunga mkono Waisrael, na hatuko tena na Wapalestina.


2. Kwa sasa tumeamua kufungua ubalozi wetu Israel, Tel Aviv, kuongeza uchungu kwenye Kidonda, tukachagua wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel katika ardhi ya Taifa la Palestina kuzindua ubalozi wetu huo. Jambo hili linafanyika kukiwa na tuhuma kuwa hata huo Ubalozi unagharamiwa na Israel yenyewe, ndio maana tumepangiwa hata kipindi cha kuufungua. Kidiplomasia kuufungua ubalozi wetu katika wakati huu ni kuazimisha uvamizi wa Israel katika ardhi ya Palestina. Maana tulikuwa na uwezo wa kuchagua wakati mwengine wowote kufanya uzinduzi wa ubalozi wetu, lakini kwa kuwa aliyegharamia uwepo wa ubalozi huo (Israel) alitaka tuufungue wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel kwa Palestina, ilitubidi tufanye hivyo. Jambo hilo limeonyesha kuwa kwa sasa hatuungi mkono tena utu (Palestina) bali tunamtumikia Kila mwenye kitu (Israel).


3. Wakati akiwa ziarani Israel, Balozi Mahiga alifika sehemu ya miji inayokaliwa kimabavu na Israel ambayo inapakana na Ukanda wa Gaza. Na baadaye alihojiwa na Televisheni ya Taifa ya Israel, ambako alionyesha tu masikitiko yake kwa Waisrael wanaokaa maeneo hayo kwa kusumbuliwa na mashambulizi ya Hamas. Lakini hakulaani kabisa uendelezaji wa Israel kujenga makazi kwenye maeneo hayo ya uvamizi kama Wanadiplomasia wengine wa nchi zenye msimamo wa ‘Two States Solution’ kama sisi wanavyofanya. Balozi Mahiga mwanadiplomasia mzoefu na mbobezi, Kutokulaani kwake makazi yale haramu ni jambo la makusudi kabisa, si bahati mbaya. Ni kitendo cha kutuma salamu kwa Wapalestina kuwa tunaunga mkono uendelezaji makazi wa Israel katika maeneo hayo iliyoyavamia.


4. Tanzania imetajwa na vituo mbalimbali vya habari vya Kimataifa kuwa ni katika nchi 33 ambazo zilihudhuria ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, Mei 14, kilele cha maazimisho ya miaka 70 tangu uvamizi wa Israel katika maeneo ya Wapalestina. Chanzo cha taarifa ya Tanzania kuhudhuria ni Serikali ya Israel, ikitaja nchi ilizozialika na zilizohudhuria. Serikali yetu inasema inapinga uwepo wa Ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, lakini hapo hapo inatajwa kuhudhuria uzinduzi huo. Picha tunayoitoa hapa kwa Wapalestina ni kuwa tunaunga mkono jambo hili la ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem.


5. Siku ya uzinduzi huo wa ubalozi wa nchi ya Marekani mjini Jerusalem, Jeshi la Israel liliwaua kwa risasi zaidi ya watu 54 wa Palestina, wakiwemo wanawake, watoto, walemavu na hata wanahabari. Nchi mbalimbali duniani zimelaani mauaji hayo. Nchi ya Afrika ya Kusini imekwenda mbali zaidi kwa kumrudisha nyumbani Balozi wake aliyeko Israel. Sisi Tanzania tulioikomboa Afrika Kusini tumekaa kimya, tumeshindwa hata kutoa kauli ya kulaani mauaji hayo. Kuhudhuria kwetu ufunguzi wa ubalozi na kukaa kimya juu ya mauaji hayo kunaonyesha tumewaacha rasmi Wapalestina.


Mambo hayo matano yanaonyesha kuwa sisi si tena ile Tanzania ya Mwalimu Julius Nyerere, sisi kwa sasa ni Tanzania Mpya (kama yasemavyo matangazo ya Ikulu yetu) - Tanzania mpya inayosimama na Waonevu wa dunia, Wauaji na Wavunja haki za wanyonge. Sisi si tena Tanzania ya kusimama na wanyonge, bali ni Tanzania ya kusimama na Wanyongaji kwa sababu ya maslahi ya kiuchumi.


Si ile Tanzania iliyoongoza Ukombozi wa Bara la Afrika kutoka kwenye makucha ya Ukoloni, bali ni Tanzania Mpya inayounga mkono na kushabikia ukoloni na Uvamizi. Sisi si ile Tanzania yenye msimamo mkali tuliyolipinga Taifa kubwa la Marekani dhidi ya Uvamizi wake kwa wanyonge wa taifa la Vietnam, bali sasa ni Tanzania mpya ya kuunga mkono Uvamizi wa Taifa onevu la Israel kule Palestina. Sisi si Tanzania ile iliyoitetea China ipate nafasi na kiti chake stahili kule UNO, bali sasa sisi ni Tanzania mpya inayowaacha watu wa Palestina bila utetezi wa hadhi, kiti na nafasi yake stahili kule UNESCO.


Sisi si ile Tanzania huru tena ya Mwalimu Nyerere, iliyowaheshimu watu na mataifa kwa sababu ya Utu wao na kuamini kwamba binaadam wote ni sawa. Sasa sisi ni Tanzania mpya, inayowapa heshima watu kwa sababu ya kitu inachotuhonga, tukiuza usuli wa Utaifa wetu kwa maslahi machache ya kifedha au kiuchumi.


Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau. Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.


  1. Kujengewa Uwanja wa Mpira na Msikiti Visiifanye Tanzania Iikumbatie Morocco na Kuacha Kuiunga Mkono Sahara Magharibi

[Sehemu ya Pili ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Bado niko kwenye Sera ya mambo ya nje ya nchi yetu, si hii ya Tanzania mpya, bali ile Tanzania ya tangu wakati wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ya kusimama na wanyonge. Wakati tulipoamua kufuata ‘Diplomasia ya Uchumi’ bado msingi wetu huu wa kusimama na wanyonge ulibaki pale pale. Ndio maana wakati wa Rais Ben Mkapa na Jakaya Kikwete bado tulibaki kuwa ni sauti ya mataifa yanayoonewa kama Cuba (tukipinga vikwazo vya Marekani dhidi yao), Palestina na Sahara Magharibi.


Msingi huo wa kusimama na wanyonge ni muhimu zaidi kwa chama chetu cha ACT Wazalendo, ndio maana tulipinga ujio wa Mfalme wa Morocco hapa nchini Oktoba 23 - 25, 2016. Kwa kuwa Taifa hilo bado linaikalia kimabavu ardhi ya wanyonge wa Sahara Magharibi. Ndio msingi pia wa kutangaza wazi mahusiano yetu rasmi na Chama cha cha siasa na ukombozi wa Taifa hilo cha Polisario kinachopigania Uhuru wa nchi ya Sahara Magharibi.


Umoja wa Afrika (AU) uliamua kukubali ombi la Morocco kurudi bila masharti kwenye jumuiya hiyo. Ikimbukwe kuwa kwa zaidi ya miaka 33 Morocco haikuwa na mahusiano na jumuiya hiyo (tangu OAU mpaka sasa AU) baada ya kujitoa kwa kupinga OAU kuitambua Sahara Magharibi kama Taifa huru na kupewa kiti rasmi ndani ya OAU mwaka 1984.


Uamuzi wa OAU wa kuiruhusu Sahara Magharibi Kuwa mwanachama wa Umoja huo ulitokana na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice - ICJ) ya mwaka 1975 iliyopinga madai ya Morocco kuwa ina mahusiano ya kihistoria na kisheria na Sahara Magharibi (na hivyo kuitawala kinguvu) na kutoa haki ya kujitawala kwa Taifa hilo.


Tunaheshimu maamuzi yale mkutano wa AU wa Januari 2017, ulioirudisha Morocco kwenye AU. Lakini tabia za Taifa hilo onevu bado hazijabadilika, ni muhimu tulieleze bunge masuala yafuatayo ili liweke msimamo wake kwa Serikali juu ya kuminywa kwa watu wa Sahara Magharibi:


1. Kikao cha AU cha Januari 28 - 29, 2018 kiliazimia kuwa Morocco iruhusu Kamati Maalum ya Uangalizi ya AU iende kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo inayakalia kimabavu ili kuja kuijulisha AU hali ya mambo ilivyo.


2. Machi 29, 2018 Morocco iliwajulisha UN juu ya kutoruhusu waangalizi wowote wa AU kwenda kwenye maeneo yote ya Sahara Magharibi inayoyakalia.


3. Tangu mwaka 1991 Morocco imetumia mbinu, hila, na uzandiki ili kuzuia Tume ya Umoja wa Mataifa kwaajili ya Kura ya Maoni ya Uhuru wa Sahara Magharibi (MINURSO) kufanya kazi yake kwenye maeneo inayoyakalia kimabavu ya Sahara Magharibi. Siku za karibuni, Umoja wa Mataifa, UN ulipitisha azimio namba 2414 (2018) la kuongeza muda wa mamlaka, uahai na madaraka ya (MINURSO) kwa miezi sita. Morocco imepinga jambo hilo na kutishia kufanya mashambulizi ya kijeshi kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo yameshakombolewa (Liberated Zones).


4. Bado Morocco inaendeleza uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam kwa watu wote wa Sahara Magharibi wanaodai Uhuru wao.


5. Kurudishwa kwa Morocco kwenye AU kulienda pamoja na Taifa hilo kuridhia ‘AU Constitutive Act’ inayoyataka mataifa ya Afrika kuheshimu maazimio ya AU na hata yale ya UN yanatolewa kwa ushirikiano na AU. Lakini kwa matendo yake tuliyoyaainisha hapo juu ni dhahiri kuwa Morocco haitaki usuluhishi na Sahara Magharibi, bado inataka kuitawala na kuikalia kimabavu, bado Morocco inataka kuendelea kuwa mkoloni. Ndio maana imekataa hata kumpa ushirikiano msuluhishi wa mgogoro huu, ndugu Horst Köhler, Rais wa zamani wa Ujerumani


6. Matendo ya Serikali yetu kwa sasa yanaonyesha hatuna msimamo kwenye mambo ya msingi ya kidiplomasia, namna tulivyoenenda kwenye mahusiano yetu na wanyonge wa Palestina ni mfano hai, sasa tukijali vitu kuliko utu kama ilivyo zamani.


Hivyo basi, nataka kulishawishi Bunge lako litoe muongozo kwa Serikali juu ya kuenenda kwenye hili jambo la Morocco na Sahara Magharibi, ili kuzuia ahadi ya kujengewa Uwanja na Msikiti na Serikali ya Morocco (Vitu) isitufanye tu waache ndugu zetu Wanyonge wa Sahara Magharibi.


Nchi yetu ni kimbilio la Nchi ya Sahara, Serikali yetu chini ya Mwalimu Nyerere ililitambua Taifa la Sahara Magharibi tangu siku za mwanzo kabisa za harakati zao, ndio maana wanao Ubalozi hapa nchini. Kumuenzi baba wa Taifa na kulinda misingi ya Taifa letu ni lazima tusimame na watu wa Sahara Magharibi, na tusiwatupe kama tulivyofanya kwa watu wa Palestina.


Naliomba Bunge liibane Serikali ili itoe ahadi hiyo hapa Bungeni, pamoja na kuitaka Serikali kutumia ushawishi wake kule AU na UN kuibana Morocco iruhusu kura ya maoni ya kuamua mustakabali wa watu wa Sahara Magharibi kama ilivyoridhiwa kwenye Azimio la UN.


Viva Sahara Magharibi

Viva Polisario

Mungu Ibariki Afrika


  1. Hakuna Diplomasia Bila Wanadiplomasia: Tuna Uhaba Mkubwa wa Watumishi Kwenye Balozi Zetu

[Sehemu ya Tatu ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Msingi wa tano wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania unatutaka tushirikiane kikamilifu na Nchi, Mashirika pamoja na Taasisi mbalimbali katika nyanja za Diplomasia, Siasa, Uchumi, Utaalam na Teknolojia. Wizara hii ina jukumu la kubuni na kusimami utekelezaji wa misingi yote ya Sera yetu ya Mambo ya Nje.


Pia Wizara hii pia ina jukumu la kusimamia na kuratibu mahusiano kati ya Tanzania na nchi pamoja na mashirika mbalimbali. Utimizaji wa jambo hilo unafanyika kupitia balozi zetu zilizotapakaa kwenye nchi mbalimbali ulimwenguni. Kwa sasa ufanisi wetu ni mkubwa kwa sababu ya uhaba wa watumishi kwenye balozi zetu mbalimbali duniani.


Kwa wastani ukimuondoa Balozi, kila kituo cha Ubalozi wetu nje ya nchi kinapaswa kuwa na Mhasibu, mtu wa TISS na pamoja na Mwanadiplomasia (FSO). Vituo vingi vya balozi zetu havina kabisa Maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Wale wachache waliokuwepo awali walirudishwa nchini kwa sababu mbalimbali (ikiwemo kumaliza muda wao wa utumishi Nje ya Nchi). Tumerudisha watu bila kupeleka mbadala wao.


Kwenye balozi zetu mbalimbali watendaji hasa wa kazi za Kibalozi na kidiplomasia ni hawa maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Sasa kwa uhaba huu tunawezaje kufanya Diplomasia ya nchi yetu? Hiyo Diplomasia ya Uchumi tunafanyaje bila kuwa na hao Wanadiplomasia?


Nitatoa tu mfano wa balozi zetu chache ulimwenguni. China, nchi ambayo ni mshirika wetu mkubwa kidiplomasia na kiuchumi, hatuna kabisa FSO huko, labda ndio sababu mauzo yetu kwenda China yameshuka mno, maana biashara ya nje ni Diplomasia, sasa wakati Spika unamtaka ndugu yangu Mwijage asafiri, ni nani atakayemuandalia hiyo mikutano ya kupata wawekezaji huko China kama hatuna FSO hata mmoja? Wenzetu Uganda wana FSO’s 8 huko China, Kenya na Sudan wao wanao 9 Kila mmoja.


Nchi nyengine ambayo hatuna kabisa FSO ni Ethiopia - Makao Makuu ya AU, utaona tunavyodharau nafasi yetu katika Afrika. Pia hatuna FSO Afrika Kusini, nchi rafiki na moja ya zenye uchumi mkubwa Afrika, hatuna kabisa FSO Ujerumani - Nchi kubwa zaidi kiuchumi katika Umoja wa Ulaya (EU). Hata India ambako tangu Bunge lianze wabunge tunalalamikia kukosa soko la mbaazi kutoka huko nako hatuna FSO hata mmoja. Tumeufanya kuwa ubalozi wa kupokea wagonjwa tu.


Nchi za Brics (ukiondoa China, India na Afrika Kusini ambazo hatuna kabisa FSO’s) zilizobaki, Brazil na Urusi tuna FSO mmoja mmoja tu. Hata DRC Congo - Nchi ambayo zaidi ya theluthi moja ya mizigo ya Transit inayopita kwenye bandari ya Dar inatoka, nayo tuna FSO mmoja tu tofauti na watatu ilivyozoeleka. Kenya - Nchi ya Afrika Mashariki tunayofanya nayo biashara zaidi nayo ina FSO mmoja tu.


Hali iko hivyo karibu katika balozi zetu nyingi ulimwenguni. FSO’s ndio maafisa hasa waliofundwa na kupikwa kutekeleza Sera yetu ya mambo ya Nje. Foreign Service Officers (FSO’s) ndio diplomats (wanadiplomasia wetu). Kama hawapo vituoni, na hatuwatumii maana yake hatufanyi diplomasia, na kwa kuangalia mbali tunaua diplomasia yetu.


Mimi sitapitisha bajeti hii mpaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itakaponihakikishia kuwa itapeleka Maafisa wa Diplomasia (FSO’s) katika vituo ambavyo hatuna kabisa na pia kuwaongeza katika vile vituo ambavyo wako wachache.


Tunasimama na Iran na Qatar, Uonevu Dhidi Yao Si Sawa - Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


Tunasimama na Iran na Qatar - Uonevu Dhidi Yao Si Sawa. Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


[Sehemu ya Nne na ya Mwisho ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Jambo la mwisho kwenye mchango wangu ni juu ya hali ya ulinzi na usalama duniani. Usiku wa kuamkia Disemba 9, 2017, tulipoteza askari wetu 14 na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa huko DRC Congo, wakiwa kwenye Jeshi la kulinda Amani la Umoja wa Mataifa. Nachukua nafasi hii kuwaombea kwa Mola awalaze pema, pamoja na kutoa pole kwa familia zao na kwa Jeshi zima la JWTZ.


Taifa letu linachangia pakubwa katika kulinda amani ya ulimwengu, wanajeshi wetu wakaiwa karibu katika nchi nane duniani. Naamini tunao wajibu kama Taifa kusaidia uwepo wa amani Ulimwenguni ili kuzuia nchi zilizo kwenye machafuko kama DRC Congo kuongezeka na askari wetu wa kulinda amani kupotea.


Tayari, katika siku za karibuni, dunia imeshughudia maafa makubwa ya vita nchini Libya (ambako Rais Kikwete ni msuluhishi), Iraq, Afghanistan, Somalia, Syria, Sudan Kusini na Yemen. Mwenendo wa migogoro na uonevu unofanyika Qatar na unaotaka kufanyika Iran unapaswa kukemewa mapema ili kuchochea amani ulimwenguni, hasa eneo la mashariki ya kati ambalo tayari limeharibiwa na vita.


Hotuba ya Waziri ya Bajeti ya Wizara hii kwa mwaka 2016/17 ilibeba pongezi kwa nchi za Iran, Marekani, China, Urusi, UN na Umoja wa Ulaya (hasa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani) kwa makubaliano ya Nyuklia ya yaliyoiondolea vikwazo Iran kwa masharti ya kutoendeleza urutubishaji wa nyuklia. Makubaliano yale ni muhimu kwa kuwa iliondoa hali ya mashaka iliyokuwa imetanda duniani.


Tumeona Marekani imejitoa kwenye makubaliano hayo, na kutishia kuweka vikwazo vipya kwa Iran. Huku wajumbe wengine wa wakiendelea kubaki kwa kuwa bado Iran imeendelea kutekeleza makubaliano husika, na kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki, IAEA ni kuwa bado Iran inafuata masharti ya makubaliano husika.


Uamuzi huu wa Marekani si mzuri, unarudisha hali ya mashaka kwenye eneo la mashariki ya kati, ni uonevu dhidi ya Iran, hasa kwa kuwa IAEA imethibitisha kuwa Iran haina makosa. Ni maamuzi ya uonevu tu na usiochochea amani, ni uamuzi unaopaswa kupingwa. Serikali yetu iitumie nafasi yake kule UN kupinga uamuzi huu, na kuitaka Marekani kurudi kwenye makubaliano haya ili kudumisha amani.


Pia Julai 26, 2017 Wizara hii ilitoa taarifa yake juu ya mgogoro wa nchi za Ghuba (GCC), baada ya hatua ya nchi nne za Saudi Arabia, UAE, Bahrain na Misri kuiwekea vikwazo vya anga, bahari na ardhini nchi ya Qatar. Msimamo wa Serikali ni kuunga mkono upatanishi unaongozwa na Amir wa Kuwait, Sheikh Sabah Al-Jaber, tunaunga mkono msimamo huo.


Lakini bado pia sisi ACT Wazalendo tunasimamia tamko letu la kupinga uonevu dhidi ya Qatar tulilolitoa July 24, 2017. Kwa karibu miezi 10 sasa watu wa Qatar wamewekewa vikwazo vya kiuchumi na kiusafiri, kwenye anga, ardhi na bahari na nchi hizo nne jirani, jambo hilo si sawa, hasa kwa kuwa masharti yaliyotolewa ili kuondoa vikwazo hivyo yanaingilia uhuru wa nchi hiyo.


Tunaitaka Serikali yetu, pamoja na kusapoti usuluhishi huu wa Kuwait, itumie nafasi yake pia kule UN kuhakikisha inachangia usuluhishi wa jambo hili ili mashaka yaliyoko na vikwazo kwa Qatar viondoshwe.


Ahsanteni kwa Kunisikiliza. Naomba Kuwasilisha


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018


Hongera na asante sana kwa andiko/hotuba/uchambuzi huu mwanana. Kama ulivyopata kusema, nchi tumewakabidhi washamba safari hii.
 
Mjomba naomba kujua, kale kakitazi ulikokuwa umekashikilia tayari kwa kunyonga mtu imekuwaje? Nakumbuka kalikuwa kameandikwa MADE IN TRILLION 1.5.
 
Asante Zitto kwa kusimamia misingi ya Dr Martin Luther King Jr aliyesema "Justice is indivisible, Injustice anywhere is a threat to justice everywhere".

Kushirikiana na Majambazi kwa sababu yanaibia wengine na kwa kuwa yanakukatia "kitu kidogo" siku mojamoja si msingi mwema kwa mwanadamu mwenye moyo na dhamira safi!

Haiwezekani tukawa na sera ya utu wa mtu ni kitu na uungwana si mali kitu!. Huko ni kupoteza moral authority, kitu kilichotupa heshima kubwa kwa miaka mingi nje na ndani ya Afrika tangu wakati wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Hao Morocco ambao leo tumefumbia ukoloni wao kwa Sahara Magharibi wameandamana vikali kupinga matendo ya Israel kwa Wapalestina ( Mkuki kwa Nguruwe)
 
Mhe. ZZK kwanza niseme nakuheshimu sana katika mambo mengi ila napingana sana na hulka yako ya kufanya kazi ya kimaslahi ili nchi yetu iwe kama huko unakotetea. Kwa hiyo inafika wakati imani ya kuunga hata kukataa maoni yako napata kigugumizi.

Najua unapenda dunia iwe na amani ila hutaki Tanzania iwe na amani. Unakaribisha hao wanaofanya hayo huko unakotetea, waje wafanye hayo kwetu. Hii ndo imani yangu inapopotea katika siasa za Tanzania.

Siasa za dunia zimebadilika sana. Maoni yenu ya sasa yalifaa sana miaka ya 80-2010 wakati dunia haijatambua utaifa. Leo Italia wanaongozwa na Wataifa na wanaotetea tunu za taifa si maslahi ya Duania. Trump anatetea nchi na si dunia, huko Poland, Uhispania, Ufaransa, Ujerumani, Hungary, Uswisi nadhani unajua zaidi nini kinaendelea. Vyama vya UTAIFA vinazidi kupaza sauti na kuungwa mkono zaidi.

Ila niseme tu, nguvu hii unayotetea maslahi ya mataifa mengine tetea hivyo hivyo taifa letu ili tuwe na amani na pia rasilimali zetu ziwe zetu. Ukifanya hayo sauti yako itaonekana kuwa inamaanisha.
 
Kwa akili yako ulitegemea afanye nini baada ya kutujulisha sisi watz kuwa kuna upotevu wa 1.5t?

Wewe kama mtz ulitakiwa kuchukua hatua, yeye alishamaliza kazi yake.

Akili ya kiccm mbaya sana.
Mjomba naomba kujua, kale kakitazi ulikokuwa umekashikilia tayari kwa kunyonga mtu imekuwaje? Nakumbuka kalikuwa kameandikwa MADE IN TRILLION 1.5.
 
Well said!

Tatizo la nchi hii haina msimamo wa kudumu, na ni watu wakufuata mkumbo tu.
Ndiyo maana hata yule mwakilishi alipiga kura ya kukubali.
Nchi inaongozwa na watu wasiofaham historia ya mambo ya mataifa tunayoyaiga kimaendeleo.
Tunasubiri tusikie Marekani kasema nini nasi tunapeperuka hukohuko.

Mchango wa Maandishi wa ndg. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mb kwenye makadirio ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


  1. Sisi si Tanzania ya Nyerere, Ni Tanzania Mpya, Tanzania Mbaya - Inayokalia Kimya Mauaji ya Kinyama ya Wapalestina, na Kusapoti Waonevu

[Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika,


Msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa Israel na Palestine unaelezwa vizuri sana na nukuu hii ya Mwalimu Nyerere aliyoitoa Mwaka 1967 na ndio umekuwa Msingi wa Sera yetu ya Mambo ya Nje kwa miaka mingi kabla ya utawala wa sasa wa CCM mpya.


“[......] Tanzania’s position. We recognize Israel and wish to be friendly with her as well as with the Arab nations. But we cannot condone aggression on any pretext, nor accept victory in war as a justification for the exploitation of other lands, or government over other peoples.”


Kwamba Tanzania inaitambua Israel na inapenda kuwa na urafiki nayo pamoja na urafiki na mataifa mengine ya kiarabu. Lakini hatuwezi kukalia kimya uvamizi kwa namna yeyote ile. Pia ushindi vitani hauhalalishi unyonyaji dhidi ya ardhi ya wengine au dhidi ya Serikali za watu wengine. Msingi huu unaendana kabisa na dhamira ya sasa ya Sera ya Mambo nje. Hata hivyo hali ni tofauti kabisa. Mambo tunayoyafanya kwenye sera yetu ya Mambo ya Nje yanamfanya Mwalimu Nyerere ageuke huko kaburini kwake. Nitaeleza kwa mifano.


Mheshimiwa Spika,


Oktoba 26, 2016 kulikuwa na kikao cha wajumbe wa Nchi 21 zinazounda ‘Kamati ya Urithi wa Dunia’ ya UNESCO - Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, kupiga kura ya kupitisha makubaliano ya kuridhia kuupa hadhi ya Urithi wa Dunia Mji wa Jerusalem pamoja na moja ya majengo ya mji huo (Temple Mount), na kufungamanishwa na uasili wake na si hali ya sasa inayotokana na uvamizi wa Israel juu ya eneo hilo la lililoko Jerusalem Mashariki (lililovamiwa mwaka 1967 na mpaka leo kutambuliwa na UN kama eneo la Palestina, ambao wanauona ndio Mji Mkuu wa nchi ya Palestina iwapo makubaliano ya ’Two States Solution’ yatafikiwa).


Tanzania ilikuwa ni mjumbe wa Kamati hiyo ya nchi 21, na kwa mshangao wa wengi duniani, ilipiga kura kuzuia Azimio hilo, na kutaka azimio ‘Laini’ zaidi kwa Israel. Nchi marafiki zetu wa asili kule Umoja wa Mataifa (UN) ambazo nazo ni wajumbe wa kamati ile, kama Cuba, Vietnam na Angola zilipiga kura kuunga mkono azimio hilo, zikitushangaa mno kwa utetezi wetu kwa Israel ambao haukutarajiwa, hasa ikiwa msimamo wetu kama nchi siku zote umekuwa ni kutambua Jerusalem Mashariki kama eneo la Wapalestina ili kupata muafaka wa nchi mbili.


Sisi ACT Wazalendo tulihoji juu ya jambo hili linalokwenda kinyume na Sera ya Nje ya Nchi yetu. Msimamo wa Tanzania ni kukubaliana na UN kupinga uvamizi wa eneo hilo uliofanywa na Israel. Serikali ilitoa majibu mepesi tu, tena pembeni, kuwa upigaji kura ule haukuwa msimamo rasmi wa nchi yetu, ni ukiukwaji wa sera yetu ya mambo ya nje, na kuwa ni jambo ambalo Afisa wetu kwenye mkutano ule wa UNESCO alilifanya kwa makosa, na hivyo hatua zingechukuliwa dhidi yake.


Ni dhahiri majibu hayo yalikuwa ni ghiliba tu, matukio ya karibuni yameonyesha kwa uwazi sura mpya ya Taifa letu, pamoja na msimamo mpya wa Sera yetu ya mambo ya nje. Kwenye Diplomasia matendo ya nchi huwa na maana zaidi kuliko maneno ya wanadiplomasia wake. Matendo yetu yafuatayo ya karibuni yameonyesha kuwa Tanzania hatuisapoti tena Palestina:


1. Baada ya kuwaangusha Wapalestina kule Paris kwenye Mkutano wa UNESCO, Serikali iliahidi kuwa ingemchukulia hatua Afisa yule wa Wizara ya Mambo ya Nje aliyekwenda kinyume na Sera yetu ya Mambo ya Nje, hatujafanya hilo, zaidi tumempandisha cheo na kumteua kuwa Balozi wetu wa Ankara, Uturuki. Jambo hilo linaonyesha kuwa tulimtuma Balozi Elizabeth Kiondo apige kura namna ile kule UNESCO, na sasa tumempa cheo zaidi kwa kazi njema aliyoifanya. Jambo hili linaonyesha kuwa kwa sasa tunawaunga mkono Waisrael, na hatuko tena na Wapalestina.


2. Kwa sasa tumeamua kufungua ubalozi wetu Israel, Tel Aviv, kuongeza uchungu kwenye Kidonda, tukachagua wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel katika ardhi ya Taifa la Palestina kuzindua ubalozi wetu huo. Jambo hili linafanyika kukiwa na tuhuma kuwa hata huo Ubalozi unagharamiwa na Israel yenyewe, ndio maana tumepangiwa hata kipindi cha kuufungua. Kidiplomasia kuufungua ubalozi wetu katika wakati huu ni kuazimisha uvamizi wa Israel katika ardhi ya Palestina. Maana tulikuwa na uwezo wa kuchagua wakati mwengine wowote kufanya uzinduzi wa ubalozi wetu, lakini kwa kuwa aliyegharamia uwepo wa ubalozi huo (Israel) alitaka tuufungue wakati huu wa maazimisho ya miaka 70 ya Uvamizi wa Israel kwa Palestina, ilitubidi tufanye hivyo. Jambo hilo limeonyesha kuwa kwa sasa hatuungi mkono tena utu (Palestina) bali tunamtumikia Kila mwenye kitu (Israel).


3. Wakati akiwa ziarani Israel, Balozi Mahiga alifika sehemu ya miji inayokaliwa kimabavu na Israel ambayo inapakana na Ukanda wa Gaza. Na baadaye alihojiwa na Televisheni ya Taifa ya Israel, ambako alionyesha tu masikitiko yake kwa Waisrael wanaokaa maeneo hayo kwa kusumbuliwa na mashambulizi ya Hamas. Lakini hakulaani kabisa uendelezaji wa Israel kujenga makazi kwenye maeneo hayo ya uvamizi kama Wanadiplomasia wengine wa nchi zenye msimamo wa ‘Two States Solution’ kama sisi wanavyofanya. Balozi Mahiga mwanadiplomasia mzoefu na mbobezi, Kutokulaani kwake makazi yale haramu ni jambo la makusudi kabisa, si bahati mbaya. Ni kitendo cha kutuma salamu kwa Wapalestina kuwa tunaunga mkono uendelezaji makazi wa Israel katika maeneo hayo iliyoyavamia.


4. Tanzania imetajwa na vituo mbalimbali vya habari vya Kimataifa kuwa ni katika nchi 33 ambazo zilihudhuria ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, Mei 14, kilele cha maazimisho ya miaka 70 tangu uvamizi wa Israel katika maeneo ya Wapalestina. Chanzo cha taarifa ya Tanzania kuhudhuria ni Serikali ya Israel, ikitaja nchi ilizozialika na zilizohudhuria. Serikali yetu inasema inapinga uwepo wa Ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem, lakini hapo hapo inatajwa kuhudhuria uzinduzi huo. Picha tunayoitoa hapa kwa Wapalestina ni kuwa tunaunga mkono jambo hili la ufunguzi wa ubalozi wa Marekani mjini Jerusalem.


5. Siku ya uzinduzi huo wa ubalozi wa nchi ya Marekani mjini Jerusalem, Jeshi la Israel liliwaua kwa risasi zaidi ya watu 54 wa Palestina, wakiwemo wanawake, watoto, walemavu na hata wanahabari. Nchi mbalimbali duniani zimelaani mauaji hayo. Nchi ya Afrika ya Kusini imekwenda mbali zaidi kwa kumrudisha nyumbani Balozi wake aliyeko Israel. Sisi Tanzania tulioikomboa Afrika Kusini tumekaa kimya, tumeshindwa hata kutoa kauli ya kulaani mauaji hayo. Kuhudhuria kwetu ufunguzi wa ubalozi na kukaa kimya juu ya mauaji hayo kunaonyesha tumewaacha rasmi Wapalestina.


Mambo hayo matano yanaonyesha kuwa sisi si tena ile Tanzania ya Mwalimu Julius Nyerere, sisi kwa sasa ni Tanzania Mpya (kama yasemavyo matangazo ya Ikulu yetu) - Tanzania mpya inayosimama na Waonevu wa dunia, Wauaji na Wavunja haki za wanyonge. Sisi si tena Tanzania ya kusimama na wanyonge, bali ni Tanzania ya kusimama na Wanyongaji kwa sababu ya maslahi ya kiuchumi.


Si ile Tanzania iliyoongoza Ukombozi wa Bara la Afrika kutoka kwenye makucha ya Ukoloni, bali ni Tanzania Mpya inayounga mkono na kushabikia ukoloni na Uvamizi. Sisi si ile Tanzania yenye msimamo mkali tuliyolipinga Taifa kubwa la Marekani dhidi ya Uvamizi wake kwa wanyonge wa taifa la Vietnam, bali sasa ni Tanzania mpya ya kuunga mkono Uvamizi wa Taifa onevu la Israel kule Palestina. Sisi si Tanzania ile iliyoitetea China ipate nafasi na kiti chake stahili kule UNO, bali sasa sisi ni Tanzania mpya inayowaacha watu wa Palestina bila utetezi wa hadhi, kiti na nafasi yake stahili kule UNESCO.


Sisi si ile Tanzania huru tena ya Mwalimu Nyerere, iliyowaheshimu watu na mataifa kwa sababu ya Utu wao na kuamini kwamba binaadam wote ni sawa. Sasa sisi ni Tanzania mpya, inayowapa heshima watu kwa sababu ya kitu inachotuhonga, tukiuza usuli wa Utaifa wetu kwa maslahi machache ya kifedha au kiuchumi.


Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau. Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.


  1. Kujengewa Uwanja wa Mpira na Msikiti Visiifanye Tanzania Iikumbatie Morocco na Kuacha Kuiunga Mkono Sahara Magharibi

[Sehemu ya Pili ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Bado niko kwenye Sera ya mambo ya nje ya nchi yetu, si hii ya Tanzania mpya, bali ile Tanzania ya tangu wakati wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ya kusimama na wanyonge. Wakati tulipoamua kufuata ‘Diplomasia ya Uchumi’ bado msingi wetu huu wa kusimama na wanyonge ulibaki pale pale. Ndio maana wakati wa Rais Ben Mkapa na Jakaya Kikwete bado tulibaki kuwa ni sauti ya mataifa yanayoonewa kama Cuba (tukipinga vikwazo vya Marekani dhidi yao), Palestina na Sahara Magharibi.


Msingi huo wa kusimama na wanyonge ni muhimu zaidi kwa chama chetu cha ACT Wazalendo, ndio maana tulipinga ujio wa Mfalme wa Morocco hapa nchini Oktoba 23 - 25, 2016. Kwa kuwa Taifa hilo bado linaikalia kimabavu ardhi ya wanyonge wa Sahara Magharibi. Ndio msingi pia wa kutangaza wazi mahusiano yetu rasmi na Chama cha cha siasa na ukombozi wa Taifa hilo cha Polisario kinachopigania Uhuru wa nchi ya Sahara Magharibi.


Umoja wa Afrika (AU) uliamua kukubali ombi la Morocco kurudi bila masharti kwenye jumuiya hiyo. Ikimbukwe kuwa kwa zaidi ya miaka 33 Morocco haikuwa na mahusiano na jumuiya hiyo (tangu OAU mpaka sasa AU) baada ya kujitoa kwa kupinga OAU kuitambua Sahara Magharibi kama Taifa huru na kupewa kiti rasmi ndani ya OAU mwaka 1984.


Uamuzi wa OAU wa kuiruhusu Sahara Magharibi Kuwa mwanachama wa Umoja huo ulitokana na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice - ICJ) ya mwaka 1975 iliyopinga madai ya Morocco kuwa ina mahusiano ya kihistoria na kisheria na Sahara Magharibi (na hivyo kuitawala kinguvu) na kutoa haki ya kujitawala kwa Taifa hilo.


Tunaheshimu maamuzi yale mkutano wa AU wa Januari 2017, ulioirudisha Morocco kwenye AU. Lakini tabia za Taifa hilo onevu bado hazijabadilika, ni muhimu tulieleze bunge masuala yafuatayo ili liweke msimamo wake kwa Serikali juu ya kuminywa kwa watu wa Sahara Magharibi:


1. Kikao cha AU cha Januari 28 - 29, 2018 kiliazimia kuwa Morocco iruhusu Kamati Maalum ya Uangalizi ya AU iende kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo inayakalia kimabavu ili kuja kuijulisha AU hali ya mambo ilivyo.


2. Machi 29, 2018 Morocco iliwajulisha UN juu ya kutoruhusu waangalizi wowote wa AU kwenda kwenye maeneo yote ya Sahara Magharibi inayoyakalia.


3. Tangu mwaka 1991 Morocco imetumia mbinu, hila, na uzandiki ili kuzuia Tume ya Umoja wa Mataifa kwaajili ya Kura ya Maoni ya Uhuru wa Sahara Magharibi (MINURSO) kufanya kazi yake kwenye maeneo inayoyakalia kimabavu ya Sahara Magharibi. Siku za karibuni, Umoja wa Mataifa, UN ulipitisha azimio namba 2414 (2018) la kuongeza muda wa mamlaka, uahai na madaraka ya (MINURSO) kwa miezi sita. Morocco imepinga jambo hilo na kutishia kufanya mashambulizi ya kijeshi kwenye maeneo ya Sahara Magharibi ambayo yameshakombolewa (Liberated Zones).


4. Bado Morocco inaendeleza uvunjaji mkubwa wa haki za binaadam kwa watu wote wa Sahara Magharibi wanaodai Uhuru wao.


5. Kurudishwa kwa Morocco kwenye AU kulienda pamoja na Taifa hilo kuridhia ‘AU Constitutive Act’ inayoyataka mataifa ya Afrika kuheshimu maazimio ya AU na hata yale ya UN yanatolewa kwa ushirikiano na AU. Lakini kwa matendo yake tuliyoyaainisha hapo juu ni dhahiri kuwa Morocco haitaki usuluhishi na Sahara Magharibi, bado inataka kuitawala na kuikalia kimabavu, bado Morocco inataka kuendelea kuwa mkoloni. Ndio maana imekataa hata kumpa ushirikiano msuluhishi wa mgogoro huu, ndugu Horst Köhler, Rais wa zamani wa Ujerumani


6. Matendo ya Serikali yetu kwa sasa yanaonyesha hatuna msimamo kwenye mambo ya msingi ya kidiplomasia, namna tulivyoenenda kwenye mahusiano yetu na wanyonge wa Palestina ni mfano hai, sasa tukijali vitu kuliko utu kama ilivyo zamani.


Hivyo basi, nataka kulishawishi Bunge lako litoe muongozo kwa Serikali juu ya kuenenda kwenye hili jambo la Morocco na Sahara Magharibi, ili kuzuia ahadi ya kujengewa Uwanja na Msikiti na Serikali ya Morocco (Vitu) isitufanye tu waache ndugu zetu Wanyonge wa Sahara Magharibi.


Nchi yetu ni kimbilio la Nchi ya Sahara, Serikali yetu chini ya Mwalimu Nyerere ililitambua Taifa la Sahara Magharibi tangu siku za mwanzo kabisa za harakati zao, ndio maana wanao Ubalozi hapa nchini. Kumuenzi baba wa Taifa na kulinda misingi ya Taifa letu ni lazima tusimame na watu wa Sahara Magharibi, na tusiwatupe kama tulivyofanya kwa watu wa Palestina.


Naliomba Bunge liibane Serikali ili itoe ahadi hiyo hapa Bungeni, pamoja na kuitaka Serikali kutumia ushawishi wake kule AU na UN kuibana Morocco iruhusu kura ya maoni ya kuamua mustakabali wa watu wa Sahara Magharibi kama ilivyoridhiwa kwenye Azimio la UN.


Viva Sahara Magharibi

Viva Polisario

Mungu Ibariki Afrika


  1. Hakuna Diplomasia Bila Wanadiplomasia: Tuna Uhaba Mkubwa wa Watumishi Kwenye Balozi Zetu

[Sehemu ya Tatu ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Msingi wa tano wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania unatutaka tushirikiane kikamilifu na Nchi, Mashirika pamoja na Taasisi mbalimbali katika nyanja za Diplomasia, Siasa, Uchumi, Utaalam na Teknolojia. Wizara hii ina jukumu la kubuni na kusimami utekelezaji wa misingi yote ya Sera yetu ya Mambo ya Nje.


Pia Wizara hii pia ina jukumu la kusimamia na kuratibu mahusiano kati ya Tanzania na nchi pamoja na mashirika mbalimbali. Utimizaji wa jambo hilo unafanyika kupitia balozi zetu zilizotapakaa kwenye nchi mbalimbali ulimwenguni. Kwa sasa ufanisi wetu ni mkubwa kwa sababu ya uhaba wa watumishi kwenye balozi zetu mbalimbali duniani.


Kwa wastani ukimuondoa Balozi, kila kituo cha Ubalozi wetu nje ya nchi kinapaswa kuwa na Mhasibu, mtu wa TISS na pamoja na Mwanadiplomasia (FSO). Vituo vingi vya balozi zetu havina kabisa Maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Wale wachache waliokuwepo awali walirudishwa nchini kwa sababu mbalimbali (ikiwemo kumaliza muda wao wa utumishi Nje ya Nchi). Tumerudisha watu bila kupeleka mbadala wao.


Kwenye balozi zetu mbalimbali watendaji hasa wa kazi za Kibalozi na kidiplomasia ni hawa maafisa wa Diplomasia (FSO’s). Sasa kwa uhaba huu tunawezaje kufanya Diplomasia ya nchi yetu? Hiyo Diplomasia ya Uchumi tunafanyaje bila kuwa na hao Wanadiplomasia?


Nitatoa tu mfano wa balozi zetu chache ulimwenguni. China, nchi ambayo ni mshirika wetu mkubwa kidiplomasia na kiuchumi, hatuna kabisa FSO huko, labda ndio sababu mauzo yetu kwenda China yameshuka mno, maana biashara ya nje ni Diplomasia, sasa wakati Spika unamtaka ndugu yangu Mwijage asafiri, ni nani atakayemuandalia hiyo mikutano ya kupata wawekezaji huko China kama hatuna FSO hata mmoja? Wenzetu Uganda wana FSO’s 8 huko China, Kenya na Sudan wao wanao 9 Kila mmoja.


Nchi nyengine ambayo hatuna kabisa FSO ni Ethiopia - Makao Makuu ya AU, utaona tunavyodharau nafasi yetu katika Afrika. Pia hatuna FSO Afrika Kusini, nchi rafiki na moja ya zenye uchumi mkubwa Afrika, hatuna kabisa FSO Ujerumani - Nchi kubwa zaidi kiuchumi katika Umoja wa Ulaya (EU). Hata India ambako tangu Bunge lianze wabunge tunalalamikia kukosa soko la mbaazi kutoka huko nako hatuna FSO hata mmoja. Tumeufanya kuwa ubalozi wa kupokea wagonjwa tu.


Nchi za Brics (ukiondoa China, India na Afrika Kusini ambazo hatuna kabisa FSO’s) zilizobaki, Brazil na Urusi tuna FSO mmoja mmoja tu. Hata DRC Congo - Nchi ambayo zaidi ya theluthi moja ya mizigo ya Transit inayopita kwenye bandari ya Dar inatoka, nayo tuna FSO mmoja tu tofauti na watatu ilivyozoeleka. Kenya - Nchi ya Afrika Mashariki tunayofanya nayo biashara zaidi nayo ina FSO mmoja tu.


Hali iko hivyo karibu katika balozi zetu nyingi ulimwenguni. FSO’s ndio maafisa hasa waliofundwa na kupikwa kutekeleza Sera yetu ya mambo ya Nje. Foreign Service Officers (FSO’s) ndio diplomats (wanadiplomasia wetu). Kama hawapo vituoni, na hatuwatumii maana yake hatufanyi diplomasia, na kwa kuangalia mbali tunaua diplomasia yetu.


Mimi sitapitisha bajeti hii mpaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itakaponihakikishia kuwa itapeleka Maafisa wa Diplomasia (FSO’s) katika vituo ambavyo hatuna kabisa na pia kuwaongeza katika vile vituo ambavyo wako wachache.


Tunasimama na Iran na Qatar, Uonevu Dhidi Yao Si Sawa - Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


Tunasimama na Iran na Qatar - Uonevu Dhidi Yao Si Sawa. Tanzania Tusaidie Amani ya Ulimwengu.


[Sehemu ya Nne na ya Mwisho ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19]


Mheshimiwa Spika


Jambo la mwisho kwenye mchango wangu ni juu ya hali ya ulinzi na usalama duniani. Usiku wa kuamkia Disemba 9, 2017, tulipoteza askari wetu 14 na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa huko DRC Congo, wakiwa kwenye Jeshi la kulinda Amani la Umoja wa Mataifa. Nachukua nafasi hii kuwaombea kwa Mola awalaze pema, pamoja na kutoa pole kwa familia zao na kwa Jeshi zima la JWTZ.


Taifa letu linachangia pakubwa katika kulinda amani ya ulimwengu, wanajeshi wetu wakaiwa karibu katika nchi nane duniani. Naamini tunao wajibu kama Taifa kusaidia uwepo wa amani Ulimwenguni ili kuzuia nchi zilizo kwenye machafuko kama DRC Congo kuongezeka na askari wetu wa kulinda amani kupotea.


Tayari, katika siku za karibuni, dunia imeshughudia maafa makubwa ya vita nchini Libya (ambako Rais Kikwete ni msuluhishi), Iraq, Afghanistan, Somalia, Syria, Sudan Kusini na Yemen. Mwenendo wa migogoro na uonevu unofanyika Qatar na unaotaka kufanyika Iran unapaswa kukemewa mapema ili kuchochea amani ulimwenguni, hasa eneo la mashariki ya kati ambalo tayari limeharibiwa na vita.


Hotuba ya Waziri ya Bajeti ya Wizara hii kwa mwaka 2016/17 ilibeba pongezi kwa nchi za Iran, Marekani, China, Urusi, UN na Umoja wa Ulaya (hasa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani) kwa makubaliano ya Nyuklia ya yaliyoiondolea vikwazo Iran kwa masharti ya kutoendeleza urutubishaji wa nyuklia. Makubaliano yale ni muhimu kwa kuwa iliondoa hali ya mashaka iliyokuwa imetanda duniani.


Tumeona Marekani imejitoa kwenye makubaliano hayo, na kutishia kuweka vikwazo vipya kwa Iran. Huku wajumbe wengine wa wakiendelea kubaki kwa kuwa bado Iran imeendelea kutekeleza makubaliano husika, na kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki, IAEA ni kuwa bado Iran inafuata masharti ya makubaliano husika.


Uamuzi huu wa Marekani si mzuri, unarudisha hali ya mashaka kwenye eneo la mashariki ya kati, ni uonevu dhidi ya Iran, hasa kwa kuwa IAEA imethibitisha kuwa Iran haina makosa. Ni maamuzi ya uonevu tu na usiochochea amani, ni uamuzi unaopaswa kupingwa. Serikali yetu iitumie nafasi yake kule UN kupinga uamuzi huu, na kuitaka Marekani kurudi kwenye makubaliano haya ili kudumisha amani.


Pia Julai 26, 2017 Wizara hii ilitoa taarifa yake juu ya mgogoro wa nchi za Ghuba (GCC), baada ya hatua ya nchi nne za Saudi Arabia, UAE, Bahrain na Misri kuiwekea vikwazo vya anga, bahari na ardhini nchi ya Qatar. Msimamo wa Serikali ni kuunga mkono upatanishi unaongozwa na Amir wa Kuwait, Sheikh Sabah Al-Jaber, tunaunga mkono msimamo huo.


Lakini bado pia sisi ACT Wazalendo tunasimamia tamko letu la kupinga uonevu dhidi ya Qatar tulilolitoa July 24, 2017. Kwa karibu miezi 10 sasa watu wa Qatar wamewekewa vikwazo vya kiuchumi na kiusafiri, kwenye anga, ardhi na bahari na nchi hizo nne jirani, jambo hilo si sawa, hasa kwa kuwa masharti yaliyotolewa ili kuondoa vikwazo hivyo yanaingilia uhuru wa nchi hiyo.


Tunaitaka Serikali yetu, pamoja na kusapoti usuluhishi huu wa Kuwait, itumie nafasi yake pia kule UN kuhakikisha inachangia usuluhishi wa jambo hili ili mashaka yaliyoko na vikwazo kwa Qatar viondoshwe.


Ahsanteni kwa Kunisikiliza. Naomba Kuwasilisha


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge, Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Bungeni Dodoma

Mei 23, 2018
 
Kwa akili yako ulitegemea afanye nini baada ya kutujulisha sisi watz kuwa kuna upotevu wa 1.5t?

Wewe kama mtz ulitakiwa kuchukua hatua, yeye alishamaliza kazi yake.

Akili ya kiccm mbaya sana.
Soma uelewe ili uweze kunielewesha mkuu punguza jazba.
 
Zitto anajikomba kwa wapalestina Na sahara magharibi.Hao Hawajawahi Toa tamko lolote la mauaji ya kimbari ya Rwanda Na Burundi,wala kutoa tamko lolote kuhusu waisalamu wanaouawa kila siku kule somalia Na Dafur Na hawajawahi Toa tamko lolote kuhusu mauaji ya boko haramu Wala kutoa pole kwa waliokufa kwa meli ya MV bukoba,waliokufa Kibiti nk ndio maana tunawaona hawana maana
 
JIWE mwenyewe exposure hana unategemea ataweza kuwa na sera za uhusiano wa kimataifa zenye mantiki?.
 
Hivi zitto kabwe Ni kiongozi wa ACT wazalendo bungeni? Kule ndani Ni mbunge tu wa kawaida huo mchango spika autupilie sababu Ni wa chama Cha ACT wazalendo.B unge si kazi take kupokea michango ya vyama bungeni
 
Sioni sababu ya kukomaa na ukombozi wa nchi zingine huku Tanzania inatudodea hapa.Kuwa mstari wa mbele katika ukombozi wa baadhi ya nchi za Afrika hatujatusaidia chochote.Ule msemo wa tenda wema uende zako unaendekeza umaskini tu maana.Ni zamu ya Tanzania kujikomboa kwa sasa.Wema mwingi tutakufa maskini tu
 
Ya nyumbani yametushinda unataka pia tuingie kwenye migogoro mingine nje......punguza akili kidogo ,
 
Zitto, mbunge ambae hajawahi kufanya kazi serikalini, much less wizara ya nje, anachambua siasa za kimataifa na historia ya foreign policy ya Tanzania kwa weledi kuliko huyo Mahiga mwenye uzoefu wa kazi za kimataifa wa muda mreeeefu lakini uzoefu wa bure, hakujifunza lolote...
 
Back
Top Bottom