Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,271
- 6,837
Zitto kuandika barua Benki ya Dunia siyo kosa ndiyo, ila kosa ni kutumia nembo ya Bunge kuiandikia Benki ya Dunia, na kusaini barua kama Mbunge wa JMT, wakati Bunge halikuwa na taarifa rasmi kuhusiana na barua yake hiyo.
Zitto alitakiwa aandike barua hiyo kama Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, na aisaini kama kiongozi wa ACT na si kama Mbunge. Au angeiandika kama mtu asiyekuwa na cheo kama mimi hapa, yaani kama raia tu mkereketwa na angeisaini kwa kutumia hadhi hiyo.
Sasa yeye analiumia Bunge la JMT kuipiga Nchi halafu bado kosa anakuwa halioni?
Ninasikitika kwamba kosa hili liko wazi na kwamba hakutakiwa kuwa angekuwa hajaliona mpaka leo, intelligent as he is!
================================
Dar es Salaam. Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania, Zitto Kabwe amesema haoni kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali atamkuta na kosa kutokana na kuiandikia barua Benki ya Dunia (WB) akitaka isiidhinishe mkopo wa Sh1.2 trilioni kwa Tanzania kwa ajili ya sekta ya elimu.
Zitto ameeleza hayo leo Jumanne Februari 18, 2020 katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu ya kutetea nafasi yake katika uchaguzi wa chama hicho.
Katika mkutano wa 18 wa Bunge uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma, Zitto alishukiwa na wabunge kwa kitendo chake hicho huku Spika Job Ndugai akisema watamsubiri arejee nchini ili wamuulize sababu za kufanya hivyo, hapohapo akamtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuangalia kama kuna uwezekano wa kuwemo jinai katika kitendo hicho.
Katika mkutano wake huo Zitto amesema, “sioni kosa lolote ambalo Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza akalikuta kwamba nimelifanya kwa kuandika barua WB. Hizi ni siasa tu ambazo zilikuwa hazifanyiki huko nyuma, au watu walikuwa wanafanya kwa kificho sasa mimi nimezifanya kwa uwazi ndio tofauti tu hiyo, haina maana kuwa ni kitu kipya sana”
Amesema kila Mtanzania ana haki ya kuwasiliana na Benki ya Dunia iwapo Serikali yake kuna mambo imekosea katika maombi ya fedha katika benki hiyo.
Chanzo: Mwananchi
Zitto alitakiwa aandike barua hiyo kama Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, na aisaini kama kiongozi wa ACT na si kama Mbunge. Au angeiandika kama mtu asiyekuwa na cheo kama mimi hapa, yaani kama raia tu mkereketwa na angeisaini kwa kutumia hadhi hiyo.
Sasa yeye analiumia Bunge la JMT kuipiga Nchi halafu bado kosa anakuwa halioni?
Ninasikitika kwamba kosa hili liko wazi na kwamba hakutakiwa kuwa angekuwa hajaliona mpaka leo, intelligent as he is!
================================
Dar es Salaam. Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania, Zitto Kabwe amesema haoni kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali atamkuta na kosa kutokana na kuiandikia barua Benki ya Dunia (WB) akitaka isiidhinishe mkopo wa Sh1.2 trilioni kwa Tanzania kwa ajili ya sekta ya elimu.
Zitto ameeleza hayo leo Jumanne Februari 18, 2020 katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu ya kutetea nafasi yake katika uchaguzi wa chama hicho.
Katika mkutano wa 18 wa Bunge uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma, Zitto alishukiwa na wabunge kwa kitendo chake hicho huku Spika Job Ndugai akisema watamsubiri arejee nchini ili wamuulize sababu za kufanya hivyo, hapohapo akamtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuangalia kama kuna uwezekano wa kuwemo jinai katika kitendo hicho.
Katika mkutano wake huo Zitto amesema, “sioni kosa lolote ambalo Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza akalikuta kwamba nimelifanya kwa kuandika barua WB. Hizi ni siasa tu ambazo zilikuwa hazifanyiki huko nyuma, au watu walikuwa wanafanya kwa kificho sasa mimi nimezifanya kwa uwazi ndio tofauti tu hiyo, haina maana kuwa ni kitu kipya sana”
Amesema kila Mtanzania ana haki ya kuwasiliana na Benki ya Dunia iwapo Serikali yake kuna mambo imekosea katika maombi ya fedha katika benki hiyo.
Chanzo: Mwananchi